Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Mkuu mimi toka mwanzo point yangu ilikuwa hapo kwenye kutubu na kusamehewa sasa nashangaa kote huku sijui hata tulifikaje! Point yangu ilikuwa hapo kwamba huo utofauti wa dhambi uko wapi ikiwa baada ya Yesu kufa msalabani wote shoga na mlevi waliahidiwa kuwa wakitubu na kuacha basi wote watasamehewa na kuurithi ufalme wa mbinguni?

Wakati kwenye agano la kale ndiyo kulikuwa na ukubwa wa dhambi na watu waliadhibiwa kutokana na ukubwa wa dhambi zao! Lakini mambo yalibadilika baada ya ujio wa Yesu na kuna sehemu Yesu mwenyewe aliwaambia watu "yeyote ambaye hajawahi tenda dhambi na awe wa kwanza kurusha jiwe" akimtetea mtu aliyetaka kuuliwa kwa kupigwa mawe!

Kwahiyo kidini tunaona kwamba tayari imeshakuwa hivyo kwamba kitendo cha Mungu kusema kwamba eti shoga na jambazi wakitubu watasamehewa na wasipotubu hawasamehewi automatically kinafanya hizo dhambi ziwe sawa kwake hivyo haina haja ya biblia kuelezea tena! Hayo mengine sasa ndiyo tunayajadili sisi kwa utashi wetu!

Kwamba tunapinga ushoga kutokana na madhara haya na haya na tulipohamia kwenye kutumia utashi ndipo na mimi nikaona nijikite zaidi kwenye kukemea dhambi ya uzinzi wewe hukujiuliza kwanini sikujikita kwenye ulevi ama ujambazi? Ni kwa sababu ushoga kwa asilimia kubwa huanzia na hufanyika kwenye mazingira ya uzinzi hilo nilishalielezea kule juu!

Laiti kama watu wangekuwa hawafanyi mapenzi kabla ya ndoa basi ushoga usingeenea kwa kiasi hiki kwa sababu haiwezekani wanaume wawili mabikira wafunge ndoa eti ili wakashikishane ukuta hiyo experience wameipata wapi? Kwahiyo hadi hapo bado hujaona tu kuwa uzinzi kwa asilimia kubwa ndiyo hupelekea vijana wengi kujaribu na ushoga pia?

Mimi binafsi sikubaliani kabisa na ushoga na nitaupinga siku zote ila point yangu ni kuwa uzinzi ndiyo umetufikisha hapa tulipo! Haya tukija kwenye suala la maadili mfano tu leo hii wanawake wamefikia hatua wanatupia picha zao mitandaoni wakiwa uchi tena kwa kujiachia kabisa na wanaume na jamii nzima wanafurahia je hayo ni maadili kwa vizazi vyetu?

Je wanaume na wanawake kuzaliana hovyo tu bila ndoa wala utaratibu maalum hadi kupelekea kuwa na wazazi wahuni na watoto wengi wahuni waliokosa malezi bora ya wazazi wote wawili ambao wengi wa watoto hao nao huishia kuwa mashoga je hayo ni maadili? Je hayo yote kwa asilimia kubwa hayasababishwi na uzinzi tukiachilia mbali uyatima mkuu?
Mommah hakika wee ni akili kubwa na uko sawa, labda nikuambie ukweli haya yote unayowaambia wanayajua na yanawaingia vilivyo, ila unafiki wao unawasumbua hapa na hawana Pa kushika.


Kwa maelezo yako haya km hatakuelewa wee muache aongee akichoka ataacha mwenyewe, yaan anajiona yeye n much know sana huyu mtu. Au hamjawahi kuona ktk nyuzi zingine masifa yake? Yaan anaona wenzie wote n makururu ila yeye ndo mjuaji, anakera sana yaan. Mie nimeshachoka kuona essay zake zisizo hata na maana.

Anaboa mnoo aaaah.
 
Back
Top Bottom