Salamu ya Rais Samia Suluhu 'Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano' ni salamu bomba sana

Angesema habari zenu ndugu zangu ingetosha?
Nikikusoma vizuri mleta mada kwangu naona hata huyo unayemsifia kwa kurekebisha naona nae hakurekebisha chochote, kwani kusema "nawasalimu kwa jina la muungano" ndio salamu ya hilo kundi kubwa unalosema halikusalimiwa mwanzo?

Nae naona amekwepa kutoa salamu stahiki kwa hilo kundi jingine kama ambavyo unamlaumu huyo wa kwanza kutokutoa salamu, alitakiwa kuwa straight kutoa salamu stahiki, sio kuleta salamu mpya ya kijanja.
 
Unakuta mtu anakulazimishia salamu ya dini yake au dhehebu lake wakati wewe huna hata habari na hiyo imani yake!
Bora hata wakiristo kidogo wako rational kidogo.

Hizi dini zimekuja kupumbaza watu, watu wajinga wamekua wapumbavu na wapumbavu wamekua mataahira kabisa.
 
Hatutaki Salamu kutoka kwa Watanzania wenzetu kwa lugha za nje, kitumike Kiswahili kutoa salamu. Vinginevyo kitumike Kingereza ambacho ni lugha yetu rasmi pia.
Kwani unajua maana ya salamu aliyoitoa katanga ni nini????

Kwa akili zenu mfu mnadhani salamu ya Katanga ni ya kidini??? Kweli hili taifa bado sana na ndo mana Mwendazake aliweza kuwa brainwash..
 
SIAFIKI HIYO SALAMU. Lazima appreciate Imani mbalimbali za watZ na hiyo inamleta karibu zaidi na Watanzania. kama makafiri na wenye imani za asili wamemwambia anapendelea basi ni dhahiri hajitambui.

Salamu zilkua mbili wakat kuna wengne hawana dini kuna wahindi hapa wana salamu zao wakat hawatumii salamu hizo je wao Au wao hawana haki ya kusalmiwa
 
4.Habari yenu ndugu zangu
5.Nawatakia amani
6.Habari za wakati huu
7.Heri kwenu
8.
Serikali ya JMT haina dini. Salamu katika shughuli za kiserikali zaweza kuwa;

1. Tanzania Hoyee!!!
2. Jambo Wananchi!!
3. Tanzania Juu!!!
4............,..

Hizi salamu za kidini kwenye mikutano ya kiserikali na vyama vya siasa zilianza kutumiwa kwa sababu ya ujinga tu.
 
Rais wetu toka akiwa Makamu wa Rais alipenda, kusalimia salaam alykum! Alikuwa hataji salamu zingine, nadhani kuna uzi humu uli hoji! Sasa kaona aje kivingine. Ila mie nasema. Kusalimiwa kwa Jamhuri ya Muungano wala haiji. Sasa tunaitikia vipi! Heri enzi za mkapa yeye alitumia Mambo!...
Yani mama kawashika pabaya mmebaki mnaongea utopolo tuuu, na mimi nasema ashikilie hapo hapo hadi mjue hii nchi ni yetu soteeee
 
Salamu za dini zitumike sehemu husika.
Hiyo ni sakaam ya kiislam acheni ubishi japo ina maana nzuri.huwezi kuitumia kanisani.ni sawa na kusena bwana asifiwe msikitini utakuwa wa ajabu.kwenye nchi ya dini kama hizi tuachane na hizo salaam za kidini au tutumie zote
 
Mama yetu ameanza vibaya. Namfuatilia sana. Kabeba sana Uislam na Uzanzibar. Sijui kama tutafika.
Na yule mwingine alibeba nini?

Najiuliza tu...mama angekuwa anatoa hotuba misikitini ingekuwaje hivi? (It's unlikely anyways).

Hebu tuache udini, tujenge Tanzania moja!
 
Kwa nini usalimie Waswahili wenzako kwa Kiarabu ? Ni bora utumie Kingereza kama hutaki kutumia Kiswahili
Kweli wajinga wengi sana na kamwe hawawezi kuisha yaani bado anajua As-salamu alaykum ni kiislam hahaaa.

As-salamu alaykum is a greeting in Arabic that means "Peace be upon you"
 
Zaidi ya nusu ya hii nchi hawajui kiarabu, hata hao wanaokifahamu ni huko kwenye mambo ya dini zaidi kwa nini usalimie Kiarabu na si Kiswahili au Kingereza ambazo ni lugha rasmi?
Nakwambia kwa Kweli. Wajinga nchi hii wako wengi sana . Hawajui hata hao waarabu wapo wakristo, waislamu na hata wasio dini na wote wakisalimiana wanatumia salamu iyoiyo.

 
Yani mama kawashika pabaya mmebaki mnaongea utopolo tuuu, na mimi nasema ashikilie hapo hapo hadi mjue hii nchi ni yetu soteeee
Sasa kashika nani. Wabongo! Haki ya kutoa maoni ni yakila mtu. Hakuna alie sema mama ni mmbaya. Ndo kwanza kashika kiti. Tuko nae pamoja ili ailetee maendeleo Tanzania.

Na tuna imani nae. Kupewa ushauri ni jambo la kawaida.
 
Zaidi ya nusu ya hii nchi hawajui kiarabu, hata hao wanaokifahamu ni huko kwenye mambo ya dini zaidi kwa nini usalimie Kiarabu na si Kiswahili au Kingereza ambazo ni lugha rasmi?
Kwani kwenye uswahili na waswahili iyo salamu haitumiki?
 
Hatutaki Salamu kutoka kwa Watanzania wenzetu kwa lugha za nje, kitumike Kiswahili kutoa salamu. Vinginevyo kitumike Kingereza ambacho ni lugha yetu rasmi pia.
Kwa akili yako fupi unadhani kiswahili kimetokana na lugha zipi??? Una elimu gani kwani?
 
Salama leko sio salumu universal. Huwezi kusalimia hivyo China, Russia, Latin America ukaacha kuonekana kituko na hiyo ni zaidi ya nusu ya dunia.
Mbona hilo hukohoji kipindi Cha mwendazake uje uhoji leo?
 
Rais wetu toka akiwa Makamu wa Rais alipenda, kusalimia salaam alykum! Alikuwa hataji salamu zingine, nadhani kuna uzi humu uli hoji! Sasa kaona aje kivingine. Ila mie nasema. Kusalimiwa kwa Jamhuri ya Muungano wala haiji. Sasa tunaitikia vipi! Heri enzi za mkapa yeye alitumia Mambo!..
Inabidi tujue Kwanz ni Mungu gani a naongelewa.

Maana Mungu wa wakristo sio wa waislam.

Na wa Islam sio wa wakristo.

WA wahindu ambao nao ni watz pia sio wa hao wawili juu.

Miungu ya makabila mengine tz yasioamini hao Miungu ya kuja pia sio ya hao wa juu.

So kwanini tuchanganye hii Miungu wakati haifanani hata chembe.

Ndo maana mwingine kazi kwa hatujaonyeshwa sababu nae alikuwa na Miungu yake ambayo inakataza Yeye kuwa live alishushwa chini.
 
Anachotaka kutuamininisha hapa ni kwamba masuala ya Mungu yakae pembeni na hii alianza tangu JPM akiwa mahututi na ndiyo maana hakusema tumwombee. Kiongozi wa nchi anapojaribu kuonyesha kuwa Mungu siyo muhimu siyo tu ushamba na ulimbukeni bali pia kukaribisha maafa ndani ya nchi. Atueleze ni akili ya namna gani aliyotumia kinyume na marais waliopita na kuamua kuwa kwenye taifa hili Mungu asitajwe kabisa?. Hili halikubaliki maani ni kuonyesha kuwa hii ni nchi ya wapagani.
kichwa kibovu
 
Back
Top Bottom