Rostam aibukia kanisani!

Rostam aibukia kanisani!

magazeti ya jpili yatusaidie jamani clip hii hasa tz daima alitoka front page
 
Viongozi wa dini ubinadamu unawapa shinikizo ambalo wanashindwa kusimamaia maandiko kwa dhati...wana mchango mkubwa kuleta mabadiliko katika jamii kwa kuwa wa KWELI DAIMAAAAAAAAAA.....Tuna matatizo ya uongozi lakini hawasimami kwa DHATIIIII.
 
kama kweli wametoa tamko,basi wamekosea sana,kanisa halikuwa na haja ya kutoa tamko lolote lile,na kitendo cha kumsimamisha mchungaji ni cha kukemewa kabisa,sijaona kosa lolote mpaka sasa,RA amekuwa akialikwa na kanisa hilo na kutoa michango bila matatizo.
Hapa ni sawa na kusema kunywa pombe ni halali ila kula nguruwe ni dhambi.kama ni ufisadi RA haja shitakiwa popote ktk jamuhuri ya tanzani kuhusiana na hizo tuhuma,Malasusa angalia usije ingia mtegoni,soma alama za nyakati


Alama za nyakati ndio hizo, mkuu. Kaa mbali inavyowezekana na yeyote yule ambaye jumuiya inamtuhumu kuwa ni Fisadi.Kwamba hajashitakiwa popote katika Jamhuri yetu hii siyo hoja. Hoja ni kwamba Chombo ambacho kina wawakilishi wetu, BUNGE, kimemtuhumu kuhusika na baadhi ya makampuni ambayo mikataba yake inatuacha hoi watanzania.
 


Nyoka ni nyoka tu, hata akija kanisani hawezi kubadilika akawa kinyonga, hawa wahuni wafukuzeni huko kanisani! Na nyinyi vibaraka wao msitubabaishe hapa na maneno mengi ya ujanja ujanja tunawajua tenma vizuri sana pamoja na majina yenu ya bandia hapa tunaweza kuwasema hapa wazi wapuuuzi nyie!


Mkuu wangu naona hapa umesema vizuri sana. Naona kama kuna mamluki humu. Hapa JF si kapu la wajinga, RA na EL wamejidefine wenyewe. Kama tunawaita mafisadi ni kutokana na vitendo vyao, kuwaita mafisadi sio kuwahukumu, ni kutoka na vitendo vyao na shughuli zao. Tunapomuita mwanamuziki mwanamuziki, ni kwa sababu yeye anafanya shughuli hiyo asiyemwanamuzi hawezi kuitwa mwanamuziki.
Lakini bahati nzuri hapa hadanganyiki mtu, fisadi ni fisadi tu, hata akiwa mheshimiwa anakaa kwenye ofisi nzuri na kutembelea shangingi, au hata akienda msikitini au kanisani. Fisadi ni fisadi tu.
 
Church reverend suspended over Rostam Aziz incident

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

A DAR ES SALAAM Church leader has reportedly been suspended for inviting the Igunga Member of Parliament on a CCM ticket, Rostam Aziz, to speak at a prayer mass last Sunday without following proper procedure.

Reverend Joseph Masege of the Kinondoni Lutheran Church is understood to have been so disciplined by the church for allowing the politician to address worshippers without being given the relevant go-ahead by his superiors.

Rostam used the occasion to deliver what has been widely interpreted as a highly-controversial speech, including remarks that may be interpreted as part and parcel of the ongoing political fallout and subsequent wrangling over the findings of the parliamentary committee that investigated the Richmond corruption scandal.

The MP was one of the most prominent casualties of the committee’s final report, along with ex-prime minister Edward Lowassa and ex-cabinet ministers Nazir Karamagi and Dr Ibrahim Msabaha.

Rev. Masege and one of the church’s choir groups, Amkeni, were reportedly suspended from the church after they were found to have been somehow behind the politician’s presence at the Sunday prayer mass, apparently as a VIP guest.

When contacted on his mobile phone yesterday, Rev. Masege himself declined to comment on his reported suspension, abruptly hanging up the phone instead.

Rostam reportedly donated a total of 7.6m/- to the Amkeni choir group, and was given the honour of addressing the church gathering.

In his remarks that received prominent coverage in a number of local newspapers, the MP said the country was passing through difficult times, claiming further that some people were being unfairly accused of corruption and thereby apparently demonised by political foes.

A statement issued earlier yesterday by the Kinondoni Lutheran Church distanced itself from Rostam’s remarks, saying his presence at the church did not follow proper procedure.

’’It has been established that Rostam was invited by a group that has no authority to issue such invitations,’’ said the church statement signed by its secretary general, Ambassador Richard Mariki.

The statement said the church had been dismayed by, and strongly rejected, the MP’s remarks to the congregation to the effect that he was a ’’clean politician.’’

The church also refused to be associated with any statements made by Rostam inside the church, saying the ’House of God’ should never be used to cleanse people from corruption allegations.

’’The church does not allow its congregations to be used as political platforms to cleanse corruption suspects. The Evangelical Lutheran Church of Tanzania has been at the forefront in the fight against corruption,’’ said the strongly-worded statement.

The church apologised to its worshippers for the incident, saying it would make sure such things never recur in future.
 
Bwana Yesu hakuja kwa ajili ya watenda mema, the church is open to every one!!! if they happen to leave several millions behind, tis even better. Imeandikwa, revenge is mine.... judgement too
 
Rostam Ni Mjinga Tu!

Rostam amepitwa na wakati na Upuuzi wake unajitokeza hadhrani na hatazuilika kuonekana kwa uhalisi ake kuanzia sasa na kuendelea.

Rostam kaishiwa na fikra timamu.... Haoni umbali zadi ya Pua yake ilipo... Kwa nini washauri wake wajinga wasimshauri akaachana na mambo yasiyo na mbele wala nyuma anayoyafanya kwa kisingizio cha kujisafisha?

Its too late...hasafishiki...The more and hader he try to do it the more it backfare...and every one get to know the true colour of the really Rostam

Wachana na kuwachanaganya waumini...si mahali salama kwako kupagusa...Uta aibika milele...ona sasa kinachokutokea..!

Rostam nyakati zako zmepita..wachana na kuhujumu waumini...!
 
USHAURI WANGU PESA ARUDISHIWE.......HUO UTAKUWA UJASIRI WA HALI YA JUU....na HIZO AHADI NAZO......sijui mtamaliza wenyewe....
 
Ni kweli revange is God's, lakini Mungu pia hataki unafiki. unafiki ni kitu kibaya sana. kwanini hakwenda msikitini?ndo akatolee machungu yake kanisani? angekuwa ameenda pale kusali, sawa, lakini hakwenda pale kusali bali kujisafisha. sidhani kama kanisani ni mahali pa kujisafishia, ni mahali pa kusalia. halafu, unajua sisi watz sio watu wajinga, hata kama hatuna ushahidi wa kutosha juu ya suala lake, tunaujua ukweli wake, tunashindwa tu pa kumkamatia, ukweli upo mioyoni mwetu, hivyo hatuwezi kuvumilia unafiki kisa tu kwamba hatuja prove kwamba yeye ni fisadi. tunaelewa kila kinachoendelea, ila tunashindwa tu kuthibitisha kwasababu ushahidi wameshaukata mirija, au kuupata kuna mlolongo. ila we know what is going on in our country, tunawajua mafisadi ni akina nani na wasio mafisadi ni kina nani.

mbona hawagusi waislam? kwasababu wangempa ukweli wake palepale, na wasingemkaribisha fisadi. akaona ngoja nikimbilie kwa wakristo wajingawajinga ambao naweza kuwapiga mchanga wa macho tu.....hahaha. kazi kwelikweli.
 
Mhhh!! Hapo ni kama wememhukumu mtu wakati sio kazi ya kanisa kufanya hivyo. Unless kama hawakutamka hivyo, otherwise hilo tamko lina walaakini.

usiwe mpungufu wa akili. wamemhukumu kivipi? unajua kitu kinachopeleka watu kanisani? ni kwenda kusali mzee, sio kwenda kuelezea private life lako ili watu wakuone msafi. watz tunajua kinachoendelea hata kama hatuna ushahidi kamili, tunashindwa tu tuanzie wapi, ila ukweli kuhusu mafisadi wote tunaujua. angeenda kusali akaondoka unafikiri hayo maneno yangetokea? unafikiri kwasababu ni kanisani ni mahali pa unafiki? mtu anajua kabisa kilichoko moyoni lakini anataka ku manupulate watu kutumia kanisa wamuelewe vinginevyo? uu ni uchafu ambao hauhitajiki kuonekana kanisani. hivi wewe haumjui rostam? ni watu wachache sana hawajui ukweli wa huyu mtu. rafiki yangu ktk maisha ogopa sana kuwa mnafiki au kuwa mtu mnafiki. usitetee mafisadi wewe, au we mwenzetu vipi ni mmojawao nini?
 
[QUOTE
mbona hawagusi waislam? kwasababu wangempa ukweli wake palepale, na wasingemkaribisha fisadi. akaona ngoja nikimbilie kwa wakristo wajingawajinga ambao naweza kuwapiga mchanga wa macho tu.....hahaha. kazi kwelikweli.[/QUOTE]


Dah.! mzee.! Wakristo wajinga wajinga tena??!!
 
Ni kweli revange is God's, lakini Mungu pia hataki unafiki. unafiki ni kitu kibaya sana. kwanini hakwenda msikitini?ndo akatolee machungu yake kanisani? angekuwa ameenda pale kusali, sawa, lakini hakwenda pale kusali bali kujisafisha. sidhani kama kanisani ni mahali pa kujisafishia, ni mahali pa kusalia. halafu, unajua sisi watz sio watu wajinga, hata kama hatuna ushahidi wa kutosha juu ya suala lake, tunaujua ukweli wake, tunashindwa tu pa kumkamatia, ukweli upo mioyoni mwetu, hivyo hatuwezi kuvumilia unafiki kisa tu kwamba hatuja prove kwamba yeye ni fisadi. tunaelewa kila kinachoendelea, ila tunashindwa tu kuthibitisha kwasababu ushahidi wameshaukata mirija, au kuupata kuna mlolongo. ila we know what is going on in our country, tunawajua mafisadi ni akina nani na wasio mafisadi ni kina nani.

mbona hawagusi waislam? kwasababu wangempa ukweli wake palepale, na wasingemkaribisha fisadi. akaona ngoja nikimbilie kwa wakristo wajingawajinga ambao naweza kuwapiga mchanga wa macho tu.....hahaha. kazi kwelikweli.


Unataka kuanzisha mzozo mwingine tena hapa...kwanini uwaite wakristo wajingawajinga??
 
Na nyinyi vibaraka wao msitubabaishe hapa na maneno mengi ya ujanja ujanja tunawajua tenma vizuri sana pamoja na majina yenu ya bandia hapa tunaweza kuwasema hapa wazi wapuuuzi nyie!

Mkuu sikuwahi kutegemea wewe kuja na maneno haya ya jazba na ya vitisho kwa watu kisa una wajua watu.Kazi yao ni kutafuta kumfahamu fulani ni nani na anachangia nini?wewe nimmojawapo ambmao mnatumia jina la bandia kama mimi..

kama wao ni wapuuzi kw amantiki ya kutumia majina yao ya bandia,basi nawewe utakuw ani Mpuuzi tu kwa maana hiyo.Usimtishe mtu sababu unaweza kujiona ni bora zaidi ya mtu mwingie .

Ibara ya 18 inatoa uhuru wa mtu kueleza habaro yoyote kwa mtu yeyote bila kuvunja sheria ya nchi.na inandelea kumruhusu mtu kushikilia habari na kumweleza yeyote habari aliyonayo.

Kama unawaju basi wataje wote ambao ni wapuuzi sababu inaruhusiwa
 
hilo kanisa halikumpa mwaliko katika misingi ya kwamba kanisa lipo duniani kwa ajili ya watenda dhambi,kilicholengwa hapo na kwaya iliyphusika ni hizo milioni saba alizotoa, si unachua siku hizi nyimbo za dini ni deal. Aidha kanisa la Kinondoni huo mchezo na wanasiasa si mara ya kwanza wala ya pili, matharan in 2005 katikati ya kampeni za uchaguzi mkuu, tukiwa na wagombea 10 wa urais, ni kanisa hili kwa unafiki mkubwa lilimkaribisha JK 'kuhubiri' mimbarani. Shame on you Lutheran church, hata hapo AZANIA FRONT Makao makuu ya dayosis tunaosali humo mnatuudhi badala ya kwaya kuimba nyimbo za kumtukuza Mungu mnaimba ari mpya, nguvu mpya, kasi mpya...SHAME,SHAME,SHAME...
 
RA alialikwa na sio mara ya kwanza kuchangia kanisani hapo, KKKT kujitoa sasa kutakuwa hakuna maana kama mpaka watu wapige kelele ndio hatua zichukuliwe.
Viongozi wa dini wamekuwa wakiwasafisha mafisadi, na hata EL alipokelewa na viongozi wa kanisa hilo hilo, na pia sio mara ya kwanza wanasiasa kunadi sera katika membari za kidini.

Viongozi wa dini wakubali kwamba nao sio wasafi na wakumbuke hakuna jiwe litakalo achwa bila kugeuzwa katika vita dhidi ya mafisadi na michango ya RA arudishiwe mwenyewe kama dhamira ni ya kweli haiwezekani Baniani awe mbaya lakini kiatu chake dawa.
 
RA alialikwa na sio mara ya kwanza kuchangia kanisani hapo, KKKT kujitoa sasa kutakuwa hakuna maana kama mpaka watu wapige kelele ndio hatua zichukuliwe.

Viongozi wa dini wamekuwa wakiwasafisha mafisadi, na hata EL alipokelewa na viongozi wa kanisa hilo hilo, na pia sio mara ya kwanza wanasiasa kunadi sera katika membari za kidini.

Viongozi wa dini wakubali kwamba nao sio wasafi na wakumbuke hakuna jiwe litakalo achwa bila kugeuzwa katika vita dhidi ya mafisadi na michango ya RA arudishiwe mwenyewe kama dhamira ni ya kweli haiwezekani Baniani awe mbaya lakini kiatu chake dawa.
 
I think this has gone too far.jamani ina maana huko makanisani mnawajua watoa sadaka wote wamepate fedha zao?waliua au wameiba au wamtoa mtu sadaka?tunafanya maamuzi ambayo kwangu nadhani siyo sahihi kabisa.Huyu mchungaji hana kosa jamani!kama ni adhabu wamuadhibu Rostam kama watamuweza kwa alichoongea kanisani.Kipindi fulani nikiwa kenya harambee zilikuwa lukuki kuna moja bwana Mkuu Moi alitoa fedha nyingi tuu ila waliomualika hawaadhibiwi.Muadhibuni aliyewakera na siyo huyo Mchungaji.Kweli this is unfair.
 
Heshima Mbele,

Awali ya yote kabla sijaandika kile kilichopo kichwani mwangu,Ningependa kutoa Pole kwa Mhe. Zitto kabwe Zuberi,Mungu akutangulie na nina Imani utarudi katika khali yako ya kawaida,na ukirudi tu usisahau kusoma PM yangu kwako.

Baada ya kusema hayo ningependa sasa kuchangia mjadala mbao nimeuanzisha,Baada ya juzi baraza kuu la kanisa la KKT kukaa na baadae kutoa tamko la kusema halitambui Rostam kualikwa katika kanisa lao,na linapinda siasa kujadiliwa katika kanisa lao.

Nimelifikiria sana jambo hili,ukiachilia umbali wa uchafu alio nao Rostam,Kwanini wamekuja na maauzi haya ya ghafla sana na kwa faida gani,Kanisa hili hili lilishawahi kumualika Rostam kcuhangia majengo yao mwaka 2005 na wakmsifia sana,ila leo baada ya vuguvugu la vyombo vya habari wameona ni kashfa kwa kanisa lao na ningependa tujiulize maswali yafuatayo

1.Je kwanini kanisa limetoa maelezo haya kwa Vyombo vya habari?Ni kwasababu ya kuhofia wakristo kulikimbia kanisa kwasabu ya kukumbatia mafisadi?

2.Au tatizo ni kuongelea mambo ya siasa kanisani?ambalo mie naona ndiyo tatizo lenyewe na siyo kama kanisa kuthibitisha kwamba Rostam ni FISADI9sitegemei kama wamesema kwenye taarifa yao ambayo sijaisoma zaidi ya kusoma habaria magazetini)

3.Kama hawaruhusu Siasa ni kwanini walimruhusu JK aongelee suala la Kadhi wakati akisimikwa naDr. Malathusa?Je Hilo siyo suala la Kiasiasa?Ndiyo sababu limo katika ilani ya CCM.walitoa tamko?

4.Viongozi wa makanisa wamekuwa wakiishi kwa kutegemea watu na hili ndilo tatizo kubwa linaloyakabili makanisa yetu,Kuna wenye sauti na ambao wan ushawishi mkubwa kanisani wanweza kuamua hata jambo baya.

5.Kama Kanisa,lengo lao ni kuhubiri injili ili watuwaache Maovu,Kwanini hata siku mmoja hawajawahi kumuita Rostam na kuwambia aache matendo ya kifisadi kama wanavyoamini?ili tujue kweli wako kazini..

Kitendo cha kukataa na kusema RA hakupata Baraka zote ni maamuzi yaliyofanywa kwa haraka bila umakini sababu nijuavyo mimi kanisa ni sehemu ya watenda dhambi na waliko wakamilifu,na kazi ya watumishi ni kuwahubiri hawa watendao maovu wabadilike?

Kama kweli Kanisa kama KKKT wameamua kuwachukia mafisadi,waanze kwanza kufanya yafuatayo

1.Kupiga Marufuku watu wote ambao wanapata pesa za kifisadi kuongea kanisani ama kutoa sadaka za kifisadi.

2.Watuambie ni kwanini walimruhusu Askofu Dr. Laizer kumpokea Lowassa kule Arusha kwa mbwembwe nyingi na hawakumkea ili khali Mhe. Lowassa alikuwa na kashfa ya ufisadi.Kwanini wanamuonea Mchungaji huyu?Je Akofu Dr. Laizer alipewa baraka na Kanisa kufanya hivi?bila kunipa majibu haya huu niuonevu kwa mchungaji wa kanisa hilo na wengine.

3.Warudishe pesa alizotoa Rostam ili tujue ni kweli wanapingana na UFISADI na hawapokei pesa ya wizi

4.Waaandike katiba yao upya ambayo itakuwa ikielezea jinsi ya watu wanotakiwa kuzungumza makanisani,na mojawapo ya sababu ikiwa ni mafisadi kutopewa nafasi ya kuzungumza makanisani

5.Kwa kuwa Muungwana aliongelea Siasa kipindi kile wakati wakimuapisha Malathusa,Basi watoe tamko lingine kama hilo.

Hitimisho
Nawaomba wawasamehe hao wanakwaya na pia mchungaji kwa wakti huu sababu hata YESU alikuwa ni mtu wa kutoa msamaha,na kama wana hasira na hao watumishi wajue wanatenda dhambi(rejea Matendo ambayo siyo ya kiroho).

Lengo la kanisa ni kuwafundisha habari njema za Yesu Kristo na pia kuwaasa watu,Kanisa linatakiwa kuwakemea viongozi hawa tunaowajua wala Rushwa kwa kuwataja majina ili waache..Ni pesa ngapi za Wizi wanapokea?kwanini wanamkataa mtenda dhambi??wampokee na wamuombee

Hili ni tatizo na naomba nisilaumiwe kwa haya ili niungwe mkono,Na siyo kwamba nampenda RA.Simpendi na Namchukia na nina sababu zangu nyingi sana,ila kwa kutumia hoja dhaifu kama hii kanisa limekosea sana.
 
Last edited:
Kumbe mtoa tamko kwa niaba ya kanisa ni mwandiplomasia pia(balozi mariki) ??
ningependa kujua alikuwa anatuwakilisha katika nchi gani kwani kauli aliyoisoma jana ina mushkeli kulingana na upeo wake!!!
Tusikurupuke sana kwa ajili ya wachache wenye nia binafsi...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom