Riwaya: See Me (Nione)

Riwaya: See Me (Nione)

SEE ME
THE STORY MASTER....
BY..................Hancy abdon
SEHEMU YA 20/50
SEASON THREE......
Misson X

Kazi ilikuwa ngumu kwa randy alipaswa kufanya kila kitu ili kumtongoza X au diana hakutakiwa kumuacha msichana huyo,ilimbidi amteke kihisia na kulala naye jambo ambalo lilikuwa ni mbingu na ardhi........
ENDELEA.......

Baada ya randy kuachana na X ufukweni maeneo ya coco beach akaondoka na gari aliyokuja nayo huku moyoni mwake akiona kazi yake haitofanikiwa hata kidogi kwani X hakuonesha matumaini yeyote yale kuhitaji mazoea na randy aliyebadirisha sura yake.
"Mkuu msichana huyu ni mgumu sana". Nikazungumza na waziri mkuu aliyenipa kazi hiyo.
" Inabidi ufanye hivyo randy huwezi pambana na maadui zako kirahisi kama huyo msichana yuko hivyo".waziri akazungumza kwa msisitizo kupitia simu.
" Kesho inabidi napo niwe huku ufukweni". Nikazungumza
" Ndiyo wewe ni mwanamume tumia kila njia kuiteka akili yake yule ni mwanamke tu".
" sawa mkuu". Nikazungumza
" Kazi njema vipi hajakushtukia"
" ndiyo hajanitambua". Nikazungumza
" kuwa makini hasijekukutambua wewe nani?"
" Sawa mheshimiwa ila bado hujanambia ilikuwaje me mpaka sasa nikawa mzima".Nikazungumza
" Ukimaliza kazi yako nitakuambia kila kitu".
" nitamuua mr zengo ili kumkomboa mke wangu mary"
" Lazima tumjue sura yake sisi maana wewe unasema huikumbuki vizuri".
" ndiyo mkuu". Waziri akakata simu nikashusha pumzi nzito huku nikimkumbuka mke wangu mary aliyekatika mikono ya yule mshenzi...
*********
Siku iliyofata nikawahi eneo la tukio huku nikiwa nimepndeza zaidi na kujipulizia manukato bomba ya bei ghali, kila mwanamke aliyenitizama siku hiyo ni dhaili nilimvutia lakini lengo langu lilikuwa ni kumteka kihisia diana, aliyejitambulisha kwangu kama rose
Nilihisi nimewahi ila nilikuwa nimechelewa kwani nilimkuta X akiwa tayari ameshafika na ameketi kwenye mchanga.
" Mambo mrembo".Nikazungumza na kumtizama akageuka na kunitizama kisha akaendelea kunywa juisi yake kupitia mrija, macho yake akarudisha baharini.
" Wewe tena". Akazungumza.
" Harufu yako ya manukato nimeisikia toka kule, nikaikumbuka harufu hii ni ya jana sikutaka kuvumilia kutokuona mrembo kama wewe nisingetulia kusema kweli bila ya kukuona". Nikazungumza ila maneno yangu hayakumtia kichwani kwani ni kama aliona ni ngonjera tu
" Kwahiyo".Akazungumza
" Rose wewe ni mzuri sana unavutia kila mwanamume". Nikazungumza
" Kwahiyo". Akazungumza huku akinyanyuka kwa bahati mbaya akateleza nikamuwahi na kumkamata kiuno chake mithili ya movie za kihindi,walahi sikuwahi gusa au kushika kiuno kilaini kama kile toka nizaliwe ata cha mage na mary niliona vilikuwa vigumu, kiuno chake kilikuwa kilaini zaidi kama ute wa yai.
" We msenge niachie". Akazungumza na nikajidai kushtuka na nikamuachia, siyo kwamba alikuwa hana uwezo wa kujizuia asianguke ila nilitumia nafasi ile kama faida ya kumteka kiakili.
" Usije shika mwili wangu tena". Akazungumza na kugeuka ila nikamuwahi mkono wake.
" Nisamehe rose sitokushika tena".
" hapo umefanya nini?" Akaniuliza nikatizama mkono na kukuta nimemshika mkono wake wa kulia, ulikuwa wa baridi kama maiti.
" Samahani Rose" .nikazungumza kwa sauti ya unyenyekevu na kumuachia mkono wake, akageuka na kunitizama.
" Unataka nini?" Swali lake likafanya nishtuke nikahisi amenitambua au ana maanisha nini?.
" Ukaribu wako rose".
Nikazungumza na hakunijibu akanipa mgongo na kuondoka huku sehemu zake ndogo za nyuma zikitingishika alionekana kukasirika zaidi huenda alitamani kuniua, lakini yeye alikuwa ni muuaji wa kupewa maelekezo nani afe au mtu aliyemkosea katika majukumu yake ya kazi ni lazima angemuua.
"Vipi kaka anakutesa huyo na mapenzi". Sauti ikasikika nyuma yangu
Nikageuka na kumuona kijana mmoja.
" Ndiyo sana tu". Nikazungumza
" asee pole sana kaka vipi hakuelewi"
" ndiyo man"
" usikonde man pambana mpaka mwisho jaribu kumpa chochote ambacho kitamfanya afurahi".
" kama nini?"
" chochote man".dogo huyo akazungumza na kuondoka nikabaki njia panda.
*******
Siku ikiyofata sikutaka kwenda kumfata nilimuona siku hiyo lakini hakuwa peke yake, alikuwa na mwanamume alijazia misuli ya kutosha mwilini mwake nilijua alifanya vile ili nisisogee eneo lile aliyopo, nikatizama watu wanavyoogelea na kumuona akiwa anatizama huko nami nilihitaji anione nikaenda eneo ilo huku nikijitahidi nikiwa bize bila ya kumtizama, sikitaka kuvua shati maana angeniona jeraha alilonikata mgongoni nikajitupa kwenye maji hivyo na kuanza kuogelea na kundi la watoto nikamuona akitabasamu...............

SEE ME
MISSION X

( sitowaacha wasomaji wangu )
NEXT EPISODE
COMING SOON
 
SEE ME

SEHEMU YA 21/50
MISSION X
SEASON THREE

Nilimuona X akitabasamu sikujua aliniona na kutabasamu na mimi alivyoona nacheza na watoto au aliona siwezi mfata maana yupo na mtu mwenye misuli.
" kaka una ogopa nini? Nenda ukaeleze hisia zako". Yule kijana wa jana akaja kunambia inaonekana alikuwa anafundisha watu kuogelea.
" Mmmh". Nikaguna
" huu ndio muda wa kueleza hisia zako kwake ili aone unavyompenda na kutomuogopa yule mtu ambaye anaonekana ni mlinzi wake na walo som mtu wake".
"Umejuaje"?
" hawaendani". Akazungumza na akili yangu ikanituma kuwa huo ndiyo wakati sahihi wa kwenda pale
" Uuuh". Nikavuta pumzi ndefu na kumtizama kijana yule aliyeonekana kunikubali zaidi nikajikaza kiume siyo kwamba nilimuogopa yule jamaa wa miraba minne hapana kwani uwezo wa kumuangusha chini ndani ya sekunde kumi tu nilikuwa nayo shida nikukubali ngumi takazokutana nazo za yule jamaa.

Nikakata shauri na kwenda kule alipo X aliponiona akamtizama yule mtu wake.
" Mambo rose". Nikazungumza yule jamaa akanikazia macho
" vipi kaka". Nikamsalimia ila hakunijibu
" Uogopi". Jamaa akazungumza
" Siwezi kukuogopa nipo kwa rose kueleza hisia zangu nampenda sana rose ni mwanamke mrembo aliyetokea kuchanganya akili yangu ghafla". Nikazungumza huku machozi yakinilenga sikutambua yalitoka wapi.
" oooh nitakuvunja".
" wewe una miraba minne lakini huwezi jua maumivu ya moyo wangu sitopata maumivu mengine zaidi ya nayopata toka kwa rose". Nikazungumza na x akanitizama kwa umakini hiyo siku nilijua maneno yangu yamezama kwenye moyo wake.
Jamaa akanisogelea ila akaja yule dogo na kusimama mbele ya yule jamaa wa miraba minne.
" Huwezi fanya chochote hapa". Dogo akazungumza kwa kujihamini na kufanya nishangae na kutizama mwili wake kama kidari cha kuku.
Akapiga mluzi na wakaja watu wengine na maua mengi mikononi mwao waliibuka tokea kwenye mwamba uliokuwa pembeni, mikononi mwao walikuwa na maua rose tena yale ya kuvutia...
Sikujua dogo kamjua jina muda gani na kafanya hayo mambo saa ngapi?
" kaka kazi uliyotutuma tumeifanya tumetafta maua rose usiku na mchana na hata lile ua ambalo kidogo likuue barabarani kwa kukoswa na gari tumekuja nalo".Akazugumza uongo mtupu nikamuona X kifua kikipanda na kushuka.
" Rose nakupenda sna sijawahi ona mwanamke kama wew". Nikapewa ua na kulipokea nikapiga goti moja chini na kumnyooshea rose mkono apokee ua ilo, yule jamaa akataka kufanya kitu ila kundi kubwa la watu lilikuwa eneo ilo uwenda angepigwa sangi na wananchi...
Rose au X midomo ikawa inamtetemeka kwa mara ya kwanza nikamuona muuaji X akiona aibu akatizama kundi la watu na kunitizama kisha akachukua ua lile na kusimama juu.
" Nakupenda". Nikazungumza na rose au X akatizama ua lile na kulivunja
" Nipishe".


SEE ME
ITAENDELEA..............
 
SEE ME
SEHEMU YA 22/50...
AGE............................18+
SEASON THREE
MISSION X

"Nipishe". Rose akazungumza na kutupa vipande vya ua alilolivunja, uso wake ulijaa hasira za wazi, nikajikaza kiume na kumfata nikamshika mikono yake iliyokuwa ya baridi kama maiti akawa anajaribu kuitoa ila akashindwa nikambana vizuri na watu wakaanza kushangilia na kupiga makofi, Rose akajitoa kwa nguvu maana nilitaka kumvuta kifuani mwangu kisha akanisogelea na kunambia maneno sikioni mwangu..
" Nitakuua". Akazungumza na kisha kuondoka watu wakampisha njia na yule baunsa naye akafata na wakaelekea kwenye gari yao. Watu wakatawanyika huku wengine wakibaki wanashangilia kwa ujasiri wangu.
" Umejuaje anaitwa rose". Nikamuuliza yule dogo
" nilikusikia siku unapomuuliza jina lake maana nami nilihitaji kumtongoza huyu binti sasa nikataka kujua hisia zako kwake".
" mmmh unamtaka".
" kwa sasa hapana".
" umewezaje kufanya hivi?"
" uwa sipendi mwanamume mwenzangu au kijana mwenzangu hisia zimtese nimeamua kufanya hivi ili huyo msichana akuwaze zaidi"
" unahisi hii njia itasaidia".
" ndiyo ila siyo sana na hatokuja hapa tena inabidi umfatilie anaweza kuhama ili eneo au akaja kwa kujificha".
" oooh inaonekana unajua sana mapenzi".
" siyo sana kaka".

**************
Mr sengo hakuamini kwa kitu anachikiona mbele ya macho yake aliona ni kama ndoto, alifumba macho na kufumbua taratibu lakini jambo lilikuwa ni lilelile alimuona mtoto wake jeradi akiwa nyuma anapiga kitumbua cha mama yake kwa kasi ya ajabu, alikuwa anasugua huku akipiga makofi makalio ya juliana na kufanya yatingishike, .
Wote wawili walishtuka walipomuona mtu aliyelala kitandani miezi miwili bila ya kufumbua macho sasa alikuwa akiwatizama kwa kitu wanachokifanya kwenye sofa, presha ikawa kubwa kwa juliana kwani mume wake alimuona vyema na machozi kumlenga lenga juu ya uchafu na dhambi iliyokuwa ikitendeka
" Baba". Jeradi akazungumza na kumchomoa jogoo wake aliyenywea ghafla kwenye kitumbua cha mama yake mlezi. Akamuona mzee wake machozi yakianza kumtoka
" Mume wa...ngu". Juliana akaita huku akinyanyuka toka kwenye sofa na kujaribu kwenda kitandani kumfata mr sengo ila jeradi akamzuia.
" haongei njoo". Jeradi akazungumza huku akitaka kuendelea na mchezo aliokuwa anaufanya kwa mama yake,Mashine inayohesabu mapigo ya moyo ikaanza kupiga alamu ya hatari kuwa maisha ya mzee huyo yapo hatarini akaanza kutetemeka kama mtu anayekata roho, kwa haraka, daktari wa familia akasukuma mlango na kuingia ndani, tukio aliloliona likafanya asimame kwa sekunde kadhaa kwani mama na mtoto walikuw uchi wa mnyama.
" Fanya kazi yako akifa nakuua". Jeradi akazungumza na kumfanya dokta arudishe mawazo yake kwa mgonjwa wake huku akiwa haamini anachokiona machoni mwake, alijua fika ndiyo kilichoperekea mzee huyo kuwa katika hali hiyo. Akaanza kushtua mapigo yake ya moyo yaliyokuwa taratibu yakitaka kumpereka mzee peponi kama siyo motoni, akajitahidi kurudisha mapigo ya moyo ya mr sengo ndani ya dakika mbili na akafanikiwa mzee mapigo yake ya moyo yakarudi kama kawaida, akaanza kupumua.
" Umeona nini?" Jeradi akamuuliza dokta na kumsogelea huku jeradi akiwa uchi wa mnyama na wakatu huo juliana alikuwa tayari kashavaa nguo zake.
" Sijaona kitu mkuu".
" wewe hujaona sisi tupo uchi" jeradi akazungumza na kushika makende ya dokta na kuyabinya kwa nguvu na kufanya dokta aanze kutetemeka na kugugumia kwa maumivu makali anayoyapata.....

***************
Hakuwahi kulala na mwanamume wala kuingiziwa jogoo wa mwanamume ndani ya kitumbua chake, alisikia wanawake wenzake na mabinti wakipata raha toka kwa wapenzi wao, alisikia mapenzi ni matamu kama asali, alijua uchungu wa mapenzi kwani miaka mingi iliyopita mpenzi wake alimkimbia kitandani tena mwanamume aliyempenda zaidi ndani ya moyo wake alimkimbia kitandani na kumtukana matusi makali na kufanya kulia na kuumia kwa uchungu na kuona mapenzi ni UONGO.
NDIYO diana au X hakuamini tena kama mapenzi ni kweli aliona ni uongo na uongo mtupu hakutaka kumpa mwanamume tena moyo wake, alijiapia kutopenda tena, akavua chupi yake na kujitizama sehemu zake za siri akajikuta akiumia na kumlahani mwenyezi mungu kwanini amemuumba hivyo, X alikuwa ameumbwa na jinsia mbili ya kike na kiume yani alikuwa na mboo na kitumbua pia, mboo ilikuwa ndogo tena iliyokuw imekosa nguvu ilikuwa haina uwezo wa kusimama lakini kitumbua chake kilikuwa na hisia za kike, akakumbuka siku mpenzi wake alipomkimbia chumbani baada ya kumuona akiwa na maumbile yale, machozi yakamtoka na akafungua maji na yakaanza kushuka mwilini mwake huku taswira ya kijana wa beach ikija kichwani mwake, alikuwa ni randy lakini hakumtambua.
" Ni kweli ananipenda ila hawezi lala na mimi lazima atanikimbia" . Akawaza
" Nitamuua". Akazungumza na kujipaka sabuni mwilini mwake, umbo lake lilikuw la kuvutia lakini sehemu zake za siri zilikuwa mbili.
" lakini kama ananipenda kweli".
" mmmh siwezi ruhusu akapenya moyoni mwangu mimi ni muuaji".
" hutaki mtoto" . Akawaza huku akijiuliza yeye mwenyewe
" hawezi lala na mimi".
" nitamuua kama akinikimbia". X akawaza na kutikisa kichwa chake sasa alihitaji kulala na randy, hakujua hisia hizo zimetoka wapi alijikuta hakihitaji mboo...


***************** USIKOSE************
SEE ME
. MISSION X
 
SEE ME
SEASON THREE
AGE.......................18+
SEHEMU YA 23/50
MISSION X

Sasa x alihitaji mwanamume hakujua kwanini hisia zimempanda ghafla hivyo hakutaka zitokee katika mwili wake,akakumbuka siku yule kijana wa beach alivyomshika kiuno chake,akafumba macho yake kwa hisia kali huku akitetemeka hisia zilimtesa lakini hakutaka kukubali mawazo yake alijihamini yeye ni shetani hawezi teswa na mapenzi.
" Siwezi kuwa dhaifu". Akazungumza na kufumba macho yake kisha akafumbua na macho yake yakawa mekundu zaidi ya mvuta bangi wa kariakoo,
" Napaswa kuwa hivi". Akazungumza na sauti nzito ikamtoka ilikuwa sauti ya jini tena jini la japani,kama angemtizama yule kijana wa beach akiwa na macho ayo basi angemtambua kuwa ni randy na angemuua hapo hapo lakini alishindwa kumtambua Maana hakumtizama kupitia jini lile lililopo mwilini mwake, lilikuwa jini hatari (TAKSUDA)
*********
" Lazima nikutane na mage". Nikawaza
" Atanijuaje sasa"
"Lazima nijue kama mke wangu alimpigia simu ". Nikwaza na kuondoka kwenda kwenye hoteli anayopiga kazi mage nikafika na wadada wote kunitolea macho nilionekana mgeni kwenye na nyuso zao na niliwavitia kutokana na USO wangu bandia.
" Samahani mage naweza muona". Nikazungumza na dada wa mapokezi.
" Mmmh mage aliacha kazi miezi miwili iliyopita".
" Ooh una mawasiliano yake unisaidie".
" Kaka yangu huogopi mage anataka kuolewa na kijana wa mr sengo na ndoa Yao kesho kutwa tu we achana naye kaka yangu sikushauli wale watu wazito". Dada yule akazungumza na kufanya nishtuke kidogo jina la Jeradi likapita kichwani mwangu maumivu makali ya kutobolewa macho yakafanya kichwa changu kuanza kuuma, hasira zikanikamata na kushuka meza nisianguke.
" Uko sawa". Akaniuliza na kutaka kunishika mikono ila nikamzuia
" Ndoa inafanyikia wapi?".
" Mlimani city". Akazungumza na kufanya moyo uanze kuniuma wivu ulianza kunishika sikutambua kwanini moyo wangu ulinisaliti na nikakili kuwa nilikuwa nampenda mage.
" Nitakuua Jeradi". Nikawaza na kuondoka nikafika kwenye gari yangu na kupanda kisha kuondoka huku mawazo mengi na hasira juu ya Jeradi ikichukua nafasi, sasa nilihitaji kumuua nilihitaji kumteketeza kwa maumivu makali.
" Nitakukata sehemu za siri". Nikazungumza na kutizama bango kubwa lililokuwa pembezoni mwa Barabara lilikuwa na picha ya Jeradi na pembeni kukiwa mage..
" Sitojali kama ana mimba Yako". Nikazungumza na kutizama tumbo la mage dogo na kuapia kuwa lazima nitamuua Jeradi.
" Nitafute tiketi". Nikazungumza na kuchukua namba zilizokuwa zimeandikwa kwenye lile bango na ilikuwa Namba kwa ajili ya kupata tiketi iliyokuwa inauzwa lakimoja.
" Mshenzi anauza tiketi laki". Nikwaza na kupiga namba zile na ikapokelewa
" Karibu tukuhudumie unaitwa nani? Unapiga simu toka wapi?". Sauti ikasikika
" Naitwa Frank wa mbezi". Nikazungumza.
" Okay unahitaji tiketi Maana zimebaki 20 pekee kwa watu wa kawaida".
" Ndiyo nahitaji tiketi".
" Tuma hela kwenye hii namba na utatumiwa tiketi Yako kwenye simu".
" Dakika mbili". Nikazungumza sikuhitaji kujiuliza maswali mengi nikanakili ile namba na kisha kutuma laki Moja, kwangu haikuwa kitu kama macho yangu hata kama dada huyo angenitapeli.
Nikapiga simu na akapokea
" Vyema sana inaonekana unapenda sana sherehe kubwa okay tiketi Yako tumekutumia". Akazungumza nikatizama simu na jumbe ikaingia .
" Inatumikaje"
" Ukifika getini hiyo siku kuna chombo kina scan hizo namba na itasoma utapita".
" Asante"
" Karibu". Nikakata simu na kutizama muda wa sherehe ile ilikuwa ni saa Moja usiku.
" Lazima nipite na kuku wangu". Nikawaza.

**************
SEE Me
Usikoseeee.......
 
SEE ME
SEHEMU YA 24/50
Season three
Mission x
Age.......................18+
Author...........................hancyabdons

***********
"Sasa nahitaji kukutana na rose(x)".Nikawaza na kuendesha gari yangu kwa ajili ya kwenda kwenye mizunguko yangu huku nikiwaza pa kumpata rose ili mission yangu iendelee kwani beach sikumkuta hiyo siku nilisubiri zaidi ya Lisaa lakini hakutokea.
" Tampata wapi huyu nyamela". Nikawaza huku akili yangu ikiwa ina list zaidi ya watu wanne ambao nilitaka kuwaua.
" Lazima kesho atakuwepo mlimani city nitajitahidi kujificha". Nikawaza huku nikitingisha kichwa nikafika nyumba nayokaa kisha nikatoka bastola ndogo kwenye droo ya kitanda nikatizama risasi na kukuta za kutosha.
" Lazima nimteke".
Nikazungumza na kuchukua ile bastola na kuitia ndani ya koti langu kisha nikachukua simu yangu na kutizama jengo la mlimani city ambalo limekwisha pambwa na linapendeza zaidi kwa jinsi lilivyopambwa na kampuni hiyo ya mapambo.
" Lazima nimteke"

**********
Mr zengo akajikuta akishtuka baada ya kumuona Mwanamke ambaye akili yake ilisema inamtambua akajaribu kupingana nayo lakini bado ilisema inamtambua Mwanamke huyo aliyesimama pembezoni mwa barabara hiyo, Mwanamke huyo alikuwa akijiandaa kuvuka barabara,
" Muiteni yule Mwanamke". Akazungumza na kuwaambia walinzi wake wawili alikuwa nao ndani ya gari akawasonteshea kidole Mwanamke yule na wale jamaa wakashuka na kumfata Mwanamke huyo.
" Nyie vipi?"
" Samahani unaitwa pale". Jamaa mmoja akazungumza na kufanya Mwanamke yule kutizama lile gari mapigo ya moyo wake yakaenda mbio na hakujua kwa nini.
" Siwajuhi". Akazungumza na kutaka kuondoka ila jamaa akamuwahi mkono na kumshika kwa nguvu
"Nitapiga kelele". Akazungumza ila jamaa akapokea maelekezo toka kwa Mr zengo kupitia kifaa cha mawasiliano kilichokuwa sikioni mwake.
" Mchukue kwa nguvu"
" Sawa mkuu".jamaa akamjibu Mr zengo kwa Kasi ya ajabu akamvuta Mwanamke yule na kumbeba.
Akaanza kupiga kelele huku akirusha rusha miguu wasamalia wema wakaja wakijaribu kumuokoa
" Hatuwezi mteka mtu hasubuhi hii
Huyu ni mwanafamilia yetu" jamaa mmoja akazungumza huku yule mwengine akifanikiwa kumuingiza kwenye gari.
" Barabara hii ina kamera hatuwezi mteka mtu sura zetu zikiwa wazi". Jamaa akazungumza na kufanikiwa kuwatongoza wale raia ambao wengi walikubali maneno yake. Kwani kelele za Mwanamke yule hawakuzisikia tena, hawakujua kuwa alikuwa amezimwa.
" Nipereke nyumba yangu ya siri".
Mr zengo akazungumza na dereva wake akatii akapangua gia na gari ikaanza kwenda sehemu aliyotaka kupelekwa ndani ya jiji kwenye nyumba yake ya siri, akamtizama yule Mwanamke kwa umakini zaidi alikuwa mzuri na wa kuvutia licha ya umri wake kuwa mkubwa.
" Nishamuona wapi? ". Akawaza na ghafla mapigo yake ya moyo yakaanza kwenda kasi,akajivuta vizuri na kumfunua Mwanamke yule kifuani kwenye ziwa lake la kushoto akashtuka baada ya kuona alama ya kovu la moto likiwa na chapa yake.
" Grace upo hai". Akazungumza huku USO wake ukionekana kupatwa na furaha ya ajabu akajihisi mshindi sasa, akaona sasa anakwenda kupata amani ya moyo wake anakwenda kumpata mtoto wake, kwani grace alitoroka na mimba yake.
Wakafika nyumba hiyo ya siri walinzi wakambeba grace na kumpeleka kitandani alipoagiza Mr zengo, wakafika na kumuweka.
" Muamshe". Akazungumza na jamaa mmoja akashtuka mishipa ya fahamu ya grace na akafumbua macho taratubu na kuninyoosha kama mtu aliyetoka kwenye dimbwi zito la usingizi alipomuona Mr zengo akashtuka na kukurupuka kitandani
" Grace". Mr zengo akamuita na kumfata na kumkumbatia kwa nguvu kitandani pale, akaanza kulia kwa uchungu, jambo lililomfanya grace kushindwa kuzuia hisia zake naye akaanza kulia
" Upo salama".
" Eeh"
" Kwanini ulinikimbia". Akazungumza kwa uchungu mr zengo
" Ulitaka nifie mikononi mwa mke wako". Akamjibu na kulia pia
" Grace ".Mr zengo akamuita
" Nimeteseka sana Mr zengo niache".
" Nisamehe".
" Nimeishi maisha magumu sana nilipojifungua mtoto".
" Uli..jifungua". Akamuuliza, grace hakutaka kuficha chochote sasa alihitaji kusema kila kitu
" Ndiyo wa kiume"
" Yuko wapi?" Mr zengo akazungumza na kutizama grace anayelia kwa uchungu zaidi.
" Mmmh Yuko wapi?".
" Umemuua mwanao". Grace akazungumza na kufanya Mr zengo kushangaa
" Miezi michache nyuma kijana waliyemtoboa macho ndiyo mtoto wako namaanisha randy". Mzee akashtuka na mapigo ya moyo kwenda kasi.

####$***
" Naua ndege wawili kwa jiwe Moja". Randy akazungumza baada ya kuwaona wageni waalikwa wa sherehe hiyo sura ya mr zengo sasa aliikumbuka vyema alimuona vyema Mzee huyo aliyekuw anakula utamu WA mke wake.
" Nitawakata vipande vipande"..


See me
Itaendelea...........
 
SEE ME
SEHEMU YA 25/50
Season three
MISSION X

******** Mr zengo alitamani ashtuke toka usingizi na kukuta anachoambiwa na grace kuwa ni ndoto, na siyo kweli randy haiwezi kuwa mtoto wake moyo wake na akili yake havikutaka kusadiki maneno ya grace.
"Unanitania?". Mr zengo akazungumza na kumtizama grace anayelia kwa kwikwi, akamshika mabega yake na kumtizama machoni, wote walikuwa katika hali mbaya ya majonzi
" Inawezekanaje"?
" Siku nayojifungua mtoto kuna mtu alimchukua". Akazungumza na akalia.
" Nani?"
" Don john".
Mr zengo akashtuka na kuzidi kuchanganyikiwa
" Nieleze ukweli wote".
Grace sasa hakutaka kuweka mambo siri alihitaji kila kitu kiweze kujulikana kwani kateseka sana mtaani sasa alihitaji aseme ukweli wake wote ili atakapokufa asidaiwe kitu, alihitaji kusema kila jambo.
"Mke wako alinifatilia sana akitaka kuniua alipogundua na mimba Yako, alifanya kila njama lakini alifeli,".
"Siku nayojifungua mtu wako wa karibu alikuwepo na alinisaidia, mkeo alikuwa karibu na Mimi alifanikiwa kunifikia, akitaka kuniua na kunipoteza duniani, kabla sijawa ki mahusiano na wewe nilikuwa natembea na mtu wako wa karibu".
Akazungumza na kumeza fundo la mate na kufanya Mr zengo amtizame kwa umakini zaidi.
"Mkeo alinishikia bastola siku nayojifungua akitaka kupiga tumbo langu risasi ila nikashtukia yupo chini na damu zilikuwa zikimtoka kichwani, alikuwa kapigwa risasi ya kichwa na mtu wako wa karibu". Mr zengo akameza mate na kuzidi kuchanganyikiwa akili yake ikawa ishamjua huyo mtu wa karibu ila alihitaji kupata uhakika zaidi.
" Alimuua mke wako ili Mimi na mwanao tubaki salama, pia alikuwa akinipenda ndiyo Maana akafanya hivyo, nikipata uchungu na nikajifungua mtoto wa kiume, na don john ndiye aliyemuita Randy". Akazungumza na kulia kwa uchungu
" Alimchukua mtoto wangu akiwa mdogo na kuniacha na watu wake walionisaidia mpaka nikawa vizuri, nilimuhitaji mwanangu ila hakunipa alisema anahitaji apite mikononi mwako awe kama wewe na akifikisha miaka 10 atakutambulisha kwake, siku mnakamata watoto wa mtaani kuwapeleka japani ile usiku nilikuwepo na nilimuona randy kwenye lile kundi la watoto baada ya ya don john kunionyesha, alikuwa ni mwanangu kweli, sikumshika ata mikono yake wala miguu yake wala kichwa chake, lakini macho yake yalikuwa Yako kabisa kipindi kile ukiwa bado kijana siyo kama sasa".
Mr zengo majonzi yakazidi kumshika
" Umemuua mtoto wako don john Amenambia kila kitu".
Mr zengo akaanza kulia kwa uchungu moyo wake uliuma na kujiona mwenye hatia, alihisi amefanya dhambi kubwa ambayo Mungu haiwezi kumsamehe, akamkumbuka randy na kujikuta akizidi kulia kwa uchungu baada ya kukumbuka ile siku anayompa mateso makali na moyo wake ukawa unauma kwa mateso Yale hakujua kwanini alimuonea huruma randy sasa alitambua damu ni nzito kuliko togwa..
" Don john". Akawaza kichwani mwake, na taswira ya mary ikaja kichwani mwake akamkumbuka jinsi alivyokuwa anamtumikisha kingono mke watoto wake, tena kukiwa na mjukuu wake ndani, akajikuta akisimama na kuuma meno yake kwa hasira, sasa alihitaji kutubu dhambi zake, alihitaji kurudi kwa Mungu na kumsujudia, akitaka kupokea huruma toka kwa muumba.
Lakini moyoni mwake akawaza kuua mtu ndiyo alihitaji kumuua don john kabla ya yote..
Grace akazidi kulia na kuanza kukohoa akaziba mdomo wake na kukohoa huku akionekana kupata maumivu makali zaidi, mr zengo akatoa mikono ya grace kwenye kinywa akashtuka baada ya kuona mikono yake ikiwa imejaa damu..
" Nini hiki"?
" Nina cancer ya damu". Akazungumza kwa uchungu na kufanya Mr zengo ashtuke na kupata majonzi zaidi.
" Daktari kanambia nina wiki chache sana za kuishi". Akazungumza na Mr zengo kumkumbatia kwa nguvu.
" Nipereke mlipo mzika mwanangu au mlipomtupa nikaone ata mifupa yake au kama mbwa wako walikula nyama yake nipereke kwa huyo mbwa nimuone". Akazungumza na kufanya Mr zengo kulia kwa uchungu mpaka kamasi kumtoka.
" Hajafa". Mr zengo akazungumza. Grace akajitoa kifuani na kumtizama Mr zengo kwa mshangao
" Don john alisema kafa".
" Yupo gerezani". Mr zengo akazungumza.
" Mmh uongo".
" Niamini Mimi". Akazungumza kwa sauti ya chini zaidi.
" Nataka kumuona".
" Nitatuma watu wamtoe na kumfanyia upasuaji wa macho yake".
" Sawa".
***************
Moyo wake haukuwa na amani alihisi siku zake zimefikia tamati, kila akikaa alihisi kujutia juu ya makosa aliyoyafanya miaka mingi iliyopita, wivu, hasira na chuki vilitawala moyo wake Wakati ule wa zamani, hakutaka kumuona Mr zengo akiishi kwa furaha na mtoto aliyezaa grace mwanamke aliyempenda kupita maelezo, akitaka kumuweka mtoto yule mbali na baba yake na alifanikiwa kufanya hivyo, hakutaka kumuua Maana alitoka kwa Mwanamke ampendaye, sasa alijihisi hatia, moyo wake ukamwambia kwa sasa yupo sehemu hatari zaidi akakusanya pesa za kutosha zaidi ya dola millioni mia mbili, na picha zake muhimu akachukua visa na pasipoti za kisafiria alihitaji kwenda mbali nje ya nchi ulaya ilipo familia yake, ni Don john.
************
Siku ya sherehe ya jeradi ikafika na mage watu wakubwa mbali mbali walikuwepo na watu wa kawaida wapatao 30 na randy alikuwa ni mmoja wapo, kazi yake kubwa ilikuwa ni kukamata kuku wake,.
Sikutaka nijulikane nikaenda sehemu ya jikoni iliyokuwa ndani kabisa ya ukumbi huo mkubwa, nilimuhitaji kupata kofia na mavazi ya kipishi.
" Samahani njoo mara Moja" .nikazungumza na mpishi mmoja aliyenipita na kutaka kuingia jikoni, nikatizama kamera na kuona ikigeuka upande wa kulia na Mimi nilikuwa wa kushoto, alipofika nikambinya shingo yake kwa haraka na akazimia na nikamdaka asidondoke kama mzigo, nikamburuza na kumuingiza jikoni na bahati nzuri hapakuwa na kamera wala mpishi mwengine, nikamkokota na kumvua nguo zake za kipishi na kofia kisha nikamlaza chini ya meza kubwa ambayo juu ilikuwa na imekandiwa ngano na chini kulikuwa na Giza kwahiyo asingeweza kuonekana kirahisi, nikavaa mavazi yale na kutoka mule ndani ya jiko.
." Unafanya nini huku wenzako wanahudumia kule".
" Samahani ". Nikamjibu mzee mwenye suti aliyeniuliza baada ya Mimi kufungua mlango
" Wahi haraka we namba ngapi kwanza"?. Akaniuliza nikajikuta nikiropoka tu
" Nane".
" Sasa unafanya nini huku ulitakiwa kuwa kwa Mr zengo kule"
Akafoka na nikafurahi kimoyo moyo
" Samahani mkuu". Nikazungumza na kuondoka chapu huku mzee yule akiendelea na taratibu zake nikafika ukumbini na kumuona jeradi akiwa amesimama huku akiwa na Pete ya uchumba mkononi, hiyo siku ilikuwa ni ya kumvalisha Pete ya uchumba mage. Mage alikuwa amesimama na jeradi kapiga goti Moja chini, nikataka kuona kama mage atakubali ila nikamuona Mr zengo akinyanyuka toka kwenye kiti na kuondoka na akafatwa na mlinzi mmoja nikataka kumfata chapu kwani alikuwa anaenda chooni, mkono wangu ukashikwa na mikono milaini, na nikavutwa na kutolewa eneo ilo la mlangoni nililiokuwa nimesimama, ilikuwa ni mlango wa kuelekea jikoni kule... Mtu huyo akanibana ukutani na kufanya nishtuke kwani alikuwa ni X ( rose,Diana)

Je nini kitaendelea......
Usikoseeeeeee...

See me
Season three
Mission x
Maoni Yako muhimu................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom