Rostam aibukia kanisani!

Rostam aibukia kanisani!

mbona hawagusi waislam? kwasababu wangempa ukweli wake palepale, na wasingemkaribisha fisadi. akaona ngoja nikimbilie kwa wakristo wajingawajinga ambao naweza kuwapiga mchanga wa macho tu.....hahaha. kazi kwelikweli.

Una uhakika na hayo maandishi yako? Just wait and see!!!!!
 
Viongozi wa dini wamekuwa wakiwasafisha mafisadi, na hata EL alipokelewa na viongozi wa kanisa hilo hilo, na pia sio mara ya kwanza wanasiasa kunadi sera katika membari za kidini.
Songambele,

Nimeshaliandikia hilo unaweza cheki thread nimeanzisha na nitandika Walaka wa kuwapelekea kama kanisa,wanawaonea wadogo na kuwasetili wakubwa,kwanini wamfungie Mchungaji lakini Askofu Laizer aliachwa?
 
Huyo Mchungaji wa Usharikwa wa Kinondoni alikuwa na nia ya kuukumbatia UFISADI kama sio tamaa ya pesa na kwa nini hajamshirikisha Askofu wake katika kumwalika RA tena mtu wa dini nyingine? Heko Askofu Malasusa na wana-KKKT kwa kung'amua hilo mapema.

Hata wale unaowapa heko wanauozo uleule. Hawana lolote. Hawa ni wakumbatia mafisadi wa siku nyingi. Wamezoea kupokewa pesa za mafisadi kwa njia mbalimbali IKIWEMO SADAKA KUBWAKUBWA NA ZAKA AMBALO NI FUNGU LA KUMI LA PESA ZINAZOPATIKANA KWA NJIA ZA UFISADI. Kama hilo hulijui basi wewe kalagabaho!
 
Kweli dunia imekwisha!!!

Sasa hilo kanisa, au huyo binadamu (askofu, Sheik) ambaye ana uwezo wa kuchambua fedha haramu na halali yuko wapi wajameni...!!! Tuache hizi siasa kila mahali hadi makanisani.

Mtu ametoa kwa moyo wake... mwenye kujua za halali au sio za halali ni Mola wake... acheni siasa wajameni!!!!
 
Taarifa ya KKKT
“Tunasikitika ya kwamba kanisa halikuwa na taarifa ya ujio wa Rostam Aziz. Tunapenda kuwataarifu kwamba, taratibu za kuwaalika wageni kwenye shughuli kama hizi hazikufuatwa,”

"Nawashukuru kwa kuamua kunialika kuwa mgeni rasmi leo. Hii ni ishara kwamba mmeamua kupuuza viji-maneno na upuuzi wa vijiweni. Nafurahi kuwa miongoni mwenu…hamtuhumu, hamshutumu, hampendi wenye wivu na wenye chuki, mnapenda haki. Ninao watoto watatu na nataka niwalee katika misingi hii",alisema Rostam huku akishangiliwa na umati wa watu walioshiriki hafla hiyo.

Hawa wakristo wamechukuliwa hatua gani??kwanini walimshangilia,ina wezekana kweli nchi hii ni ya mandondocha,siye tunasumbua kila siku kupinga hawa ila hawa wanawasaidia Mafisadi..watanzania ni watu wa kushangilia kila siku.

"Kutokana na ukiukwaji taratibu hizi, hayo madai yaliyonukuliwa katika vyombo vya habari kwamba ujio wa Rostam katika Usharika wa Kinondoni na tafasiri ya ujio huo kuwa kanisa linatambua usafi wake, si sahihi na ni madai potofu,”

Mwanakijiji nahitaji walaka wako kwa viongozi wa dini uliowaandikia,nimeopoeteza ila naendelea kuutafuta
 
2.Watuambie ni kwanini walimruhusu Askofu Dr. Laizer kumpokea Lowassa kule Arusha kwa mbwembwe nyingi na hawakumkea ili khali Mhe. Lowassa alikuwa na kashfa ya ufisadi.Kwanini wanamuonea Mchungaji huyu?Je Akofu Dr. Laizer alipewa baraka na Kanisa kufanya hivi?bila kunipa majibu haya huu niuonevu kwa mchungaji wa kanisa hilo na wengine.

Gembe, kwanza heshima mbele!

Pili kuhusu hii mada yako umechanganya mambo mengi sana, ambapo mengine yana majibu ya papo hapo na mengine ni kwa wale wenye kujua muundo na utendaji wa KKKT.

Kuhusu matukio ya "Askofu Laizer + Mh. Lowassa" na "Mch Massege + Mh. Rostam" yote yana sura ya kisiasa lakini yametokea katika mazingira tofauti.

Askofu Laizer alikuwa mmojawapo wa waalikwa katika mkutano wa kumpokea Mh. Lowassa kule Monduli kwenye uwanja wa mpira, wakati Mh. Rostam Aziz alikuwa mwalikwa rasmi kwenye ibada iliyofanyikia kanisani!

Sasa ukiangalia vizuri utaona tofauti hapo, kwanini KKKT imeweza kuingilia hili la Rostam, ni kwa sababu aliaalikwa kanisani (kama Mgeni rasmi) bila kufuata utaratibu wa KKKT, wakati Askofu Laizer alialikwa kama mtu binafsi na hata alipopewa nafasi ya kuongea kule Monduli aliongea kama mtu binafsi na si kama Askofu wa KKKT (ninayo hotuba aliyoongea naweza kukutumia).

Kila kanisa lina taratibu zake kuhusu mialiko ya watu (ususani wale mashuhuri) katika kushiriki ibada zake, na tena kwenye tendo kubwa kama lile ya uzinduzi wa CD ya kwaya. Utaratibu nijuavyo uko kama ifuatavyo.

Mchungaji Mkuu (KKKT Kinondoni) ---> Mkuu wa Jimbo (Kinondoni) ---> Katibu Mkuu wa KKKT (Dayosisi) ama Msaidizi wa Askofu Mkuu (Dayosisi). Katika hili la Rostam suala la mwaliko liliishia kwa pale pale KKKT Kinondoni halikwenda mbele kwa viongozi wa juu!! Kwa hiyo katika hili kuna walakini.
 
Kweli dunia imekwisha!!!

Sasa hilo kanisa, au huyo binadamu (askofu, Sheik) ambaye ana uwezo wa kuchambua fedha haramu na halali yuko wapi wajameni...!!! Tuache hizi siasa kila mahali hadi makanisani.

Mtu ametoa kwa moyo wake... mwenye kujua za halali au sio za halali ni Mola wake... acheni siasa wajameni!!!!

Kasseshe ndiyo maana nasema hapa kuna Tatizo,Kanisa imekuwa sehemu ya kufanyia mambo ya siasa.

Yes I said Warudishe pesa za Rostam kwanza
 
Jamani ndugu zangu mimi narudi palepale tunawajua watoa sadak wote uhalali wa fedha zao?Katika kanisa la Korongoni zamani hizo sijui mpak leo kama bado yanaendelea,kulikuwa na mama mmoja anaitwa Mama Devotha huyu mama alikuwa anajulikana ni mchawi.Yaani beleive it or not it was an open secret na kila mtu alikuwa ana muona anatoa check tuu lakini hata siku moja sijawahi kusikia watu wakisema hizo check zirudishwe.Sasa ni hivi,ni wangapi tunajua chanzo za pesa zao?wamekill,wameroga au wamemtoa sadaka mtu?Lets be realistic na haya mambo.Suala la kurudisha fedha mimi haliniingi hata kidogo.
 
Du mwacheni aende kanisani kutubu. Tusimhukumu RA kwani hukumu ataitoa Mungu mwenyewe. Yesu Kristo alisema, acheni wenye dhambi waje kwangu na atazisafisha dhambi zao nyekundu kama damu ziwe nyeupe kama theluji. Ukweli sikubaliani na ufisadi kwani ndio umetufikisha hapa tulipo kwenye lindi la umaskini kwa watz walio wengi na matajiri wachache.
RA anastahili kutubu kwani amefanya maovu makubwa sana yakiwemo kusuka mipango na kuwaondoa kabisa au kuwahamisha viongozi shupavu kwenye nafasi zao za kazi pale ambapo anaona kiongozi huyo anakwamisha mambo yake fulani fulani. Wewe utasikia tu Mkurugenzi fulani kapelekwa Rukwa au Kusini kuwa RAS. Sasa Je kuhusu RA kuwa rais kivuli ya awamu ya nne tusemeje? CCM inavuna ilichokumbatia na kupanda kwa magabachiori na Wairan. Nina hasira sana na huyu RA acha tu aungame jamani aanze maisha upya na mali zake ahakikishe anagawia maskini. Imesemwa kuwa ni rahisi ngamia kupenya tundu la sindano kuliko tajiri kuingia ufalme wa mbingu. Pengine RA ameshaliona hilo na anajisafisha. Sasa ndugu sijui Waislam watamwita haramu maana kakanyaga kanisani na watamtenga au watamwogopa kwa sababu anachangia sana maendeleo ya waislam? Haki ya nani najua Shekhe Mkuu hatasema neno ng'o, yaani apoteze mafyeza ya msaada toka kwa RA? Kweli pesa ni hatari, yatoa uhai wa mtu, cheo, stahili nk. Sooorry imekuwa ndefu like a book but ni dukuduku langu kwa RA.
 
Roastam ana connection na wafanya biashara wengi tu wanaotoka huko KKKT na sasa pia na wachungaji!

Hilo tunajuwa na ndio maana wanasusua kuzirudisha pesa hizo!

Kuna matajiri wengi sana tu huko KKKT...Na hivyo Kumwita RA kwasababu ya milioni saba unusu ni sababu za kisiasa tu!

Kuna matajiri wenye utajiri wa ajabu humo ndani na nadhani hao wameguswa na kashfa za sirikali na sishangai wakiwa wao ndio waandaaji wa hii propaganda yote kwani hata wao wanajuwa kuwa wamo hatiani kwenye ufisadi.

Tulishawaambia warudishe pesa hizo wamekataa!

Yani kuna watu hawana akili timamu kabisa na kweli kama nchi ikiingia matatani...Basi wao ndiyo watakuwa sababu kubwa sana ya machafuko hayo kwani wao ni BEI RAHISI MNO!

Yani kweli milioni SABA INANUNUA UHURU WA KANISA NA WAUMINI?
TENA HATA UHURU WAO WA KUFIKIRI?

Jamani...Huko makanisani kama kunawafanya watu wafikiri namna hiyo then ni kweli bado kuna watu wanaong'ng'ania kuwa watumwa wa mtu yeyeto yule almradi anawapa kula na wao wanaendelea kuomba Mungu!?

Sasa ni Mungu gani huyo waliyomuomba akawaambia waende kumwalika RA ili awape kwaya milioni saba na na genereta?
 
Gembe, kwanza heshima mbele!

Pili kuhusu hii mada yako umechanganya mambo mengi sana, ambapo mengine yana majibu ya papo hapo na mengine ni kwa wale wenye kujua muundo na utendaji wa KKKT.

Kuhusu matukio ya "Askofu Laizer + Mh. Lowassa" na "Mch Massege + Mh. Rostam" yote yana sura ya kisiasa lakini yametokea katika mazingira tofauti.

Askofu Laizer alikuwa mmojawapo wa waalikwa katika mkutano wa kumpokea Mh. Lowassa kule Monduli kwenye uwanja wa mpira, wakati Mh. Rostam Aziz alikuwa mwalikwa rasmi kwenye ibada iliyofanyikia kanisani!

Sasa ukiangalia vizuri utaona tofauti hapo, kwanini KKKT imeweza kuingilia hili la Rostam, ni kwa sababu aliaalikwa kanisani (kama Mgeni rasmi) bila kufuata utaratibu wa KKKT, wakati Askofu Laizer alialikwa kama mtu binafsi na hata alipopewa nafasi ya kuongea kule Monduli aliongea kama mtu binafsi na si kama Askofu wa KKKT (ninayo hotuba aliyoongea naweza kukutumia).
Mkuu think BIG,
simple Logic,Kwani Rostam hakualikwa kama mtu binafsi?na hata Rostam aliongea kama mtu Binafsi na si kama Mbunge sema aliongea mambo yanayohusu Siasa na vivyo hvyo alifanya Askofu Dr.Laizer.

Lengo si kumtetea Rostam,ila uhalali wa jambo lenyewe tu na uhalisia wa Maisha ya kila siku katika makanisa yetu
 
RA alialikwa na sio mara ya kwanza kuchangia kanisani hapo, KKKT kujitoa sasa kutakuwa hakuna maana kama mpaka watu wapige kelele ndio hatua zichukuliwe.
Viongozi wa dini wamekuwa wakiwasafisha mafisadi, na hata EL alipokelewa na viongozi wa kanisa hilo hilo, na pia sio mara ya kwanza wanasiasa kunadi sera katika membari za kidini.

Ninaomba tunapojadili suala hili, tuchangie tukiwa na uelewa haswa wa suala lenyewe.

Kuhusu matukio ya "Askofu Laizer + Mh. Lowassa" na "Mch Massege + Mh. Rostam" yote yana sura ya kisiasa lakini yametokea katika mazingira tofauti.

Askofu Laizer alikuwa mmojawapo wa waalikwa katika mkutano wa kumpokea Mh. Lowassa kule Monduli kwenye uwanja wa mpira, wakati Mh. Rostam Aziz alikuwa mwalikwa rasmi kwenye ibada iliyofanyikia kanisani!

Sasa ukiangalia vizuri utaona tofauti hapo, kwanini KKKT imeweza kuingilia hili la Rostam, ni kwa sababu aliaalikwa kanisani (kama Mgeni rasmi) bila kufuata utaratibu wa KKKT, wakati Askofu Laizer alialikwa kama mtu binafsi na hata alipopewa nafasi ya kuongea kule Monduli aliongea kama mtu binafsi na si kama Askofu wa KKKT (ninayo hotuba aliyoongea naweza kukutumia).

Kila kanisa lina taratibu zake kuhusu mialiko ya watu (ususani wale mashuhuri) katika kushiriki ibada zake, na tena kwenye tendo kubwa kama lile ya uzinduzi wa CD ya kwaya. Utaratibu nijuavyo uko kama ifuatavyo.

Mchungaji Mkuu (KKKT Kinondoni) ---> Mkuu wa Jimbo (Kinondoni) ---> Katibu Mkuu wa KKKT (Dayosisi) ama Msaidizi wa Askofu Mkuu (Dayosisi). Katika hili la Rostam suala la mwaliko liliishia kwa pale pale KKKT Kinondoni halikwenda mbele kwa viongozi wa juu!! Kwa hiyo katika hili kuna walakini.
 
Sasa ni Mungu gani huyo waliyomuomba akawaambia waende kumwalika RA ili awape kwaya milioni saba na na genereta?

inawezekana ni maono yao,ila ningependa kupata Maoni ya Mchungaji ni yapi?inawezekan alifuata Taratibu zote.hawa wanweza kutumia kulinda heshima ya Kanisa kwa kumkandamiza Mchungaji.

Najua kusimamishwa kwa wana kwaya kutaleta mzozo mkubwa sana,wangapi wanahcngia kwaya ila ni majambazi na wanassali makanisani.
 
Mkuu think BIG,
simple Logic,Kwani Rostam hakualikwa kama mtu binafsi?na hata Rostama liongea kama mtu Binafsi na si kama Mbunge sema aliongea mambo yanayohusu Siasa na vivyo hvyo alifanya Laizer.

Lengo si kumtetea Rostam,ila uhalali wa jambo lenyewe tu na uhalisia wa Maisaha ya kila siku katika makanisa yetu

Mkuu Gembe, nakubaliana na wewe moja kwa moja! Kosa si la Rostam Aziz, kosa ni la uongozi wa Kanisa KKKT Kinondoni. Kwanini hawakutoa taarifa za mwaliko wa Rostam kwenye uongozi wa juu? Hapa ndipo kwenye tatizo, lakini Rostam kama Rostam yeye hana tatizo!
 
Na pesa warudishe sasa!
Maana kama wamekiri it was an attempt to politically cleanse himself..Then the means he used to do so "MONEY" Should not only be unequovically condemened..But also THE MONEY SHOULD ALSO BE RETURNED inorder to validate their claim that CHURCH SHOULD NOT BE USED FOR CORRUPTION LEADERS OBJECTIVES!
THIS TIME USING MONEY TO CLEANSE THEMSELVES.
 
Mkuu Gembe, nakubaliana na wewe moja kwa moja! Kosa si la Rostam Aziz, kosa ni la uongozi wa Kanisa KKKT Kinondoni. Kwanini hawakutoa taarifa za mwaliko wa Rostam kwenye uongozi wa juu? Hapa ndipo kwenye tatizo, lakini Rostam kama Rostam yeye hana tatizo!
Ben Carson..
 
Makosa ni ya MAFISADI WOTE WALIOALIKA NA WALIOALIKWA!
Eti RA hakuwa na makosa!?
Huu upuuzi!
Yeye tena inawezekana ndie ana makosa wa kwanza kwani labda hata waumini hao labda hawakujuwa kuwa atalitumia kanisa kama jukwaa la kisiasa na kutoa vijembe kwa wazalendo.
Na PESA aliyotoa ilimpa free ride na masikini wakaziba masikio na KAZI YA IKAWA NI VIGELE GELE TUUU!
 
Mkuu think BIG,
simple Logic,Kwani Rostam hakualikwa kama mtu binafsi?na hata Rostama liongea kama mtu Binafsi na si kama Mbunge sema aliongea mambo yanayohusu Siasa na vivyo hvyo alifanya Laizer.

Lengo si kumtetea Rostam,ila uhalali wa jambo lenyewe tu na uhalisia wa Maisaha ya kila siku katika makanisa yetu


Yaani Gembe hapo umesema kweli. Inabidi tufikie mahali tuache unafiki katika kupambana na ufisadi. Maana sasa inasikitisha sana. Hawa hawa viongozi wa dini walisema mafisadi ni chaguo la Mungu. Wakaja wakati wa kiapo wakawaombea kwa Mungu awalinde. Wakiujuzulu wakawapa sifa. Leo hii mchungaji wa chini amefanya kama wakubwa wanavyofanya anasimamishwa kweli ukistaajabu ya Musa utaona...
 
Mwizi ni mwizi tu. Kuna ambao hawakamatwi, kuna walioiba juzi hawakuonekana, lakini hiyo haibadilishi kuwa wao ni nani. Kama alihonga pesa zamani bila wahongwa kujijua sio kosa lao. RA hakwepi hii hata kwa kujaribu kuhonga au kununua makanisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom