Sababu kuu zenye Mantiki zilizowafanya na zinazowafanya Wayahudi wengi Wasimuamini Yesu Kristo

Yesu mbona kauokomboa tayari ulimwemgu kwa wale watiifu kondoo wake ila wale wakaidi mbuzi hajakombolewa na majina yao hayapo katika kile kitabu..so pemgine mtoa mada na mimi ni muda wetu sasa wa kumfuatisha yesu na kuubeba msalaba wetu wenyewe km ambavyo yeye ameubeba msalaba wake .
 
Sema wayahudi/israel tuwape heshima yao Aisee...Ni kataifa kadogo sana na wala hakajawahi kutawala dunia, sanasana kenyewe ndiyo kalikuwa kanaonewa na kutawaliwa.
Lakini pamoja na hayo bado kamefanikiwa kutengeneza dini kuu 3 ambazo zinatawala dunia sasa (Uyahudi,Ukristo na Uislam)
Hivyo influence ya hako kataifa kadogo itadumu kuliko mataifa makubwa yaliyotawala dunia kama Ugiriki,Uyunani,Uajemi,Rumi,Uingereza,Ujerumani,USA nk. nk.
Uislamu umetengenezwa na roman catholic.
 
Nyuzi za hivi hata ujibiwe namna gani, ligi itaendelea tu.

Tuwaache wayahudi na dini yao ya kiyahudi.
Mkiri kristo rohoni mwako si lazima mpaka uone wayahudi wamemkubali na wewe ndio umkubali.
 
Hapo unazungumzia Silika na hulka ambavyo having uhusiano wowote na mambo ya Kujua au kutokuijua(Akili au utashi)
Unaposema kujua, kufahamu au kuelewa unazungumzia AKILI.

Kitu ku-operate ndani ya mwili wako haimaanishi unakijua au kukifahamu kitu hicho.
Kwa mfano unaweza kuwa unaumwa Malaria lakini usijue kuwa ugonjwa unaokusumbua ni Malaria.

Mwanadamu amezaliwa akiwa na Akili ambayo haijui Jambo lolote lile, liwe jema au Baya.

Hata Adamu aliumbwa akiwa hajui jema na Mabaya.
Mbona useme kuwa Mwanadamu anazaliwa anamjua Mungu?
Ilhali Watu huzaliwa wakiwa hawajui Jambo lolote lile
Labda nianze na swali hili...

Mtu anaye mjua Mungu anakuwa na vigezo gani, utajuaje kama namjua MUNGU?

Hata Adamu aliumbwa akiwa hajui jema na Mabaya.
Hili ndio lilikuwa lengo la MUNGU binadamu asijue jema au baya.
Maana yake adamu asingekula tunda kamwe asingeweza kutambua jema au baya, na wanae(ambao ni sisi) wangekuwa hawajui jema au ovu.

Kujua kwetu maovu na mabaya (sisi binadamu wa leo) ni sababu adamu ali asi.

Hapa nakufungua kua kujua jema au baya siyo utashi wako wala akili yako ya saivi... Bali mema au mabaya unayajua toka ukiwa tumboni kwa mama.

Vizazi vyote vya adamu baada ya kuasi vyote vinajua mema na mabaya haijalishi kina akili au hakina.
Vivyo hivyo na kumjua Mungu akili na utashi havitumiki bali utamjua tu haijalishi una akili au hauna.
 
Nyuzi za hivi hata ujibiwe namna gani, ligi itaendelea tu.

Tuwaache wayahudi na dini yao ya kiyahudi.
Mkiri kristo rohoni mwako si lazima mpaka uone wayahudi wamemkubali na wewe ndio umkubali.

Tunachoangalia ni hoja zao, Kwa nini wamkatae,
Kisha tunaangalia hoja zao zinamashiko au wameghafilika.
Hilo ndio lengo la Mjadala.

Huwezi kukubali au kukataa kitu pasipo kukijadili, kukichambua, na kuona ubora na madhaifu.

Je Wayahudi wanahoja?
Au je Wakristo wako na hoja?
 
Sema wayahudi/israel tuwape heshima yao Aisee...Ni kataifa kadogo sana na wala hakajawahi kutawala dunia, sanasana kenyewe ndiyo kalikuwa kanaonewa na kutawaliwa.
Lakini pamoja na hayo bado kamefanikiwa kutengeneza dini kuu 3 ambazo zinatawala dunia sasa (Uyahudi,Ukristo na Uislam)
Hivyo influence ya hako kataifa kadogo itadumu kuliko mataifa makubwa yaliyotawala dunia kama Ugiriki,Uyunani,Uajemi,Rumi,Uingereza,Ujerumani,USA nk. nk.
Acha hadithi za kusadikika jibu hoja.

Labda hao wayahudi wako kama walianzisha Ukristo na uyahudi lakini sisi waislam baba yetu wa imani ni nabii Ibrahim ambaye asili yake ni mkurudi kutoka Iraq na sio mayahidi.
 
Labda nianze na swali hili...

Mtu anaye mjua Mungu anakuwa na vigezo gani, utajuaje kama namjua MUNGU?


Hili ndio lilikuwa lengo la MUNGU binadamu asijue jema au baya.
Maana yake adamu asingekula tunda kamwe asingeweza kutambua jema au baya, na wanae wangekuwa hawajui jema au ovu.

Kujua kwetu maovu na mabaya (sisi binadamu wa leo) ni sababu adamu ali asi.

Hapa nakufungua kua kujua jema au baya siyo utashi wako wala akili yako ya saivi... Bali mema au mabaya unayajua toka ukiwa tumboni kwa mama.

Vizazi vyote vya adamu baada ya kuasi vyote vinajua mema na mabaya haijalishi kina akili au hakina.
Vivyo hivyo na kumjua Mungu akili na utashi havitumiki bali utamjua tu haijalishi una akili au hauna.

Sasa mbona unasema kujua Mema na Mabaya ndio unakuhusisha na kumjua Mungu?

Yaani ukiibiwa au ukichukuliwa MKE au Mume kunauhusiano gani na kumjua Mungu?
Ilhali mambo hayo yapo automatically kulingana na maumbile ya Mwanadamu.

Kitendo cha kusema tuu unamjua Mungu au MTU yeyote akisema hivyo tayari anaingia kwenye kundi la Watu waongo. Tena waongo Wakubwa.

Huwezi mjua MTU ambaye hujawahi kumuona, kumsikia Sauti yake, kumgusa wala usiye na namna ya kumuelezea. Huo ni Uongo.
 
Hapa kuna mpambano mkali unakuja kati ya wafia dini waisrael wa buza (wakristo) na wale waisrael original wa Israel (wayahudi) ambao inaonekana hawapo ila wanawakilishwa na mleta mada.

Ama hakika dini ni zaidi ya upofu kwa wale waliodandia treni kwa mbele. I mean walioletewa dini na wazungu pamoja na waarab
Duh! Huyu jamaa alitudiss Sana 🤔
 
Sio kweli.wapo Watu hawaamini na hawajui kuwa kuna MUNGU.
Yaani hata hiyo dhana tuu ya Mungu hawajawahi hata kuisikia. Watu wa hivyo wapo.

Watu wangekuwa wanamjua Mungu tangu wakiwa wadogo zisingekuwepo Dini
Kwahiyo uwepo dini ndio sababu ya kushawishi kuwa watu wanazaliwa hawamjui MUNGu... Sababu hiyo haina mashiko hata kidogo.

Dini ni mpango wa Binadamu kumtawala binadamu mwenzie, fikria dini ilifikaje Afrika.
Dini ni kwa ajili ya kunufaisha wachache wenye akili.

Leo watu wanajazana kwenda hija uarabuni, huoni jinsi gani watu wa uarabuni waliweka hija iwe kwao tu ili akili chache wapeleke hela zao kwa wananchi wa uarabuni?
Walijua wakiweka hija kwao kwanza wataongeza watalii kila mwaka na Mashirika yao ya ndege yatakuza biashara.

Kwahiyo lengo la dini ni kushikria akili yako ili utumike kwa ajili ya kuwanufaisha walio anzisha.
 
Kwahiyo uwepo dini ndio sababu ya kushawishi kuwa watu wanazaliwa hawamjui MUNGu... Sababu hiyo haina mashiko hata kidogo.

Dini ni mpango wa Binadamu kumtawala binadamu mwenzie, fikria dini ilifikaje Afrika.
Dini ni kwa ajili ya kunufaisha wachache wenye akili.

Leo watu wanajazana kwenda hija uarabuni, huoni jinsi gani watu wa uarabuni waliweka hija iwe kwao tu ili akili chache wapeleke hela zao kwa wananchi wa uarabuni?
Walijua wakiweka hija kwao kwanza wataongeza watalii kila mwaka na Mashirika yao ya ndege yatakuza biashara.

Kwahiyo lengo la dini ni kushikria akili yako ili utumike kwa ajili ya kuwanufaisha walio anzisha.

Naomba unipe maana ya msingi ya istilahi "DINI"
Achana na nadharia kuhusu Dini.
 
Acha hadithi za kusadikika jibu hoja.

Labda hao wayahudi wako kama walianzisha Ukristo na uyahudi lakini sisi waislam baba yetu wa imani ni nabii Ibrahim ambaye asili yake ni mkurudi kutoka Iraq na sio mayahidi.
Nabii Mussa je?Haruni? Nabii Suleman? Nabii Jona, Nabii Yusuf, Nabii Elisha, Nabii Eliah, Nabii Ezekiel, Nabii Yakobo(Israel mwenyewe), Mfalme Daudi, mfalme Sauli, Nabii Issa, Mariam na wengine wengi tu.
hawa ni wayahudi ndani ya Quran.

I mean Quran inataja wana waisrael mara nyingi kuliko hata inavyotaja waislam. Ni chizi tu atakayebisha influence ya uyahudi kwenye uislam.

Utaniambia Ibrahim ndio baba wa iman wa waislam lakini ukija uzao wa Ishmael hata haujulikani, ila uzao wa Isaka na yakobo unajulikana na umejaa kwenye Quran.
 
Nabii Mussa je?Haruni? Nabii Suleman? Nabii Jona, Nabii Yusuf, Nabii Elisha, Nabii Eliah, Nabii Ezekiel, Nabii Yakobo(Israel mwenyewe), Mfalme Daudi, mfalme Sauli, Nabii Issa, Mariam na wengine wengi tu.
hawa ni wayahudi ndani ya Quran.
I mean Quran inataja wana waisrael mara nyingi kuliko hata inavyotaja waislam.
Ni chizi tu atakayebisha influence ya uyahudi kwenye uislam.
Utaniambia Ibrahim ndio baba wa iman wa waislam lakini ukija uzao wa Ishmael hata haujulikani, ila uzao wa Isaka na yakobo unajulikana na umejaa kwenye Quran.

Mwambie Quran inawataja Wayahudi Kwa 90% kuliko huyo Ibrahim, Muhammad mwenyewe na jamii yoyote hapa Duniani.
 
Tunachoangalia ni hoja zao, Kwa nini wamkatae,
Kisha tunaangalia hoja zao zinamashiko au wameghafilika.
Hilo ndio lengo la Mjadala.

Huwezi kukubali au kukataa kitu pasipo kukijadili, kukichambua, na kuona ubora na madhaifu.

Je Wayahudi wanahoja?
Au je Wakristo wako na hoja?
Ndio wako sahihi kwa imani yao na jinsi wao walivyotafsiri maandiko.

Na ndio maana hata huu ukristo una madhehebi kibao kulingana na jinsi kila watu walivyoitafsiri biblia. Na kila mmoja yuko sahihi kwa kile anachoamini.

Labda useme tujadili kuhusu hicho wanachoamini na kwa nini wanaami ila kwenye usahihi, wako sahihi kulingana na mapokeo yao.
 
Anaandika, Robert Heriel
Kuhani.

Leo Taikon atajadili sababu zinazopelekea wayahudi wengi kutokumuamini Yesu Kristo Kama Masihi wao na waulimwengu.

Andiko hili lijadiliwe Kwa Hoja zisizo na mihemko ya kidini. Kama unajijua Akili yako imefungwa fungwa hii mada haitakuhusu.

Hivi uliwahi kujiuliza ni Kwa nini Wayahudi hawamuamini Yesu Kristo? Yaani Kwa nini wamuamini Musa, Daudi, yona, Daniel, Isaya, Ezra, Joshua, n.k lakini Kwa nini hawataki kumuamini Yesu Kristo?

Embu nawe Fikiria hapo. Kumbuka hata huyo Yesu naye NI Myahudi.

Je, ni Yesu pekeake aliyekataliwa na Wayahudi au kuna manabii Masihi wengine waliokataliwa n mayahudi?
Ikiwa wapo je nini sababu ya wao kukataliwa? Nisirefushe andiko.

Twende sasa!

Wayahudi wanasababu kadhaa za kutokumzingatia Yesu kama Masihi au Nabii aliyetabiriwa katika maandiko kaa sababu kuu zifuatazo;

1. Yesu Mnazareth Hakutimiza Unabii hivyo anakosa vigezo vya kuwa Masihi mtabiriwa.
Hapa kuna mambo ambayo Masihi aliyetabiriwa alipaswa kuyatimiza Siku atakapokuja. Mambo hayo ni pamoja na;

a). KUSHUSHA UTAWALA WA MUNGU NA KUKOMBOA WANADAMU
Masihi aliyetabiriwa moja ya majukumu yake akija ni kukomboa Wanadamu na kushusha utawala wa Mungu. Wayahudi hawamuamini Yesu Wa Nazareth Kwa sababu hakutimiza Jambo Hilo. Hakuushusha utawala wa Mungu na wala hakumkomboa Mwanadamu.

Hii ni Kwa sababu mpaka hapa tunapozungumza Bado Dunia haijakombolewa, madhambi ni mengi, na utawala wa Shetani ndio umetamalaki.

Soma utabiri wa Isaya juu ya Masihi atakayekuja kisha linganisha, je Yesu Mnazareth analingana na utabiri huo;

Isaya 9:6
6 . Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,
Tumepewa mtoto wa kiume;
Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake;
Naye ataitwa jina lake,
Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu,
Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.

Ukichambua Unabii huo sentensi Kwa sentensi, je Yesu Mnazareth anatimiza Unabii huo. Embu tuone, "Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake;"
Je Yesu alikuwa na uwezo wa kifalme began mwake? Je alitimiza vigezo vya kuitwa Mfalme? Labda Kwa vile hapa Tanzania kizazi cha sasa hakijaongozwa na wafalme. Lakini tunaweza kuchukulia mfano WA mamlaka ya Rais.

Je Yesu Mnazareth alikuwa anauwezo wa kirais, yaani mamlaka kama tuyaonayo Kwa Rais? Zingatia Mfalme ni zaidi ya Rais Kwa mambo mengi.

Ukisoma maandiko Yesu hakuwa na uwezo wowote wa Kifalme, alikuwa ni nabii kama walivyomanabii wengine.
Hivyo Sifa hii hakuwa nayo.
"Naye ataitwa jina lake,
Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu,
Baba wa Milele, Mfalme wa Amani
"

Je, Yesu Mnazareth alitimiza Unabii wa kuwa na Sifa ya kuitwa Mungu mwenye nguvu? Je Yesu alileta Amani? Maana Unabii unasema ataitwa Mfalme wa Amani.

Je ni kweli Yesu alileta Amani Duniani? Jibu ni Hapana, Yesu Mnazareth hakuleta Amani. Msikilize Yesu mwenyewe;

Mathayo 10:34 BHN​

“Msidhani kwamba nimekuja kuleta amani duniani. Sikuja kuleta amani bali upanga.​

Yesu hakuleta Amani Duniani isipokuwa Upanga. Hivyo anakosa kigezo cha Nabii aliyetabiriwa na manabii wa zamani.

Kwa tuliosoma Histori ya Ulimwengu. Ukristo ndio dini pekee iliyoua Watu wengi Duniani katika kuueneza.
Watu wengi wameuawa Kwa sababu ya Kristo au Kwa jina la Kristo. Hivyo hakuwa Mfalme wa Amani Bali alikuwa Mfalme wa machafuko.

Ukombozi uliolengwa na manabii waliotabiri Ujio wa Masihi ulikuwa ukombozi wa Kimwili. Lakini Yesu hakuja kukomboa yeyote Kimwili. Hiyo ni hoja inayofuata baadaye

b) MASIHI LAZIMA AZALIWE KATIKA UKOO WA DAUDI LAKINI YESU HAKUZALIWA KATIKA UKOO WA DAUDI.

Wayahudi wanamkataa Yesu Kwa sababu yupo Kinyume na Unabii wa Masihi aliyetabiriwa. Ndio maana wao wanamsubiri huyo Masihi Kwa jinsi vitabu vyao vinavyoeleza.

Maandiko yanaonyesha kuwa Yesu hakuwa Uzao wa DAUDI. Hii ni Kutokana na sababu zifuatazo;

I) Yesu alizaliwa pasipo na Baba.
Maandiko yanaeleza kuwa Yesu alizaliwa Kwa Njia ya Roho mtakatifu. Hana Baba wa kibinadamu. Jambo ambalo linampotezea Sifa ya kuwa Masihi aliyetabiriwa.

Wayahudi wanaeleza kuwa Masihi aliyetabiriwa angezaliwa kikawaida kama binadamu wengine tena angetoka katika Uzao WA Daudi. Yaani Baba yake lazima awe katika ukoo wa Daudi (Daudi mtoto wa Year).

Mwanzo 49:10 BHN​

“Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala miguuni pake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamtii.​

Soma Unabii wa Isaya;
ISAYA 11
1 Kutatokea chipukizi katika kisiki cha Yese,
tawi litachipua mizizini mwake.
2Roho ya Mwenyezi-Mungu itakaa kwake,
roho ya hekima na maarifa,
roho ya shauri jema na nguvu,
roho ya ujuzi na ya kumcha Mwenyezi-Mungu.
3Atafurahia kumcha Mwenyezi-Mungu.
Hatahukumu kadiri ya mambo ya njenje,
wala kuamua kufuatana na yale anayosikia.
4 Atawapatia haki watu maskini,
atawaamulia sawasawa wanyonge nchini.
Kwa neno lake ataiadhibu dunia,
kwa tamko lake atawaua waovu.
5 Haki itakuwa kama mkanda wa kujifunga,
uaminifu utakaa naye kama mkanda kiunoni.
6 Mbwamwitu ataishi pamoja na mwanakondoo,
chui watapumzika pamoja na mwanambuzi.
Ndama na wanasimba watakula pamoja,
na mtoto mdogo atawaongoza.
7Ngombe na dubu watakula pamoja,
ndama wao watapumzika pamoja;
na simba atakula majani kama ng'ombe.
8Mtoto mchanga atacheza kwenye shimo la nyoka
mtoto ataweza kutia mkono shimoni mwa nyoka wa sumu.
9 Katika mlima mtakatifu wa Mungu
hakutakuwa na madhara wala uharibifu.
Maana kumjua Mwenyezi-Mungu kutaenea pote nchini,
kama vile maji yajaavyo baharini.
10 Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa ishara kwa mataifa; mataifa yatamtafuta na makazi yake yatatukuka.
11Siku hiyo, Bwana ataunyosha mkono wake tena kuwarejesha watu wake waliosalia huko Ashuru, Misri, Pathrosi, Kushi, Elamu, Shinari, Hamathi na sehemu za pwani


Unabii huu unaeleza Sifa za Masihi atakayekuja, yaani sharti atokee Katika ukoo wa Daudi. Jambo ambalo Yesu Mnazareth maandiko yanaeleza kuwa hajatokea kwani hakuwa na Baba.

Hata Mariam mamaye Yesu angetokea ukoo wa Daudi bado isingemsaidia lolote Yesu kwani kiunabii au kimaandiko Uzao unatoka Kwa Baba.

Hoja hii inaungwa mkono na Wayahudi wengi na kufikia hitimisho kuwa Yesu sio Masihi aliyetabiriwa. Yesu hakuwa na Baba, huyo Yusufu ambaye ukoo wake umetajwa kwenye Biblia hakuwa Baba mzazi wa Yesu. Ndio maana alitaka kumkimbia Mariam.

Wayahudi wanadai kuwa Masihi angezaliwa kikawaida, Kwa kuwa Na Baba mzazi na Mama mzazi na sio kutumia njia ya miungu kutunga mimba. Jambo ambalo Wayahudi wanaliita ni dhana ya upagani wa Kirumi.

C) MASIHI LAZIMA AWARUDISHE WAYAHUDI WOTE WALIOTAWANYIKA DUNIANI WARUDI ISRAEL.
Yesu Mnazareth hakutimiza hilo. Wayahudi walichukuliwa uhamishoni huku na Huko. Na wapo wengine waliobakizwa Uyahudini.

Masihi aliyetabiriwa moja y majukumu yake ilikuwa kuwakusanya na kuwarejesha waisrael wote waliotawanyika warudi nyumbani Yesu hakufanya hilo. Hivyo anakosa Sifa za kinabii za Masihi aliyetabiriwa

ISAYA 11:
10 Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa ishara kwa mataifa; mataifa yatamtafuta na makazi yake yatatukuka.
11. Siku hiyo, Bwana ataunyosha mkono wake tena kuwarejesha watu wake waliosalia huko Ashuru, Misri, Pathrosi, Kushi, Elamu, Shinari, Hamathi na sehemu za pwani.


Yesu Mnazareth hakumrejesha hata myahudi mmoja Israel. Hivyo anakosa Sifa za kinabii za Masihi.

Wakristo wanadai Yesu Mnazareth atatimiza hayo kwenye Ujio wa Pili Wakati upande Kwa Wayahudi na vyanzo vya Kiyahudi vinaonyesha kuwa MASIHI atatimiza utume wake Moja Kwa Moja. Katika Biblia hasa ya Unabii wa Masihi aliyetabiriwa hakuna dhana "Masihi Kurudi/kuja Mara yapili.

d) MASIHI ATAKUJA KUKOMESHA MAGONJWA, VITA, TAABU, NJAA N.K
Masihi aliyetabiriwa na manabii moja ya Kazi yake akija atakomesha magonjwa, Vita, Taabu, njaa na majanga mengine. Lakini Yesu Mnazareth hakukomesha chochote Kati ya hivyo kwani mpaka hivi leo, Mambo hayo yapo.
Hivyo anakosa Sifa za Masihi aliyetabiriwa.

Hoja ya kusema kuwa Yesu Mnazareth alikuja Kwa mambo ya ufalme wa Kiroho inazidi kumuondoa Yesu kwenye Sifa za Masihi aliyetabiriwa.

Labda tuseme, Yule Aliyetabiriwa na Yesu Mnazareth kuwa atakuja ambaye Wakristo wanamuita Roho mtakatifu ndiye Masihi ambaye kwa HAKIKA bado hajaja.

E) Masihi hataleta mambo ya utatu mtakatifu ambayo Kwa Torati ni Shirki, ibada za Sanamu.
Masihi ataleta ufalme wa Mungu, Haki yake, na utawala wake. Ataleta Amani Duniani. Hatakuwa sehemu ya Mungu, Ila atakuwa ni sehemu ya Uzao wa DAUDI. Utatu mtakatifu pekee yake unamuondoa Yesu Mnazareth katika Sifa za Masihi aliyetabiriwa na vitabu vya Kale.

Hao ni Wayahudi wanavyomchukulia Myahudi mwenzao yaani Yesu Kristo.

Maswali ambayo tunatakiwa tujiulize;

1. Ikiwa Yesu alitoka mbinguni, Kwa nini hakuandaa makao ya Watu wake Kabla hajaja Duniani kuwakomboa?
Badala yake Akaja Duniani kwanza ndipo akaenda kuandaa Makao. Hii maana yake ni nini?

Mungu aliumba makazi, Dunia ndipo akaumba MTU. Nuhu alijenga Safina ndipo akawakomboa Watu wake. Iweje Yesu aanze na ukombozi kwanz alafu ndio akaandae Makao?

2. Je Yesu na Ukristo, Yesu kama mwenye uwezo na Nabii. Kabla hajaja hakuona hatari ya Ujio wake kuwa mamilioni ya Watu watauawa kisa jina lake.

Yaani watalazimishwa kukubali jina lake kilazima hata kama hawataki? Kwa maana mpaka sasa jina la Yesu ndio linashikilia nafasi ya Kwanza Kwa Watu kuuawa ili tuu Watu waupokee Ukristo au waukatae Ukristo.

3. Iweje Yesu Mnazareth alishindwa kutimiza kazi yake Kwa miaka 33 aliyokaa Duniani mpaka awape majukumu Wanafunzi wake?

Je, hakuona kuwa kuna upotoshaji ungeweza kujitokeza Wakati ambapo hatokuwepo?
Ikiwa alilisha Watu zaidi ya elfu tano Kwa mikate mifano na samaki Wawili, akafufua Watu, na miujiza mingine, kumaanisha alikuwa na uwezo.

Ni kipi alishindwa kuhakikisha kila binadamu anayezaliwa automatically, amjue Mungu na habari zake pasipo kufundishwa na yeyote, ili kuepusha kile kiitwacho uongo na habari zake kuingiziwa hadithi za Uongo. Huo ungekuwa muujiza mzuri na wala asingewapa Wanafunzi wake kazi ya Kutangaza habari zake na habari za Mungu.

4. Yesu aliwaagiza Wanafunzi wake kuhubiri Injili. Je hakujua kuwa Miaka na miaka itapita, Vizazi na Vizazi vitapita.

Je, Vizazi ambavyo havikuwepo Wakati wake(Wakati WA Yesu) Sisi tukiwa miongoni mwa Vizazi hivyo, tunapata mamlaka ipi na uthibitisho upi kuwa Injili tuliyonayo ndio Ile aliyoitoa Yesu? Je, tutatumia kipimo kipi kuthibitisha ukweli WA kile tukisemacho?

5. Ikiwa lengo la Kufa Kwa Kristo ni kuwakomboa wanadamu na kuifia dhambi. Je kama dhambi ilikomeshwa na Kifo cha Yesu, ni kwanini Watu wanaendelea kutenda dhambi?

6. Swali la mwisho, ni Jambo Gani linalopelekea Wakristo kuamini Yesu Mnazareth ndiye Kristo/Masihi ilhali hajatimiza robo tatu ya Masihi aliyetabiriwa na manabii?

Kwa mfano, swali alilouliza Yohana Mbatizaji kuwatuma Wanafunzi wake wakamuulize Yesu kuhusu, Je Ni yeye Masihi au wamsubiri mwingine na jibu la Yesu kuwa viwete wanapona, vipofu wanatembea, viziwi wanasikia, na wafu wanafufuliwa. Je hiyo ndio ilikuwa misheni kuu ya Yesu?

Vipi kuhusu kuwarejesha Wayahudi Israel, vipi kuhusu yeye kuwa Mfalme na kuleta Amani na Haki Duniani, vipi kuhusu kuadhibu na kuhukumu?

7. Je Yesu anapowaambia Wanafunzi wake kuwa atarudi tena, je anaongea hayo Kwa kutimiza Unabii upi wa Masihi?

Maana hakuna sehemu Huko Nyuma ambayo ilitabiriwa ataondoka kisha atarudi tena. Ikiwa ndiye aliyetabiriwa, hiyo dhana aliitolea wapi?

Karibuni kwenye mjadala.
Mihemko hapa haitakuwa sehemu yake.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Dini na fasihi ni vitu viwili tofauti. Kwa taarifa yako mitume wote 12 walikuwa wayahudi. Manabii walikuwa wanapewa dokezo la kimungu nao wanaliandika au kulihubiri kibinadamu.
 
Huu Uzi hauhusu kumjua MUNGU Mkuu!
Embu usome VIZURI.
Uzi unahusu Wayahudi, Yesu Mnazareth na Unabii wa Masihi.
Unajitekenya then unajicheka.

Ni kipi alishindwa kuhakikisha kila binadamu anayezaliwa automatically, amjue Mungu na habari zake pasipo kufundishwa na yeyote, ili kuepusha kile kiitwacho uongo na habari zake kuingiziwa hadithi za Uongo. Huo ungekuwa muujiza mzuri na wala asingewapa Wanafunzi wake kazi ya Kutangaza habari zake na habari za Mungu

Hoja zangu nililenga kupinga hapo...
Wala sishughuliki na wayahudi tatizo lao ni lingine "hawana imani.*
 
Back
Top Bottom