Rostam aibukia kanisani!

Rostam aibukia kanisani!

JF ilikuwa mstari wa mbele katika mjadala huu, na hatimaye mawazo ya wengi kama yalivyotolewa hapa ukumbini kwa mara nyingine tena yameshinda!!. Hongereni JF.

Makanisa yaonywa kuepuka Mafisadi

2008-07-09 09:20:14
Na Anneth Kagenda

Viongozi wa dini, wameonya makanisa yasitumike kama uwanja wa kuwasafisha watu wanaotuhumiwa kuhusika katika kashfa ya ufisadi nchini.

Hatua hiyo, imekuja siku chache baada ya Mbunge wa
Igunga (CCM), Bw. Rostam Aziz, anayetajwa katika kashfa hizo, kukaririwa mwishoni mwa wiki, akitoa kauli zenye mwelekeo wa kuwatetea watuhumiwa wa ufisadi nchini.

Bw. Aziz, alisema kualikwa kwake kuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuzindua albam ya Amkeni ya kwaya ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) ushirika wa Kinondoni jijini Dar es Salaam, ni ishara ya kupuuza vijimaneno ya upuuzi wa kijiweni.

Mbunge huyo, alitajwa katika kashfa ya Richmond, iliyotolewa bungeni na Kamati Maalumu ya Bunge, iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela (CCM), Dk Harrison Mwakyembe.

Wakizungumza na waandishi wa habari jijini hapa jana, wachungaji sita wa madhehebu tofauti, walisema hatua ya Mbunge huyo kutumia `madhabahu` ya KKKT, ni kutaka kulihusisha kanisa hilo na utetezi wa watuhumiwa wa ufisadi.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Mchungaji Christopher Mtikila, alisema ingawa alifanikisha kulitumia kanisa hilo, lakini hatua hiyo haipaswi kutafsiriwa kama ni msimamo wa KKKT.

``Tunajua katika KKKT kuna waadilifu, wanaopiga magoti kwa ajili ya kuombea haki, amani na usawa, ukweli ambao hawa mafisadi wanaukiuka,`` alisema.

Alisema, kuna haja kwa makanisa kusimama imara na kuepuka kutumika kama `mapango\' kwa ajili ya kuwaficha watu wanaohusishwa na ufisadi.

Wachungaji wengine walioshiriki kutoa tamko hilo na makanisa yao kwenye mabano ni Gordon Kiyalo (Pentecostal Fellowship Church Int), Gwakisa Mwaibasa (True Light Shining Ministry), Isaac Kalenge (Pentecostal Vision), Ibrahim Sabuni (Jesus Ark Int Ministry) na Primus Ishobeza (Upendo Pentecostal).

Mchungaji Mtikila, alisema Bw. Aziz, anakabiliwa na shutuma za ufisadi zilizomfanya ashindwe kupata mwanya wa kujitetea ndani ya Bunge na katika majukwaa ya siasa.

``Huyu ndugu yetu amebanwa, amekosa pa kutokea, si ndani ya Bunge, katika chama chake cha CCM wala majukwaa ya siasa, kwa wapiga kura wake, ameona mahali pekee ni katika kanisa la KKKT,`` alisema.

Mchungaji Mtikila, ambaye mara kwa mara alirejea madai yake kuwa Mbunge huyo ni raia wa Iran alidai, kwa uzalendo wa wabunge na vyombo vya habari, Bw. Aziz ni mhusika katika kashfa ya Richmond, na baadaye Dowans zinazohusika katika kashfa ya kulipwa isivyo halalali, Sh. milioni 154 kila siku.

Pia alidai kuwa Bw. Aziz, anahusika katika vitendo vya uhujumu uchumi kutokana na kuitumia kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, `kukomba` Sh bilioni 33 kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Aidha, Mchungaji Mtikila, alimshutumu Mkuu wa KKKT, Askofu Alex Malasusa, kwa kushindwa kudhibiti vitendo vya kanisa hilo, kutumiwa na wanasiasa, katika kukidhi matakwa yao.

Askofu Malasusa hakupatikana kuzungumzia madai hayo, licha ya jitihada za Nipashe kumtafuta hadi kupitia simu yake ya kiganjani, lakini hakupatikana.

Mchungaji Mtikila, alidai kuwa miongoni mwa wanasiasa waliowahi kuichangia KKKT kwa ushirikiano na Askofu Malasusa, ni Rais Jakaya Kikwete, alipokuwa katika kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2005.

Mchungaji Mtikila, alidai kuwa vitendo vya wanasiasa kuitumia KKKT kwa maslahi yao binafsi, ni kielelezo cha Askofu Malasusa kushiriki katika mtandao ulioshinda Uchaguzi Mkuu uliopita.

``Lakini huyu alikuwa mtu mmoja tu, na siyo KKKT?ieleweke kuwa kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe na kuhukumiwa kwa yale aliyoyanena mwenyewe,`` alisema.

Alisema KKKT kama kanisa, halipaswi kuhusishwa na kashfa ya kutumiwa na Bw. Aziz, kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutaka kujisafisha.

Hata hivyo, alikifananisha kitendo kilichofanywa na Mbunge huyo, kama matendo yenye kulinajisi kanisa hilo nchini.

SOURCE: Nipashe
 
Mbona katika hao wachungaji hayupo wa Kilutheri?

Hawa ni wakina Mtikila na wengine.

Kwa Mtikila hii ni political game na sio masuala ya kiroho .......

Kuna haja ya kuliangalia hili kwa tahadhari kubwa kwani huyu RA hakwenda akiwa hayuko sawa ila wamejipanga .........

Kaeni macho na kuangalia dramma itakavyoweza kuendelea hapa utawasikia wakisema kuwa kanisa kazi yao sio kuwahukumu watu bali ni kuwaombea na kuwasogeza karibu na Mungu.

Wapo watakaojitokeza usharika huo huo na kudai huyu katibu mkuu aombe radhi kwani amejichukulia nafasi ya kuhukumu na hapo ndio patakuwa mwanzo wa kitimtim........

Wanasema kuwa nyumba ya Mwendawazimu imeingiliwa na mlevi......wataelewana?
 
nadhani katika nyumba hiyo swali ni kuwa nani atakuwa ameshika kisu na nani ana fagio!
 
Balozi Mariki naye kakurupuka na wote waliofikia uamuzi huo nao wamekurupuka, Hela za Rostum ni za kifisadi na hela za waumini wa hapo ndo salama? wanajuaje?
Stupid!

Hawawezi kujua!!!!! ndio maana hawazilalamikii. Za RA zinajulikana ni za kifisadi!! ndio maana wanazilalamikia
 
kama kweli wametoa tamko,basi wamekosea sana,kanisa halikuwa na haja ya kutoa tamko lolote lile,na kitendo cha kumsimamisha mchungaji ni cha kukemewa kabisa,sijaona kosa lolote mpaka sasa,RA amekuwa akialikwa na kanisa hilo na kutoa michango bila matatizo.
Hapa ni sawa na kusema kunywa pombe ni halali ila kula nguruwe ni dhambi.kama ni ufisadi RA haja shitakiwa popote ktk jamuhuri ya tanzani kuhusiana na hizo tuhuma,Malasusa angalia usije ingia mtegoni,soma alama za nyakati
 
Habari za kuaminika zinasema hatua fulani zimechukuliwa ikiwemo kusimamishwa kwa mchungaji wa Kanisa hilo na pia kuamuru fedha zilizopokelewa kurudishwa kwa Rostam//


Kaka huu ni mchanga wa macho tu hakuna lolote zaidi ya kutoana kafara tu hapo, kama kweli wanachukia pesa za kifisadi wawe wanarudisha SADAKA za E.Lowassa yes wawe wanarudisha sadaka za E.Lowasa pale azania front........ Na hata makanisa mengine ambayo mafisadi wanakosali wawe wanarudisha hapo tutaona kweli wapo serious na kuchukia ufisadi.......... Naanza kupata kigugumizi na maswali mengi kuwa JE KAMA ANGELIKUWA LOWASSA NDIO AMETOA PESA HIZO ZINGELETA HAYA YOTE?? Note:- Malasusa ni mshikaji wa karibu sana wa Lowassa sasa............. Ukipata jibu kaa kimya
 
Habari za kuaminika zinasema hatua fulani zimechukuliwa ikiwemo kusimamishwa kwa mchungaji wa Kanisa hilo na pia kuamuru fedha zilizopokelewa kurudishwa kwa Rostam//


Kaka huu ni mchanga wa macho tu hakuna lolote zaidi ya kutoana kafara tu hapo, kama kweli wanachukia pesa za kifisadi wawe wanarudisha SADAKA za E.Lowassa yes wawe wanarudisha sadaka za E.Lowasa pale azania front........ Na hata makanisa mengine ambayo mafisadi wanakosali wawe wanarudisha hapo tutaona kweli wapo serious na kuchukia ufisadi.......... Naanza kupata kigugumizi na maswali mengi kuwa JE KAMA ANGELIKUWA LOWASSA NDIO AMETOA PESA HIZO ZINGELETA HAYA YOTE?? Note:- Malasusa ni mshikaji wa karibu sana wa Lowassa sasa............. Ukipata jibu kaa kimya

Kuhusu Askofu Malasusa kuwa karibu na LOWASSA nakataa tena kwa nguvu zote kwani najua kuwa huyu ana msimamo na hana mahusiano ya karibu kihivyo na mafisadi.
 
Habari za kuaminika zinasema hatua fulani zimechukuliwa ikiwemo kusimamishwa kwa mchungaji wa Kanisa hilo na pia kuamuru fedha zilizopokelewa kurudishwa kwa Rostam//


Kaka huu ni mchanga wa macho tu hakuna lolote zaidi ya kutoana kafara tu hapo, kama kweli wanachukia pesa za kifisadi wawe wanarudisha SADAKA za E.Lowassa yes wawe wanarudisha sadaka za E.Lowasa pale azania front........ Na hata makanisa mengine ambayo mafisadi wanakosali wawe wanarudisha hapo tutaona kweli wapo serious na kuchukia ufisadi.......... Naanza kupata kigugumizi na maswali mengi kuwa JE KAMA ANGELIKUWA LOWASSA NDIO AMETOA PESA HIZO ZINGELETA HAYA YOTE?? Note:- Malasusa ni mshikaji wa karibu sana wa Lowassa sasa............. Ukipata jibu kaa kimya

Na sadaka ya Mkapa nayo ni halali? Sina uhakika kama Chenge ni muumin mzuri, hiyo itakuwa nafuu kwake maana atakuwa kaamua kuwa dini yake ni ufisadi, sio mnafiki?
 
mpaka kieleweke :- Kuhusu Askofu Malasusa kuwa karibu na LOWASSA nakataa tena kwa nguvu zote kwani najua kuwa huyu ana msimamo na hana mahusiano ya karibu kihivyo na mafisadi:


Kakaka kaaga hivyo hivyo na ubishi wako we unafahamu hata wakati Eddo amerjra kutoka dodoma pale alipoandika barua ya kuresign alifanya kikao cha kiaina pale kwake na MALASUSA alikuwa mmoja wa watu walienda kumpokea airport na hata kwenda naye pale nyumbani kwake o'bey?? hiyo ndo hali halisi mzee wacha kubisha
 
Hivi zile pesa aliwachangia hawa KKKT au?
 
Ngoja nitoke kidogo na ninaomba niishie hapa kumzungumzia askofu wangu maana ndiye kiongozi wa kanisa langu.... Mnisamehe waumini.
Ciao
 
Hivi Anglikana nao, wameanza kupokea misaada toka kanisa la anglikan USA????

Kuna wakati nao walizua zogo, POKEA, KATAA!!!! kisa ushoga!!!!!!!!

Mara nyingine, hata huoni rationality ya uwepo wa taasisi za dini!!!!!
 
Ngoja nitoke kidogo na ninaomba niishie hapa kumzungumzia askofu wangu maana ndiye kiongozi wa kanisa langu.... Mnisamehe waumini.
Ciao

Ni ukweli Mafisadi wamepenyeza INFLUENCE ZAO MAKANISANI!
Na KKKT wako kwenye HARD TIMES.
Wengi wa waumini wake wamekumbwa na UFISADI na sasa Influence waliyo nayo kwasababu ya pesa na mcconnection vitaliyumbisha sana Kanisa hilo.
 
Jana tulisema haya chini:-

.....According to the dataz nilizozipata sasa hivi ni kwamba leo wakuu wa makanisa karibu yote nchini wamekutana na kuongea na waandishi wa habari kuhusiana na kitendo cha juzi cha Rostam kwenda kanisani,

1. Kwanza imefahamika kuwa aliye-engineer huo mpango wa Rostam kwenda kanisa hilo ambalo Spika ni mzee wa kanisa, ni mkulu Lowassa.

2. Wakuu hawa wa makanisa ambao pia walimjumuisha Mtikila kwenye maelezo yao kwa waandishi w habari wamekilaani sana kitendo hicho cha Lowassa na Rostam kujaribu kuyaingilia makanisa.

3. Wamemtaka kiongozi wa kanisa lililopokea pesa za Rostam, kuzirudisha mara moja kwa Rostam, kwamba kanisa halihitaji hela hizo za ufisadi na wamemuonya sana Rostam kuwa sasa he is out of control ajiepushe kabisa in the future na makanisa.

Ahsante wakuu hii nimeipata sasa hivi baada tu ya viongozi hao wa makanisa kumaliza mkutano wao na waandishi.

Naomba Mods ikisha-expire hii iunganishwe na ile thread ya Invisible.

Na leo imekuwa haya chini:-

Re: BREAKING News: KKKT wamkana Rostam

Mungu Aibariki JF maana always one step ahead!, wembe ni ule ule inabidi kuwamulika kila wanapojaribu kujiingiza hawa mafisadi, mpaka kieleweke!
 
Hivi Anglikana nao, wameanza kupokea misaada toka kanisa la anglikan USA???? Kuna wakati nao walizua zogo, POKEA, KATAA!!!! kisa ushoga!!!!!!!!
Mara nyingine, hata huoni rationality ya uwepo wa taasisi za dini!!!!!

yule Askofu wa Anglikana Dodoma, naye according to the dataz ni fisadi tena wa hatari sana, maana ni kweli anapokea waumini mashoga toka majuu inasemekana huwa anakatiwa mpango, lakini it is only a matter of time kabla hajaadhirishwa maana watu wanamlia deep, pole pole ataupanda mkenge,

Lakini sio siri kuwa ana lake jambo na waumini mashoga kutoka majuu! Lakini everything is under control na yeye hajui hilo kuwa kuna wanaommulika tayari!
 
Na sadaka ya Mkapa nayo ni halali? Sina uhakika kama Chenge ni muumin mzuri, hiyo itakuwa nafuu kwake maana atakuwa kaamua kuwa dini yake ni ufisadi, sio mnafiki?

Chenge anaamini VIJIUNGA na VIJISENTI.
 
Hawawezi kujua!!!!! ndio maana hawazilalamikii. Za RA zinajulikana ni za kifisadi!! ndio maana wanazilalamikia

....nenda Arusha ukaone Askofu Laizer anavyokumbatia pesa za majambazi..........mijitu inajulikana kabisa kuwa ni mijimbazi.......lakini ndio hao hao wazee wa makanisa.......dah siku ya kiama.........itakuwa sooo........wee acha tu.................
 
Mhhh!! Hapo ni kama wememhukumu mtu wakati sio kazi ya kanisa kufanya hivyo. Unless kama hawakutamka hivyo, otherwise hilo tamko lina walaakini.


Sasa tutakuwa wajinga kama Rostam akiwekwa kwenye kundi la wanaolitakia mema taifa. Kanisa sio sehemu ya kutoa hukumu nadhani mahakama ni sehemu inayoweza kutoa hukumu. Mtazamo wa kanisa au mtazamo wa waumini wa dhehebu hilo na watanzania kuhusu Rostam siyo hukumu, ametufanya tumuone hivyo kutokana na vitendo vyake. Kama angehukumiwa nadhani sasa asingekuwa hata na attempts za kulihonga kanisa.
Na ni mjanja sana amechagua kanisa kwa sababu amejua wakristo wanaweza kumpa shavu la pili, angeenda msikitini angekiona cha moto.
 
Kinepi alishawahi kusema pale misikiti na makanisa yatakapowakimbiza mafisadi na wezi na kuweza kuwaita kwa majina kwamba wao ni wezi na mafisadi taifa litaendelea. Kijiko kikubwa hakiwezi kuwa beleshi. Ukweli na uwazi wa ukweli unatakiwa uwe sehemu ya ibada na mahakamani ni pahali pa sheria za nchi husika. Hata Yesu alimwambia Zakayo aende akauze mali alizowaibia masikini awagawiye kisha amfuate. Vilevile aliwahi kuwafukuza watu kanisani kwa kuwaambia nyumba ya baba yangu sio pango la wezi na wanyanganyi. Sasa mnataka viongozi wa dini wahubiri nini??? au waseme nini. Mtafikishwa mahakamani msiogope kwani nitawafundisha nini la kusema Yesu aliwaambia wanafunzi wake. Wote mnaoona Kuitwa kwa Rostam mwizi na fisadi haikuwa sahihi eti kwa sababu hakuna hukumu ni wanafiki na mnalinda uharamia na ushenzi. Rostam ni mwizi na Fisadi.

"It is a poverty to decide that a child must die so that you may live as you wish."
Mother Teresa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom