Riwaya: See Me (Nione)

Riwaya: See Me (Nione)

hancy Abdon

Member
Joined
May 24, 2026
Posts
85
Reaction score
58
THE STORY MASTER.
Mapenzi,Ujasusi,usaliti na mambo yasiyotazamiwa. BY HANCY ABDON

"SEE ME"

SEHEMU YA KWANZA 1/1O
***** ******
"Mpigie simu Randy mara moja mtumie location hawahi sehemu ya tukio".

"Boss hata me naweza hiyo kazi nipe tafadhali". Jamaa mmoja akazungumza huku akimtizama boss wake kwa ukakamavu lakini boss wake akatingisha kichwa kumkatalia.

"Fanya nilivyokwambya". Akazungumza na akaingia ndani ya gari na jamaa akaenda kufunga mlango huku akiuma meno kwa hasira kwani hakufurahishwa na maamuzi ya boss wake aliyeyatoa juu yake kwani alihitaji kifanya kazi hiyo ili kumuonesha boss wake kuwa naye ni bora kama Randy au zaidi yake. Akachukua simu na kumpigia mtu aloelekezwa ampigie ambaye ni randy. Simu ikaita na ikapokelewa.

"Order toka kwa boss nakutumia location nenda sehemu hiyo mara moja alaotekwa amepatikana kamuokoe". Jamaa akazungumza na akakata simu bila ya randy kusema kitu kisha akatuma location ya eneo ambalo inasadikika kuna mtu alitekwa yupo eneo hilo. Akafungua mlango na akaingia ndani ya gari na kuvaa mkanda

"Tayari boss nishampata". Akazungumza na boss akatikisa kichwa,alikuwa ni mwanamume wa makamo miaka 53 hata mvi zake zilikuwa bado hazijaanza kukolea kichawani, msafara wa magari mawili ukaanza kutoka eneo hilo la hotel kubwa ya kifahari yenye hadhi ya nyota tano ambayo kabwela kama sisi hatuwezi kuingia kirahisi kutokan na ulinzi mkali pamoja na hadhi ya hotel hiyo ambayo vyakula vyake au chochote kinachopatikan ndani ya hoteli hiyo bei yake ni ghali zaidi.

Randy akatizma location na akajikuta akiguna na kutingisha kichwa.

"Duuh tanga". Akazungumza na akanyanyuka toka kitandani na kumtizma msichana aliyekuwa amelala naye,akahamisha macho na kutizama saa ya ukutani na kukuta ni saa kumi za usiku.

"Itanichukua masaa mangapi toka dar mpaka tanga aseeh wangeniacha nilale". Akzungumza na kufanya binti alokuwa amelal naye anyanyuke kwa uchovu huku akipikinya pikinya macho akamtizma mteja wake anayevaa nguo harka harak taribu akawasha taa kubwa na kufanya chumba kiwe na mwanga mkubwa tofauti na ule wa mwanzo ambao taa ya mezani ilikuwa inawaka mwanga hafifu.

"Vipi ujapenda huduma yangu mbona mapema randy leo siyo kama siku zote". Mwanamke huyo akazungumza na akashuka kitandani taratibu na kumsogelea randy ambaye alikuwa anamalizia kuvaa viatu.
"Vipi leo ".

"Nawahi sehemu hela yako hiko hapo tutawasiliana Mage". Randy akazungumza na kumsogelea mage na kumnyonya denda la nguvu huku akibinya binya kiuno cha mwanamke huyo ambacho kilijaa shanga nyembamba na kufanya kivutie kila mtu akitizamapo. Akamuachia na kuchukua simu yake juu ya meza ya kioo pamoja na funguo ya gari iliyokuwa hapo mezani.

"Tukikutana nakuhitaji pesa yangu haijaisha ".akazungumza na kugusa kitasa cha mlango akajaribu kuminya ila akikufunguka akageuka na kumtizma mage ambaye akamletea funguo na akafungua mlango na kumrushia kisha kumuaga kwa busu la mbali, moja kwa moja akaanza kupita kwenye korido ya geust hiyo huku akipishana na baadhi ya watu ndani ya geust hiyo ambao wengi walikuwa wanatoka kuzini.

Akajikuta akishtuka baada ya kumuona mke wake akitoka ndani ya geust hiyo na mwanamume mmoja ambye ki umri alikuwa ni mkubwa kumzidi mke wake hakuamini macho yake alihisi ni ndoto akasogea kwa ukaribu zaidi huku akijibanza kwnye kona za ukuta wa geust hiyo kubwa jijini hapo alitaka aone ni yeye kweli au kamfananisha kadiri alivyokuwa akisogea ndivyo moyo wake ulizidi kuingiwa na uchungu wa ajabu akamtizma mwanamume mwenye mke wake hakufanikiwa kumuona sura yake kwani alivalia kofia kubwa nyeusi aina ya cow boy iliyoficha paji lake la uso mpka macho yake. Akawafatilia na kuwaona wakifika mpaka kwenye lifti wakapanda ndani ya lifti na ikaanza kushuka chini...

Randy akachomoa bastola yake aliyokuwa ameibana kwenye kiuno chake na mkanda wa suruali yake kifua kilijaa hasira na wivu ulioambatana na jazba pamoja na harufu ya damu sas aliwaza kuwaua wote wawili akasahau yeye pia katoka kumcheat mke wake..

ITAENDELEA USIKOSE SEHEMU YA PILI YA MKASA HUU WA KUSISIMUA JE NINI KITATOKEA ENDELEA KUFATILIA MPAKA MWISHO
*******

SEE ME"​
 
SEE ME

SEHEMU YA PILI 2/10

RANDY akachomoa bastola yake aliyokuwa ameibana kwenye kiuno chake na mkanda wa suruali yake,kifua chake kilijaa hasira na wivu ulioambatana na jazba pamoja na harufu ya damu sas aliwaza kuwauwa wote wawili akasahau yeye pia katoka kumcheat mke wake..

ENDELEA

Kitu alichoweza kujua ni kuwa yule mtu mwenye mke wake ni mtu mzima yani mzee kutokana na anavyotembea na umbo lake lilivyo ila sura yake hakufanikiwa kuiona mpka wanapopanda kwenye lift na kuanza kushuka chini, Randy hakuhitaji kupanda lifti kwa haraka hakanza kuteremka chini kupitia ngazi za hotel hiyo huku bunduki yake akiwa amerudisha kiunoni ili wafanyakazi au watu atakaopishana nao wasiweze kuona chochote na kuhamaki alitaka kupiga tukio na kupotea kimya kimya kwani ilikuwa ni alfajiri sasa ya saa 11 giza lilikuwa bado lipo, akazidi kushuka kwa kasi kwenye ngazi huku akipishana na watu ambao baadhi aliwagonga kikumbo na kufanya wamshangae.

Sasa akafanikiwa kufika chini na kumkuta mke wake na mzee huyo wakipanda kwenye gari nyeusi ilikuwa ni hammer ya kifahari milioni kama 600 na ndani kulikuwa na dereva maana alitangulia mzee kuingia nyuma ya siti ya gari baada ya kufunguliwa mlango na mwanamume mmoja aliyepanda hewani mithili ya wapiganaji wa miereka wa marekani WWE. Alikuwa ameshachelewa ata angechomoa bastola wahusika wote walikuwa tayari washapanda kwenye gari.

Akataka kuchomoa bastola ila simu yake ya mkononi ikaita akaitoa mfukoni na kukuta jina limeseviwa BOSS. Ndita zikajichora kwenye uso wake akatamani kuiacha mpaka ikate ila ilikuwa ni lazima apokee simu hiyo kwani huyo ni mkubwa wake akashusha pumzi na kupunguza hasira huku akishuhudia gari lile likiondoka bila ya yeye kufanya kitu.

"BOSS". Randy akazungumza kwa sauti ya chini kidogo
"Uko wapi ushaanza safari kwenda tanga".
"Ndiyo kiongozi".
"Mbona simu yako inaonesha bado upo dar tena hotelini". Sauti ikasikika na kufanya randy akunje sura kwani hapendi kufatiliwa katika majukumu ya kazi
"Samahani bossi ndo natoka".
"Hebu changamka randy ili dili nishachukua na pesa ya watu". Akafoka
"Sawa ". Randy akazungumza na kukata simu mawazo yakamzonga kuwa afanye kazi ya kuokoa mateka aliyeko tanga au amfatilie mke wake na huyo mtu anayemcheat

"Randy tulia". Akazungumza na kujaribu kushusha presha ila akajikuta anazidi kuumia zaidi, akasogelea gari yake na kufungua mlango na kupanda huku akitizma mafuta ya gari hilo.

"Nafika tanga " Akazungumza na kutizma location iliyoko kwenye simu yake akaondoa gari baada ya kupangua gia huku akili yake ikimtuma kwenda jijini tanga kukamilisha kazi hiyo ilompeleka kuokoa mateka wakiwa wao ni kundi la kukodi amabalo ni la siri serikali haifahamu zaidi ya viongozi baadhi wanalolitumia katika kazi zao za siri kama kuua wasumbufu wa serikali kisirisir au kuua mtu yeyote yule watakayetumwa kuua, na linamilikiwa na kiongozi mkubwa ambaye mpaka sasa hakuna anayemfahamu na ukienda kinyume na wao wanakuua mara moja..

RANDY akazidi kukanyaga mafuta huku jaziba zkimuingia mwilini mwake sumu kali ikazidi kujengeka moyoni mwake juu ya mke wake.

"Sasa mary hapo mume wako hatakuwa salama yani ilikuwa jambo dogo tu we kulala na mimi" Mzee mwnye kofia yake kichwani inayoficha sura yake akazungumza huku akiwa anapekenyua pekenyua simu yake akaplay video na kumuonesha mary ambaye akajikuta akishtku kwani alikuwa kitandani yeye na mzee huyo uchi wa mnyama tena akiwa ameweka kifo cha mende akujua alirekodiwa muda gani.

"Nikiwa na hitaji ukikataa video hii tamuonesha mume wako Randy". Mzee huyo akazungumza na kufanya mary machozi yaanze kumtoka.
"Hayakuwa makubaliano yetu lakini eeh". Kwa uchungu mary akazungumza
"We mtoto una utamu wa kipekee kwanza ni mzuri kupindukia toka siku tulipokutana kwenye mgahawa wako ule nilivutiwa na wewe na chakula chenu kitamu sana aseee na mume wako kajitahidi sana kukufungulia mgahawa mkubwa vile ila tambua hawezi kukumiliki mwanamke mzuri kama wewe". Mzee huyo akazungumza huku akimfuta machozi mwanamke wa randy.

Mary akazidi kuumia na kulia kwa uchungu kwani hakuamini kama kuna siku atamsaliti mume wake hakutegemea kuwa angelal nje ya nyuma yake lakini alifanya hivyo kumlinda randy baada ya kupokea vitisho vikali toka kwa mzee huyo ambaye mpaka alimuonesha picha za mume wake akiwa katika mizunguko yake kuwa anamfatilia na kama akimwambia basi angeua familia yake na kumuacha randy kitu ambacho mary hakuwa tayari kuona kikitokea..

"Unajua mume wako anafanya kazi gani".. mzee huyo akazungumza na kushika paja la mary

ITAENDELEA USIKOSE SEHEHEMU YA PILI YA MKASA HUU WA KUSISIMUA UNGANA NA MIMI MPAK MWISHO WA SIMULIZI HII JE HUYO MZEE NI NANI NA RANDY ATAMUUA MKE WAKE.......?

"SEE ME "​
 
Horror - Macabre_1 (1).jpg


SEE ME..

SEHEMU YA TATU (3/10)

"Unajua mume wako anafanya kazi gani?" Mzee yule alizungumza huku akisogeza mkono wake na kushika paja la Mary.

Akawa anampapasa taratibu mithili ya mtu anayekanda unga wa ngano—bila papara ya kuwahi wateja, wala njaa ya kutaka kula yeye mwenyewe. Mary alimtazama kwa hofu, kisha akatingisha kichwa kuashiria kuwa anajua kazi inayomfanya Randy ashindwepo nyumbani.

"Waooh! Kumbe anafanya kazi?" Mzee yule alimuuliza huku akivua kofia yake na kumuachia Mary nafasi ya kupumua. Alikuwa ni mzee mwenye kipara kilichong'aa bila chembe ya nywele. Kidevu chake kilijaa ndevu fupi za mvi zilizokolea weupe kama chokaa. Alikuwa mweupe wa ngozi, na juu ya paji la uso wake kulikuwa na kidoti cheusi palepale palipozoeleka kusugunika wakati wa kusujudu—alama tosha kuwa mzee huyo alikuwa mcha mungu wa kusali kila siku, tena kwa msisitizo wa mashehe wa msikitini.

"Ni Meneja wa Madini," Mary alidondosha maneno hayo kwa sauti ya chini sana, iliyosheheni unyonge. Mzee yule aliangua kicheko cha dharau huku akimkodolea macho Mary. Mary alikuwa amepooza kwa uoga; akili yake yote ilikuwa juu ya ile video ya siri waliyomrekodi. Hakutaka kabisa kuharibu ndoa yake ambayo ilikuwa imetimiza mwaka wa pili tu, japo kwa sasa alikuwa ameshakutana na misukosuko ambayo hakuwahi hata kuiwaza katika maisha yake yote.

"Oooh, Randy ni meneja wa madini? Kumbe pesa anazo!" Mzee alizungumza huku akichomeka simu yake mfukoni, huku tabasamu la kinafiki likichanua usoni mwake. "Usiniogope Mary. Nitakupa kila kitu na nitakufanya uwe wangu. Kwa sasa nakupa muda wa kujifikiria. Usisite kuniomba chochote, na nitakupeleka kila kona ya dunia hii unayotaka, sawa mama?"

Mzee aliongea kwa sauti ya upole ya kuliwaza, upole uliotofautiana kabisa na ukali wake wa mwanzo. Akatupia jicho saa yake ya mkononi; mishale ilikuwa inasomeka saa moja na dakika zake.

"Sasa tunakushusha uende kwako, lakini kumbuka makubaliano yetu," alisisitiza huku macho yake yakisafiri kwenye urembo wa binti huyo wa kitanzania. "Naomba hiyo bahasha," mzee aliamuru akimwambia dereva wake ambaye alikuwa anapaki gari pembezoni mwa barabara, mita imposes kama ishirini kabla ya kufika getini kwa Randy.

Dereva aligeuka na kumkabidhi bahasha nene iliyokuwa imetuna vilivyo pale kwenye siti ya mbele. Mzee akaipokea akiwa siti ya nyuma na bila kusita, akamnyoshea Mary. Mary alisita kwa sekunde kadhaa kuipokea.

"Chukua, hii ni zawadi yako," mzee alisisitiza. Mary alijishauri moyoni, kisha akanyosha mkono na kuichukua; hofu yake ilikuwa ishaanza kuyeyuka na kubadilika kuwa unyonge. Mzee alimsogelea karibu na kumkumbatia kwa hisia kali sana. Ilikuwa wazi kuwa mzee huyo alikuwa amezama kabisa kwenye dimbwi la mahaba kwa binti huyo tangu siku ya kwanza alipomwona. Kwake yeye, Mary alikuwa kiumbe wa kipekee mwenye kila sifa ya urembo hapa duniani. Bila kupoteza wakati, alimshika Mary mashavu yake na kumnyonya midomo yake kwa nguvu, kisha akambusu kwenye paji la uso na kumtakia mapumziko mema.

"Tutawasiliana... I LOVE YOU," mzee alizungumza kwa lafudhi ya kimahaba.
Mary alishuka kwenye gari huku moyo wake ukiwa mzito na kifuani kukiwa hakuna amani hata chembe. Alijihisi kuwa mtu mchafu asiyestahili tena kuitwa mke wa mtu; alijihisi mwenye hatia kuu. Aligeuka nyuma na kutazama yale magari mawili yakiondoka kwa kasi kuelekea kusikojulikana. Hadi sasa, alikuwa hamfahamu yule mzee ni nani. Akili yake ilirudi nyuma, ikakumbuka siku ya kwanza mzee huyo alipomfuata akiwa na bastola, akamwonyesha picha ya Randy na kumtishia kuwa akiripoti sehemu yoyote, huo ndio utakuwa mwisho wa maisha ya Randy...

* TANGA *

Ndani ya jiji la Tanga, kuelekea vijiji vya ndani kabisa ambako miundombinu ya kisasa bado haijafika, barabara zilikuwa za vumbi, zimejaa makorongo na mashimo makubwa ya kutisha. Gari aina ya Toyota Land Cruiser ya rangi ya kijivu ilikuwa ikitembezwa mchapo mithili ya magari ya mashindano ya Safari Rally. Gari zima lilikuwa limefunikwa na vumbi jeneza pande zote, huku magurudumu yake yakizunguka kwa kasi ya ajabu bila kujali ubovu wa njia. Ilikuwa dhahiri kuwa mtu aliyekuwa nyuma ya usukani alikuwa ama anawahi eneo la dharura, au alikuwa amechanganyikiwa vibaya sana.

Huyo alikuwa Randy. Alikuwa akielekea kukamilisha kazi yake huku moyo wake ukiwa umebeba hasira kali na sumu ya usaliti dhidi ya mke wake, Mary.

Alitupa jicho kwenye mfumo wa ramani (GPS/Location) kwenye simu yake iliyokuwa imethibitishwa mbele kidogo ya usukani. Taratibu, alianza kupunguza mwendo wa gari lake. Akakata kona kushoto na kukutana na pori nene lililojaa vichaka vya kutisha. Pembezoni mwa pori hilo, kulikuwa na gari lingine jeusi limepaki.

"Washenzi wako hapa!" Randy alizungumza peke yake kwa sauti ya chini iliyojaa chuki. Alisimamisha gari lake umbali wa mita 20 nyuma ya lile gari lingine, ambalo sasa aligundua kuwa ni Toyota Noah ya rangi nyeusi tii.

Alifungua droo ya mbele ya gari (dashboard) na kutoa bastola ndogo—silaha ileile aliyokuwa anataka kumpiga nayo mke wake na yule mzee kule jijini. Alikagua chemba ya risasi (magazine) na kuridhika kuwa zilitosha kabisa kwa ajili ya kazi iliyokuwa mbele yake. Japo hakuwa anajua idadi kamili ya watekaji waliokuwepo eneo lile, alijiamini kupita kiasi kutokana na mafunzo makali ya kijeshi na mapigano aliyowahi kuyapitia nchini JAPANI.

Alifungua mlango wa gari taratibu, akashuka na kuufunga kwa weledi bila kupiga kelele.

"Nyoosha mikono juu, weka bastola chini na upige magoti!" sauti nzito na ya amri ilisikika kwa nyuma yake.
Kwa sababu jua lilikuwa linawaka kwa mbele, Randy hakuweza kugeuka, lakini alifanikiwa kuona vivuli vya watu watatu vikitanda ardhini. Vivuli vile vilitosha kumthibitishia kuwa maadui zake walikuwa wanaume wenye maumbile makubwa na waliojipanga.
"Fuata amri, Randy!" sauti ile ilisikika tena, safari hii ikimfanya Randy ashtuke na moyo kumlunda. Swali kubwa likamjia kichwani: Wamejuaje jina lake wakati yeye hakuwahi kujitambulisha?

ITAENDELEA! USIKOSE MUENDELEZO WA KISA HIKI CHA KUSISIMUA. KUWA NAMI MPAKA MWISHO!

SEE ME​
 
SEE ME....

* SEHEMU YA NNE (4/10)*

ENDELEA......

Sasa tayari Randy alikuwa mikononi mwa watu wabaya. Ilibidi anyooshe mikono juu kutii amri ya watu wale wanaomwambia atii, huku mkono wa kushoto ukiwa juu na wa kulia ukishusha bastola yake chini."Ipige teke mbele!" Sauti ikazungumza kwa msisitizo na Randy akatii, akapiga teke bastola yake ikasogea mbele zaidi.

Haikuwa hatari kusema kwamba risasi zingefyatuka maana ilikuwa bado imepigwa pini.Jamaa wale watatu wakaanza kumsogelea taratibu huku wakiwa wamenyooshea bastola."Mikono nyuma!"Randy akatii na kwa haraka wakamuwahi kumbana mikono yake kisawasawa. Ndipo Randy alipoziona sura zao; walikuwa wanaume watatu wenye miili mikubwa na sura zilizokomaa. Mmoja alikuwa mweupe na wengine wawili walikuwa weusi tii kama Wasomali. Wale weusi wawili ndio waliomkwida mikono yake huku yule mmoja akivua mkanda wa suruali yake. Ulikuwa mkanda wa ngozi mweusi tii kama wale jamaa.

Wakamsogelea Randy na jamaa akaanza kumfunga mikono yake, akambana kisawasawa mpaka ngozi ya Randy ikajichora. Wakamkamata vizuri wale weusi wawili huku wakitembea mbele kwenda sehemu ambayo Randy hakuijua. Yule mweupe akafungua mlango wa gari ya Randy na kuanza kuikagua, akakuta simu ndogo ikiita:"WIFE"Jamaa akaiacha iite mpaka ikate, kisha akachukua simu ile na kutoa laini za simu hiyo na kuivunja.

Akafungua mlango baada ya kufanya ukaguzi wake."Mkagueni!" Jamaa huyo mweupe akazungumza na kuwapa amri wenzake huku yeye akiokota ile bunduki ndogo ya Randy na kuitazama. Haikuwa na namba ya usajili kwahiyo ilikuwa haramu.Wakamkuta na simu kubwa ambayo ndiyo Randy alikuwa anatumia kama location. Wakaitupa chini na kuikanyaga, ikavunjika kioo maana buti zao zilikuwa kubwa kama za jeshi na zenye visigino㶪 kubwa na vigumu."HIYO SIMU UTALIPIA," Randy akazungumza kwa kujiamini na kumfanya jamaa anayeivunja kutabasamu na kumkazia macho.

Randy akamsogelea na kumpiga ngumi ya tumbo na kumfanya Randy apige kelele na kuinama huku akisikia maumivu makali ya tumbo. Mikono yake kwa jinsi ilivyobanwa kwa nyuma ilizidi kutoa macho huku mishipa midogo midogo ikitokeza kwenye paji la uso wake, kwani ngumi ile ilipenya na ilikuwa ya kushtukiza. Wakamnyanyua na kuanza kuingia naye porini huku wakiwa wanambinyabinya ilimradi tu kumuumiza."Nini kinaendelea?" Randy akajiuliza huku akizidi kuzamishwa ndani ya msitu.

Randy alichoamini katika kundi lao na wao kama wauaji wa kukodishwa, huwezi kuuzwa au kusalitiwa na wenzako hata kidogo. Hii ni kutokana na mafunzo waliyopewa Japani yeye na wenzake 8 waliokuwa watoto wa mtaani, japokuwa kundi lina watu wengi zaidi ya wao 8.Jumba kubwa la gofu ndilo lilikuwa mbele ya Randy.

Lilionekana jumba la kale lililokosa matunzo, huenda familia iliyokuwa inaishi hapo walikufa wote au kuhama kabisa kutokana na eneo lililopo. Wakamuingiza ndani ya jumba hilo bovu na mbele ya sebule pana kulikuwa na meza iliyojaa tando za buibui, huku juu ya meza hiyo kukiwa na pombe tatu kali aina ya KONYAGI na vipande vya sigara vilivyozimwa baada ya kutumika. Vilikuwa vipande kama 50.Akatama kushoto na akashtuka kumuona mwanamke mtu mzima, wa umri kama miaka 47, akiwa amefungwa kwenye kiti huku uso wake ukiwa umejaa makovu na jicho lake la kushoto likiwa limevimba."Wote mnakufa!" jamaa aliyeambiwa na Randy atalipia simu akazungumza na kumkazia macho Randy.

Ni kama alimtamani kumkata vipande vipande."Msaada wako tumeupata. Huyo ndiye alikuwa ametumwa kuja kukuokoa. Mume wako tumemwambia asitoe taarifa polisi, ameamua kutafuta muuaji hahahaha!" Jamaa mweupe akazungumza na kumtazama mwanamke yule."MUME WAKO KWANINI ANATAKA KUGOMBEA MWAKA HUU? Kwanini hasikii kuhusu kuachia hiyo fomu?" Akazungumza yule jamaa mweupe na kumshika kichwa mwanamke yule."Anapenda sana siasa eeh?" Akamshika nywele na kuanza kuzivuta vuta."Chukua kamera turekodi, na huyo muuaji tumtumie mume wake kuwa muuaji wake tumemkamata.

Sasa asipoachia fomu tunamuua mke wake!" Yule jamaa mweupe akazungumza na akafuata kinyago kilichokuwa pembeni kwa ajili ya kuficha sura yake. Hakuwa na hofu maana aliamini mateka wake lazima watakufa tu, au kuwatoboa macho kabisa na kuwaacha hai; ndio uliokuwa mpango wake.Akavaa kinyago na akatoka nje baada ya simu yake kuita. Kitu anachojiuliza Randy, hawa jamaa wamejuaje anakuja na wamemjuaje jina lake kuwa anaitwa Randy?"Kuna msaliti!" Akawaza.Jamaa aliyokuwa amemshika akamuachia baada ya mwenzake kumuita. Wakaseti camera, akamkalisha Randy kwenye kiti.

Lilikuwa kosa kubwa mno kumuachia Randy...Mary baada ya usaliti alioufanya, na kila alipopiga simu ya mume wake akaona haipokelewi na mwisho kutopatikana kabisa, alikosa amani. Alikosa raha na kuona kuliko kuwa anamshauri mume wake kila siku ni bora ajiue. Kuliko utupu wake kuupeleka kwa lizee na kurekodiwa, ni bora apoteze maisha na kumuacha Randy. Hakuhitaji kumsaliti mume wake.Machozi yalimtiririka, macho yalivimba kwa kulia. Akatazama paa la nyumba yake na kuona feni ikiwa imesimama.

Akatazama pembeni na kuona shuka iliyokuwa imetandikwa na mfanyakazi wake wa ndani. Wazo la kujiua likamjia. Akafunyanyuka na kufunga mlango kwa ndani, kisha akavuta shuka na kuanza kuitengeneza iwe kamba ya kujitundika kitanzi.

USIKOSE SEHEMU YA TANO YA KISA HIKI! TAFADHALI UNGANA NAMI MPAKA MWISHO.

JE, RANDY VIPI KULE TANGA? NA MKE WAKE ITANAKUWAJE?

Je, unadhani Mary atafanikiwa kujiua au Randy atawahi kutoroka kule gofuni kuja kuokoa jahazi? Drop comment yako hapo chini twende sawa!

SEE ME......​
 
SEE ME

* SEHEMU YA TANO 5/10 ****


Mary akutaka kujiuliza mara mbilimbili akatia kamba juu ya feni huku akiwa amebebanisha kiti juu ya meza ya mbao ya chumbani kwake, akafunga vizuri na kukaza shuka ile ambayo amehakikisha ameifunga vyema, sas akaanza kutengeneza kitanzi akapima na kuona kinatoshea vizuri kwenye shingo yake.

Randy baada ya kukalishwa kwenye kiti akaanza kufanya utaratibu wa kujitoa ila akawa anshindwa kujifungua kutokana na mkanda wa ngozi aliokazwa nao,akaanza kutafuta kitasa ila akashindwa kukifikia maan alibanwa ipasavyo kila akijaribu kushika kitasa alishindwa alizidi kujipa maumivu makali zaidi ya mikono yake..kitu pekee alichofanikiwa kukiona ambacho kingeweza kumsaidia NAIL CUTTER kifaa cha kukukatia kucha kilikuwa mezani huo ndio ulikuwa msaada wake wa pekee ijapokuwa asingeweza kukata mkanda ule kwa kisu kidogo cha kifaa kile, jamaa mweusi akageuka na kumtizama akamshtukiza akitizama mezani na randy kwa haraka akakwepesha macho ila jamaa tayari alikwisha jua akatabasamu na kuacha camera kwani tayari walishamalizana nayo, akasogea mezani na kuchukua kifaa kile na kukirusha rusha huku akimsogelea randy akamkaba shingoni na kumnyanyua toka kwenye kiti akamsukumiza ukutani na kumbana

" Unajaribu kutaka kutoroka". Jamaa akazungumza na kumbana hukutani randy ambaye mikono yake yote miwili ikiwa nyuma
"Randy okoa NAFSI YAKO". Jamaa yule akazungumza kwa sauti ya chini sana huku akimkabidhi randy kikatia kucha na kumlegezea mkanda,Kitendo kilichomshangaza randy kwani mpaka sas haelewi.
" AMIDU mlete huku". Sauti ikasika ya yule jamaa mweupe na jamaa alokuwa amemkwida randy jina lake kumbe alikuwa anaitwa amidu na ndiye aliyeitwa na yule jamaa mweupe, akamkamata randy kwa nguvu na kumkokota mpaka upande wa pili wa kamera na kumpigisha magoti pembezoni mwa yule mwanamke
Kisha Amidu akatoka na kuwa nyuma ya kamera yeye na yule jamaa aliyepasua na kuivunja vunja simu ya randy
"START". jamaa mweupe akazungumz na mara moja akawa mbele ya kamera na bastola ndogo
"MR sOlO bado mpaka sasa hutaki kuhamini mke wako anakufa tizama muuaji wako naanza naye afu mwisho nafata mke wako nakupa lisaa limoja rudisha fomu ya urais mke wako habaki salama,sisi tuna mtandao mkubwa sana popote pale tupo umetuma muuaji tumejua sasa namuua afu atafata mke wako usipotii". Jamaa kazungumza na kumsogelea randy akamshika bega na kuanza kumbinya kwa nguvu huku akimtingisha tingisha hakujua kuwa kwa wakati huo randy ndiyo alikuwa anatumia kujifungua maana mkanda ulikuwa tayari ushalegea na kikatia kucha kile kilikuwa kinafytua kitasa cha mkanda..
Sauti ya maumivu makali na bastola kupaa angani ndiyo vilivyomkuta jamaa yule mweupe alipigwa kikumbo kikali cha taya ya kulia na kufanya bastola yake kuiachia na kushika taya yake ya meno ambayo alihisi imevunjwa tayari randy alikuwa huru, akapiga pigo jengine kwa yule jamaa mweusi aliyekuwa anakuja kwa kasi akijaribu kurusha teke ni ngumi ya uso baada ya jamaa kurusha teke na randy kulikwepa maumivu makali aliyapata kwani pua yake ilivunjwa yani ilipinda tena ilipindia kushoto damu zikamvuja akainama huku akishika pua yake , yule Amidu akaja kwa kasi ya ajabu akarusha ngumi ila randy akaikwepa na kwa haraka sana amidu akamkonyeza na randy akaelewa kuwa alitaka ampige teke la mguu randy akafanya hivyo na jamaa akaenda chini kama mzigo. Jamaa mweupe akataka kuwahi bastola iliyokuwa chini ila hakuamini kama angejikuta akitema damu hii ni baada ya kupigwa ngumi nyengine ya taya na kufanya meno mawili kutoka,
Ngumi za randy zilikuwa nzito kama nyundo ukijumlisha na maumivu ya kusalitiwa na mke wake ndiyo alizidi kuongeza nguvu ya kushambulia maadui zake
" Nani aliyewaambia nitakuja "?. Ndiyo swali lake la kwanza huku akinyoosha bastola kwa yule jamaa mweupe ambaye alimtizma randy huku akiwa aamini kwa kilichotokea akajishika paja lake ili anyanyuke ila akashika ugumu wa kitu akatabasamu kwa kejeli kwani alikuwa na bastola nyengine ile aliyokuwa nayo randy akawaza amzubaishe na kumtandika ya kichwa aliyekuwa mateka wake

"Hahah randy " . Jamaa akazungumza na akacheka kwa dharau huku akitema fundo la damu na kijifuta mdomo wake
Randy akampiga risasi ya mguu yule jamaa aliyevunja simu yake na kufanya jamaa yule kupiga kelele huku akionekan kutia huruma kutokan na maumivu akafytua risasi nyengine ya mguu kwa yule jamaa mweupe na kufanya jamaa ashuke chini na kupiga got moja huku akishika sehemu aliyopigwa risasi ya mguu na kulia kwa uchungu

Akapiga risasi nyengine tena ila chini karibu na mguu wa amidu na hakuna aliyefanikiwa kuona kitendo kile amidu naye akaanza kupiga kelel za uongo kama kwel kaumia sasa wote walikuwa chini
" jina langu nani kawaambia".
"Tuue" yule jamaa mweusi akazungumza na sauti ya risasi ikasikika ukimya ukatulia ni yule jamaa mweusi alosema wauwawe kwa dakika sekunde hizo paji lake la uso lilikuwa tayari na shimo la risasi.

Jamaa mweupe kwa haraka akachomoa bastola na kufyatua risasi kule alipo randy, sauti ya mtu ikasikika akienda chini kama mzigo alikuwa ni amidu ambaye alikwenda kukinga risasi ile ambayo moja kwa moja ikapenya kwenye moyo na kuacha jamaa yule mweupe kutoa macho kwa mshangao akapiga risasi kwa randy tena ila randy akajibanza kwa haraka sana kwenye nguzo kubwa ya jumba lile, jamaa mweupe akutaka kusubiri aliona kifo kipo karibu yake kwa haraka sana huku akichechemea akajitosa dirishani na kutua chini vibaya kitendo kilichopelekea kuvunjika mkono wake risasi zikawa zinamkosa nyuma akafanikiwa kuingia msituni.
Randy akarudi kwa amidu haraka haraka na kumkuta ndyo yupo katika hatua zake za mwisho akampakata mapajani kwani risasi hiyo ilikuwa ni yake maswali mengi yalikuwa kichwani mwake kuwa huyu ni nani
" ka...man.da" .Amidu kazugumza kwa shida sana na kishika mikono ya randy kwa nguvu
" Nime..fanikiwa ku..mju..a baba yako mza...zi" Amidu akazungumza na kufanya randy atoe macho kwa mshangao kwani hakuna anayejua siri ya maisha yake ata mke wake wazazi alitafuta wa mchongo akamuoa
"Ba..ba yan..gu"?
Randy akazunguma na kumtingisha yule jamaa anayefumba macho taratibu na taratibu akakata moto
(AKAFA)

Maswali yakawa mengi kwa randy akabaki pale chini kwa sekunde kadhaa akataka kunyanyuka ila akatizma mifuko ya amidu na kwa haraka akaanza kumsachi na akafanikiwa kukuta funguo pekee iliyokuwa imeandikwa namba 28 juu ya kitako chake cha kushikia akataka kuiacha ila akachukua na kuitia mfukoni akavua glovu zake zilizotapakaa damu na kuzitia mfukoni kisha akamfata yule mwanamke ambaye alishazimia toka risasi ya kwanza inasikika

" uuuh ". Randy akapumua na kumfungua kamba mwanamke yule mnene kidog akamtia begani kisha akafata ile camera na kuchukua memory iliyorekodi tukio zima kwani bado ilikuwa ina rekodi akujiuliza mara mbili zaidi ya kuivunja.
******** *****
" Dada yako bwana ni mjamzito" . Sauti ya daktari ikasikika na kumfanya mfanyakazi wa mary afurai na kuruka ruka
" Ni mzima lakini eeh ". Akauliza kwa upole
" Ndiyo ni mzima ila shingo yake kidogo imeumia mana kamba ilimban kisawa sawa ilikuwa kidogo tu tuseme mengine ila tunashukuru mungu uliwahi mapema na kuomba msaada kwa majirani".
" Asee sijuhi kwanini dada anafanya ivyo dokta chesko".?
" Randy anajua hili?"
" hapana sitomwambia mpka dada mwenyewe akirudi kwenye hali yake"
" aseeh siwezi kukaa kimya kwa jambo hili Nuru". Dokta chesko akazungumza na kumtizama nuru
" wamegombana"
" sifahamu yani maan muda mwingi uwa wana kuwa na raha muda wote na amani sa siwezi jua kusema kweli".

"Okay nisubiri ".
Dokta chesko akazungumza na kuondoka kwenda kumtizama mary

JE NINI KITAENDELEA RANDY ANAKUJA KUMUUA MKE WAKE NA JE AKIJUA NA MIMBA NDO ATAFANYA NINI ATAHISI NI YA YULE MZEE AU ITAKUWAJE NA VIPI KUHUSU BABA MZAZI WA RANDY NI NANI???? NA AMIDU JE????

SEE ME
 
SEE ME

*SEHEMU YA SITA 6/10

Randy akamuweka nyuma ya siti ya gari yake yule mwanamke kisha yeye akaenda kwa mbele kwa ajili ya kuendesha gari akatizama laini zake zilizovunjwa na simu yake vyote akachukua akutaka kuacha kitu kinachomuhusu..lile gari jeusi la wale watekaji bado lilikuwa pale pale akutaka kujiuliza mara mbili mbili akapangua gia ya gari yake na kuanza kuliondoa kwa kasi huku asijue ni muda gani kwani akuwa na saa ya kutizama ila alihisa huenda ni saa 8 za mchana,

"Msaliti kwangu ni shetani mary nakuja kukuua". Randy akazungumza huku akiwa anakumbuka tukio la mke wake kumuona na mwanamume geust alisahau kuwa naye alitoka kumcheat mke wake kwa mage dada anayejiuza na ni mteja wake mkubwa mno.
Randy akuwa na huruma ata kidogo alizamilia kufanya tukio lake na alipanga kumuua kwa kifo cha kikatili ikiwezekana kumchoma kabisa na moto
" INABIDI nipate simu wenye mtu wao wamfate sina sehemu ya kumpeleka ". Akazungumza huku akikunja kona kufat njia ya barabara ya kisasa baada ya kuacha barabara ya vumbi.

******* ****** *******

Miguno ya mahaba ilizidi kusikika ndani ya chumba kilichoshesheni vitu vya thamani ata kitanda chake kilikuwa cha ghalama kubwa mno, mwanamume mmoja alikuwa amemkamata mwanamke kisawa sawa kambana kwenye kiuno chake akawa anafanya kwa nguvu zake zote alizojaliwa na muumba ni kama sasa alikuwa anafika mshindo alikuwa anafika ambako wanaume wote rijali huwa wanafika
" OOOH mage ". Mwanamume huyo akazungumza huku akigugumia kwa utamu anaoupata akajitoa na kujitupa kitandani na kutizam paa la nyumba huku akipumua juu juu
" aseeh we mtoto balaa nikija kukufuma na mtu nakuua na mtu wako". Mwanamume huyo akazungumza na kumgeukia mage ambaye akatabasamu
"haitotokea Jeradi siwezi kukusaliti maana kila kitu inanipa".
Mage akazungumza na kumshika jeradi kifuani na kuanza kumshika shika
" Mwezi ujao uchaguzi unaanza baba akishinda na kuwa Raisi nitakuoa" . Jeradi akazungumza na kumfanya mage ashtuke kwani akutegemea kama itakuwa haraka kiasi icho
" vipo hujapenda".
" hapana beiby nimependa nitafurahi sana mume wangu " mage akazungumza kujilaza kifuani mwa jeradi
" Kazi yako uliacha" jeradi akamuuliza
" Kwanini unihamini mume wangu nishaacha sijiuzi tena". Mage akazungumza huku akimtizama mwanamume huyo aliyempatia Club na kujikuta akimdatisha mtoto wa rais na kufanya mahusiano yao kuwa ya siri sana
" Nikuambie kitu unanijulia sana" Mage akazungumza na kumfanya jeradi afurahi kusikia ivyo
"Jeradi lazima nikuue". Mage akajisemea moyoni huku akimpapasa papasa jeradi kifuani. Akakumbuka miaka 2O iliyopita

MIAKA 2O ILIYOPITA

" Mume wangu wauzie tu kiwanja sisi twende mjini tutapata chengine". Mage akasikia sauti ya mama yake mzazi akizungumza wakat huo yeye akiwa na miak 8
" Mama mage siwezi uza kiwanja hiki nimepewa urithi na mzee wangu tena mzee wangu kapewa na babu yangu ko siwezi kuwasaliti sikutambua kama kina dhahabu ni mali yetu siwezi uza ".
Baba mage akaongea kwa ukali na kusogeza chemli iliyokuwa inawaka akataka kuizima ila mke wake akamuwahi na kumshika mkono
" kwanini we siyo muelewa millioni kumi ni nyingi mbona". Mama mage akazungumza kwa upole na kumtizma mume wake huku dhaili tamaa ya pesa ikionekana machoni mwake
Alitamani naye kuvaa mawigi na kupendeza kama wanawake wa kisasa wa mjini alichoka nguo na kanga zilizochakaa alihitaji kupendeza kwani umri wake ata miak 30 haikuwa bado na mimba alibeba yupo shule alihitaji kuwavimbia kijijini pale mume wake atakapo kubali kuchukua pesa toka kwa kampuni iliyotaka eneo hilo ambalo linadai lipo chini ya serikali

Mage ugomvi huu alishauchoka kwani ni wiki sasa anasikia malumbano ya mama yake na baba yake alikuwa mtot mdogo sana lakini mwenye uelewa mkubwa mno kichwani mwake wazazi wake hawakuelewana mpaka mafuta yalipoisha kwenye chemli ndipo kila mtu alikuwa kimy huku mama yake akiendelea kufyonza fyonza mpaka alipopitiwa na usingizi.
********
"Naenda shamba" . Mama mage akazungumza na kuondoka kwa kisirani huki akiwa na jembe mkononi ilikuwa majira ya saa moja hivi
" nenda na mtoto maan na mimi leo naenda mahakamani kupeleka kesi". Baba mage akazungumza huku akiwa anajza baskel yake upepo na kumtizama mtot wake mage ambaye anakula kipolo cha kiazi na so kwenda shule kama watot wengine

"Jitot likubwa hivi kubaki nyumbani haliwezi emu twende". Mama mage akazungumza na akafoka huku akiwa na hasira kusikia mume wake anaenda mahakamani..

Nyumba ikabaki tupu mage akiwa shambani na mama yake ngurumo ya gari ikasikika pembenizoni mwa shamba lao ambalo pembeni kidogo kuna vichaka afu nyuma yake kuna barabara kubwa ya kijiji

" Juliana". Sauti ikasikika toka kwenye gari na mama mage akatabasamu kwani ni jina lake
"ABEEH nakuja, we mage nisubiri hapo" juliana ambaye ndiye mama yake akazungumza na kumuacha mtot wake huku akitoa kanga yake iliyochakaa na akabaki na kimini kidogo alichoomba kwa rafiki yake kiufupi alikuwa ni mwanamke mzuri sana, mage akuwahi muona mam yake katika mavazi hayo
Akutaka kubaki nyuma akajisogeza taratibu na kujificha kwenye kile kichaka
" WAOOH SOLO nimekumiss sana " mage akamsikia mama yake akizungumza na akamkumbtia kwa nguvu sana
" Hata mimi asee" solo akazungumza na kubinya binya makalio ya mama mage

****** ITAENDELEA USIKOSE MUENDELEZO HUU SEE ME. JE MAGE NI NANI NA JE RANDY MWANAMKE ALIYEMUOKOA NDO JULIANA AU VIPI NA VIPI KUHUSU RANDY ...... NA MKE WAKE NA BABA YAKE JE NI NANI COMMENT hapo chini nione maoni yako kuhusu simuliz yetu tafadhali


SEE ME
 
SEE ME

***** SEHEMU YA SABA 7/10*******

Kitu alichokiona Mage ni kumuona mama yake akishikwa shikwa makalio na mtu ambaye akufanikiwa kumuona sura yake
"Mume wako anasemaje"? Solo akazungumza huku akimvuta juliana kiuno chake na kumuegemeza kwenye ubavu wa gari yake, mage alichofanikwa kuona ni suti pekee nyeusi na mgongo wa mwanamume huyo
"Aah yani ana kichwa kigumu sana"
"Bado anakataa". Solo akazungumza na kumuachia juliana kiuno chake
" sasa mambo yanakuwa magumu pale kuna mali kuna dhahabu za kutosha".
"Nifanye nini solo". Juliana akazungumza huku akimtizama mwanamume huyo aliyempa lifti mwezi mmoja ulopita na kuweka naye mazoea akijua kuwa solo alimfatilia kitambo sana na familia yake kwahiyo alitaka ukaribu na kumtega kimapenzi hili aweze kupata kile alichokusudia siyo kwamba hafahamu kuhusu icho kiwanja anakijua kwani katumwa hapo na mzee wake ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa babu yake mage.
" Kwahiyo kaenda mahakamani"
"Ndiyo".
" Unampenda ?" Solo akamuuliza juliana ambaye bila woga na macho kumtoka akamjibu
" hapana simpendi nakupenda wewe".
Mage akasikia jibu lile toka kwa mama yake machozi yalikuwa yashajaa machoni mwake alijua kila kitu kinachoendelea
" Fanya jambo langu moja afu tutaenda mjini". Solo akazungumza na kufanya juliana kutoa macho kwa mshangao huku furaha isiyopimika ikijieleza machoni mwake


"Baby ! Baby ". Sauti ya jeradi ikamfanya mage ashtuke toka kwenye dimbwi la mawazo na kumbukumbu yake ya miaka 20 iliyopita
"Vipi uko sawa".
" ndiyo nipo sawa jeradi usiwaze". Mage akazungumza na kujikaza akamsogelea jeradi na kumbusu mdomoni na kumshika shika kifuani.

** **** *******
"Samahani dada ". Randy akazungumza huku akimtizama binti mweupe mwenye uzuri wa aina yake
" nambiye kaka angu".
"Nashukuru kama utojali simu yako ina salio unisaidie mara moja".Randy akazungumza na msichana yule akatingisha kichwa kukubali akafungua zipu ya pochi yake na kutoa simu yake kubwa na kutoa paswed kisha kumkabidhi Randy
" laini one" akazungumza na kumkabidhi randy
" nashukuru". Randy akazungumza na kuchukua simu ile na kujaza namba ambazo zilikuwa za mkuu wake wa kazi ilikuwa ni sheria lazima namba ya mkuu wako iwe kichwani, simu ikaita na kupokelewa hapo hapo randy akasogea pembeni kidogo

" G145 Randy hapa kazi imekamirika nipo na mateka fuatilia hii simu hiki kituo waje wamchukue yumo kwenye gari namba MC5733 simu ikiondoka msifuatilie location bali hiki kituo nilichopo ndo muhusika yupo ".Randy akazungumza na kukata simu akutaka kujibiwa wala nini akutaka kueleza kuwa kwenye kundi kuna msaliti akakafuta ile namba na kuiblack list kisha kumrudishia dada yule na kumshukuru.

" Mary nakuja kukuua " .Randy akazungumza na kuondoka eneo hilo kwa miguu maana tayari alikuwa dar es salaam na gari lake alijua watalichukua na wahusika watakao kuja kumchukua yule mwanamke aliyezima ndani ya gari nusu kaputi.
Randy safari ya kwenda kwake ikaanza huku kumbukumbu ya kuchitiwa na mke wake ikiwa kichawani mwake kwa sasa alitaka akifika apatene na boss wake kwa ajili ya malipo ya kazi aliyofanya akutaka kusema kuwa kuna msaliti alitulia tuli kufanya uchunguzi wake taratibu na kupata ushahidi uliokamirika.

Nyumba haikuwa na mtu hali ambayo hakuizoea hata mfanyakazi wake wa ndani hakuwepo kitu kilichomshangaza ni kukuta shuka ikiwa imefungwa juu ya feni ya chumbani huku meza na kiti vikiwa chini na chumba kuvurugika
" Hofu ikamuingia japo alikuwa na hasira na mke wake ". Inabidi nipate simu mara moja akazungumza na kufungua droo ya chumbani mwake na kutoa kitita cha noti ambacho hakutaka ata kukihesabu akakitia mfukoni na kutoka nje wakati anatoka akakutana na dada wa kazi
" Nuru vipi hapa". Randy akamuuliza nuru dada wa kazi, nuru akatizama chini huku machozi yakianza kumlenga lenga
" Nimeona chumbani kamba yani hapaelweki kuna nini? ". Akamuuliza na kumkazia macho huku akimsogelea.
" Ni dada mary alitaka kujiua". Nuru akazungumza na kufuta machozi yake huku akitizima chini kwa masikitiko randy akashtuka na kumshika nuru mabega yake
"Ntizame usoni Nuru yuko wapi" randy akazungumza kwa sauti ya msisitizo ambayo nuru toka amjue hakuwahi kusikia sauti ya boss wake kama ya siku hiyo ilikuwa nzito na ya kutisha sauti hiyo ilionesha upande wa pili wa randy ambao nuru hakuwahi kuuona
"Yupo hospitali"
" Nieleze maelezo yanayoeleweka ". Randy akazungumza na kumkazia macho nuru ambaye akamtizama boss wake kwa huruma
" dada mary alitaka kujiua bahati nzuri nilimuwahi nilikuwa napita na kusikia kishindo cha kitu kikianguka nikapiga hodi ila kukawa ndani sikuelewi nikachungulia kwenye tundu la ufunguo na kuona kiti chini huku miguu ya mtu akitapatapa ikiwa ina ning'inia nikaanza kupiga kelele za msaada bahati nzuri akaja yule mzoa takataka na ndo alivunja huo mlango ". Randy akageuka na kutizama mlango akuona mwanzo kwani pazia lilifunika sehemu ya kitasa
" kwa sasa yupo hosptali na ni Mjamzito". Kauli hiyo ya nuru ikafanya randy huruma iliyokuwa ina muingia kumtoka kwa akili ya haraka harak akahisi mary alitaka kujiua baada ya kugundua mimba siyo ya randy ni ya yule mwanamume, akatingisha kichwa huku akiuma meno kwa hasira na kufanya taya zake zivimbe
" kumbe alitaka kujiua " akazungumza na kumuacha nuru mabega yake aliyokuwa ameyakamata muda wote
"Jana alilala nje sindy". Randy akazungumza na kumtizama nuru ambaye uwoga ukaanza kumvaa baada ya kuona sura ya randy isiyokuwa na chembe ya huruma hata kidog
" Inaonekana unajua siri nyingi sana za mary ni siku ngapi au miezi mingapi uwa halali nyumbani". Randy akamuuliza nuru, alikuwa amechanganyikiwa zaidi kusikia mary ana mimba na kutaka kujiua akahisi kabisa alitaka kujiua maana amejua mimba siyo ya randy sumu kali ikamjaa moyoni mwake, akamchukia mary mazima na kutamani kumkata kata vipande
" b...o..os.s ni ja...na tu". Nuru kwa uoga akazungumza kabla randy ajafanya kitu simu ya nuru ikaita
" pokea " Randy akazungumza na nuru akaitoa kwenye mkoba wake jina la dada mary ndiyo lililokuwa mbele ya kioo cha simu na randy aliona.
" Weka loud speaker akinulizia sema sipo".
Mary akatingisha kichwa kukubali akapokea na kusikia sauti ya mary ya upole na akamtizma randy anayeuma meno kwa hasira na kufanya taya zake kujichora
"Haloh nuru"
" Ab..ee da.da" Nuru akazungumza kwa sauti ya uwoga kidogo
"Upo salama".
" Ndiyo dada nipo salama". Akajikaza na kuzumgumza
" wew upo salama pia". Nuru akazungumza tena
" Usijali vipi Randy yupo"? Mary akauliza na nuru akamtizma randy ambaye akatingisha kichwa kuwa aseme hayupo
" hayupo"
"Afadhali sikia safisha humo chumbani haraka tafuta fundi atengeneze icho kitasa na usimwambie chochote kuhusu yani hilo tukio, na mimba tamwambia mwenyewe".
"Sawa dada".
"Natoka kesho hasubuhi,utasema nimeenda kwa mama kama jana nilivyokwambia". Mary akazungumza na kufanya randy kurudi chumbani mwake akajitupa kitandani huku machungu ya usaliti yakiumiza moyo wake akapata jibu kuwa huenda kila siku anasalitiwa na mary mke wake, akatizama picha yao ya ukutani na kuona tabasamu zuri la mary sasa aliona ni kama unafiki toka kwa mke wake,alichowaza ni kuua tena kumkata kata vipande na kuwapa mbwa wake wakubwa alipanga tukio la kikatili kwa mary ndiyo randy hakuwa na huruma ata kidog kwa msaliti alifundishwa kuua na alifundishwa kuua kikatili msaliti na alihamini msaliti hapaswi kuishi yeye akasahau kuwa amemsaliti mke wake kwa mage tena zaidi ya mara 5

" KEsHO NAKUUA" .Akazungumza na kutizama picha ya mary alipanga kumuua mke wake kwa maumivu makali alitaka awe ana mkata kata kipandi kimoja kimoja cha mwli wake na kumtoa mtot ambaye tumboni bado ni kijusi kichanga......

********* ITAENDELEA ENDELEA KUFATILIA KISA HIKI MPKA MWISHO SITOKUACHA MDOMO WAZI *****

SEE ME
 
SEE ME

SEHEMU YA NANE 8/10**

Jumba kubwa la kifahari lenye ulinzi mkali wa CCTV CAMERA na walinzi walojazia miili yao kwa mazoezi makali waliyokuwa wanapiga walikuwa makini kulinda eneo hilo wakizunguka kila sekunde na kila hatua waliyopiga macho yao yalikuwa makini kutizama kila kona ya jumba hilo.
Mlango ukafunguliwa na kufanya walinzi wale wageuke na kukuta ni kiongozi wao wa ulinzi akiwa na microphone sikioni mwake na siyo yeye tu mpaka wenzake.
" MR SOlO anakuja sasa hivi kuweni makini maana sahivi ni usiku hatutaki jambo lolote litokee".
"Sawa mkuu". Wakajibu kwa pamoja na jamaa yule akarudi ndani na akiwa amevalia suti nyeusi kama wenzake, Mbalamwezi ilikuwa ikizidi kumurika kama kawaida na kufanya anga lizidi kupendeza huku nyota nazo zikiendelea kutoa mwanga wake na kufanya anga lizidi kupendeza zaidi, ulikuwa ni usiku wa saa 2 kwenda saa tatu honi ya gari ikasikika nje ya geti la jumba lile la kifahar na walinzi wawili wakenda getini na kuchungulia kisha wakafungua geti na kutoka nje na kukuta gari mbili kali na za ghalama ya juu, haikuwa kuna haja ya utambulisho kwani kwenye plate namba kulikuwa na namba ya usajili wa gari na juu jina lilisomeka SOLO
Wakaruhusu gari kuingia ndani ya geti na jengine likafata nyuma na zikaenda kupaki sehemu waliyoelekezwa na walinzi wale, kisha mlango ukafunguliwa na akatoka jamaa mwenye umbo kama la wale walinzi wa jumba lile na akafungua mlango kiatu kikatangulia chini ya ardhi huku suti kali nyeusi ya bei mbaya ikionesha na kufanya mtu huyo kuwa nadhifu zaidi
Walinzi wate wakamuinamia kwa sekunde kadhaa na kunyanyua shingo zao akapiga hatua chache na kuwapungia mkono walinzi wale wa ile nyumba, mlango wa nyumba ile ukafunguliwa na akatoka yule mzee mwenye kipara na kidoti juu ya paji la uso yule mzee aliyefanya mapenzi na mary na kumtumia vibaya ili kukidhi haja zake
" Waoooh my friend". Mzee yule akazungumza na kumkumbatia Mr Solo
" Aseeh Mr Zengo una jumba kali". Mr solo akazungumza na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani ya jengo hilo la kifahari mlango ukafunguliwa na sebule kubwa ikaonekan ikiwa na vitu vya thamani vya bei ghali vilivyovutia kila mtu alipotizama huku tv kubwa ikiwa ukutani yani tv ile mpaka jasho la mtu ulikuwa unaliona.
"Karibu". Mr zengo akazungumza na na wakaketi kwenye sofa pale pale wakatokea wafanyakazi wa kike takribani wanne wakiwa katika fomu moja na kufanya wapendeze zaidi yani unaweza sema wapo hotelini
" Shikamoo". Wakazungumza huku wakibiga goti moja kama tamaduni za kiafrika kwa baadhi ya nchi kama kwetu hapa tanzania
" Marahaba wazima". Akazungumza kwa uchangamfu na wakatingisha vichwa kukubali kisha wakatoka sekunde kama tano wakarudi na vyakula lain lain pamoja na vinywaji
" okaya nendeni".Mr zengo akazungumza na wadada wale wakatii

" aseeh watoto wazur hawa"
" hahah hatari lakini una mke" mr zengo akazungumza kwa utani na kufanya wazee wale wacheke kwa sauti ya juu. Ndani humo walikuwa watu wanne pekee mr solo na mlinzi wake na mr zengo na mlinzi wake ukitoa wale wafanyakazi wanne
" Umemuona mpinzani wako " mr zengo akazungumza na akawasha tv kupitia remote na picha ya mzee mfupi akiwa katika jukwaa ikaonekana huku kundi kubwa la watu likiwa chini kusikiliza hoja zake
" Jamaa ana upepo sana"
" Ndiyo ila nahitaji kumuangusha lazima niwe rais".
" Unahis unakuwa rais kirahisi bila kumwaga damu?"
" Nipo tayar kwa lolote na mpaka sasa nina chuki na hasira kubwa sijuhi nani alomteka mke wangu". Mr solo akazungumza kwa uchungu
" Umefanikiwa kumpata JULIANA".
" Ndiyo mzee wangu mke wangu kaumwiza sana nimetoka naye mbali sana" mr solo akazungumza kwa unyonge na mr zengo akatoa ishara kwa walinzi wale wawili kuwa watoke nje na wakatii wakatoka nje mpaka mlinzi wa mr solo ambaye alisubiri amri kwa boss wake na akatii akatoka nje na yeye palepele Mr solo akapiga magoti chini ya vigae na kuinamisha kichwa chake chini kwa mr zengo

" Nifanye kuwa rais wa Tanzania nakuomba ". Akazungumza na kushika miguu ya mr zengo na kumfanya mzee huyo kuanza kucheka kwa dharau
" Unahitaji nikuweke madarakani kama rais aliyepita ". Mr zengo akazungumza na kumkanyaga mr solo mgongoni mwake na mr solo akatingisha kichwa kukubali
" Utakuwa kibaraka wangu kama sasa" .
" Ndiyo ndiyo mheshimiwa".
" Nitakufanya rais katika nchi hii kwa kunitii mimi" akazungumza na kuchukua kipande cha nyama kisha akakiweka mdomoni na kukitupa chini
" okota na ule" akazungumza kwa amri na mr solo akamtizama kwa mshangao
" amri ni moja " akazungumza na mr solo kwa haraka akaokota nyama ile na kuitafuna, na mzee akatabasamu
" Kaa kwenye sofa Rais" mr nzega akazungumza na kufany mr solo afurahi akujali kuwa alikula nyama ya mdomoni akujali kuwa alikanyagwa yeye alihitaji kuwa rais wa nchi hii alikuwa na tamaa
" Mke wako ulimpata ulimtuma nani,?"
" Ni lile kundi mkuu ulonielekeza nipige namba na kutuma pesa"
" Okay huyo huyo alomuokoa mke wako wiki ijayo mpinzani wako ana mkutano mbeya inabidi auwawe" .

" mkuu itawezekanaje"
"Ili uwe rais inabidi yule mzee afe"
" uoni kama vyombo ya habari vitanichafua"
" hahah bila ushahidi uwezi chafuliwa maana muuaji atakayefanya ilo tukio hawezi acha ata unyayo wa kiatu".
" Nashukuru sana mzee "
" Nakupa billioni 2 uendeshe uchaguzi" mzee akazungumza na kumfanya solo ajawe na furaha huku uso wake ukiwa na tamaa...
"Asante sana asante sana" akazungumza na kupiga magoti chini na mzee yule kumkanyaga mgongo wake
" Miaka 20 iliyopita ulimchinja mume wa juliana kikatili sana". Mr zengo akazungumza na kufanya mr solo ashtuke kwani siri hiyo ana imani kuwa hakuna anayehifahamu macho yakamtoka na kumtizma mr zengo ambaye anacheka


******** ITAENDELEA USIKOSE MUENDELEZO WA KISA HIKI CHA KUSISIMUA MAONI YAKO NI MUHIMU*********

SEE ME
 
SEE ME

****** SEHEMU YA TISA 9/10******

"Miaka 20 iliyopita ulimchinja mume wa juliana kikatili sana".Mr zengo akazungumza na kufanya mr solo ashtuke kwani siri hiyo ana imani kuwa hakuna anayehifahamu zaidi yake,macho yakamtoka na kumtizama mr zengo ambaye akacheka kwa sauti kubwa
"Usiwe na wasi wasi mr solo sasa unaweza kunyanyuka".
Mr solo akanyanyuka huku maswali mengi yakiwa kichwani
" kwa sasa focus na kampeni zako ili uweze kupata wafuasi wa kutosha maana vyama vyengine havina wafuasi wa kutosha kwahiyo atakapokufa yule wewe utashinda kiti cha urais inibidi auwawe kabla ya kura kuanza kupigwa".
"Asante sana mheshimiwa kwa msaada wako nakuahidi nitakutumikia mpaka mwisho wa maisha yangu". Akazungumza na kuchukua kipande cha nyama mezani akaanza kula huku akicheka kinafiki baada ya siri yake ya kuua miaka 20 iliyopita akiwa nayo mzee mwenzake.
" Naenda chooni mara moja". Mr zengo akazungumza na kuondoka kwenda chooni akapanda ngazi kuelekea vyumba vya juu vya jumba lake.
" Nikiwa rais takuua". Mr solo akazungumza kwa sauti ya chini sana na kuuma meno kwa hasira huku akimtizma mzee huyo anavyoishia vyumba vya juu vya jengo hilo
"Siri yangu amejuaje "
" juliana au ananizunguka". Akawaza na kumfikiria mke wake juliana akakumbuka jinsi alivyomuuza mume wake usiku wa kutisha wenye mvua kali na radi zilizopiga na kuvunja vunja baadhi ya miti, akakumbuka jinsi anavyomkata shingo mume wa juliana bila huruma woga ukamuingia na kwa haraka akachukua vidonge kwenye koti lake na kumeza ndiyo huwa anatumia vidonge kila anapokumbuka tukio lile alilolifanya bila kutegemea tamaa ya mali inaweza badirisha mtu nakuwa katili na muuaji wa kupindukia ili tu atimize jambo lake na kufurahisha nafsi yake amekuwa mraibu wa vidonge ivyo ambavyo uwa vinamtuliza lakini tamaa bado ipo mbele ya macho yake


******* ***** ******* ******

Saa 4 hasubuhi randy akapanda ndani ya gari yake kwa ajili ya kwenda hosptali kumfata mke wake baada ya simu toka kwa dokta chesko kuwa ilibidi kwenda kumfata mke wake hospitali na hataki mambo hayo yafike mbali mpaka polisi maana chesko amesoma na mary hakutaka mambo yawe mengi alimpigia simu randy aje amfate mke wake hosptali na kwenda kumfariji nyumbani chesko hakujua anampa fisi mifupa
" Asante sana chesko kwa kumtizam mke wangu". Randy akazungumza na kumshika mkono chesko kama ishara ya kumshukuru huku uso wake ukiwa na tabasamu bandia, tabasamu la uongo
Akamfata mke wake na kumkuta macho kitandani randy akaonesha sura ya huruma na kumfata mke wake
" pole mke wangu nasikia ulianguka bafuni chesko kanambia " .Randy akazungumza na kumtizama mary anayejinyanyua kitandani huku shingoni kukiwa na bandeji ambalo alijakazwa sana
" Asante mume wangu na niliangukia shingo" mary akazungumza kwa sauti ya upole na kumtizama randy ambaye anaonekana kujali sana,Randy chuki ikaongezeka kuona mwanamke huyu ni muongo sana tena uongo ulopindukia, akambusu kwenye paji la uso na kumnyanyua kitandani na mke wake akaanza kujiandaa akatizama makalio ya mke wake jinsi yalivyonona afu akakumbuka yule mwanamume alotoka na mke wake geust hasira zikampanda zaid baad ya kuona katumbo kadogo ka mke wake mary akakunja ngumi na kujialpizia leo anakwenda kumpasua tumbo.
" Nakupenda sana mume wangu" mary akazungumza huku machozi yakimlenga lenga na kufanya randy moyoni aone mwanamke huyo ni muigizaji mkubwa mno tena wa HOLLYWOOD
" Nafahamu mke wangu leo nahitaji nikufanyie kila kitu".randy akazungumza na kumfata mke wake
" kipi mume wangu"
" nahitaji leo uende peponi ukapumzike huko mpaka upone".
" mmh twende wote mume wangu huko peponi".
" usijali mke wangu tutaenda wote sawa mke wangu mzuri". Wakakumbatiana huku mary akionesha hisia kali kwa mume wake huku kila muda machozi yalikuwa yakimtoka na kauli nakupenda randy ilikuwa kama wimbo kwa randy.
Wakaingia ndani ya gari na safari ya kwenda kwao ikaanza
"Mume wangu ujue nakupenda sana" Mary akazungumza na kumshika randy mapaja yake
"Nafahamu mke wangu nami pia nakupenda sana".
"Unizidi randy me nakupenda sana ". Mary akazungumza mara hii kwa hisia kali sana kitendo kilichomshangaza randy lakini hakutaka kukubali kirahisi akili yake ilimtuma ni maigizo ya kihindi ya star kunyanyua gari

Wakafika nyumbani na kuingia mpaka chumbani, Randy akafunga mlango na kumgeukia mke wake na kumfata kitandani akaketi.
" Vipi nikupeleke peponi saa ngapi".
" Mmmh mume wangu nimechoka siwezi ata kidogo show zako" mary akazungumza akijua ni peponi ya kitandani
" Mmh utaki kunipa ". Randy akazungumza kwa sauti nzito na kufanya mary ashtuke na kumtizma randy kwa macho ya udadisi
" Pesa za kwenye bahasha za nani?"

Randy akazungumza na kufanya mke wake kumeza mate na kuwa mnyonge
" Mume wangu nitakwambia tu usijali". Mary akazungumza na kupanda kitandani alikuwa bado amechoka mwili wake haukuwa na nguvu
" Nakuja" Randy akazungumza na kuondoka
"RANDY unaenda wapi lakini me nakuhitaji mume wangu "
" Nakuja usijali mke wangu".Akazungumza na kutoka nje ya chumba chao kabla ajafanya chochote alichokuwa anawaza ujumbe ukaingia kwenye simu yake aliyonunua leo hasubuhi kipindi anamfata mke wake na ku-renue laini zake upya, Ujumbe uliingia kwa njia ya Email kwani kwake kulikuwa na Wif na hakuwa ameizima ya kwenye simu ni kutokana na kazi zake alizokuwa anafanya akafungua ujumbe ule.

"HONGERA SANA RANDY KWA KAZI YAKO NZURI ULIYOFANYA TUNAJIVUNIA WEWE KIJANA WETU NA PESA YAKO INAINGIZWA SASA HIVI KWENYE NAMBA YA AKAUNTI YAKO ASANTE". Akamaliza kusoma ujumbe ule na ukaingia ujumbe mwengine ukithibitisha pesa aliyowekewa kwenye akaunti yake
E-MAIL ikaingiza ujumbe mpya akafungua na kukuta kuna picha ya mwanamume mfupi mzee wa makamo miaka kama 50 akavuta picha kuwa alishamuona wapi akashtuka baada ya kuikumbuka sura hiyo
" MGOMBEA URAIS".Akazungumza kwa sauti ya chini sana na kuzoom picha ile akashuka chini na kukuta jumbe ndogo
" MUUE".
"Hapana". Akajisemea kimoyo moyo na kutoka nje huku akifikiria jambo ilo alijua ni hatari alijua anasogelea kifo alijua atawindwa nchi nzima mpaka atakapokamatwa.
"Siwezi fanya kazi peke yangu".Akazungumza na kutoka nje ya nyumba yake alihitaji kwenda duka la madawa kununua dawa za usingizi mzito nusu kaputi ili amlaze mke wake akiamka akute tayari kashamfunga kwenye stoo yake ya siri ili aanze kumkata kata vipande alidhamilia kuua hakuwa na huruma na msaliti alijiapia toka akiwa japani msaliti ni lazima afe.

"***** ******* ******

"Baba kama nilivyokwambia nahitaji kuoa nishapata mwanamke sahii kwenye maisha yangu ukishinda uchaguzi nafikiri ndoa hii itakuwa kubwa kuliko zote zilizowahi kutokea"
" Sasa umekuwa mwanangu umeacha kuchezea wanawake" Mr solo akazungumza na kumtizma jeradi na kumshika kichwa
" Kamuone mama yako ndani amepatikan"
" Waooh kwel" jeradi akazungumza na kunyanyuka kwa haraka kwenye sofa na kuwahi chumbani kwa mama yake na mzee wake akubisha hodi akazama ndani na kumkuta Juliana akiwa uchi wa mnyama huku akiwa anajipaka mafuta mapajani mwake cha ajabu hakuna aliyeshtuka zaidi ya jeradi kurudi nyuma na kufungua mlango alipoona baba yake anatoka na walinzi wake na magari matatu akarudi ndani ya chumba kile na kufunga mlango na kitasa akamsogela juliana ambaye ni mama yake ila siyo mama mzazi

"Pole mke wangu".Akazungumza na kumshika shika mama yake mapaja akamtizma jinsi alivyovimba uso akamshika uso na kuubinya binya taratibu
" Naumia jeradi" mama yake mlezi ambaye ni mama yake na mary akazungumza kwa sauti ya madeko, jeradi akasogeza mdomo wake kwenye kinywa cha mama yake huyo na juliana akafungua kinywa chake na wakaanza kunyonyana denda akawa anamchezea chezea mwili wake akawa anamshika shika kila kona ya mwili wake na kufany juliana alale kitandani na kumtanulia mapaja MTOTO WAKE.....


ITAENDELEA USIKOSE KISA HIKI CHA KUSISIMUA**

SEE ME
 
SEE ME

SEHEMU YA KUMI 1O/1O*

CHAPTER ONE ( 1) MWISHO***.

Juliana akatanua mapaja yake kwa ajili ya kupata penzi toka kwa mtoto wake jeradi ni tabia waliyokuwa wanafanya pindi ambapo mzee wake akiwa anatoka basi jeradi alitumia muda huo kupiga anapopiga baba yake mzazi
Akazidisha utundu wake na ujuzi wake kumchezea juliana ambaye alikuwa amelegea kwa wakati huo jeradi akatoa nguo zake harak haraka na kushika kifaa chake ambacho tayari kilikuwa kishawika akaingiza na chote kikazama na kufanya wagugumie kwa sauti za utamu, jeradi alitaka kupiga ambavyo anapiga siku zote lakina hakufanya hivyo zaidi ya kwenda kistaharabu mpaka wote walipomaliza na kukimbatiana
"Nilikumiss sana tunda langu".Jeradi akazungumza
" Kwanza nasikia unatak kuoa"
"Ndiyo lakini siwezi acha kukupa haki yako ya msingi".
" Mmmh ila sijapenda jeradi"
" Najua lakini inabidi nioe kuna mtoto mkali amezama moyoni mwangu".
" Mmh ananizidi"
"Eeh afu ujue kidogo unafanana ne" jeradi akazungumza na kufanya juliana acheke huku akishika silaha ya jeradi ambayo ikaanza kutii wito
" sikia hii ya mwisho piga kwa nguvu kama siku zot".Juliana akazungumza kwa sauti tamu ya kimapenzi
" hautoumia "?
" Fanya hivyo maana si unajua baba yako sikuhizi yuko bize sana " akazungumza bila aibu na jeradi akanyanyuka na kumgonesha doggy style mama yake mlezi

******** ****** *********

Randy akarudi kwake na kumkuta mary akiwa amekaa kitandani
" si ulikuwa umelala"
" Usingizi hauji mume wangu".
Randy akauma meno baada ya kuitwa ilo jina la mume wangu
"Ngoja nikuletee maji" .Akazungumza na kunyanyuka toka kitandani
" Mume wangu kuna jambo natak nikwambie". Mary akazungumza huku machozi yakianza kumtoka tena kwa wingi mno huku midomo ikiwa ina mtetemeka.Randy akasimama na kumtizam kwa kumkazia macho
"J.aan sijalala nyumbani ". Akazungumza kwa uwoga aliona bora ajilipue kuliko kuishi kwa mateso aliamua aseme ambacho kina msumbua moyoni wake hakutaka kuendelea kumsaliti mwanamume anayempa kila kitu mary alikuwa jasiri alikuwa shupavu na alitaka kusema kila kitu kilichotokea
" Endelea " Randy akazungumza na kumtizama mke wake kwa kumkazia macho na kufanya mary azidi kuogopa na kulia kwa uchungu
" Ja..naa mimi nililala nje" akazungumza na kufanya randy atingishe kichwa kwa mara ya kwanza akawa na huruma na mke wake
"Mume wangu me naomba nikwambie ukwel mume wangu,"
" Upi na ulilala wapi "?
" kuhusu mimi na mzee mmoja"
" ebu eleza ". Kwa upole muuaji hatari akanywea na mpka yeye akajishangaa hiyo ilikuwa nguvu ya mapenzi aliyokuwa nayo kwa mke wake mary alijikaza asipatwe na huruma lakini bado nafsi yake iliendelea kupambna na nafsi nyengine juu ya kutoa maamuzi kwa mke wake

" Miezi miwili iliyopita kwenye mgahawa ulonifungulia alikuja mzee mmoja na vijana wake wanne nilitoa oda wahudumiwe lakini mzee yule akahitaji kuzungumza na boss ambaye ndiyo mimi nikaenda kumsikiliza lakini akusema kitu zaidi ya kunitizama kwa zaidi ya sekunde 30 alidai nimefanana na mke wake alokufa"

"Mmh endelea " .Randy akazungumza
" Yule mzee akaanza kuwa anakuja kila siku pale huku akiwa anadai nafnana na mke wake akaanza kunitongoza, nisamehe mume wangu ,"

" Endelea"
mary akaanza kulia huku nafsi nyengine ikisema kwanini imemwambia

" Nikitaka nikwambie mume wangu ila ulikuwa hauji nyumbani mpaka week, nilikuwa muda mwengine sikupati kwenye simu randy, nilikataa sana nilikataa mume wangu sikuwa tayari kukusaliti ila siku moja nilishangazwa alikuja nyumbani na watu wake akiwa na picha zako pia walikuwa na bastola akanitisha sana kuwa atakuua nisipomkubalia alidai nafanana na mke wake kila kitu mume wangu nuru shahidi sikuwa tayari kwa jambo lake lakini niliogopa kukupoteza, akanipa siku moja lasivyo atakuua ndiyo jana hiyo nikaenda mume wangu nisamehe ".
Mary akazungumza na akashuka chini na kupiga magoti na kuanza kulia kwa uchungu siyo yey tu nuru pia akatoka chumbani mwake nakuja kumpa sapoti bossi wake
Hasira zote za randy zikaondoka majuto yakaja ni kwanini alitaka kumfanyia mke wake jambo la kikatili
" nina mimba mume wangu ni ya kwako randy na mtot wako pia nilihitaji kijiua.." KABLA ajamaliza kuzungumza mlio wa risasi ukasikika na kishindo cha mtu kikasika na damu kutapakaa chini ya vigae huku kichogo kikiwa na tundu la risasi alikuwa ni nuru mfanyakazi wa ndani alikuwa chini akitapa tapa kukata pumzi yake ya mwisho kabla randy ajajiuliza cha kufanya na mary kuwa ameduwaa bomu la moshi likatupwa kupitia dirisha na kuachia gasi kali na kufanya chumba kizima kujaa moshi randy akamuwahi mke wake na kujaribu kufungua kitasa ila kilikuwa kimebanwa na mtu upande wa pili wa mlango.wakaanza kukosa nguvu randy akajuta kwanini hakutembea na bastola akamtizama mke wake ambaye saa nyingi alikwishazimia akazidi kuchanganyikiwa akajaribu kufanya kila njia ila akashindwa na taratibu giza zito likatanda machoni mwake akazimia na mlango ukafunguliwa taratibu wanaume wanne wakaingia huku wakiwa na vifaa maalumu puani mwao wakatingisha vichwa na wakambeba randy na mke wake, haijulikani wametoka wapi na wamepitaje bila mbwa kubweka ila mbwa walionekana kuwa chini huku sindano zikionekana katika miili yao
Wakatoka nje ya geti na kuwaingiza mary na randy kwenye gari nyuma ya siti za nyuma ya gari lao kubwa jeusi tii..
****** ******* ******

MWISHO SEASON ONE

ITAENDELEA USIKOSEE CHAPTER 2 YA MKASA HUU WA KUSISIMUA........
COMING SOON
SEE ME (SEASON 2)
 
SEE ME

* CHAPTER TWO ( 2)**
(THE DEVIL)

SEHEMU YA KWANZA 1/50****

Watoto wa mtaani hawakuwa na makazi zaidi ya kulala nje chini ya madaraja makubwa ya jiji la dar es salaam baadhi walikufa kwa magonjwa huku wengine wakiugua na kuwa hali mahututi, wa mikoani,yatima,na hata wale waloachwa na wazazi wao mfano kutelekezwa,walokimbia kwao na kuja mtaani kupambna na shida wakihamini dar es salaam ni jiji la kutoboa
" Unaitwa nani"?
"Randy "
" waoh una jina la kizungu vipi umekula" mzee mmoja akazungumza na kumtizama kijana randy ambaye alikuwa amepauka na vumbi la kutosha pamoja na ukurutu wa kutokuoga huenda mwaka mzima
"Sote hapa hatujala".Randy akazungumza na kuwatizama wenzake ambao nao walikimbilia upande aliokuwa randy na yule mzee ambaye yumo ndani ya gari na akiwa amefungua kioo cha dirisha ili aweze kuongea na randy,ulikuwa ni usiku wa saa 4 kwenda saa chini ya daraja kubwa jijini hapo
" Una miaka mingapi".
"12".Randy akajibu na mzee yule akatingisha akaingiza mkono kwenye droo na kutoa bahasha ya kaki akashuka ndani ya gari na vijana wale wa mtaani wakamzunguka walikuwa wapatao 8 wote walihitaji chochote toka kwa yule mzee, akaanza kuwapatia mabunda ya hela ambayo kwa haraka haraka kila mmoja alipata efu50.
"Asante mzee ubarikiwe sana" wakazungumza na mzee yule akawaaga na kuingia ndani ya gari na kuacha wakimshangilia
" Ni vijana wadogo sana ila watatufaa katika kazi zetu miaka ijayo" Mzee huyo akazungumza na mzee mwengine aliyekuwa nyuma ya siti ambaye sura yake haikuonekana wakaondoka na gari lao la kifahari.
" Yule RANDY siyo muoga ni kijana mdogo anajihamini wenzake mwanzo waliogopa kuja wakijua sisi watekaji lakini yeye amejihamini na kuja ni kijan wa kitofauti sana" Mzee wa nyuma ya gari akazungumza
" week ijayo mje muwateke wote "
" sawa mheshimiwa "
" Hakikisha huyo kijan naye anakuwepo"
" sawa mkuu nitafanya hivyo".

Vijana wale walipagawa kwa pesa walizopata zilikuwa nyingi mno
" kesho tunaenda kununua nguo".
"Ndiyo tutapendeza" wakazungumza na kucheka na kifurahi pamoja hawakujua nini kitafata kwao walihisi ni msamalia mwema tu kapita kuwasaidia.....

Randy akakurupa toka kwenye kumbukumbu baada ya kumwagiwa maji ya baridi usoni mwake akawa ana hema juu juu, na kujaribu kunyanyuka ila akashindwa akahisi kichwa kizito huku macho yake yakiwa hayana nguvu ya kutizama vizuri bado aliona mawenge mawenge na taa iliyokuwa ikimulika sehemu hiyo alokuwepo akaona mwanamume mmoja akiwa na ndoo ya maji akija tena kummwagia huku uso wake ukiwa umefunikwa na kinyago sasa akashtuka alipoona mnyororo umefungwa miguuni mwake na mikononi pia afu kalalia mgongo juu ya meza ya chuma na mikono na miguu ikiwa imetanuliwa na kufungwa na minyororo, kumbukumbu zake zikaanza kurudi taratibu na akashtuka alipokumbuka kuwa alitekwa na mke wake na pia dada wa kazi kupigwa shaba ya kichogo akatoa macho na kumtizama yule mtu mwenye ndoo ya chuma yenye maji ya baridi,jamaa akaja na kumwagia usoni na kufanya randy azidi kuweweseka.
"We nani ? ".Randy akauliza na kujaribu kifanya chochote ila akashindwa
" Mke wangu yuko wapi?".Randy akazungumza na jamaa yule akageuka nyuma na kuondoka
"Jambo lolote likimkuta nakuapia shingo yako itakuwa halali yangu". Jamaa yule akageuka na kumtizama randy kisha akamnyooshea dole la kati
" *** you" akazungumza na kufanya randy ashtuke kwani na mwili wote ule kumbe alikuwa mwanamke alihisi ni mwanamume kwa jinsi mwili wake ulivyo na hata kifua chake akikuonesha kuwa ana maziwa
" We nani? " Randy akazungumza na kumtizama mwanamke yule ambaye sura yake hakuweza kuitambua.
Mlango ukafungwa na taa iliyokuwa inawaka ikazima na kufanya chumba kiwe giza na cha kutisha
" Ninyi kina nani" Randy akazungumza huku akijitingisha kwenye minyororo lakini hakufanikiwa kufany chochote
" Muacheni mke wangu" akazungumza na ghafla taa ikawaka na mlango ukafunguliwa wakaingia wanaume watano na mzee mmoja mfupi, wale wanaumea wakamfata randy na kumfungulia pingu za mikono kisha kumkalisha kwenye meza ile ya chuma huku miguu yake ikiachwa bado imefungwa.
Randy akamtizama mzee yule kwa kina huku akivuta kumbukumbu kuwa amemuona wapi akakumbuka kuwa muda mchache au siku chache zilizopita maana ajuhi hapo amekaa au amelala siku ngapi akakumbuka kuwa kundi lao lilimtumia Email ya picha na ujumbe mfupi kuwa mzee huyo anatakiwa kumuua , Ndiyo alikuwa ni mgombea urais wa chama kikubwa hapa nchini ni yule mzee ambaye mr solo na mr zengo walipanga kumuulia mbeya.

" Wewe ndo ulikuwa unatumwa uje uniue mbeya". Mzee huyo akazungumza na kumtizama randy kwa macho makali
" Kuna msaliti". Akawaza kuwa huenda kwenye kundi lao kuna msaliti anamwaga siri zao maana tanga alipoenda kumuokoa juliana alikamatwa na ilibaki kidogo afe.
" Unafikiria nimejuaje".
" Mzee mimi siyo muuaji " Randy akazungumza kwa upole kwani aliona kifo kipo pembeni.
" hahahah THE DEVIL " .Mzee huyo akazungumza na kufanya randy ashtuke kwani jina hilo ni jina lake la kazi na yeye ndiye muuaji hatari kuliko wote.
" Unataka nini? Na mke wangu yuko wapi" Randy akazungumza kwa sauti nzito na kumkazia yule mzee macho
" Hahaha Nahisi unajiuliza sana msaliti ni nani? Eeh DEVIL".Mzee yule akazungumza na kupiga makofi mara mbili.Mlango ukafunguliwa na wakaingia watu wawili alimuona mke wake akiwa mzima akiwa ajaumia popote uli macho yake yakiwa mekundu kwa kulia na kufanya make up yake ichafuke usoni na kuwa kituko jambo lililomkera ni kuona amefungwa minyororo,Randy akauma meno kwa hasira akawa anajitingisha kwenye minyororo na kufanya mzee yule acheke na kutingisha kichwa kwa masikitiko ya kinafiki, Mary alipomuona randy akafyatuka kama mshale na minyoror mkononi akamuwahi mume wake na kuanza kulia kifuani mwake mary alishindwa kumkumbatia vizuri kutokana na minyororo aliyofungwa, randy akamkumbatia mke wake kwa nguvu na wote wakaanza kulia kwa uchungu
" Mume wang nini kinaendelea" .Mary akazungumza
" Una mjua anayekaa na mke wako kipindi hiki tunakuhitaji". Mzee akazungumza na kutabasamu
" Maselo njoo ndani"
Mzed akazungumza na mtu anayeitwa maselo akaingia ndani huku akiwa anatumia gongo la chuma kutembelea na mguu wake ukiwa umefungwa na bandeji inaonekana alikuwa hatua za mwisho kupona.
Randy akashtuka kumuona yule jamaa mweupe wa tanga aliyempiga risasi ya mguu na kumvunja taya na meno matatu kutoka.

******* ***********
" ITAENDELEA USIKOSE KISA HIKI CHA KUSISIMUA " .....

SEE ME ( CHAPTER TWO )
THE DEVIL
 
NAKOSEA BAADHI YA MANENO ILA SEHEMU IJAYO NITALIFANYIA KAZI WA KUU......
 
SEE ME (THE DEVIL)

*CHAPTER TWO *
SEHEMU YA PILI 2/50

" Hatimaye tumekutana tena ". Maselo akazungumza huku akishika gongo lake ambalo anatumia kutembelea
"Umenifanya kilema wa maisha Randy nakuahidi mke wako atapitia kila aina ya mateso". Maselo akazungumza na kufanya mary moyo wake kwenda mbio kwani haelewi kichwa wala miguu
" Mtoeni huyu mwanamke" Mzee akazungumza na kufanya randy kumkumbatia mke wake kwa nguvu na kufanya mary alie zaidi ila jamaa wakamshinda nguvu wakamtoa mary mwilini mwa randy
" Jambo lolote likimpata mke wangu hii minyoror nitaikata". Randy akazungumza na kufanya maselo acheke kwa sauti.
" kwa sasa yupo salama ila usipofanya kazi yetu tutaanza na mtoto wako tumboni tutapasua tumbo na kutoa kijusi cha ndani na kuwapa mbwa".
Maselo akazungumza kwa kujihamini na kumsogelea randy
" Mnataka nini?" Randy akauliza
" Fanya kazi waliyokutuma nikienda mbeya nipige risasi ya kifua halafu jikamatishe kwa polisi useme mr solo ndiye aliyekutuma kuniua".
" Unataka nifie jela" Randy akazungumza na kumtizama mzee yule
"Ili maisha ya mary yawe salama fanya hivyo lasivyo tutamuua kama yule binti yako wa kazi". Mzee akazungumza na kufanya randy atokwe na machozi alitamani mungu afanye muujiza mnyororo ukatike kwani hakuna aliyemuweza ata kwa kumpiga ngumi ya bahati mbaya.
" nitavaa bulletproof risasi haitozama piga upande wa kulia wa kifua na kama ukitaka kuniua kweli mke wako maselo atadili naye usiku kucha na kisha hasubuhi kumuua kwa TINDIKALI".
" Nipo tayari kwa kazi yenu na nikimaliza nitahaminije mke wangu atakuwa salama wakati nitakuwa gerezani"
" Hahaha ili ni deal randy ukishafanya ilo tukio mr solo atapoteza wafuasi wake nchi itamkataa sitokuwa na shida na wew tena". Mgombea urais akazungumza
" Siwezi kukuamini ".
" Itakubidi unihamini" .Mgomba akazungumza kwa sauti ya msisitizo
"Nina siku ngapi hapa"?
" leo siku ya pili na nina siku tano za kujiandaa kwenda mbeya".
"Kwanini nisishirikiane na wewe badala ya njia unayotaka kutumia maana wenzangu wananisaliti". Randy akazungumza na kufanya maselo amtizame boss wake na kutingisha kichwa kuwa asikubali ofa hiyo.
" Unahisi upo salama ujiulizi kwanini kwenye kazi nyingi natumiwa mimi"? Randy akaendelea kumtongoza mgombea urais
" Acha kuzungumza upuuzi". Maselo akazungumza kwa kufoka
" Imagine mlinzi wako nilimvunja vunja unahitaji kunitoa sadaka". Randy akazungumza na kufanya mgombea kukunja ndita zake
" Kama msingekuwa mmenifunga muda huu wote mngekuwa vilema". Akazungumza randy kwa kujihamini na kufanya jamaa mmoja kumsogelea na kutaka kumkwida
" Boss usikubali ku make deal na huyu mpuuzi"
" Unahitaji nini ? Randy". Mzee akazungumza na kumtizama randy
" unahisi ukiwa rais utakuwa salama bila ya kundi langu kuhangamia kwenye serikali utakayotawala kwanzia askari ambaye hana cheo mpaka wa juu wote wana mizizi yetu"
"Kama ukinitoa sadaka utajutia kuwa rais"
" Unanitisha randy"
"Sikutishi ila fahamu mizizi ya serikali imepita kwenye makundi mabaya ambayo hata huyafahamu ".
" mkuu usikubali" Maselo akasisitiza
" Ukiwa rais utakufa mapema kama nisipokuwepo kipindi naenda tanga mmoja kati ya askari wako Amidu alinisaidia kufungua mkanda,nilokuwa nimefungwa na ndiyo nikapambana na kumvunja huyo taya, je kama amidu aliwasaliti wenzake vipi hawa watu walokuwemo humu ndani unawaamini wote"Randy akazungumza na kufanya mzee ashtuke na kumtizama maselo
" Amidu yuko wapi"? Mzee akauliza
"Hahaha kumbe ata ajakwambia amidu ni marehemu kwa sasa na alikinga risas iliyotaka kuniua mimi na me amidu simfahamu lakini akanisaidia vipi humu ndani wote unawaamini?". Randy akapiga msumari wa moto na kumfanya mzee aanze kuhisi ubaridi
" nipo tayari kwa kazi yako nitafanya ulivyotaka". Randy akazungumza huku moyoni akijua hiyo kazi mzee lazima asiitake tena maana randy alihakikisha anatumia UJASUSI WAKE KUMTONGOZA NDEGE WAKE


******* ******* ** *****
" Mkuu tumepeleleza tumegundua Amidu amefariki "
"Oooh *** vipi funguo mmepata"
"Funguo hatujaupata mkuu"
" Endeleeni kufanya uchunguzi ile funguo ipatikane ".kiongozi anayempaga kazi randy akazungumza huku akishushia mvinyo mkali wa konyagi huku akivuta na sigara kubwa ya kimarekani akazungumza huku akijaribu kupiga simu kwa randy ila haikuwa hewani toka jana mchana, Alihitaji kumpa randy information kuhusu kazi ya mbeya,kama alivyompa ya tanga akaifanya sasa alitaka kumpa kazi ya mbeya baada ya kupokea maelekezo toka kwa Mteja wake ambaye ni Mr solo
"Huyu bwege kaenda wapi na kwake siwezi kwenda". Akawaza

Mr zengo alikosa usingizi hakujua ni kwanini simu ya mary ilikuwa haipatikani kwani alihitaji tena penzi toka kwake mwanamke huyo ambaye anafanana sana na marehemu mke wake.
" Mary utajuta kunizimia simu". Akawaza na kukata simu hiyo ambayo ilidai haipatikani
" Niandalie suti nahitaji kutoka". Akazungumza na kunyanyuka uchi toka kitandani huku mfanyakazi wake wa ndani akificha macho yake.
" Njoo" akazungumza
" Boss samahani niliingia bila taarifa sikutaka kukuhamsha nilikuwa nataka nikuandalie nguo". Akazungumza kwa uwoga
" inama chini unyonye" Mr zengo akazungumza, binti yule akaanza kushuka chini taratibu na akapiga magoti na kushika kifaa cha mzee yule na kuingiza mdomoni hakuwahi kufanya ivyo ila ilimbidi kutii mana Mr zengo arudii amri yake
" Asssss ooh we kabila gani? " Mr zengo akazungumza huku akigugumia kwa utamu
" M..zaramo" binti akazungumza huku akiendelea kufanya alichoambiwa
"Oooh ingiza yote" mr zengo akazungumza na kushika kichogo cha binti yule na kusukuma kwa mbele na kufanya kifaa chake chote kuzama akambana binti yule na akashindwa kupumua akawa anagugumia sauti za kutaka kutapika mr zengo akamchomoa jogoo wake aliyejaa utelezi wa kutosha na kufanya mdomo wa yule binti kujaa mbegu zake.

****** ***** ***** ***
Mlango ukagongwa na kufanya mr zengo aache kitendo alichokuwa anafanya
" Ingia " akazungumza huku akianza kumvua binti yule nguo zake, akaingia mlinzi wake na alipoona kilichokuwa kinaendelea akatizama pembeni
" Kuna nin?"
" Ni kuhusu THE DEVIL"
" Amekuwaje?"
" Profile yake haipo katika kundi detail zote hazipo zinazomuhusu"
" oooh shit hatari mshenzi katugeuka"
Mzee akazungumza na hamu yote ikamuisha kihualisia hakuna mtu mmoja kati yao aliyetaka randy kuondoka kwa sasa walihitaji kumtumia mpaka mambo yao yakamilike

" MTAFUTE AMIDU ALETE FUNGUO NAMBA 28"

" Boss samahani AMIDU AMEFARIKI"

ITAENDELEA USIKOSE SEHEMU IJAYO HUYO KUHUSU AMIDU NA FUNGUO NA VIPI KUHUSU RANDY NI KWELI KAWAGEUKA WENZAKE NA MSALITI NI NANI.........????

SEE ME. ( THE DEVIL)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom