SEE ME
SEHEMU YA 28/50
SEASON THREE
Age.............................18+
MISSION X
*******
Sikujiuliza maswali mara mbili nikampiga risasi ya mguu Mr zengo na akashuka chini kama mzigo na akaanza kulia kwa uchungu.
" Unataka nini?". Akaniuliza huku akishika mguu wake nilioupiga risasi, ulikuwa mguu wa kushoto nikamsogelea na kuinama kisha nikabinya sehemu ile yenye tundu la risasi na mdomo wa bastola nikawa nasiginia hapo kwenye kidonda akapiga kelele kwa sauti kuu na damu zikaanza kumchuruzika kwa wingi kama chemchem ya maji. Nikashika ule mguu na kuanza kumburuza kwenda kule kwenye kale kajumba kadogo ka zamani, nikamburuza na kufanya suti yake ya gharama kuharibika, nikamkokota mpaka ndani ya kajumba hako ambako nishaanda kila kitu nachohitaji, kalikuwa kamejificha sana kwenye mitimiti mingi iliyokuwa eneo ilo, nikawasha taa za chemli zilikuwa nne ambazo nilikwisha zitia mafuta ya kutosha na chumba kile kikajaa mwanga wa kutosha na kufanya kila kitu kuonekana
" kama ni pesa sema nikupe". Akazungumza, sikumjibu nikachukua kisu kikubwa na kumsogelea mpaka pale chini, nikainama na kutoa kifaa kidogo mfuko wa nyuma wa suruali yangu, kilikuwa ni kifaa cha kumkagua mwili mwake au sehemu yeyote ya nguo yake kama angekuwa na kifaa chochote kile ambacho kingewajulisha walinzi wake sehemu aliyopo boss wao, nikaanza kukipitisha juu ya suti yake na kikapiga alamu upande wa kushoto wa kifua chake, nikachana suti yake kwa kisu kisha nikaona kifua chake ambacho kilishaanza kushuka kutokana na umri wake kwenda nikaona sehemu iliyoshonwa na nyuzi sikujiuliza mara mbili nikaichana na ncha ya kisu na akapiga kelele za maumivu kwani hakukuwa na ganzi, damu zikamtoka nikaingiza kidole na kupekechua na nikatoa cheap ndogo mithili ya memory kadi ilikuwa ikiwaka waka nikaikanyaga na ikazima, nikatoa saa yake ya mkononi nayo nikaivunja simu yake nikaizima na kutoa laini zote.
" unataka nini?".
" Mary yuko wapi?". Sauti nzito ikanitoka na akatoa macho kama mjusi kabanwa na mlango wa chooni.
" weee..we nani?".
" Israel". Nikamjibu na kuchoma kifua chake upande wa kushoto na kisu kikazama mita ndogo akapige kelele na kuanza kulia kwa maumivu
" naagiza askari wangu wanamleta". Akazungumza kwa shida
" waambie namuhitaji mary ndiyo watakupata wewe ". Nikazungumza na kutoa kile kisu na akapiga kelele na kuanza kugalagala chini huku akilia kwa sauti iliyojaa maumivu makali.
" wewee ni nani sitaki kuhamini kama wewe ni Randy". Akazungumza huku akinikazia macho na kunitizama kwa kunikagua lakini alishindwa kunijua maana madaktari walifanya kazi kubwa mno ya kunibadili umbile langu la sura,
" wee nani?". Akazungumza tena na mara hii akanikazia macho zaidi.
" haaaa me kum* la mama yako". Nikamjibu na kumtia ngumi ya pua na kufanya ashike pua yake na kutizama viganja vyake akaona damu, akauma meno kwa maumivu na akanitizama kwa huruma, aliona sikuwa na huruma kabisa, nikachukua simu yangu
" taja namba za mtu wako unayemjua".
"Sawa" akanijibu na akataja namba nikaziandika na kupiga namba hiyo iliyopokelewa kwa haraka
" haloo". Sauti ikasikika ya mwanamke alikuwa ni X moyo ukapiga paah kwani namuogopa kupita maelezo.
" boss yenu niko naye". Nikazungumza kwa sauti nzito ambayo nilijua X hawezi ntambua kiurahisi.
" Unataka nini? ". Akazungumza
" namuhitaji marry". Nikazungumza na kumpa simu mr zengo akaichukua na nikamuwekea bastola kichwani.
" Fanyeni atakavyo mchukueni mary mumlete kwake".akazungumza kwa shida na nikachukua simu.
" Mleteni mary maeneo ya Daraja la MAGU, kesho saa moja usiku tubadilishane na mtu wenu mkifanya chochote kile nitamuua". Nikazungumza na kukata simu kisha nikampiga picha mr zengo na kutuma wasapu ile namba maana ilikuwa ya wasapu pia, nikaifuta na kuiblock nikatoa laini yangu na kuweka mfukoni.
" Anaitwa X atakukata kata vipande vipande vipande hahahaha". Mr zengo akazungumza na kucheka kwa dharau.
" X atakuua kijana hahaha pole sana". Akazungumza nikamsogelea na kumpiga shingo yake akazima, nikachukua bandeji na pombe kali nikamwaga kwenye kidonda chake cha mguu ile pombe kisha nikafunga kile kidonda na bandeji,nikamwaga pia pombe ile kifuani na kuchukua tape (gundi ya karatasi jina limenitoka)na bandeji nikagundisha kisha nikachukua kudu na kufunga miguu na mikono yake....
" MISSION X ". Nikazungumza na kupiga meza kwa nguvu mpaka nikaumia mkono, kwani nilijilaumu kwanini ule muda kwenye gari sikumtomba X, nilimuacha na kama kesho nikienda ni hatari lazima ataniua maana yule haonekani, ilinibidi nilale naye ili nguvu zake zipotee asiweze kupotea, sasa nilihitaji kulala na X leo au hiyo kesho kabla ya saa moja usiku...
" MISSION X " . Nikazungumza na kutingisha kichwa kuwa lazima nilale naye leo au kesho nikatizama muda na kukuta ni saa 6 kasoro usiku.
" X nakutomb**". Nikawaza na kutoka ndani ya jengo lile dogo nikafata pikipiki yangu na kupanda kisha nikaitoa baru, taa za chemli nilizima zote kumuacha yule mzee ambaye masaa sita yajayo lazima atashtuka, nikafika napokaa na kwenda bafuni nikavua gloves na kuzitupa kwenye sinki la kuogea, kisha nikafungulia maji ya bomba la juu na kusimamapo na yakaanza kunimwagikia mwilini mwangu huku nikiwa na nguo zangu, nikalowa huku mawazo yakiniandama nikatoa kadi mfukoni aliyonipa X ulikuwa na namba zake na ilikuwa bahati nzuri ya kisasa hata ikilowa maji nikatoa simu yangu mfukoni nayo ilikuwa ya kisasa zaidi, nikatoka bafuni na kuelekea chumbani huku nikiwa tayari nishavua zile nguo, nikachukua laini yangu nyengine yenye sms na dakika za kutosha nikaweka kwenye simu na kuandika namba zile za X.
" Mambo". Nikatuma meseji huku nikisubiri kujibiwa, haikujibiwa mpaka nikapitiwa na usingizi,
************
Kelele ya notification ( arafa)ikafanya nishtuke toka kwenye dimbwi zito la usingizi nikatizama saa na kukuta ni saa kumi za usiku au tuseme alfajiri, nikafungua sms na kukuta namba ya X
" Powa nani?". Nikatabasamu huku uso ukiwa na huzuni kwani leo saa moja nitakipata cha mtema kuni kama nisipotimiza hitaji langu.
Nikatulia kama dakika kumi nikaijibu
" Mmh beiby me ally". Nikatuma sms kama dakika 2 ikajibiwa
" ooh ally nambie mzima huko".
" eeh vipi wewe lakini".
" me mzima tu leo niko bize sana ally"
" Ujue nimeshindwa kulala mwenzako"
" mmh kwa sasa sipo vizuri". Akanijibu
" nateseka rose na penzi lako kwanini hunipi nafasi japo kutuliza hisia zangu".
" Mmh".
" nakupenda rose usiku nimeshindwa kulala kwa amani nimefikiria sana lile tukio".
" mmh una maana gani lakini?".
" nakuhitaji rose ata sasa hivi nifanye kile nilichooanzisha nimegundua nilifanya kosa kukuacha vile".
" mmmh kwa sasa hapana maana kuna kazi moja tu naenda kufanya ally". Akanijibu na kufanya nimeze mate kwani nitachinjwa leo
" lisaa tu rose nakuhitaji mpenzi wangu nahitaji sana ety" nikatuma txt na nikapiga na simu hapo hapo.
Akapokea
" mmh ally nambye".
" nielwe ety yani mara moja tu nagusa mpenzi wangu nakuhitaji sana ety me nakupenda sana rose yani sipo sawa kabisa".
" Nielewe". Akazungumza kwa ukali na akakata simu.
" Duuuh leo". Nikawaza, nikanyanyuka toka kitandani na kuopga tena ile namba ikaita bila kupokelewa
" Ukimuomba mwanamke jaribu zaidi ya mara elfu moja maana wewe kwa muda huo ndiyo unahitaji ukishapiga anza na wewe kumlingia sasa, ila kwa kipndi ajakupa omba sanaaaa tena na tena na tena". Maneno ya mwalimu wangu mnoko yakaninijia kichwani yalikuwa maneno ya don john, kuna kipndi mary alinisumbua kunipa showa kipindi bado naanza naye mahusiano na don john alinishauri kuwa niombe sanaaa.
" najaribu"
Nikazungumza na kuanza kutuma sms za kubembeleza sms zenye hisia kali zaidi sms za kulilia penzi lake, sms za kuhitaji joto lake nikatuma sms kama 15 kisha nikatulia.
Nikapiga chai chapu chapu iliyokuwa imeandaliwa na mfanyakazi wa kiume ambaye nakaa naye hapo yeye alikuwa mlinzi wa getini, alikuwa anajuana na waziri aliyenipa kazi.
" chai tamu sana dogo". Nikazungumza na akatabasamu nikatizama saa na kuona ni saa 2 hasubuhi
" nahitaji kwenda kule na chakula" . Nikawaza na kisha kutoka nikaenda kwenye gari na safari ya kwenda hotelini kuchukua chakula ikaanza, simu ikapigwa na kukuta namba ya waziri.
" Shikamoo mzee"
" marahaba randy kwema"
" ndyo mkuu"
" za chini chini mr zengo ametekwa bila shaka ni wewe". Akazungumza.
" ndiyo mkuu"
" usimdhuru kama ni mke wako ukimpata sawa ila huyo mzee muache utapata matatizo".
" lakini yupo kwenye plan zetu"
" nafahamu ila usimuue kumbuka bado tunafatilia kutaka kujua sura kamili ya mtu aliyetoa amri ya raisi kuuwawa miaka iliyopita na akauliwa".
" nafahamu mkuu"
" hao watauwawa na sheria". Akazungumza na kukata simu
" *** you" nikatukana, ujumbe ukaingia kwenye simu yangu,
" okay tukutane saa 4 utakaponambia nije mana me sijuhi chochote nipo". Nikafurahi kwani ujumbe huo ulikuwa ukitoka kwa X
" NAENDA KUIPIGA"
" MISSION X COMPLETED". nikazungumza kwa furaha.
*****************
ITAENDELEA..........
SEE ME
MISSION X
( TRH28 takuwa free kabisa ila kila nikipata muda nawakumbuka)
SEASON THREE