jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 26,375
- 25,453
Mkuu ES,
Naomba nikuulize kaswli kadogo tu. Assume wewe ni mwalimu na upo darasani unawafundisha wanafunzi namna ya kusolve swali moja la hesabu, then anatokea mmojawapo wa wanafunzi anasimama na kusema mwalimu unavyofanya sio sahihi? Je utampa nafasi huyo mwanafunzi aonyeshe njia yake ilivyosahihi au utamfukuza darasani?
Inategemea..Walimu wengine wanaweza kuchukulia tofauti wakaleta bifu.
Wengine sivyo..Inategemeana..Mimi nilikuwa darasani na kijana muhindi na alikuwa akienda ubaoni na kushuka equation ambayo imemtatiza mwalimu na wala hakuwa na bifu wala nini!
Lakini hatahivyo sisi tuliosoma na wahindi ilikuwa ni nadra sana kwa wao kulimwa bakora ukilinganisha na weusi.
Hii ni kwasababu wahindi walikuwa wakiwahonga pesa tosha kuliko hata mishahara yao.
Wahindi Walikuwa na vitabu vizuri kuliko hata hao waalimu wanavyovitumia kwenye syllabus!
Na ndio maana hata sisi tulikuwa tukienda majumbani kwa wahindi hao kwa ajili ya tuition ya kulipia!
Ni baadhi ya walimu wenyewe HOVYO TU!
Na ndio maana taaluma hiyo watu hawaitaki kwani walimu wenyewe wameidhalilisha mara baada ya wao kudhalilishwa na serikali kwa kutolipwa mishahara yao!
Na mafrustrations wanaenda kuwatolea wanafunzi wengine ambao hata ada yao ni familia inabidi ijifunge mkanda ki kweli kweli.
Sasa na wakati huu kila mtu anajuwa kuwa watoto wa Tanzania nzima wanaoendelea na masomo yao mara baada ya elimu ya msingi hawafikii hata nusu ya watoto wote Tanzania!
Sasa si kizazi cha watumwa tunatengeneza?
Tena na wachina na kila mtu wako mtaani hapo bongo?
Samahani Nyangumi kama nimetoka nje ya kusudio la swali lako lakini nilionelea nigusie hili.
Ahsante.