Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Aiseee hivi ni kwanini mkishashikiwa pabaya huwa mnakimbilia kusema kuwa siyo wote wanaoamini dini wala uwepo wa Mungu? Na huwa mnakimbilia kwenye mwamvuli wa sheria na tamaduni kwani kila mtu anafuata hizo tamaduni?

Sasa kama wewe hauwaheshimu mashoga kwanini unanilazimisha mimi niwaheshimu watu wasioamini Mungu katika kundi la watu wengi wanaoamini Mungu? Je vipi dunia nzima tukasema tusimuamini Mungu hali itakuwaje?

Halafu pia kwanini ulazimishe kila mtu aamini sayansi what is sayansi? Wakati hata sayansi nayo kuna vitu havijawa proven kwa asilimia mia moja kama ambavyo atheists wanaamini kuna vitu kuhusu deity havijawa proven kwa asilimia mia moja?
yaan leo umejua kuwapa watu challenge, wakabaki kutoa hoja zisizo na mashiko, mie ndo nlikua nasoma huku nakufa mbavu yaan, mweeeeh.
 

Yaani ukae kimya!
Nimecheka sana.
Nisomee wapi,nishatupia kwenye zile takataka zangu kwa kile kitufe.

Bangi ni mbaya.
Ah huyu si ashawahi kupachika ndugu zake kwenye comment yangu.
Akawapachika na kina Billgate kwahiyo wala sishangai. .bahati nzuri nilikuwa kwenye mood yangu nzuri ya maombi.


Hata hii mada naona alijipachika kwenye comment zenu.
Ndio hapo sasa
 
Haaaa mimi uwa yanaishia hapa hapa mchumba! Nikiwa na Jack daniels yangu uwa nachat for fun tu

Sina sababu ya kuanzisha uzi may be siku moja nikipata sababu nitaanzisha.
Unaanzisha tu hata kwa ajili ya kuchitchat.
Sawa mkemia wetu.

Kuna mwenzio jana ndugu yangu amenivunja mbavu,
image-edit-20211203230527.jpg
image-edit-20211203230745.jpg
 
Mkuu mbona unazunguka tu wakati mimi nimeenda straight to the point? Mimi siungi mkono mapenzi ya jinsia moja bali nawacrush wale mnaowarushia mawe wanaofanya mapenzi ya jinsia moja ilihali na ninyi ni wazinzi, majambazi, wakana Mungu nk na ndiyo maana nikakuuliza utofauti wa hizo dhambi uko wapi ikiwa adhabu ya mzinzi na shoga ni moja wote wataenda kuchomwa moto wa milele wasipotubu?

Wengi mmeng'ang'ania huo mfano wa Sodoma na Gomora ila hamtaki mfano wa Mungu kuangamiza dunia kwa gharika sababu ya dhambi nyinginezo! Haya je tangu Mungu aangamize hiyo Sodoma na Gomora mbona mashoga wamezidi kuongezeka je kuna adhabu nyingine ya hapa duniani ambayo mmeona amewapa hawa mashoga wanaozidi kuongezeka mbona kuna wengine ndiyo kwanza maisha yao yanazidi kuwanyookea mmebaki ninyi ndiyo mnateseka?

Mkuu narudia kwa sisi wakristo maandiko yako wazi kwamba baada ya Yesu mwana wa Mungu kutufia msalabani dhambi zote zikawa sawa kasoro dhambi moja tu ya KUMDHIHAKI ROHO MTAKATIFU! Kwamba mtu yeyote mwenye dhambi yoyote ile isipokuwa hiyo tajwa basi akitubu kwa roho na kweli atasamehewa na asipotubu hatasamehewa na ataenda kuface hukumu na moto wa milele!

Mbona mnajifanya mnajisahaulisha kwamba kwenye agano jipya baada ya Yesu kupaa mbinguni sheria nyingi za agano la kale zilibadilishwa? Kwa taarifa yako hayo mambo ya kupimiana ukubwa wa dhambi yalikuwa kwenye agano la kale enzi ambapo torati au sheria ya Musa ilikuwa inafuatwa ila kwenye agano jipya hakuna hayo mambo!

Na Yesu alishasema mtu hataenda mbinguni kwa matendo yake tu bali pia anatakiwa amuamini yeye kama njia ya kwenda mbinguni kwa Baba yake na hayo maneno yamekuwa yakihubiriwa hadi wa leo! Hivyo watu kutokujua uwepo wa Mungu hapo zamani siyo excuse ya kwamba hata ulimwengu wa sasa ambao umeshaijua injili nao usiamini eti kisa tu babu zetu hawakuijua dini!

Nilikupa andiko linalosema kwamba mtu ambaye anatoa boriti kwenye jicho la mwenzie ilihali hajatoa kibanzi kilichopo kwenye jicho lake mwenyewe biblia inamuita mnafiki! Kwa sababu kazi ya kuhukumu Mungu alishaitoa mikononi kwa wanadamu akaiweka mikononi mwake ndiyo maana hayo mambo ya kupigana mawe na kunyongana kwenye dunia ya leo hayapo kwa wanaoamini Mungu!

Hakuna kitu kibaya kama kujihesabia haki yaani Mungu anachukia sana mtu anayejihesabia haki na kujiona yeye mtakatifu na wengine wana dhambi kuliko yeye na hicho ndicho ambacho wazinzi mnafanya kwa mashoga! Hata Musa pamoja na kwamba Mungu alimpenda hadi alikubali amuone!

Lakini kosa lake kubwa lillilomfanya Mungu amnyime neema ya kuingia Kanaani ni kujihesabia haki akaishia tu kuoneshwa Kanaani ile na akafia kule kule! My point from the beginning is acheni kujihesabia haki na kujiona ninyi ni watakatifu sana binafsi nachukia sana uzinzi na sipendi kuona mijitu inajisifia uzinzi eti ni kawaida hivyo kwangu (na kwa Mungu ofcourse) wazinzi na mashoga wote wana dhambi na watahukumiwa!

Usijifiche kwenye kichaka cha sijui eti "hiyo hoja yako ni mfu" bila kutoa ufafanuzi ukidhani kwamba tunashindania hoja mimi siko hapa kushindana ila inabidi tukubali tu kwamba tuache unafiki kuhukumu watu kama biblia inavyotuita! Wewe unavyowaona na kuwachukulia mashoga ndivyo mimi ninavyowaona na kuwachukulia wazinzi na wakana Mungu na kiuhalisia wote hao ni threat kwa dunia ya sasa hakuna mwenye afadhali kama unavyotaka kuniaminisha hapa!
Mommah hakika shule ulienda kuchukua maarifa sio kusoma, wallah na niko serious, naomba tukutane nina zawadi yako kubwaaa, yaan nimesoma huku nashusha tabasamu zito lenye uvugu vugu la furaha,

Nakuambia wazi kwa madini haya, kuna watu wanaumia na kuteseka ndani kwa ndani, wasomapo hii convoy yako, ba hawaamuni ndo wee unapasua ukweli iv.

Ubarikiwe sana.
 
Kuna watu humu ni walevi kupindukia ila wapo kuwaandama wenzao
Ila dunia hii
Cha ajabu walevi na wazinzi wapo kujiona watakatifu sana

Wakati nao tunawavumilia tu humu na pombe zao.
dada leo umeamua wallah, mie huku natabasamu tyuuh.
 
Back
Top Bottom