Nifundishe plz nijaribu maana Kuna siku nilinunua njegere na nyama nataka nipike nikaishia kuzigawa tu
Haya nakueleza wali maua
Hiyo ya kuchanganya na nyama sijawahi naona vitakuwa vingi labda uunge nyama pembeni
Mahitaji
Vitunguu 2
Carroti 2
Hoho 1 kubwa
Njegere kikombe 1
Wali vikombe viwili
-Iliki
-Njegere
-Kitunguu saumu
-Chumvi
Mandalizi
-Osha njegere zitoe kwenye maji
-Chambua iliki kisha zisage ziwe unga/robo kijiko cha chai
-Chambua mchele na uoshe
-Chambua kitunguu saum menya tangawizikisha visage
-Katakata karoti na hoho muundo wa vibox vidogodogo
Jinsi ya kupika
-Bandika sufuria yako jikoni,weka mafuta kidoogo saaana
-Kisha kabla hayajapata moto weka njegere hii inazuia njegere kutorukaruka,koroga hadi njegere zibadilike rangi
-Kisha weka Karoti endelea kukuroga
-Weka mchanganyiko watangawiz na kitunguu saum koroga hapa usichelewe sana maana vitunguu huwa vinawahi kushika chini
-Weka unga wa iliki kisha mchele
-Koroga hadi vichanganyike haswaaa
- Weka maji kisha weka chumvi koroga na ufunike
Baada ya muda angalia wali wako kama umekauka kisha palilia(weka moto juu na chini kidogo)
Subiri kama dk 20 angalia kama umeiva weka hoho ulizokwisha zikata hapo awali kisha geuza kidoogo na funika tena kwa dk 5.
Baada ya hapo waweza pakua wali wako ukiwa na harufu nzuuri na mauwa yake ambayo ni karoti ,njegere na hoho