Waache waendelee kujihesabia haki my dear hawajui mtu jinsi unavyiona dhambi fulani ni mbaya ndivyo unavyotafuta nafasi ya kuitubu hiyo dhambi! Mtu ukishaichukulia dhambi fulani ni ya kawaida basi utabweteka hutatubu ukijua kwamba utasamehewa tu kwa sababu eti kuna watu wenye dhambi kubwa zaidi yako ila hautaamini utakachoenda kukutana nacho!
Pale mwisho wa siku mlevi ,mzinzi ,msengenyaji na shoga wote wanajikuta wanaogelea ziwa la moto.
Neno: Bibilia Takatifu
Mfano Wa Farisayo Na Mtoza Ushuru
9 Yesu alitoa mfano huu kwa ajili ya wale waliojiona kuwa wao ni wenye haki na kuwadharau wengine. 10 Watu wawili walikwenda hekaluni kusali, mmoja wao alikuwa Farisayo na mwingine alikuwa mtoza ushuru. 11 yule Farisayo alisimama akasali kimoyomoyo. ‘Ninakushukuru Mungu kwa sababu mimi si kama watu wengine: wany ang’anyi, wadhalimu, wazinzi, au kama huyu mtoza ushuru. 12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma na kutoa sehemu ya kumi ya mapato yangu.’ 13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali. Hakuthubutu hata kuinua uso wake kutazama mbinguni; bali alijipiga kifuani kwa majuto akasema, ‘Mungu, nihurumie, mimi mwenye dhambi.’
14 Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amehesabiwa haki mbele za Mungu na wala si yule Farisayo. Kwa maana ye yote ajikwezaye atashushwa na ye yote ajinyenyekezaye, atainuliwa.”
Luke 18:9-14
New International Version
The Parable of the Pharisee and the Tax Collector
9 To some who were confident of their own righteousness and looked down on everyone else, Jesus told this parable: 10 “Two men went up to the temple to pray, one a Pharisee and the other a tax collector. 11 The Pharisee stood by himself and prayed: ‘God, I thank you that I am not like other people—robbers, evildoers, adulterers—or even like this tax collector. 12 I fast twice a week and give a tenth of all I get.’
13 “But the tax collector stood at a distance. He would not even look up to heaven, but beat his breast and said, ‘God, have mercy on me, a sinner.’
14 “I tell you that this man, rather than the other, went home justified before God. For all those who exalt themselves will be humbled,and those who humble themselves will be exalted.