Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Niambieni madam nani huyo😅😅😅
FB_IMG_1655566507147.jpg
 
Haya nakueleza wali maua
Hiyo ya kuchanganya na nyama sijawahi naona vitakuwa vingi labda uunge nyama pembeni

Mahitaji
Vitunguu 2
Carroti 2
Hoho 1 kubwa
Njegere kikombe 1
Wali vikombe viwili
-Iliki
-Njegere
-Kitunguu saumu
-Chumvi

Mandalizi

-Osha njegere zitoe kwenye maji
-Chambua iliki kisha zisage ziwe unga/robo kijiko cha chai
-Chambua mchele na uoshe
-Chambua kitunguu saum menya tangawizikisha visage
-Katakata karoti na hoho muundo wa vibox vidogodogo

Jinsi ya kupika

-Bandika sufuria yako jikoni,weka mafuta kidoogo saaana
-Kisha kabla hayajapata moto weka njegere hii inazuia njegere kutorukaruka,koroga hadi njegere zibadilike rangi
-Kisha weka Karoti endelea kukuroga
-Weka mchanganyiko watangawiz na kitunguu saum koroga hapa usichelewe sana maana vitunguu huwa vinawahi kushika chini
-Weka unga wa iliki kisha mchele
-Koroga hadi vichanganyike haswaaa
- Weka maji kisha weka chumvi koroga na ufunike


Baada ya muda angalia wali wako kama umekauka kisha palilia(weka moto juu na chini kidogo)

Subiri kama dk 20 angalia kama umeiva weka hoho ulizokwisha zikata hapo awali kisha geuza kidoogo na funika tena kwa dk 5.

Baada ya hapo waweza pakua wali wako ukiwa na harufu nzuuri na mauwa yake ambayo ni karoti ,njegere na hoho
Nikajaribu hili pishi, huenda mtoto wa mama mkwe atatangaza ndoa karibuni
 
Back
Top Bottom