Rostam aibukia kanisani!

Rostam aibukia kanisani!

Rostam Aziz ahusishwa ufisadi mabilioni ya Japan

Ni za Mfuko wa Chakula
Zilizochotwa ni bilioni 200
Toleo Na. 090
Rostam Aziz ahusishwa ufisadi mabilioni ya Japan

Na Waandishi Wetu
Mwanahalisi

MBUNGE wa Igunga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rostam Aziz, ni miongoni mwa wafanyabiashara kadhaa wanaotajwa kufilisi Mfuko wa Chakula (FACF) baada ya kuchotewa na serikali zaidi ya Sh. 200 bilioni.

Taarifa za ukakika zilizothibitishwa na Serikali, zinasema Rostam alichotewa mabilioni hayo ya shilingi kupitia kampuni yake ya African Trade Development.

Mfuko huo unaoendeshwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Japan.

MwanaHALISI imeelezwa kwamba Rostam, pamoja na wafanyabiashara wenzake kadhaa wameshindwa kurejesha fedha hizo kama walivyotakiwa na serikali.

Kampuni ya Rostam ilichotewa zaidi ya Sh. 2.012 bilioni Novemba 1999, lakini hadi mwishoni mwa mwaka jana, fedha hizo hazikufanya kazi iliyokusudiwa.

Aliyekuwa Waziri wa Kilimo na Chakula katika serikali ya rais mstaafu Benjamin Mkapa, Charles Keenja, ameithibitishia gazeti hili kutolewa fedha hizo.

Alisema, “ni kweli wapo wafanyabiashara ambao walipewa fedha kutoka katika mifuko hiyo. Na hadi naondoka ofisini (mwaka 2005), nyingi ya fedha hizo zilikuwa hazirudishwa.”
 
Rostam: Nimeshtushwa

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
July 11, 2008

SIKU moja tu baada ya Dayosisi ya Mashariki na Pwani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) kutoa tamko dhidi yake, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM) ameeleza kushtushwa na kusikitishwa na tukio hilo.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa simu jana, Rostam ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisema alikuwa akitarajia kuitisha mkutano na waandishi wa habari wakati wowote kuanzia sasa, ambao atautumia kueleza msimamo wake kuhusu tamko hilo la KKKT.

‘‘Nimeshtushwa na tamko hilo. Ingawa nazungumza nikicheka, lakini kwa kweli nina masikitiko makubwa. Ninachoweza kukueleza kwa sasa ni kwamba, nimefikia uamuzi wa kuitisha mkutano na waandishi wa habari katika siku chache zijazo, na kueleza kile nilichonacho kuhusu tukio hili zima,” alisema Rostam.

Alipotakiwa kueleza iwapo bado alikuwa akiamini kwamba tamko hilo la KKKT lilitolewa kwa shinikizo lolote kama alivyogusia siku moja kabla ya tukio hilo, Rostam hakuwa tayari kueleza lolote, zaidi tu ya kusema kwamba atasema kila alichonacho katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Iwapo Rostam ataitisha mkutano na wanahabari, inaweza ikawa ni mara ya kwanza kwa mwanasiasa huyo kufanya hivyo tangu alipoingia katika siasa za wazi nje ya ubunge wake wa Igunga.

Ingawa Rostam hakuwa tayari kueleza nini alichokuwa akikusudia kusema, mmoja wa wanasiasa wa karibu naye, alilieleza Tanzania Daima kwamba, Rostam amepata kualikwa katika usharika wa Kinondoni siku zilizopita.

‘‘Ninachojua mimi ni kwamba haikuwa mara ya kwanza kwa Rostam kualikwa KKKT Kinondoni na kutoa mchango. Amepata kualikwa hapo mwaka 2005 au 2006 hivi kwa barua aliyopewa na mzee mmoja wa kanisa hilo, ambaye ni kiongozi wa juu kisiasa. Tafuteni hili mtalijua hilo,” alisema mwanasiasa huyo.

Taarifa kutoka katika usharika huo zinaonyesha kwamba, viongozi wawili wanasiasa ambao ni wazee wa kanisa katika kanisa hilo la Kinondoni, ni Mbunge wa Urambo Mashariki, Samuel Sitta na Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa, wote wa CCM.

Uamuzi huo wa Rostam kuahidi kuitisha mkutano na wanahabari, unakuja kutokana na tamko la KKKT lililotolewa juzi ambalo lilikana kutambua mwaliko na kauli zilizotolewa na mbunge huyo mwishoni mwa wiki katika usharika huo wa Kinondoni.

Tamko hilo la KKKT lililotolewa juzi baada ya kikao cha dharura cha Halmashauri Kuu ya Dayosisi hiyo, linaeleza kusikitishwa kwake na matamshi yaliyotolewa na Rostam wakati alipozungumza katika usharika huo Jumapili iliyopita.

Kwa mujibu wa tamko hilo lililosainiwa na Katibu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP), Balozi Richard Mariki, KKKT imekana kutambua usafi wa Rostam dhidi ya tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwake.

Kanisa hilo pia lilikanusha kuwa na taarifa zozote kuhusu uamuzi wa kwaya ya Amkeni kumwalika Rostam katika hafla yao ya uzinduzi wa mkanda wao.

“Tunasikitika ya kwamba kanisa halikuwa na taarifa ya ujio wa Rostam Aziz. Tunapenda kuwataarifu kwamba, taratibu za kuwaalika wageni kwenye shughuli kama hizi hazikufuatwa,” linasomeka tamko hilo la KKKT katika sehemu moja.

Tamko hilo la KKKT lilitolewa siku chache tu baada ya Rostam kualikwa na kuwa mgeni rasmi katika Usharika wa Kinondoni wa kanisa hilo Jumapili iliyopita na kutoa matamshi mazito kuhusu masuala yanayohusu maadili na hali ya siasa.

Katika matamshi yake hayo, Rostam alilishukuru kanisa kwa kumwalika, na akatumia fursa hiyo kueleza kuwa taifa lilikuwa likipita katika kipindi kigumu kisiasa na kijamii, na akawataka waumini waliombee ili kulirejesha katika mstari ulio sahihi.

Mbunge huyo ambaye katika siku za hivi karibuni jina lake limetajwa katika tuhuma za ufisadi, hususan katika sakata la Richmond, aliwashukuru waumini wa Kikristo kwa kutenda haki, na kwa kutomtuhumu na kumshutumu mtu sambamba na kuwapinga watu wenye wivu na chuki.

Rostam alisema ana watoto watatu ambao aliahidi kanisani hapo kwamba, anataka awalee katika misingi safi ili wawe wananchi bora na waadilifu hapo baadaye.

“Nawashukuru kwa kuamua kunialika kuwa mgeni rasmi leo. Hii ni ishara kwamba mmeamua kupuuza viji-maneno na upuuzi wa vijiweni. Nafurahi kuwa miongoni mwenu…hamtuhumu, hamshutumu, hampendi wenye wivu na wenye chuki, mnapenda haki. Ninao watoto watatu na nataka niwalee katika misingi hii,’’ alisema Rostam huku akishangiliwa na umati wa watu walioshiriki hafla hiyo.

Alisema hivi sasa nchini, watu wameanzisha tabia ya kuchukiana, hata kufikia hatua ya kuzushiana uchawi na kuombeana vifo, kauli ambayo baadhi ya watu waliiona kuwa ilikuwa ikimlenga Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambaye ni mmoja wa wazee wa kanisa wa usharika huo huo alioalikwa Rostam.

Kutokana na matamshi na mwaliko huo wa Rostam, KKKT katika tamko lake la juzi, lilieleza kwamba, uchunguzi wao uliwawezesha kugundua kuwa, mbunge huyo alialikwa kanisani hapo na kikundi ambacho hakikuwa na mamlaka ya kufanya hivyo.

“Kutokana na ukiukwaji taratibu hizi, hayo madai yaliyonukuliwa katika vyombo vya habari kwamba ujio wa Rostam katika Usharika wa Kinondoni na tafasiri ya ujio huo kuwa kanisa linatambua usafi wake, si sahihi, na ni madai potofu,” alisema Mariki katika taarifa yake.

Kanisa hilo katika tamko lake hilo linasema msimamo wao hauruhusu sharika zake kutumika kama majukwaa ya kisiasa kujisafisha au kuwasafisha watuhumiwa wa ufisadi.

“KKKT imekuwa mstari wa mbele katika kupinga na kukemea mambo ya ufisadi, na linaunga mkono juhudi zote za kutokomeza uovu...kanisa litachukua tahadhari kuhakikisha jambo kama hilo, halitatokea tena,” linasema tamko hilo.

Katika hatua kubwa zaidi, kanisa hilo limefikia hatua ya kuwaomba radhi waumini wake wote wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani ikiwa ni pamoja na kanisa zima la KKKT kutokana na tukio hilo.

“Dayosisi ya Mashariki na Pwani inapenda kuwaomba radhi waumini wake wote, kanisa zima la KKKT na wale wote wenye mapenzi mema kwa nchi yetu ambao kwa namna moja au nyingine wamekwazwa na tukio hili,” linasema tamko hilo.

Likiendelea, tamko hilo linaeleza kuwa, jukumu la kanisa ni kuokoa roho za watu na si kukumbatia mafisadi na walarushwa.

Pamoja na ukali wa maneno katika tamko hilo, KKKT haikueleza iwapo mchango wa shilingi milioni tano zilizotolewa na Rostam katika hafla hiyo zitarudishwa.
 
Au, alitaka kusema hiki kitu ni ridiculous, kinachekesha, akashindwa kujieleza. Kauli sio kitu muhimu Tanzania.

Watanzania tumemshtukia na wala asipoteze muda wake kuitisha mkutano kuzungumzia upupu wake aliozungumza pale kanisani. Kama anataka kuzungumza basi azungumze yale ambayo alizuiliwa na Sitta kuyazungumza Bungeni.
 
Rostam hilooo!usitutishie na vijisenti vyako!sisi maskini jeuri ipo siku utalitambua hili!
ulifikiri utafanikiwa kujisoap kupitia kanisa sasa umeula wa chuya!

First Lady RA hatishi mtu...Bali yeye ndiye ameshtushwa na kauli pamoja na maamuzi ya Usharika huo wa mashariki na Pwani chini ya Bwana Mariki.
Sasa hapa ni kama RA anawaambia wafikiri mara mbili kauli zao kwani na yeye kashtushwa na kasema ni jambo zito kidogo hili!
Kama maneno yake hapa chini..Nanukuu...
``Hilo ni jambo zito kidogo, ngoja nipate muda wa kutafakari,``alisema.

 
I wonder what will he say? Kuna mengi ya kumuuliza. Kuhusu chakula alichokula na Balali, Dowans, Caspian, EPA, Richmond, etc etc kama waandishi wakikomalia hiyo issue ndogo ya KKKT itakuwa kichekoesho. Let's wait and see.
 
Hapa umeongea ukweli ndugu yangu maana RA amekuwa akitupiwa lawama bila sababu za maana.
RA alialikwa hapo kanisani, hakujipeleka. Aliombwa msaada wa kuchangia hiyo kwaya na yeye kwa uzalendo na upendo aliokuwa nao aliamua kutoa sh mil 7.6, sasa kwanini leo alaumiwe kwa hilo?.
Na hata kama alikwenda kanisani mwenyewe kuna ubaya gani?, kanisa ni nyumba ya Mungu kila mtu anaweza kuingia humo. Yesu mbona alikuwa anaongea na watoza kodi pamoja na kula nao chakula pamoja?.
Jamani KKKT ni wanafiki na si vyema kumtupia lawama RA ambazo si zake.

Unatia kichefuchefu!!!!! Rostam na uzalendo wap na wapi???????
 
Rostam: Nimeshtushwa

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
July 11, 2008

SIKU moja tu baada ya Dayosisi ya Mashariki na Pwani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) kutoa tamko dhidi yake, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM) ameeleza kushtushwa na kusikitishwa na tukio hilo.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa simu jana, Rostam ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisema alikuwa akitarajia kuitisha mkutano na waandishi wa habari wakati wowote kuanzia sasa, ambao atautumia kueleza msimamo wake kuhusu tamko hilo la KKKT.

‘‘Nimeshtushwa na tamko hilo. Ingawa nazungumza nikicheka, lakini kwa kweli nina masikitiko makubwa. Ninachoweza kukueleza kwa sasa ni kwamba, nimefikia uamuzi wa kuitisha mkutano na waandishi wa habari katika siku chache zijazo, na kueleza kile nilichonacho kuhusu tukio hili zima,” alisema Rostam.

Alipotakiwa kueleza iwapo bado alikuwa akiamini kwamba tamko hilo la KKKT lilitolewa kwa shinikizo lolote kama alivyogusia siku moja kabla ya tukio hilo, Rostam hakuwa tayari kueleza lolote, zaidi tu ya kusema kwamba atasema kila alichonacho katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Iwapo Rostam ataitisha mkutano na wanahabari, inaweza ikawa ni mara ya kwanza kwa mwanasiasa huyo kufanya hivyo tangu alipoingia katika siasa za wazi nje ya ubunge wake wa Igunga.

Ingawa Rostam hakuwa tayari kueleza nini alichokuwa akikusudia kusema, mmoja wa wanasiasa wa karibu naye, alilieleza Tanzania Daima kwamba, Rostam amepata kualikwa katika usharika wa Kinondoni siku zilizopita.

‘‘Ninachojua mimi ni kwamba haikuwa mara ya kwanza kwa Rostam kualikwa KKKT Kinondoni na kutoa mchango. Amepata kualikwa hapo mwaka 2005 au 2006 hivi kwa barua aliyopewa na mzee mmoja wa kanisa hilo, ambaye ni kiongozi wa juu kisiasa. Tafuteni hili mtalijua hilo,” alisema mwanasiasa huyo.

Taarifa kutoka katika usharika huo zinaonyesha kwamba, viongozi wawili wanasiasa ambao ni wazee wa kanisa katika kanisa hilo la Kinondoni, ni Mbunge wa Urambo Mashariki, Samuel Sitta na Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa, wote wa CCM.

Uamuzi huo wa Rostam kuahidi kuitisha mkutano na wanahabari, unakuja kutokana na tamko la KKKT lililotolewa juzi ambalo lilikana kutambua mwaliko na kauli zilizotolewa na mbunge huyo mwishoni mwa wiki katika usharika huo wa Kinondoni.

Tamko hilo la KKKT lililotolewa juzi baada ya kikao cha dharura cha Halmashauri Kuu ya Dayosisi hiyo, linaeleza kusikitishwa kwake na matamshi yaliyotolewa na Rostam wakati alipozungumza katika usharika huo Jumapili iliyopita.

Kwa mujibu wa tamko hilo lililosainiwa na Katibu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP), Balozi Richard Mariki, KKKT imekana kutambua usafi wa Rostam dhidi ya tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwake.

Kanisa hilo pia lilikanusha kuwa na taarifa zozote kuhusu uamuzi wa kwaya ya Amkeni kumwalika Rostam katika hafla yao ya uzinduzi wa mkanda wao.

“Tunasikitika ya kwamba kanisa halikuwa na taarifa ya ujio wa Rostam Aziz. Tunapenda kuwataarifu kwamba, taratibu za kuwaalika wageni kwenye shughuli kama hizi hazikufuatwa,” linasomeka tamko hilo la KKKT katika sehemu moja.

Tamko hilo la KKKT lilitolewa siku chache tu baada ya Rostam kualikwa na kuwa mgeni rasmi katika Usharika wa Kinondoni wa kanisa hilo Jumapili iliyopita na kutoa matamshi mazito kuhusu masuala yanayohusu maadili na hali ya siasa.

Katika matamshi yake hayo, Rostam alilishukuru kanisa kwa kumwalika, na akatumia fursa hiyo kueleza kuwa taifa lilikuwa likipita katika kipindi kigumu kisiasa na kijamii, na akawataka waumini waliombee ili kulirejesha katika mstari ulio sahihi.

Mbunge huyo ambaye katika siku za hivi karibuni jina lake limetajwa katika tuhuma za ufisadi, hususan katika sakata la Richmond, aliwashukuru waumini wa Kikristo kwa kutenda haki, na kwa kutomtuhumu na kumshutumu mtu sambamba na kuwapinga watu wenye wivu na chuki.

Rostam alisema ana watoto watatu ambao aliahidi kanisani hapo kwamba, anataka awalee katika misingi safi ili wawe wananchi bora na waadilifu hapo baadaye.

“Nawashukuru kwa kuamua kunialika kuwa mgeni rasmi leo. Hii ni ishara kwamba mmeamua kupuuza viji-maneno na upuuzi wa vijiweni. Nafurahi kuwa miongoni mwenu…hamtuhumu, hamshutumu, hampendi wenye wivu na wenye chuki, mnapenda haki. Ninao watoto watatu na nataka niwalee katika misingi hii,’’ alisema Rostam huku akishangiliwa na umati wa watu walioshiriki hafla hiyo.

Alisema hivi sasa nchini, watu wameanzisha tabia ya kuchukiana, hata kufikia hatua ya kuzushiana uchawi na kuombeana vifo, kauli ambayo baadhi ya watu waliiona kuwa ilikuwa ikimlenga Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambaye ni mmoja wa wazee wa kanisa wa usharika huo huo alioalikwa Rostam.

Kutokana na matamshi na mwaliko huo wa Rostam, KKKT katika tamko lake la juzi, lilieleza kwamba, uchunguzi wao uliwawezesha kugundua kuwa, mbunge huyo alialikwa kanisani hapo na kikundi ambacho hakikuwa na mamlaka ya kufanya hivyo.

“Kutokana na ukiukwaji taratibu hizi, hayo madai yaliyonukuliwa katika vyombo vya habari kwamba ujio wa Rostam katika Usharika wa Kinondoni na tafasiri ya ujio huo kuwa kanisa linatambua usafi wake, si sahihi, na ni madai potofu,” alisema Mariki katika taarifa yake.

Kanisa hilo katika tamko lake hilo linasema msimamo wao hauruhusu sharika zake kutumika kama majukwaa ya kisiasa kujisafisha au kuwasafisha watuhumiwa wa ufisadi.

“KKKT imekuwa mstari wa mbele katika kupinga na kukemea mambo ya ufisadi, na linaunga mkono juhudi zote za kutokomeza uovu...kanisa litachukua tahadhari kuhakikisha jambo kama hilo, halitatokea tena,” linasema tamko hilo.

Katika hatua kubwa zaidi, kanisa hilo limefikia hatua ya kuwaomba radhi waumini wake wote wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani ikiwa ni pamoja na kanisa zima la KKKT kutokana na tukio hilo.

“Dayosisi ya Mashariki na Pwani inapenda kuwaomba radhi waumini wake wote, kanisa zima la KKKT na wale wote wenye mapenzi mema kwa nchi yetu ambao kwa namna moja au nyingine wamekwazwa na tukio hili,” linasema tamko hilo.

Likiendelea, tamko hilo linaeleza kuwa, jukumu la kanisa ni kuokoa roho za watu na si kukumbatia mafisadi na walarushwa.

Pamoja na ukali wa maneno katika tamko hilo, KKKT haikueleza iwapo mchango wa shilingi milioni tano zilizotolewa na Rostam katika hafla hiyo zitarudishwa.


Welcome Rostam. At last your out of the closet. Now we wanna see all your skelotons!

Press conference iwe ya kusema "Mimi Si FISADI, KKKT ni WAONGO", halafu utaona moto wake.

Fahamu kuwa walikuwaalika mwaka 2005 na 2006 wakati huo kila mtu alikuwa anakutazama kinafiki, lakini baada ya Septemba 15, 2007 Dr Slaa na Tundu Lissu kukanika wazi kwenye list of shame na Mwanahalisi, This Day na Kulikoni kuanika wazi kuhusu Kagoda na EPA, Kuhusu Richmond/Dowans, Kuhusu CIC na Japanese Support nk nk nk. Wewe sasa unanuka!

Najua utaonyesha vijibarua vyako vya kualikwa! Ulifuata utaratibu wakati huo lakini si sasa.

Na hata kama ulifuata utaratibu waandishi watakuuliza, NANI ALIKWAMBIA KWA KUALIKWA KANISA LIMETAMKA KUWA WEWE NI MTU SAFI NA KWAMBA TUHUMA ZAKO ZOTE NI UZUSHI?

Bahati nzuri tu, najua unatishia wewe-hutafanya mkutano wa wazi wa waandishi. Utaita watu wako wachache na kuzungumza nao.

Shame on you mjumbe wa Kamati kuu ya Chama Cha Mafisadi

Asha
 
Huyo jamaa I think fedha zake zinampa kiburi na dharau.yaani ni bonge la dont care.Shame on him.
 
Watanzania watakuwa wanafanya kosa kubwa sana kama watayapuuza haya anayoyafanya Rostam. Huyu mtu ana werevu wa kishetani na kila anachokusudia kufanya huangalia madhara yake baadaye kwa umakini sana. Tusipokuwa makini, huyu atalisambaratisha taifa na kutuacha na laana ya kupigana wenyewe kwa wenyewe. Kwa walioiona press release ya RPC wa Dodoma jana, lazima kuna mkono wa Rostam pale.
 
Kila kitu kwake ni sarcastic.Hivi huyu mtu ana nini mpaka rais anashindwa kum question?There alot going on than what meets the eye.Something has to be done hawezi kutufanya Watanzania so stupid.Sisi watu Wazima Bwana.
 
haawa kkkt wanan kamchezo wa wanataka sitaki we soma between the line utagundua


nao pia ni mafisadi
 
hata yule Yuda Iskarioti wa Biblia alipopewa pesa ya kifisadi, baadaye alitaka kuirudisha lakini wenye pesa wakamwambia kiendacho kwa mganga hakirudi.
Aliishia kujiua.
Wana kwaya wale tu hizo milioni zao 7 na kazi kwa RA sasa kupata hukumu.
Na asulubiweeeeeeeeeeeeeee.
Wanakwaya?? au Kanisa..Kanisa limeingia katika mtego ambao hawakutegemea na nimesikia wantaka waongee na RA asieleze ni nani alimwalika.

Inasemekana alialikwa na mmoja wa viongozi wa juu wa kanisa tena kw akuuatwa physical
 
Watanzania watakuwa wanafanya kosa kubwa sana kama watayapuuza haya anayoyafanya Rostam. Huyu mtu ana werevu wa kishetani na kila anachokusudia kufanya huangalia madhara yake baadaye kwa umakini sana. Tusipokuwa makini, huyu atalisambaratisha taifa na kutuacha na laana ya kupigana wenyewe kwa wenyewe. Kwa walioiona press release ya RPC wa Dodoma jana, lazima kuna mkono wa Rostam pale.

Sorry mkuu hiyo press ilikuwa nanini? japo kwa kifupi mkuu..
 
tusubiri tuone PICHA NDO KWANZA LINAANZA..
UNAFIKI UNA MWISHOOOO.
 
Hivi kanisa lina Msemaje wake?Kanisa ni chama cha Siasa..Kwamba Katibu akisema basi hakuna mwingine anweza kutoka na kutuambia ukweli kuhusu hili.

Nahisi Tabia ya CCM imeingia Makanisani..Nafikiria kuiacha CCM
 
Sasa Rostam Azizi anaitisha mkutano na waandishi ili iweje.

Kanisa tayari limesema (na nategemea huo nduo msimamo wao) Rostam Azizi alikuwa akishirikiana na kikundi cha watu ndani ya kanisa ambao hawana mamlaka ya kumnadi kwa njia yoyote ile.

RA akae pembeni na asijiingiza tena na shughuli za kanisa, na hao waandishi watakaopoteza muda kwenda kumsikiliza wananipa wazo la "spinning around" wimbo ulioimbwa na mwanadada mrembo Kylie Minogue.

Hebu tujiburudishe kidogo:

Spinning around
Oooh-oh

Im spinning around
Move out of my way
I know youre feelin me cuz you like it like this
Im breakin it down
Im not the same
I know youre feelin me cuz you like it like this

Clearin this house out of joy that I borrowed
From back in the day
Threw away my old clothes
Got myself a better wardrobe
I got something to say

Im through with the past
Aint no point in looking back
The future will be
And did I forget to mention that I found a new direction
And it leads back to me?

Im spinning around
Move out of my way
I know youre feelin me cuz you like it like this
Im breakin it down
Im not the same
I know youre feelin me cuz you like it

Mistakes that I made givin me the strength
To really believe
And no matter how I take it
Theres no way Im gonna fake it cuz its gotta be real

Ive got nothin left to hide
No reason left to fight
cuz the truths given me a new freedom inside
Gettin rid of my desire
Do you like what you see?

Im spinning around
Move out of my way
I know youre feelin me cuz you like it like this
Im breakin it down
Im not the same
I know youre feelin me cuz you like it like this

Ooh-oh baby, baby, baby
You know you like it like this
Ooh-oh baby, baby, baby
You know you like it like this
Ooh-oh baby, baby, baby

Im spinning around
Move out of my way
I know youre feelin me cuz you like it like this
Im breakin it down
Im not the same
I know youre feelin me cuz you like it like this

Oh, Im not the same
You like it like this
Ooh-oh

Rostam Azizi asipewe chance ya kufanya spinning around antics.
 
Tunaomanini Mungu yupo ni wakati kama huu ndo unapoweza kuielewa busara yake ya kutotaka kuonekana kwani watu kama RA wasingesita kutaka kwenda kumpa mlungula.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom