Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga




286_muganyizi.jpg



  • Orodha ya watuhumiwa ndefu, msako wa polisi
  • waendelea

WINGU limeendelea kutanda kuhusu mkanda wa video wenye picha ya Mkurugenzi wa Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni Mbunge wa zamani wa Bukoba Mjini, kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Wilfred Lwakatare.

Wingu la sasa linahusisha taarifa za uhakika ambazo gazeti hili limezipata zinaendelea ya kuwa operesheni ya kusaka watuhumiwa zaidi katika sakata hilo imeshika kasi, ikiwa ni matokeo ya mahojiano yaliyoendeshwa kati ya maofisa wa polisi na Lwakatare, pamoja na mwenzake, Ludovick Rwezaura.

Swali kubwa sasa ni je, nani wengine wataingizwa katika orodha ya watuhumiwa wa vitendo dhidi ya baadhi ya watu, akiwamo Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda, aliyetekwa, kupigwa na kujeruhiwa vibaya kiasi cha kupoteza jicho lake moja.

Wingu hilo linazidi kutanda katika wakati ambao Lwakatare amefikishwa mahakamani akishitakiwa kwa makosa manne, likiwamo la kula njama ya kutenda kosa la jinai la kutoa sumu kwa nia ya kumdhuru Dennis Msacky, ambaye ni Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, njama ambazo wanadaiwa kuzipanga eneo la King’ong’o, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Shitaka jingine la pili linalomkabili Lwakatare na mwenzake, Ludovick Rwezaura ni kula njama ya kufanya kosa la jinai kinyume cha kifungu cha 24 cha Sheria dhidi ya Ugaidi. Na tatu ni kufanya mkutano wa vitendo vya kigaidi, kinyume cha kifungu cha 5 (a) cha sheria namba 21 inayopinga ugaidi, wakati shitaka la nne dhidi yao ni kudaiwa kuhamasisha vitendo vya ugaidi.

“Baada ya mahojiano na Lwakatare kuna masuala ya msingi ambayo ni kama yameelekeza polisi kuendelea na msako wa baadhi ya watuhumiwa katika matukio haya ya utekaji na utesaji.
Unaweza kushangazwa na majina makubwa ya watu wengine wanaoweza kunaswa,” anaeleza mmoja wa maofisa wa polisi aliyezungumza na mwandishi wetu kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, inadaiwa ya kwamba, baada ya mahojiano na Lwakatare ndipo polisi walipobaini umuhimu wa kumsaka Ludovick Rwezaura na kwamba, wapo watuhumiwa wengine watatu wanasakwa na polisi katika mazingira ya usiri mkubwa.

Hata hivyo, pamoja na kuwapo kwa taarifa hizo kutoka ndani ya Jeshi la Polisi bado haijawekwa wazi kama wengine watakaokamatwa watafunguliwa mashitaka au watatumika kama mashahidi wakati wa usikilizaji wa kesi hiyo dhidi ya Lwakatare na mwenzake, Ludovick.

Taarifa zilizovuja siku moja kabla ya Lwakatare kufikishwa mahakamani zinadai ya kwamba, yapo baadhi ya mambo ambayo Lwakatare aliyakana na kutoyatambua ambayo yamejionyesha katika picha ya video iliyopachikwa kwenye mtandao wa jamii forum, wiki iliyopita lakini pia, kwa upande mwingine, inadaiwa kuna ambayo yaliyomo kwenye video

hiyo kuwa alikiri kuyatambua. Gazeti hili linashindwa kufichua yapi aliyakana Lwakatare na yapi aliyatambua kutokana na suala hilo kufikishwa mahakamani tayari.

Lwakatare alifikishwa mahakamani Jumatatu wiki hii na kunyimwa dhamana na hadi jana Jumanne tunakwenda mitamboni, bado dhamana ilikuwa haijapatikana, huku mawakili wa pande zote wakiendelea kupambana kisheria ili ama apate dhamana hiyo au anyimwe.

Katika kesi hiyo, upande wa mashitaka unaongozwa na Wakili wa Serikali, Prudence Rweyongeza na upande wa utetezi unawahusisha mawakili, Peter Kibatala, Tundu Lissu, Profesa Abdalah Safari na Nyaronyo Kicheere
.
http://www.raiamwema.co.tz/lwakatare-utata











Kweli wapo wajinga watakaoshangazwa na majina kama Mbowe na Slaa kuhusishwa kushiriki katika mikakati hii ya kigaidi lakini wenye akili zetu hatutashangaa!..Si walisema wenyewe kwamba watahakikisha nchi hii haitatawalika?...kumbe walilenga kuigombanisha Serikali na wananchi kwa kuua watu wasio na hatia ili kujenga chuki baina ya Serikali na watu wake!... laana inawatafuna sasa!
 
Kwaheri CCM ....haya yanayoendelea ni kutapatapa tuu. Kizuri zaidi wananchi wameshawaelewa! Kwaheri CCM!
 
Nataka Mwigulu, Membe na wengine waingizwe kwenye hili sakata. Wasipowaingiza hao na wengine, kesi hii ni upuuzi mwingine na dhulma dhidi ya upinzani.


Acha pupa subiri hii yenye vithibitisho vya wazi ikamilike kwanza ili jamii hasa waandishi, viongozi wa dini na madaktari watambue nani mbaya wao!
 
Kesi yenyewe kama magumashi vile,ya kuchongwa chongwa au ya kuungaunga. Hao wengine basi wakamatwe mapema.

Kina Lwakatare wameshaanza kutaja wahusika wenzao wanaoshiriki katika matukio ya kigaidi wewe unasema kesi ya kuungaunga? wee kweli hopeless!
 
Acha pupa subiri hii yenye vithibitisho vya wazi ikamilike kwanza ili jamii hasa waandishi, viongozi wa dini na madaktari watambue nani mbaya wao!

Mnakera sana na vielelezo vyenu vya kuchonga!

Lazima tupambane na utawala dharimu mbaka mwisho!
 
Mnakera sana na vielelezo vyenu vya kuchonga!

Lazima tupambane na utawala dharimu mbaka mwisho!

Lwakatare mwenyewe amekiri video yake na ameanza kuwataja wauaji wenzake, wewe hutaki kukubali!...ndio kusema unampenda sana Lwakatare kuliko unavyoupenda ukweli au?
 
Nataka Mwigulu, Membe na wengine waingizwe kwenye hili sakata. Wasipowaingiza hao na wengine, kesi hii ni upuuzi mwingine na dhulma dhidi ya upinzani.

Ikumbukwe katika moja ya mada yangu wiki iliyopita nilisema Rwekatare anaweza kukumbuka tukio ambalo alikuwepo na movie kuchuliwa. Hiyo movie ndiyo iliyotumika kuhariri uingizwaji wa editing ya sauti.

Mhusika mkuu hapa ni Ludovick ambaye anaonekana ni wa TISS alikuwa kazini. Baada ya tukio tukio la kuwa pamoja siku hiyo na Rwekatare Tundu Lissu anasema Ludovick aliwasiliana na Mwigulu Mchemba kwa simu. Siku mbili baada ya tukio hilo la Rwekatare na Ludovick kuwa pamoja Mwigulu Mchemba alijitokeza TV kutoa tamko kwamba anao ukanda wa movie unaoonyesha Chadema kupanga mikakati ya mauaji. Huyu ndiye mhusika mkuu aliyejivika ngozi ya kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu mkali.

Baada ya kushikwa Rwekatare Ludovick alikimbilia Iringa kwa kumwambia Mjengwa kwamba ana shughuli ya kufanya Iringa. Ameitwa baada ya Rwekatare kumtaja kwamba siku hiyo walikuwa pamoja.

Unaona mtu huyu Ludovick alijipenyeza hadi kwa Mjengwa blog eti alifanya kwa kujitolea kumbe alikuwa kazini.

Kuna uwezekano anayosema Mwampamba kuwa Ludovick alikuwa anafanya kazi makao makuu Chadema, possible alipenyezwa huko ili awe anachota habari za Chadema toka chunguni.

Hata hapa Jamii forums wapo tena baadhi ni moderators utaona kukiwa na mada ambazo zinahusu sana serikali na CCM baadhi zinaonekana kunyofolewa haraka au kuyumbishiwa jukwaa ambalo halichangiwi na watu wengi.

Siri moja ya kuwajua hawa wa TISS utaona wanalazimisha sana urafiki hata wako tayari kujitolea kwa kila njia na hapo utafikiri ni rafiki mzuri sana kumbe yupo kazini.
 
Kalaghabaho acha kujitekenya na kucheka.ngoma inogile na magamba wameshikwa pabaya.

hapa aliyeshikwa pabaya nani? Magamba au wale wanaojikanganya kukiri au kuikana video inayoonyesha mipango ya mauaji ya watanzania wasio na hatia? usiwe na pupa! Uchunguzi wa Gazeti lenu tukufu la Raia Mwema linasema kuna orodha ya washiriki wa matendo ya kigaidi itakayowasononesha sana!
 
Ikumbukwe katika moja ya mada yangu wiki iliyopita nilisema Rwekatare anaweza kukumbuka tukio ambalo alikuwepo na movie kuchuliwa. Hiyo movie ndiyo iliyotumika kuhariri uingizwaji wa editing ya sauti.

Mhusika mkuu hapa ni Ludovick ambaye anaonekana ni wa TISS alikuwa kazini. Baada ya tukio tukio la kuwa pamoja siku hiyo na Rwekatare Tundu Lissu anasema Ludovick aliwasiliana na Mwigulu Mchemba kwa simu. Siku mbili baada ya tukio hilo la Rwekatare na Ludovick kuwa pamoja Mwigulu Mchemba alijitokeza TV kutoa tamko kwamba anao ukanda wa movie unaoonyesha Chadema kupanga mikakati ya mauaji. Huyu ndiye mhusika mkuu aliyejivika ngozi ya kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu mkali.

Baada ya kushikwa Rwekatare Ludovick alikimbilia Iringa kwa kumwambia Mjengwa kwamba ana shughuli ya kufanya Iringa. Ameitwa baada ya Rwekatare kumtaja kwamba siku hiyo walikuwa pamoja.

Unaona mtu huyu Ludovick alijipenyeza hadi kwa Mjengwa blog eti alifanya kwa kujitolea kumbe alikuwa kazini.

Kuna uwezekano anayosema Mwampamba kuwa Ludovick alikuwa anafanya kazi makao makuu Chadema, possible alipenyezwa huko ili awe anachota habari za Chadema toka chunguni.

Hata hapa Jamii forums wapo tena baadhi ni moderators utaona kukiwa na mada ambazo zinahusu sana serikali na CCM baadhi zinaonekana kunyofolewa haraka au kuyumbishiwa jukwaa ambalo halichangiwi na watu wengi.

Siri moja ya kuwajua hawa wa TISS utaona wanalazimisha sana urafiki hata wako tayari kujitolea kwa kila njia na hapo utafikiri ni rafiki mzuri sana kumbe yupo kazini.

kwani si Dr slaa alisema nusu ya usalama wa Taifa wanaripoti kwake? leo hii wamekuwa maadui?...na bado kuna mengi sana yakakuja yatakayowaacha midomo wazi!
 
UGAIDI_Rwakatare.jpg

Rwekatare kitabasabu baada ya kuwa chini ya ulinzi


Ikumbukwe katika moja ya mada yangu wiki iliyopita nilisema Rwekatare anaweza kukumbuka tukio ambalo alikuwepo na movie kuchuliwa. Hiyo movie ndiyo iliyotumika kuhariri uingizwaji wa editing ya sauti.

Mhusika mkuu hapa ni Ludovick ambaye anaonekana ni wa TISS alikuwa kazini. Baada ya tukio la kuwa pamoja siku hiyo na Rwekatare Desemba tarehe 28, Tundu Lissu anasema Ludovick aliwasiliana na Mwigulu Mchemba kwa simu. Siku mbili baada ya tukio hilo la Rwekatare na Ludovick kuwa pamoja Mwigulu Mchemba alijitokeza TV kutoa tamko kwamba anao ukanda wa movie unaoonyesha Chadema kupanga mikakati ya mauaji. Huyu ndiye mhusika mkuu aliyejivika ngozi ya kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu mkali.

Movie hiyo haijawekwa hadharani licha ya kuambiwa aionyeshe tangu Desember 28 mwakajana Mwigulu alipotoa tamko hilo, maana yake muda wote huu alikuwa anaifanyia editing. Nikawaida ya tabia ya hawa watu kuwa marafiki wakaribu sana ili kujifunza mengi ikiwa tabia, sauti, miondoko na mengineyo wanayokusidia kufanya kwa mtu yule wakiwa na mtu mmoja wa karibu sana ili kutengeneza image wanayokusudia. Pengine hulazimisha urafiki hata uonyeshe hali ya kutomtaka anakuwa mvumilivu na kufanya kila awezacho hata kujitolea ili mradi awe karibu nawe.


Baada ya kushikwa Rwekatare Ludovick alikimbilia Iringa kwa kumwambia Mjengwa kwamba ana shughuli ya kufanya Iringa. Ameitwa baada ya Rwekatare kumtaja kwamba siku hiyo walikuwa pamoja.

Unaona mtu huyu Ludovick alijipenyeza hadi kwa Mjengwa blog eti alifanya kwa kujitolea kumbe alikuwa kazini.

Kuna uwezekano anayosema Mwampamba kuwa Ludovick alikuwa anafanya kazi makao makuu Chadema, possible alipenyezwa huko ili awe anachota habari za Chadema toka chunguni.

Hata hapa Jamii forums wapo tena baadhi ni moderators utaona kukiwa na mada ambazo zinahusu sana serikali na CCM baadhi zinaonekana kunyofolewa haraka au kuyumbishiwa jukwaa ambalo halichangiwi na watu wengi.

Siri moja ya kuwajua hawa utaona wanalazimisha sana urafiki hata wako tayari kujitolea kwa kila njia na hapo utafikiri ni rafiki mzuri sana kumbe yupo kazini.
 
Mkuu Pasco,naomba leo tutofautiane kidogo.hakuna mamlaka isiyohojiwa ktk dunia hii labda ya Mungu tu.sheria zipo ili zilinde haki za watu.kama DPP hawezi kuhojiwa mamlaka,then hiyo sheria inayompa mamlaka hayo hata kama ni katiba ya nchi is against human rights.lazima tuihoji hata hiyo sheria na sheria is subject to change(na ni muhimu sana kwa sheria kuwa subject to change).Pili,ni hatari kwa Chadema kumkana Lwakatare wakati uhusika wake is still a legal and technical debate !kumkana lwakatare itakuwa ni ku-justify uhusika wake,kitu ambacho hakijawa proven na chenye madhara kwao kisiasa.Tatu,suala la hii case kuwa legal ni la sasa,lakini baadae kwa kadri proceedings zinavyokwenda,ni lazima iwe political case,na kuna kila harufu ya kuwa political case.Lwakatare ni political figure kupitia Chadema na jamii inamtazama hivyo.naamini wanasheria wa Chadema wana uwezo wa kutosha kuhandle case hii kisheria na kisiasa bila kuathiri defence yao na wakifanya hivyo watakuwa wamemmaliza adui yao.tuwe wazi tu,hii case imelenga kumchafua lwakatare na Chadema kisiasa na kijamii,kwa vile kidhibiti kikuu cha mashtaka ambacho ni ile video,kuna maneno mle yanayojenga picha hiyo!let them hit the main target.hamna haja ya kuzunguuka.!you know always WHAT GOES AROUND.....!
Mkuu Juve, kwanza asante kwa maoni yako, hili la mamlaka ya DPP, mimi nimeisha lizungumza sana humu jf, mfano hapa katika uzi huu wa Andrew Nyerere, Topic: Omega Ngole,Never Say Never - Jamii Forums
Mkuu Andrew, kumbe huyajui mamlaka ya DPP!, hafanyi kazi kwa shinikizo la yoyote, akisema fulani hana kesi, hana kesi na sio hana kosa!. Kagoda imekwapua bilioni 40 kwa ajili ya kugharimia uchaguzi wa Chama chako CCM!, DPP ameangalia watu wa kuwakamata angeanzia kwa aliyekuwepo, aliyepo, MOF, Director wa TISS na hao players wa RA, akaona sii busara kuwakamata, akaamua wasikamatwe na Kagoda haina kosa. Maamuzi ya DPP ni final na hayahojiwi na mamlaka yoyote!.
Kwa kukusaidia tuu, pia DPP anayo mamlaka yanaitwa Nolle ambayo ana uwezo wa kuingilia kesi yoyote ya jinai ikiwa katika hatua yoyote kabla ya hukumu na kuiondoa mahakamani pasi kutoa sababu wala kuhojiwa na yoyote!.

Kwa maoni yangu, uamuzi wa DPP kutoishitaki Kagoda, ni uamuzi wa busara sana unaozingatia maslahi ya taifa kama alivyofanya kwa kutoichunguza Meremeta na Deep Green etc, kwa maslahi ya Taifa!.

Wewe hili ulilijua?. Na baada ya kukutajia wahusika wakuu wa Kagoda, bado ungependwa wachunguzwe?.

Pasco.


Mwaka 2009 katika uzi wa Mkuu BAK, DPP wetu kizuizi katika mapambano dhidi ya ufisadi - pia nilizungumzia mamlaka ya DPP,
Sio tuu mimi na wewe hatuwezi kumbana DPP, bali hakuna yoyote mwenye uwezo wa kumbana, hata rais hawezi!.
Mzee MMKJJ, yote uliyosema kuhusu DPP ni kweli, lakini pia kwa mujibu ya sheria iliyounda ofisi ya DPP, havunji sheria yoyote kwa kutofanya uchunguzi wowote kwa vile hayo ndio mamlaka yake ambayo kisheria, anayatumia at his discretion as he pleases at his pleasure na sheria inamlinda.
Kwa maoni yangu, tatizo sio DPP, tatizo ni mamlaka ya ajabu yaliyochini ya DPP.
Niliwahi kuchangia mahali nikaainisha sheria yetu iliyounda ofisi ya DPP, amepewa mamlaka makubwa yac ajabu, na hayo aliyoyaainisha MMKJJ ni dibaji tuu, nguvu haswa za DPP ni pamoja na 'power to declare nolle proseque' yaani hakuna kesi ya kujibu. DPP huyu anauwezo wa kuingilia kesi yoyote ya jinai, ikiwa mahakama yoyote na ikiwa katika hatua yoyote kabla ya hukumu, kuisimamisha, kingilia, ama kuifuta bila kulazimika kutoa sababu zozote wala maelezo yoyote.
Sheria ya DPP inamtaka kutimiza wajibu wake bila shinikizo lolote kutoka popote na hata akiletewa kesi yoyote ni discretion yake aprosecute ama asiprosecute na hakuna chombo chochote ndani ya JMT chenye mamlaka ya kumuuliza lolote DPP, hata rais hana mamlaka hayo, sembuse MMKJJ?.

Naungana na WoS sisi mwisho wetu ni kupiga tuu kelele, japo za mlango, siku moja moja mwenye nyumba atakosa usingizi kwa sababu nyingine na atazisikia hizi kelele za mlango na ama ataamka na kuubana mlango, ama atautia kizuizi ili usiendelee kupiga kelele.

Enzi za Mwalimu kulikuwa na sheria ya 'Presidential Preventive Detention Orders' iliyompa rais mamlaka ya kumuweka mtu yoyote kizuizini kwa kipindi chochote bila kutoa sababu yoyote. Mwalimu Nyerere aliitumia kipindi chote cha utawala wake. Kipindi cha Mwinyi, wanasheria wa chuo kikuu wakiongozwa na Shivji na Mgongo Fimbo, waliichalenge sheria hii kwa 'court review' na mahakama ikatamka its a bad law, hivyo ikamlazimisha rais, kila akisaini 'preventive detention order' lazima atoe sababu. kuna detention moja ya Mwinyi ilipigwa chini na mtuhumiwa kuachiwa huru.

Kama wanasheria wetu, waliweza kufanya hivi dhidi ya mamlaka ya rais, wanashindwa nini kwenye mamlaka ya DPP?.
Kwa mawazo yangu, 'Tatizo sio Feleshi as DPP, ni mamlaka yake makubwa mno anayatumia atakavyo bila kuvunja sheria. Tazizo ni the institutional of the DPP.
Hivyo kwenye hili la Chadema kuhoji mamlaka ya DPP sina cha kuongeza zaidi ya haya ambayo nilikwisha kuyasema nyuma.
Pasco

 
kwani si Dr slaa alisema nusu ya usalama wa Taifa wanaripoti kwake? leo hii wamekuwa maadui?...na bado kuna mengi sana yakakuja yatakayowaacha midomo wazi!

Kwa taarifa yako hawa TISS ni kama walivyo CIA hawako kwa masilahi ya taifa au serikali au chama fulani. Wapo kwa shughuli zao binafsi na huko serikalini wameshinikiza na kujishikiza ili kulazimisha serikali ziwape mafao wanayotaka. Ndio maana Taifa la Marekani iliamua kuanzisha taasisi nyingine ya uchunguzi ya FBI. Kama CIA wangefanya kazi kwa weledi kulikuwa na haja gani ya kuwa na Taasisi nyingine ya uchunguzi?

Tanzania licha ya kuwa na TISS mambo ya rushwa hayakwisha na kuendelea kushamiri ndipo serikali ilipolazimika kuanzisha idara nyingine ya uchungu ya TAKUKURU, kama TISS wangekuwa wanafanya kazi yao kwa weledi na kutoa ushirikiano kwa serikali sioni kama kungekuwa na sababu ya kuwa na TAKUKURI.

Hawa TISS wanatumiko kote kote mradi kuna masilahi, wamegawanyika na kila kukiwa na donge zuri wanakugeuka kisiri huku wakionekana kufanya kazi nawe. Inabidi kuwa na uangalifu katika sharing ya habari.

Ludovick mhusika mkuu kuchukua movie ya Rwekatare
 
Taarifa zilizovuja siku moja kabla ya Lwakatare kufikishwa mahakamani zinadai ya kwamba, yapo baadhi ya mambo ambayo Lwakatare aliyakana na kutoyatambua ambayo yamejionyesha katika picha ya video iliyopachikwa kwenye mtandao wa jamii forum, wiki iliyopita lakini pia, kwa upande mwingine, inadaiwa kuna ambayo yaliyomo kwenye video

hiyo kuwa alikiri kuyatambua
. Gazeti hili linashindwa kufichua yapi aliyakana Lwakatare na yapi aliyatambua kutokana na suala hilo kufikishwa mahakamani tayari.

Hapo ndio najiuliza na kutaka kupata ukweli kumbe hata madai kuwa ni video fake yanaweza yasiwe na mashiko tena !!
 
SAKATA la Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare, kufunguliwa kesi ya ugadi akidaiwa kupanga mikakati ya kudhuru watu, limechukua sura mpya baada ya chama hicho kudai kunasa mawasiliano ya watu kinaowatuhumu kuandaa video hiyo.
Pia CHADEMA imesema kuwa mawakili wake wamepeleka hati ya dharura katika Mahakama Kuu wakiiomba iingilie kati kwa kuitisha mafaili yote mawili ya kesi hiyo inayomkabili Lwakatare na mwenzake Ludovick Joseph.
Lwakatare alikamatwa Machi 13 mwaka huu na kuhojiwa kwa siku nne kisha kufikishwa mahakamani Machi 18 na kufunguliwa kesi namba 37/2013 yenye mashtaka manne huku Ludovick akisomewa mashtaka matatu.
Akizungunza na waandishi wa habari jana makao makuu ya CHADEMA, mwanasheria wa chama hicho, Tundu Lissu, alidai kuwa wamenasa mawasiliano ya watu mbalimbali wanaowahisi kuhusika kurekodi video hiyo.
Lissu aliwataja watu hao kuwa ni Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mwananchi, Dennis Msacky, Ludovick na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Mwigullu Nchemba.
Alifafanua kuwa Desemba 27 siku moja kabla ya video hiyo haijarekodiwa kulikuwa na mawasilano ya simu kutoka kwa Msacky kwenda kwa Lwakatare akimuulizia sehemu alipo.
Alisema katika mawasiliano hayo, Msacky anayetajwa kudhuriwa na mkakati huo alimpigia simu Lwakatare na kumuulizia mahali alipo ambapo alijibiwa kuwa alikuwa yuko njiani kurejea Dar es Salaam.
Lissu ambaye pia ni mmoja wa jopo la mawakili wanaomtete Lwakatare, aliongeza kuwa Desemba 28, Ludovick alifika nyumbani kwa Lwakatare siku ambayo video hiyo ilirekodiwa saa 11:59.
Aliongeza kuwa kulikuwa na mawasiliano baina ya Ludovick na Nchemba kwa kutumia namba za simu ya Nchemba inayoonekana katika kitabu cha Bunge.
Lissu alidai kuwa baada ya mawasiliano hayo kati ya Desemba 29 mwaka jana na Januari 2 mwaka huu, Nchemba alinukuriwa katika kituo cha televisheni akisema anayo video inayowaonyesha viongozi wa CHADEMA wakipanga njama za mauaji.
"Tumegundua mengi katika haya na kama tutafika mahakamani jaji au hakimu atakayekuwa anasikiliza tukiwa na hoja zetu atamaliza kesi hii ndani ya saa zisizozidi tatu," aliongeza Lissu.
Alipotafutwa Msacky kwa simu yake ya kiganjani ili afafanue madai hayo, alikataa akidai kuwa kesi iko mahakamani.
Kuhusu kupeleka hati ya dharura kuiomba mahakama iitishe mafaili yote mawili na kutengua uamuzi wa Mkurugenzi wa Mashtaka wa kumfutia Lwakatare mashtaka uliotolewa juzi, Lissu alisema wanatambua mamlaka ya kiongozi huyo katika kufungua na kuiondoa kesi mahakamani.
Alisema lengo ni kulinda maslahi ya taifa au kuboresha utendaji wa haki, suala alilodai halikufanyika katika dhamira nzima ya kufuta kesi ya kwanza ya Lwakatare.
"Tumekaa jopo la mawakili watano; tumeiomba mahakama kuu iingilie kati na kuitisha mafaili yote mawili ya kesi hii na kisha ijiridhishe kama sababu ya kufutwa kwa kesi ya kwanza ni kwa ajili ya maslahi ya taifa," alisema.
Alisema maombi mengine katika hati hiyo ni pamoja na kuiomba mahakama ichunguze ili kuona kama haki imetendeka kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, pia wameiomba ifute hati ya kufutiwa mashtaka kwa Lwakatare na ifute amri ya kumaliza kesi hiyo.
Pia alieleza kuwa wameiomba mahakama kuu iiamuru mahakama ya hakimu mkazi kisutu kuendelea na kesi ya awali iliyofunguliwa Machi 18 mwaka huu na pia itamke kuwa kilichofanywa na mawakili wa serikali ni kuingilia uhuru wa mahakama wa kufanya uamuzi.
Aliongeza katika kesi ya awali walihoji uwepo wa hati ya ridhaa ya DPP juu ya mteja wao kushtakiwa kwa sheria ya kupambana na ugaidi na wakaonyeshwa makaratasi yasiyokuwa na nembo yoyote ya taifa, hali iliyowafanya wahoji na kumuomba hakimu aifute kesi hiyo ombi lililokuwa linatarajiwa kutolewa uamuzi juzi.
Lissu alisema kuwa kwa mujibu wa sheria ya ugaidi ili kosa liwe la kigaidi lazima maelezo ya kosa hilo yaonyeshe kuwepo kwa malengo ya ugaidi hali aliyosema katika mashtaka yote mawili suala hilo halionekani


Baada ya matukio hayo, sasa naomba kuhitimisha kwamba,
1) Kwamba Chadema inapambana na Dola siyo ccm tena.
2) Kwamba kuna hujuma dhidi ya Chadema ni kitu kilicho wazi, siyo ishu ya mjadala tena.
3) Kwamba serikali inabagua wataznania kwa sababu juhudi zinazotumika kumlinda Msacky na kuwapata wauaji wa Barlow ingetumika pia kuwasaka kwa wahusika wa mateso na mauaji ya akina Mwangosi,Padre, Dr Ulimboka na Kibada. Na, Mwigulu Nchemba aliyedai kwamba ana video inayoonesha viongozi wa Chadema wakipanga mauaji siku chache baada ya video hiyo kurekodiwa ambayo kimazingira anaizungumizia video hii hii ya Lwakatare mbona hajahojiwa? R. Igondhu wa TISS Mbona hajahojiwa kuhusu Ulimboka pamoja na kutajwa na Ulimboka mwenyewe?. Kwa nini ya Lwakatare iwe ndo hoja nzito sana serikalini??. A million dolar questions!!


[TD="bgcolor: #ffffff"]
Soma habari yenyewe kwa ufipi hapa.

[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #ffffff"]
amka2.gif

[/TD]
 
Nataka Mwigulu, Membe na wengine waingizwe kwenye hili sakata. Wasipowaingiza hao na wengine, kesi hii ni upuuzi mwingine na dhulma dhidi ya upinzani.

Like kubwaaaaaaa sanaaaaa, pamoja na OSCAR NYERERE aliyeingiza sauti ya Kamanda lwakatale kwenye mkanda.
 
Mwigulu nae,iramba kuna umasikini wa kutupwa yeye yupo dar anatengeneza video!hivi huyu ana hata kibanda huko kwao kiteka sidhani
 
Back
Top Bottom