Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,209
Sina uhakika sana ina madhara gani kisheria kuongelea suala lililoko mahakamani kwenye public. Nilifikiri ni kosa kisheria kusema haya kwenye vyombo vya habari ilihali kesi ipo mahakamani.Mkuu Lukolo , Tatizo la watanzania ni wepesi kuamini maneno kutoka kwa wanasiasa bila kuyachuja.
Hebu chukua kiti na ufikirie, unataka kuamini kama Mh. Lissu angeitisha press conference na kusema Lwakatare ni GUILT?.
Wanasheria wa CHADEMA wamekuja kwenye public court kutafuta sympathy na kutaka kubadilisha mtazamo wa watu kuhusiana na hili swala.
Hatuwezi kuanza kujenga mitazamo kuhusiana na kesi kwa sababu hata hatujasikia upande wa pili wa marumbano kisheria.
Nia ya Mh. Lissu ni kutaka kuwavuta viongozi wa CCM ili kuifanya kesi iwe ya kisiasa ndiyo maana ameanza kuwachokonoa ili waanze kutoa matamko ya kisiasa.
Kama kesi atashinda, kulikuwa na umuhimu gani basi wa kuanza kuwahubiria waandishi wa habari?. He's just pre-empting the coming court ruling for political reason. Hata hivyo kwenye maelezo yake aliyotoa kuna mapungufu kibao.
Let's wait and see. Imesemwa, hakuna haja ya kuandikia mate na wino upo.
Ninachokiona hapa Ng'wamapalala, ni kwamba Lissu hajaweka wazi kama ile video inayomwonyesha Lwakatare ni fake au ni halisi isipokuwa alichezewa akili ili aseme yale aliyosema. Maana anakubali kwamba Ludovick alikwenda kwa Lwakatare. Then alifanya nini? Ikawaje? Mimi simtetei sana Lwakatare, japo naamini kwa kiasi kikubwa ile video ni mchezo tu wa CCM. Siwezi kabisa kuamini kwamba eti Lwakatare alikuwa anawakilisha mipango ya chama, hicho ni kitu kisichowezekana.
Lets wait and see, litaishaje hili.
Last edited by a moderator: