Rostam aibukia kanisani!

Rostam aibukia kanisani!

Jamani tusiwe tunakurupuka kujikatisha tamaa, mimi binafsi nimefurahi sana huyu Rostam kupata mwaliko huo maana hakika nimemfahamu vizuri kwamba alipanga kuoga sehemu salama kama kanisa. Aliyoyatoa tumeyasikia na sasa tunatafakari. KKKT safi sana.
 
Well ujumbe wa kanisa ni KUOKO ROHO, well Rostam alikuja kanisani badala ya Kanisa kumuhubiria ili kumuokoa na roho ya kifisadi linamuhukum na hivyo kumtenga; hii nadhani siyo sahii. Mimi nafikiri katika hili kanisa limekurupuka na kwenda na wimbi lakushambulia mafisadi which is good, lakini nawaomba wawe waangalifu na wasije wakatumbukia kwenye mtego. lakini kama Rostam kafanya alivyofanya na Kanisa likamkaanga, vipi kwa hao wengine wanaokumbatiwa na kanisa kwa kuwa wanachochote?... Kwa upande mwingime kwenye gazeti la leo la ‘This Day’ kuna picha ya askofu wa huko Meru na balozi wa Marekani wakifungua HIV/AIDS care and treatment center. Je, hao wamarekani ni wazuri sana au wema sana kuliko Rostam? Je, kwa kuwa wao memekuja kwa mtazamo huo ndiyo wanaonekana ni better of kuliko rostam? au ni double standards? Kanisa linabidi liende extra step kujisafisha au linafikiri waumini hawaoni hayo yanayotokea?
 
Hapo unakosea mkuu, hawa viongozi wetu ktk siasa za nchi wamekuwa wakishiriki mara kwa mara ktk hafla za dini tofauti na imani zao.

Kanisa lenyewe si mahakama wala si Bunge, narudia tena "kila nyumba ya ibada ni mahala wakutanapo wadhambi na kumlilia mungu ili awasamehe na pia kumtukuza kwa wepesi wa hasira na msamaha wake kwetu wanadamu" Amb.Mariki amekwenda mbali sana ktk hilo juu ya Rostam. Nakukumbusha siku JK alipolizungumzia suala la Kadhi ilikuwa na Ktk kanisa la hawahawa akina Mariki pale Luther House Azania Front. Nchi yetu ni moja yenye dini nyingi na makabila mengi.

JK aliinuka na kucheza ktk maazimisho ya kitaifa ya Uhuru pale Dodoma pindi kijana Bon Mwaitege alipohubiri kwa wimbo " Utanitambuaje kuwa nimeokoka?" Ni wimbo wa Injili lakini serikali iliridhia uje uimbwe ktk hafla ya kiserikali tena ktk wakati Rais wa nchi muislam.

WAKUU TUNAWEZA FURAHIA KITENDO CHA KKKKT MASHARIKI NA PWANI CHINI YA MKUU WAO WA KANISA KIJANA MALASUSA LAKINI NINAPENDA KUTOA MAANGALIZO YA MWENENDO WA ULUTHERI KTK SIASA ZETU TZ NA PENGINGINE NIANZIE NA HISTORIA YA ULUTHERI HAPA DUNIANI.

1. MARTIN LUTHER MJERUMANI NDIYE CHANZO CHA KANISA HILO BAADA YA KUHITILAFIANA NA CATHOLIC WA ROMA KTK MAMBO YAO HUKO NYUMA,ALIADHIBIWA NA MOJA YA ADHABU ILIKUWA NI KUTEREMKA KWA MAGOTI TOKA GHOROFANI ALIKO POPE MPAKA DOWN FLOOR HUKU AKITUBU KWA WAKUU, ALIIANZA HIYO ADHABU LAKINI KATIKATI YA ADHABU HIYO AKABAINI KUWA KATI KATI YAKE NA MUNGU NI BIBLIA ITAKAYOWAUNGANISHA NA SIYO POPE HIVYO AKAGOMA KUENDELEA NA ADHABU HIYO KWA MSIMAMO HUO NA AKAREJEA GERMANY NA NDIPO ULUTHERI ULIPOANZIA.

NILIWAHI KULIELEZA HILI LA UDHAIFU WA KKKKT KTK KUWASAIDIA WAUMINI WAKE PINDI WAINGIAPO KTK MAMLAKA ZA KIDINI NA NILIDIRIKI KUSEMA SALAMA YA SUMAYE ILIKUWA NYUMA YA MKAPA NA UKATOLIKI WAKE AMBAO ULIJITAHIDI SANA KUIKEMEA SERIKALI YA MKAPA KILA WALIPOPATA VIJIHABARI VIBOVU JUU YA UTAWALA WAKE,WALIWEZA KUMDHIBITI KWENYE YALE WALIOKUWA WANA HABARI NAYO HII IKIWA NA PAMOJA KUMSHAURI PM WAKE LAKINI NILIWAHI KUWAHUKUMU KKKT NA CCT KUWA HAWAKO MAKINI KTK KUWAJENGA WAUMINI PINDI WANAPOFIKIA NGAZI ZA JUU KIMAMLAKA . NINAWAKUBALI WAISLAMU KUWA SASA WAMEKUWA KAMA WAKATOLIKI ,WANAJITAHIDI SANA KUMJENGEA HALI NZURI KIUTENDAJI MUUNGWANA ILI ASIHARIBIKIWE.

UKIANGALIA WASIFU HUU UNAONA KABISA KKKT KUNA MATATIZO MKUBWA SANA, HAWA JAMAA WALIPOKEA 3MILLION ZA LOWASA KULE ZENJ BAADA TU YA KUACHIA NGAZI U-PM, MALASUSA NA MENGI WALISHIRIKI SHUGHULI HIYO NA KUNA VIJINENO VILIJITOKEZA KULE ZENJ.

NASIKITIKIA SANA UPUUZI WA KIMAADILI UNAOFANYWA NA KKKT KWA KISINGIZIO CHA VITA DHIDI UFISADI, HUKU NI KUJIFANYA MUNGU MTU ILIHALI MUNGU HANA MSHIRIKA.

KUWASIMAMISHA HAO JAMAA K'NONDONI NI KINYUME NA MATARAJIO YA WENGI NA KIBAYA ZAIDI HAYA YANATENDEKA CHINI MKUU WA KANISA LA KKKT.

LEO TUNASHANGILIA HILI KUWA WAKO SAHIHI LAKINI HATUJUI SIKU LIKIJITOKEZA KAMA HILI KWA UPANDE WA PILI WA IMANI? J E CHAGUZI ZIJAZO ZITAJIEPUSHA VIPI NA MIKONO HII YA KIDINI? BISHOP MDEGELA AMESHATAMKA KUWA HAYUKO TAYARI KUONA 2010 IRINGA INAKUWA NA MBUNGE FORM IV, NA AMEAPA KUWA ATAPANDA JUKWAANI KUPINGANA NA YEYOTE WA AINA HIYO.

WAPI TUNAENDA KKKT?
 
Sasa tutakuwa wajinga kama Rostam akiwekwa kwenye kundi la wanaolitakia mema taifa. Kanisa sio sehemu ya kutoa hukumu nadhani mahakama ni sehemu inayoweza kutoa hukumu. Mtazamo wa kanisa au mtazamo wa waumini wa dhehebu hilo na watanzania kuhusu Rostam siyo hukumu, ametufanya tumuone hivyo kutokana na vitendo vyake. .

Mkuu

Mbona mnakuwa waoga sana hukumu iko wapi?

Kusema ukweli, kwani Dowans na mdogo wake Richie walikuwa hawalipwi mamilioni ya pesa kila siku? Mangapi tunasikia kuhusu huyu bwana kwanini kama anazungumza asiende moja kwa moja kwenye point zinazohusu ufisadi wake badala yake anakuwa kama mzee wa masasi?

Si tumesikia Serikali ikisema kuwa ni Dowans na mdogo wake ni makampuni ya mfukoni?

Sasa nani alikuwa anakinga mkono kuchukua pesa?

Kama anajulikana nikisema aliyekuwa anakinga pesa ni FISADI si ni haki yangu?

Mimi nawapongeza KKKT kwa kutokumungunya maneno, mbona Mkuu Dr. Slaa, na waheshimiwa wabunge wanaotutakia maendeleo walisema moja kwa moja kuwa hawa ni mafisadi?

Tusiogope kusema ukweli pale ambapo unatakiwa katika kuokoa Taifa. Tusisubiri eti mahakama kwa sababu hakuna wa kuwapeleaka huko. Kwani ni wangapi ni mafisadi na hawajafikishwa mahakamani?

Mimi bado nitaendelea kutoa wito maana hata waziri Mkuu amesema kwamba hawatakurupuka kuwakamata, sasa kwa nini mafisadi wasipelekwe au wasijipeleke wenyewe mahakamani hili wakajisafishe huko?

Kwa nini wasumbue vichwa vya watu mara msikitini, mara makanisani, mara misibani nk, nafikiri sasa watavamia hata harusi.

Wito, serikali kama imeshindwa kuwafungulia mashitaka na kuwapeleka mahakamani basi iruhusu wananchi wahukumu wenyewe na kuchukua hatua za kinidhamu dhini ya mafisadi hii itatuondolea ghadhabu za kuwasikia wakitukejeli kila siku.
 
Hapo Tunaliona Tatizo La Wazi Kwetu Watanzania, Kkkt Wameingia Tena Mtegoni.

Hawakuwa Na Sababu Ya Kufanya Hicho Kilichofanywa Na Ndg.mariki, Huo Ni Upotofu Mkubwa Ktk Imani.

Kanisani Ni Mahala Pa Wadhambi Na Si Vinginevyo.

Kanisa Lipo Kutuunganisha Na Mungu Na Si Kututenganisha Naye.

Rostam Anaweza Kuwa Ni Mdhambi Kama Tulivyo Sote Hapa , Je Ni Nini Hatima Yetu Mbele Ya Mungu Endapo Watumishi Wa Mungu Wataanza Kututenga Na Upendo Wake??

Mariki Anapaswa Awajibike Mbele Ya Mungu Na Waumini Wote.

Rostam Aziz hakuja pale kanisani kama mwenye dhambi kuomba msamaha alikuja kujikosha na huku anajua ni mwenye dhambi kubwa tu. Angeomba msamaha kwa Mungu kanisani yangekuwa mengine.
 
Na sadaka ya Mkapa nayo ni halali? Sina uhakika kama Chenge ni muumin mzuri, hiyo itakuwa nafuu kwake maana atakuwa kaamua kuwa dini yake ni ufisadi, sio mnafiki?

Na EL je ambaye ni muumini mzuri tu au alipoenda Israel kuhiji alisamehewa. (Kama anatoa sadaka kanisani)
 
Mkuu

Mbona mnakuwa waoga sana hukumu iko wapi?

Kusema ukweli, kwani Dowans na mdogo wake Richie walikuwa hawalipwi mamilioni ya pesa kila siku? Mangapi tunasikia kuhusu huyu bwana kwanini kama anazungumza asiende moja kwa moja kwenye point zinazohusu ufisadi wake badala yake anakuwa kama mzee wa masasi?

Si tumesikia Serikali ikisema kuwa ni Dowans na mdogo wake ni makampuni ya mfukoni?

Sasa nani alikuwa anakinga mkono kuchukua pesa?

Kama anajulikana nikisema aliyekuwa anakinga pesa ni FISADI si ni haki yangu?

Mimi nawapongeza KKKT kwa kutokumungunya maneno, mbona Mkuu Dr. Slaa, na waheshimiwa wabunge wanaotutakia maendeleo walisema moja kwa moja kuwa hawa ni mafisadi?

Tusiogope kusema ukweli pale ambapo unatakiwa katika kuokoa Taifa. Tusisubiri eti mahakama kwa sababu hakuna wa kuwapeleaka huko. Kwani ni wangapi ni mafisadi na hawajafikishwa mahakamani?

Mimi bado nitaendelea kutoa wito maana hata waziri Mkuu amesema kwamba hawatakurupuka kuwakamata, sasa kwa nini mafisadi wasipelekwe au wasijipeleke wenyewe mahakamani hili wakajisafishe huko?

Kwa nini wasumbue vichwa vya watu mara msikitini, mara makanisani, mara misibani nk, nafikiri sasa watavamia hata harusi.

Wito, serikali kama imeshindwa kuwafungulia mashitaka na kuwapeleka mahakamani basi iruhusu wananchi wahukumu wenyewe na kuchukua hatua za kinidhamu dhini ya mafisadi hii itatuondolea ghadhabu za kuwasikia wakitukejeli kila siku.

Kwa taarifa ya hukakika Dowans+Rostam=Rostam Aziz
 
Ila wakati mwingine makanisa yanapelekwa Vibaya sana,Wao kama Kanisa wana uhakika Gani kama Rostam ni mwenye Dhambi?Maandiko yanakataza kuhukumu mtu ila wao wamemhukumu,

Wamejichukulia maamuzi ya kimungu,na kwa kifupi imenisikitisha sana hata kama Rostam ni Fisadi ila Dini ilipofika ni pabaya sana na watahukumiwa kwa kiasi walichokosea

Embu chukua Mfano huu mdugu ,Wakiwaalika watu wengine ambao wao wanawaona wasafi,wana uhakika gani kwamba pesa wanayotoa siyo ya wizi
 
Sawa ndugu yangu' hiyo ingekuwa sahihi kama Rastam angechanga pesa tu bila kutoa kauli yoyote, hapo tungemtetea kuwa mdhambi ameingia kanisani, lakini si kutumia jukwaa hilo kubeza yote yanayosemwa kumhusu. Ningeelewa kuwa mdhambi ameingia kanisani kama angetubu dhambi zake na kuokoka.
 
Wasalaam

Wapendwa naomba mwenye clip ya Rostam alipohutubia wanakwaya wa kanisa la KKKT Kinondoni aiattach hapa tuione tuna hamu nayo sana.

Rostam alilishukuru kanisa kwa kumwalika na akatumia fursa hiyo kueleza kuwa taifa lilikuwa likipita katika kipindi kigumu kisiasa na kijamii, na akawataka waumini waliombee ili kulirejesha katika mstari ulio sahihi.

"Nawashukuru kwa kuamua kunialika kuwa mgeni rasmi leo. Hii ni ishara kwamba mmeamua kupuuza viji-maneno na upuuzi wa vijiweni. Nafurahi kuwa miongoni mwenu…hamtuhumu, hamshutumu, hampendi wenye wivu na wenye chuki
 
Kwani wahubiri wanpoongele mambo ya UFISADI kanisani huwa wnafanya kosa lipi?

sijaona kosa la mkapa liko wapi,na hii inaonesha ni jinsi walivyo na ugomvi wao kwa wao,wamefikia hatua ya kulitumia kanisa kuchafuana?

Na hili naweza kumlaumu SPika,kwa nji moja au nyingie itakuwa amechangia sababu yeye ni mzee wa kanisa..
 
1. Wakuu msijaribu kutuchanganya hapa, Rostam na Lowassa, ni mafisadi period na ndio hasa chanzo cha ufisadi Tanzania.

2. Kama wanataka kujaisafisha na Mungu wao, hakuna sababu ya kupiga kelele wanweza kwenda kanisani wao wawili tu na Mchungaji wakamwambia Mungu matatizo yao, na sio lazima liwe kanisa la Spika.

3. Hawa watu wamezoea kuishi kwa rushwa period, hawajui anything else, wao wamezoea kuona dunia nzima iwe inazunguka arround wao kwa sababu ya mapesa yao waliyoliibia taifa letu, sasa hivi they are almost running our government, kila kitengo cha serikali yetu kinawaogopa hawa, sasa wameshituka kuwa kanisa halimo katika payroll yao ndio wamelianza.

Wa-Tanzania tusitishike na haya maneno mengi ya vibaraka wao, kuna maneno humu ukiyasoma vizuri between the lines utayaona kuwa yameandikwa na vibaraka wao, matatizo ya makanisa yetu na connection yao na Mungu, it is none of our business hapa JF, our business ni taifa tu,

Kwenye hili la Lowassa kwenda kutengeneza njama na baadhi ya viongozi wabovu ndani huko KKT na kuweka njia ya Rostam kwenda huko kama mualikwa na kutoa hela, ni nothing but Rostam kwenda kutoa rushwa kwa kanisa na kutaka kulitumia kwa ajili ya kujisafisha kisiasa, tabia ambayo wao wawili Rostam na Lowassa, wanaonekana kuijua sana kuliko anything else, yaani ya kutoa mapesa kwa wenye shida ya pesa ili wajisafishe,

Tunasema tena kwa nguvu sana kuwa huu wao ni uhuni kwa taifa tena wa mchana na hatupendi kabisaa baadhi yetu sisi wananchi kwa sababu ukisoma hii topic utaona kuwa kuna wanaoukubali huu ujinga, Mkapa alipoamua kuchukua mpango wa mtandao na kuwapa power, na yeye pia alikimbilia kwenye mkutano wa viongozi wa makanisa kuhalalisha uhuni wake, yaani ufisadi wake, sasa na hawa tena wanajaribu kufuata njia hiyo hiyo, tunasema kuwa warudishiwe hela zao wakampe Serukamba,

Nyoka ni nyoka tu, hata akija kanisani hawezi kubadilika akawa kinyonga, hawa wahuni wafukuzeni huko kanisani! Na nyinyi vibaraka wao msitubabaishe hapa na maneno mengi ya ujanja ujanja tunawajua tenma vizuri sana pamoja na majina yenu ya bandia hapa tunaweza kuwasema hapa wazi wapuuuzi nyie!
 
Huyo Mchungaji wa Usharikwa wa Kinondoni alikuwa na nia ya kuukumbatia UFISADI kama sio tamaa ya pesa na kwa nini hajamshirikisha Askofu wake katika kumwalika RA tena mtu wa dini nyingine? Heko Askofu Malasusa na wana-KKKT kwa kung'amua hilo mapema.
 
Huyo Mchungaji wa Usharikwa wa Kinondoni alikuwa na nia ya kuukumbatia UFISADI kama sio tamaa ya pesa na kwa nini hajamshirikisha Askofu wake katika kumwalika RA tena mtu wa dini nyingine? Heko Askofu Malasusa na wana-KKKT kwa kung'amua hilo mapema.

Conduct yourselves wisely toward outsiders - Col. 4:5
 
NASIKITIKIA SANA UPUUZI WA KIMAADILI UNAOFANYWA NA KKKT KWA KISINGIZIO CHA VITA DHIDI UFISADI, HUKU NI KUJIFANYA MUNGU MTU ILIHALI MUNGU HANA MSHIRIKA.


Mkuu kwa hili natofautiana na wewe 100%. Huwezi kusema tamko la KKKT ni upuuzi, hawa viongozi wa kanisa wana haki ya kusimamia na kurekebisha kasoro zozote zinazojitokeza kwenye kanisa lao. Sehemu ya taarifa iliyosema

"KKKT na wale wote wenye mapenzi mema na nchi yetu ambao kwa namna moja au nyingine wamekwazwa na tukio hili. Jukumu la Kanisa ni kuokoa roho za watu na si kukumbatia mafisadi na wala rushwa."

Nakubaliana na wewe sehemu hii ya taarifa iliyotelewa na KKKT inaweza kutafsiriwa kinyume, lakini KKKT hawako responsible na tafsiri ambazo watu wanajijengea wenyewe watakavyo.

Ni muhimu tuelewe kuwa kilichowastua Watanzania na kupelekea KKKT ni kauli ya Rostan Aziz kwenye Madhabahu ya Kanisa, kauli ambayo ilikuwa na lengo la kujisafisha machoni mwa watanzania. Ni hii kauli iliyotokana na tabia chafu ya Rostam Aziz iliyopelekea kanisa kujitenga naye. Sasa iwapo Rostam Aziz anataka kujisafisha anaweza kwenda Mahakamani au atumie Bunge.


KUWASIMAMISHA HAO JAMAA K'NONDONI NI KINYUME NA MATARAJIO YA WENGI NA KIBAYA ZAIDI HAYA YANATENDEKA CHINI MKUU WA KANISA LA KKKT.

WAPI TUNAENDA KKKT?

Hapa mimi naona umefikia hukumu pasipo kujua kwa nini wamesimamishwa. KKKT ni lazima ifanye mambo yake kwa miongozo iliyojiwekea hata kama wakati mwingine itakuwa kinyume na matarajio ya wengi. Iwapo hao jamaa wamefanya kosa katika process ya kumualika Rostam Aziz basi ni lazima wawajibishwe kwa mujibu wa taratibu za KKKT. Tuwe tusichange maamuzi ya KKKT na maamuzi ya kisiasa, na kutegemea kuwa wafuate “matarajio ya wengi”.

Mimi naunga mkono kauli ya KKKT kwa 100%. Huu ni wakati mgumu kwa Taifa letu sababu hatujui kwa 100% ni nani mzalendo wa kweli na nani ni adui. Hivyo juhudi zozote zinazofanywa na watu, vikundi au jumuiya pamoja na za kidini katika katika kulinda heshima ya Taifa letu ni vizuri tuzikaribishe.

Binafsi, nimesubiri miaka mingi kusikia viongozi hawa wa kidini wakikemea tabia chafu za baathi ya viongozi wetu. Nimefurahi kuwa sasa wokuvu wa kweli umeingia Tanzania. KKKT wamefungua njia, wengine watafuata kwa vitendo……

Naomba kuwakilisha.
 
Jamani inaonekana jamii bado twajichanganya sana. KKKT wanamjenga huyu RA kwani sioni sababu yeyote ya kutoa tamko hilo tena na wazee ambao ni wa kanisa. Kwani kanisa hilo si ndo mgogoro kibao ambao UFISADI lazima ni sehemu ya chanzoooo???
wasiwaonee wanakwaya kwani wanajitafutia riziki pamoja na kumtukuza muumba.
KKKT mashariki wamepotokaaaaaaaaa.....Yesu mwana wa Mungu alikuja kwa ajili ya wadhambi sasa kama RA ni kati yao sisi ndani ya kanisa hatuwezi kumhukumu TUMWOMBEEE AOKOKE KABISAAA. ITAKUWA NI MWANZO MPYA WA UFUFUKO WA MAADILI KATIKA UMMA. kulaumu hakujengi tena hukumu ambayo wa kuitanzua ni waumini. ufisadi umetapakaaaa mnooooo kuanzia..UTUMISHI WA UMMA(HUDUMA MBOVU), VIONGOZI WAWAKILISHI WANAFIKI(REF DK SLAAA NDANI YA BUNGE TUTETEE MASLAHI YA WANANCHI). Jamiii ingamue na kuchukua hatua stahili mapema kurukia mambo yasiyojenga utaratibu ni kupoteaa.
 
Ok sawa lakini mbona Kanisa halikumsimamisha Askofu Laiza wa Diyosisi ya Arusha Mkoani alipokwenda kumpokea Lowasa alipotinga Moduli baada ya kujiuzulu? kanisa halikusema lolote!!! sina maana lisiseme kwa yaiyotokea kinondoni, ila kwa sasa limejikanganya na kujiweka mahali pagumu. waaumini tunaangalia kama lita-maintain misimamo huu mpaka lini!!! Mungu atasaidie kanisa lisijemeguka na kuwatosa wenye imani ndogo!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom