benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Hatua hiyo inataokana na mikakati mbalimbali ikiwemo kufanya mabadiliko ya Sheria ya Madini ya mwaka 2010, yaliyotekelezwa mwaka 2017, hivyo kuundwa Tume ya Madini.
-
Mikakati hiyo imebainishwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba alipozungumza na waandishi wa habari, jijini Dodoma.
-
"Kuanzia mwezi Julai hadi Septemba, 2023 Tume ya Madini imepokea maombi mapya ya leseni za madini 7596. Yote yaliidhinishwa baada ya kukidhi vigezo," amesema mhandisi huyo.
-
Amesema katika ukusanyaji maduhuli kuanzia Julai hadi Septemba 2023, Tume ya Madini imekusanya Sh bilioni 184.53.
-
"Mikakati kabambe imewekwa na tume kuhakikisha lengo la kukusanya Sh bilioni 882.12 linafikiwa katika mwaka wa fedha 2023-24," amesema Samamba.
-
Amesema tume inahimiza wananchi kuwekeza katika sekta ya madini, kuanzia kwenye uchimbaji, uchenjuaji, biashara na utoaji huduma migodini.
-
"Bado tunaendelea na uhamasishaji wa wachimbaji wadogo wa madini wasio rasmi kuwafanya rasmi kwa kuwasajili sambamba na kutatua changamoto ili uchimbaji wao ulete tija," ametanabahisha kiongozi huyo.
-
Amewataka wadau wa madini nchini kufanya shughuli zao kwa uzalendo, kufuata sheria ya madini na kanuni zake sambamba na kujiepusha na vitendo vya utoroshaji wa madini.
-
-
Mikakati hiyo imebainishwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba alipozungumza na waandishi wa habari, jijini Dodoma.
-
"Kuanzia mwezi Julai hadi Septemba, 2023 Tume ya Madini imepokea maombi mapya ya leseni za madini 7596. Yote yaliidhinishwa baada ya kukidhi vigezo," amesema mhandisi huyo.
-
Amesema katika ukusanyaji maduhuli kuanzia Julai hadi Septemba 2023, Tume ya Madini imekusanya Sh bilioni 184.53.
-
"Mikakati kabambe imewekwa na tume kuhakikisha lengo la kukusanya Sh bilioni 882.12 linafikiwa katika mwaka wa fedha 2023-24," amesema Samamba.
-
Amesema tume inahimiza wananchi kuwekeza katika sekta ya madini, kuanzia kwenye uchimbaji, uchenjuaji, biashara na utoaji huduma migodini.
-
"Bado tunaendelea na uhamasishaji wa wachimbaji wadogo wa madini wasio rasmi kuwafanya rasmi kwa kuwasajili sambamba na kutatua changamoto ili uchimbaji wao ulete tija," ametanabahisha kiongozi huyo.
-
Amewataka wadau wa madini nchini kufanya shughuli zao kwa uzalendo, kufuata sheria ya madini na kanuni zake sambamba na kujiepusha na vitendo vya utoroshaji wa madini.
-