SINA CHAGUO
Simulizi tamu ya maisha, iliyosheheni visa na mikasa ya kuzisisimua hisia chanya za msomaji. Ukafumbuka macho uone, yazibuke masikio usikize kwa usahihi kila kilichotamkwa na kuzungumzwa na mwandishi kupitia wahisika bora waliochorwa kwa taswira za kuvutia.
Utavutiwa na mengi; yatakayouteka umakini wako, utamani kujua nini kiliendelea nje ya kile kilichoongelewa. Ni wazo la mwandishi kwamba ukajizatiti zaidi kunako maudhui mazuri yaliyofichwa ndani ya kila sentensi inayounda tungo tamu za simulizi hii.
Hakuna wazo hewa, kila aliyewaza alikuwa na sababu ya kufanya hivyo. Aliyezungumza alilenga kufikisha kile kilichoujaza mtima wake. Macho hayana pazia, kuna anayeona kwa kukusudia mwingine akakusudiwa na alichokiona. Matendo ndiyo hutoa tafsiri halisi ya mtu.
✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️
Karibuni sana wapenzi wa simulizi. Leo naitambulisha kwenu simulizi hii tamu iendayo kwa jina la SINA CHAGUO. Mwandishi anakukaribisheni sana kutoa maoni, kwa wakati wote usomapo simulizi hii.
SEHEMU YA KWANZA.
(Hakika mimi sijui, Fungu jema kuchagua,)
Huenda kile nilichopitia enzi za utoto wangu ndicho kimeniumba na kunifanya niwe hivi nilivyo sasa. Mimi ni nani? Swali hili huzisumbua sana fikra zangu kila nikiutafakari uhusika wangu ndani ya simulizi ya dunia. Mala zote siachi kujiuliza chaguo lipi huwa ni zuri kwangu kupita yote, maana sijui kuchagua. Si kwamba sioni, hapana. Nimejaaliwa bahati ya kukutana navyo, jicho zuri la kuona na kuvitambua vilivyo vizuri. Huwa natamani sana kuvipata, lakini sina uhakika kama nimeshawahi kujutia kuvikosa. Kuna wakati huwa naafikiana na kile wakisemacho wengi juu yangu, “wewe si mtu wa kawaida, ni mtu wa ajabu sana; unayefurahia kupata au kukosa kile ukitakacho.” Wakati mwingine siafikiani nao, kwasababu huwa ninapatwa na hisia tofauti katika kukosa na kupata, ijapokuwa huwa ninalidhishwa na yote. Kipi sasa hunifurahisha zaidi? Swali hili ndilo limenisukuma kuyaandika haya machache, yamebeba mwanga utakaokuongoza, uone na kufahamu mengi juu yangu. Mwisho unishauri, NIMPENDE NANI, maana sijui kuchagua.
KARIBU🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏.
Tarehe tano ya mwezi wa sita, SALATOBA BUS, siti namba ishirini na tatu, saa 12:00 asubuhi. Niliyasoma maneno haya, nikayanena na kuyaimba ilimradi tu yanikae kichwani nisiyasahau nikiamini ile ilikuwa ni kalatasi tu ambayo ingeweza kupotea wakati wowote. Nilihakikisha nimeyakalili vema zaidi, nisiyasahau kama vile nilivyozisahau kanuni za mahesabu ya kukokotoa siku ya mtihani wangu wa kidato cha nne. Baada ya kuridhika na kile nilichokifanya, niliikunja kwa umakini kalatasi ile nikaitia ndani ya mfuko wa shati langu la kitenge nililolivalia, niliuamini sana mfuko huu kwakuwa haukuwa na rekodi mbaya ya kudondosha vitu vyangu. Hakuna lililokuwa mhimu kwangu kwa wakati huu; zaidi ya kuhakikisha usalama wa ile tiketi yangu ya basi. Nililazimika kwenda kituo cha mabasi kukata tiketi ili niwe na uhakika zaidi wa safari yangu niliyoitarajia siku tatu zijazo. Mda huu nilikuwa nikikatisha katikati ya vichaka vya msitu wa kipopo kwa mwendo wa harakaharaka sana; nikishindana na giza lililokaribia kuuteka uso wa dunia. Sikuwa na mzigo wowote zaidi ya begi dogo la mgongongoni, hivyo nilimudu vyema kutembea mwendokasi kwa namna ile niipendayo.
Japo nilibeba vitu viwili tu ndani ya begi langu, nilikuwa na uhakika usio na shaka kwamba ningepokelewa kwa shangwe na wadogo zangu mala nitakapofika nyumbani. Kwanza ulikuwa mfuko wa samaki pendwa aina ya mgebuka ambao ungelilazimisha tabasamu la mama yangu mzazi aliyewapenda sana samaki wale. Pili nilibeba pipi kadhaa za kijiti ambazo bila shaka zingenipatanisha vema na wadogo zangu, wasingesita kunisaidia kufua nguo zangu pale nitakapowaomba kufanya hivyo. Nilichagua kupitia njia hii ya mkato ili kuepuka gharama kubwa ya nauri ambayo ningelazimika kuitoa kama ningechukua usafiri wa kunifikisha nyumbani. Nilitembea mpaka pale nilipokaribia kijiji kwetu ndipo nikaanza kutimua mbio ili niwahi nyumbani. Siyo kwamba nilikuwa mshamba wa safari, hapana. Nilishawahi kusafiri mala nyingi tena safari ndefu ambazo zilinichosha na kunifanya nichukie kusafiri kwa wakati huo. Ule upekee wa safari ya awamu hii ndiyo ilikuwa siri ya shauku niliyokuwanayo. Safari hii imekuja kama matokeo ya wazo la mafanikio ya mda mrefu nililokuwa nalo...
Baada ya kumaliza elimu yangu ya kidato cha nne ndipo nilianza kuionja radha halisi ya maisha. Wazazi wangu walifurahia sana kunipata nikiwa huru sasa, wakiamini ningewasaidia shughuli mbalimbali za nyumbani kabla ya kulejea tena shuleni. Kutokana na historia nzuri ya ufaulu niliyokuwa nayo, wazazi wangu, wanafunzi wenzangu, ndugu na wote walionijua; waliniamini sana linapokuja suala la masomo, wakaamini ningefaulu vizuri mtihani wangu. Imani yangu ilikuwa tofauti, nilitofautiana nao kwa kiwango kikubwa sana, nilikijua vema kile nilichokipanda hivyo sikuwa na matalajio makubwa. Imani yangu ilinisukuma kuanza kutafuta namna ya kutoka nyumbani, nitoweke kijijini mapema kabla matokeo hayajatoka kwani nilijua hakutokuwepo na maelewano tena. Mala kadhaa nilishawahi kumshuhudia mzee wangu akijigamba kwenye vijiwe vya kahawa kuhusu mimi, kwamba mwanae nilikuwa namba moja pale kijijini na hakuna mtoto wa yeyote angenizidi katika mtihani wa mwisho. Simlaumu kwa hilo, huenda ni kwasababu ya matokeo mazuri niliyoyapata katika mtihani wa kidato cha pili ndiyo maana aliniamini sana. Jambo ambalo wengi hawakulijua ni kwamba mambo yalishabadilika sana, ya jana yasingekuwa ya kesho. Ukweli huo niliujua mimi mwenyewe, ndiyo maana nilipambana sana, nikafanikiwa kuwashawishi wazazi wakaniruhusu kwenda kukaa kwa mjomba; zikiwa zimebakia wiki mbili tu kabla ya matokeo kutoka. Ruhusa hiyo ilikuwa zaidi ya fulsa kwangu, sikutaka kulaza damu hata kidogo. Niliondoka mbio pasipo hata kugeuka nyuma nikihofia kuiona aibu iliyoningojea.
Nilipokelewa vizuri sana. Mjomba na shangazi walinipongeza kwa kufanikiwa kuhitimu masomo yangu ya kidato cha nne, kisha wakanipatia rundo la ushauri kwamba nikishaenda kidato cha tano nihakikishe nasoma kwa bidii sana, nije kuisaidia familia yangu. Walinikumbusha kama nilikuwa mtoto wa kwanza; tena mwanaume, nikishafanikiwa itakuwa rahisi kuwawezesha wadogo zangu. Kusemakweli ushauri wao ulikuwa mzuri sana, niliupenda bure lakini bado sikuuzingatia. Sikuuzingatia kwa sababu sikuwa tena wa kuziishi ndoto zao. Nilibaki kujichekesha tu kama chizi, nikaitikia ahsante kwa ushauri mzuri, japo maneno hayo yalikuwa ya mdomoni tu. Moyoni niliumia, akili ikachemka maana sikuona utofauti wa hapa nilipo sasa na kule nilikotoka. Ilikuwa kama nimeruka maji nikakanyaga tope, nilihisi kinyaa lakini nikakaza; potelea mbali, bora lawama kuliko fedheha. Nilikuwa tayali inifike nusu shali kuliko shali kamili la kijijini kwetu, yaani kila mtu anicheke, si bora huku nisikojulikana. Nani angehangaika nami zaidi ya ndugu wachache tu walionijua? Siku zangu chache za kufurahia maisha ya utukufu kwa mjomba nilizitumia kuweka mambo sawa, nilielewa kwamba ule mda wa kula mema ya nchi ulikaribia kuisha. Nilianza kufanya kazi ndani ya karakana ya mjomba ya kutengeneza vyombo vya usafiri, pikipiki na gari chache zilizofika pale kijijini. Hiyo ndiyo fani pekee niliyoijua vema kwa kipindi hicho. Nikawa fundi gereji wa kujitolea.
Kudhalilika ni kubaya sana asikwambie mtu; maana hakuji peke yake, huambatana na jamaa zake ambao hukera sana. Dharau na kudharauliwa, fedheha na kufedheheka, masimango na kusimangwa, chuki na kuchukiwa, kejeli, kusemwa, kutukanwa, kununiwa na kukataliwa. Yote hayo niliyapitia kwa namna tofauti mpaka nikamkumbuka muumba wangu. Nikaanza kusali, kuhudhuria kanisani kwani ndiyo malezi niliyolelewa, yaani kumshirikisha Mungu wangu; magumu yangu.
Mpaka leo naamini ni Mungu alijibu maombi yangu kupitia njia ile ambayo ilinishangaza sana. Imani za kishirikina! acha ziwepo tu kwa sababu ziliniponya na mengi. Ilianza kama kauli ya mtu mmoja, mwisho ikasambaa, ukawa wimbo ulioimbwa na kijiji kizima kwa sauti nzuri zilizoyavutia masikio yangu kusikiliza. Atakuwa alilogwa huyu, siyo bure lazima kuna mchezo mchafu alifanyiwa na wenzake, yaani mtoto aliyekuwa namba moja kwa kila mtihani halafu leo hii afeli, lazima walimzungukia mbuyu. Imani hiyo ilisaidia kwa kiasi kikubwa kurudisha ule uhusiano mzuri baina yangu na wazazi na ndugu zangu ambao ilifikia hatua wakaniona kama niliyewadhalilisha sana. Sasa kila mtu akawa ananihurumia, wengine wakidiriki hata kunipatia pole kwa yaliyonikuta, wakanishuri nimwachie Mungu kwani yeye ndiye hakimu wa kila mtu. Nilizipokea pole hizo, nami nikatoa za kwangu maana sikuwa gizani kama wao, niliijua siri ya maiti maana mimi ndiye nilikuwa muoshaji halisi. Licha ya yote hayo, bado baba yangu alikuwa mgumu sana, hakunikunjulia nafsi kama ilivyokuwa mwanzo. Ilinilazimu kukaa kijijini kwa miaka miwili, nikaijenga upya imani ya wazazi wangu kwa kuishi maisha ya kuwapendeza, maisha safi ambayo nadiliki kusema kwamba ndiyo yalikuwa maisha yangu bora sana. Zile tambo za baba yangu zikalejea tena, akaanza kujisifu kwamba mwanaye nilikuwa na tabia njema kuliko vijana wote pale kijijini. Hapo ndipo nilimshirikisha wazo langu la kurudi shule naye akaniunga mkono kwa zaidi ya asilimia miamoja. Kwa kutumia watu aliojuana nao alifanikiwa kunitafutia shule, mipango ya maandalizi ikakamilika. Sasa nipo najiandaa kwa safari, narudi shuleni kwa awamu nyingine nikiwa na kumbukumbu mbaya ya matokeo ya kidato cha nne. Naenda kuwa mwanafunzi wa chuo cha ufundi (VETA).
ITAENDELEA.
(Kila kitu kimeshakamilika, Simulizi ipo tayali. Ili kujua nini kiliendelea, tembelea uzi huu jioni ya kila siku kuanzia leo.)
Utavutiwa na mengi; yatakayouteka umakini wako, utamani kujua nini kiliendelea nje ya kile kilichoongelewa. Ni wazo la mwandishi kwamba ukajizatiti zaidi kunako maudhui mazuri yaliyofichwa ndani ya kila sentensi inayounda tungo tamu za simulizi hii.
Hakuna wazo hewa, kila aliyewaza alikuwa na sababu ya kufanya hivyo. Aliyezungumza alilenga kufikisha kile kilichoujaza mtima wake. Macho hayana pazia, kuna anayeona kwa kukusudia mwingine akakusudiwa na alichokiona. Matendo ndiyo hutoa tafsiri halisi ya mtu.
✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️
Karibuni sana wapenzi wa simulizi. Leo naitambulisha kwenu simulizi hii tamu iendayo kwa jina la SINA CHAGUO. Mwandishi anakukaribisheni sana kutoa maoni, kwa wakati wote usomapo simulizi hii.
SEHEMU YA KWANZA.
(Hakika mimi sijui, Fungu jema kuchagua,)
Huenda kile nilichopitia enzi za utoto wangu ndicho kimeniumba na kunifanya niwe hivi nilivyo sasa. Mimi ni nani? Swali hili huzisumbua sana fikra zangu kila nikiutafakari uhusika wangu ndani ya simulizi ya dunia. Mala zote siachi kujiuliza chaguo lipi huwa ni zuri kwangu kupita yote, maana sijui kuchagua. Si kwamba sioni, hapana. Nimejaaliwa bahati ya kukutana navyo, jicho zuri la kuona na kuvitambua vilivyo vizuri. Huwa natamani sana kuvipata, lakini sina uhakika kama nimeshawahi kujutia kuvikosa. Kuna wakati huwa naafikiana na kile wakisemacho wengi juu yangu, “wewe si mtu wa kawaida, ni mtu wa ajabu sana; unayefurahia kupata au kukosa kile ukitakacho.” Wakati mwingine siafikiani nao, kwasababu huwa ninapatwa na hisia tofauti katika kukosa na kupata, ijapokuwa huwa ninalidhishwa na yote. Kipi sasa hunifurahisha zaidi? Swali hili ndilo limenisukuma kuyaandika haya machache, yamebeba mwanga utakaokuongoza, uone na kufahamu mengi juu yangu. Mwisho unishauri, NIMPENDE NANI, maana sijui kuchagua.
KARIBU🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏.
Tarehe tano ya mwezi wa sita, SALATOBA BUS, siti namba ishirini na tatu, saa 12:00 asubuhi. Niliyasoma maneno haya, nikayanena na kuyaimba ilimradi tu yanikae kichwani nisiyasahau nikiamini ile ilikuwa ni kalatasi tu ambayo ingeweza kupotea wakati wowote. Nilihakikisha nimeyakalili vema zaidi, nisiyasahau kama vile nilivyozisahau kanuni za mahesabu ya kukokotoa siku ya mtihani wangu wa kidato cha nne. Baada ya kuridhika na kile nilichokifanya, niliikunja kwa umakini kalatasi ile nikaitia ndani ya mfuko wa shati langu la kitenge nililolivalia, niliuamini sana mfuko huu kwakuwa haukuwa na rekodi mbaya ya kudondosha vitu vyangu. Hakuna lililokuwa mhimu kwangu kwa wakati huu; zaidi ya kuhakikisha usalama wa ile tiketi yangu ya basi. Nililazimika kwenda kituo cha mabasi kukata tiketi ili niwe na uhakika zaidi wa safari yangu niliyoitarajia siku tatu zijazo. Mda huu nilikuwa nikikatisha katikati ya vichaka vya msitu wa kipopo kwa mwendo wa harakaharaka sana; nikishindana na giza lililokaribia kuuteka uso wa dunia. Sikuwa na mzigo wowote zaidi ya begi dogo la mgongongoni, hivyo nilimudu vyema kutembea mwendokasi kwa namna ile niipendayo.
Japo nilibeba vitu viwili tu ndani ya begi langu, nilikuwa na uhakika usio na shaka kwamba ningepokelewa kwa shangwe na wadogo zangu mala nitakapofika nyumbani. Kwanza ulikuwa mfuko wa samaki pendwa aina ya mgebuka ambao ungelilazimisha tabasamu la mama yangu mzazi aliyewapenda sana samaki wale. Pili nilibeba pipi kadhaa za kijiti ambazo bila shaka zingenipatanisha vema na wadogo zangu, wasingesita kunisaidia kufua nguo zangu pale nitakapowaomba kufanya hivyo. Nilichagua kupitia njia hii ya mkato ili kuepuka gharama kubwa ya nauri ambayo ningelazimika kuitoa kama ningechukua usafiri wa kunifikisha nyumbani. Nilitembea mpaka pale nilipokaribia kijiji kwetu ndipo nikaanza kutimua mbio ili niwahi nyumbani. Siyo kwamba nilikuwa mshamba wa safari, hapana. Nilishawahi kusafiri mala nyingi tena safari ndefu ambazo zilinichosha na kunifanya nichukie kusafiri kwa wakati huo. Ule upekee wa safari ya awamu hii ndiyo ilikuwa siri ya shauku niliyokuwanayo. Safari hii imekuja kama matokeo ya wazo la mafanikio ya mda mrefu nililokuwa nalo...
Baada ya kumaliza elimu yangu ya kidato cha nne ndipo nilianza kuionja radha halisi ya maisha. Wazazi wangu walifurahia sana kunipata nikiwa huru sasa, wakiamini ningewasaidia shughuli mbalimbali za nyumbani kabla ya kulejea tena shuleni. Kutokana na historia nzuri ya ufaulu niliyokuwa nayo, wazazi wangu, wanafunzi wenzangu, ndugu na wote walionijua; waliniamini sana linapokuja suala la masomo, wakaamini ningefaulu vizuri mtihani wangu. Imani yangu ilikuwa tofauti, nilitofautiana nao kwa kiwango kikubwa sana, nilikijua vema kile nilichokipanda hivyo sikuwa na matalajio makubwa. Imani yangu ilinisukuma kuanza kutafuta namna ya kutoka nyumbani, nitoweke kijijini mapema kabla matokeo hayajatoka kwani nilijua hakutokuwepo na maelewano tena. Mala kadhaa nilishawahi kumshuhudia mzee wangu akijigamba kwenye vijiwe vya kahawa kuhusu mimi, kwamba mwanae nilikuwa namba moja pale kijijini na hakuna mtoto wa yeyote angenizidi katika mtihani wa mwisho. Simlaumu kwa hilo, huenda ni kwasababu ya matokeo mazuri niliyoyapata katika mtihani wa kidato cha pili ndiyo maana aliniamini sana. Jambo ambalo wengi hawakulijua ni kwamba mambo yalishabadilika sana, ya jana yasingekuwa ya kesho. Ukweli huo niliujua mimi mwenyewe, ndiyo maana nilipambana sana, nikafanikiwa kuwashawishi wazazi wakaniruhusu kwenda kukaa kwa mjomba; zikiwa zimebakia wiki mbili tu kabla ya matokeo kutoka. Ruhusa hiyo ilikuwa zaidi ya fulsa kwangu, sikutaka kulaza damu hata kidogo. Niliondoka mbio pasipo hata kugeuka nyuma nikihofia kuiona aibu iliyoningojea.
Nilipokelewa vizuri sana. Mjomba na shangazi walinipongeza kwa kufanikiwa kuhitimu masomo yangu ya kidato cha nne, kisha wakanipatia rundo la ushauri kwamba nikishaenda kidato cha tano nihakikishe nasoma kwa bidii sana, nije kuisaidia familia yangu. Walinikumbusha kama nilikuwa mtoto wa kwanza; tena mwanaume, nikishafanikiwa itakuwa rahisi kuwawezesha wadogo zangu. Kusemakweli ushauri wao ulikuwa mzuri sana, niliupenda bure lakini bado sikuuzingatia. Sikuuzingatia kwa sababu sikuwa tena wa kuziishi ndoto zao. Nilibaki kujichekesha tu kama chizi, nikaitikia ahsante kwa ushauri mzuri, japo maneno hayo yalikuwa ya mdomoni tu. Moyoni niliumia, akili ikachemka maana sikuona utofauti wa hapa nilipo sasa na kule nilikotoka. Ilikuwa kama nimeruka maji nikakanyaga tope, nilihisi kinyaa lakini nikakaza; potelea mbali, bora lawama kuliko fedheha. Nilikuwa tayali inifike nusu shali kuliko shali kamili la kijijini kwetu, yaani kila mtu anicheke, si bora huku nisikojulikana. Nani angehangaika nami zaidi ya ndugu wachache tu walionijua? Siku zangu chache za kufurahia maisha ya utukufu kwa mjomba nilizitumia kuweka mambo sawa, nilielewa kwamba ule mda wa kula mema ya nchi ulikaribia kuisha. Nilianza kufanya kazi ndani ya karakana ya mjomba ya kutengeneza vyombo vya usafiri, pikipiki na gari chache zilizofika pale kijijini. Hiyo ndiyo fani pekee niliyoijua vema kwa kipindi hicho. Nikawa fundi gereji wa kujitolea.
Kudhalilika ni kubaya sana asikwambie mtu; maana hakuji peke yake, huambatana na jamaa zake ambao hukera sana. Dharau na kudharauliwa, fedheha na kufedheheka, masimango na kusimangwa, chuki na kuchukiwa, kejeli, kusemwa, kutukanwa, kununiwa na kukataliwa. Yote hayo niliyapitia kwa namna tofauti mpaka nikamkumbuka muumba wangu. Nikaanza kusali, kuhudhuria kanisani kwani ndiyo malezi niliyolelewa, yaani kumshirikisha Mungu wangu; magumu yangu.
Mpaka leo naamini ni Mungu alijibu maombi yangu kupitia njia ile ambayo ilinishangaza sana. Imani za kishirikina! acha ziwepo tu kwa sababu ziliniponya na mengi. Ilianza kama kauli ya mtu mmoja, mwisho ikasambaa, ukawa wimbo ulioimbwa na kijiji kizima kwa sauti nzuri zilizoyavutia masikio yangu kusikiliza. Atakuwa alilogwa huyu, siyo bure lazima kuna mchezo mchafu alifanyiwa na wenzake, yaani mtoto aliyekuwa namba moja kwa kila mtihani halafu leo hii afeli, lazima walimzungukia mbuyu. Imani hiyo ilisaidia kwa kiasi kikubwa kurudisha ule uhusiano mzuri baina yangu na wazazi na ndugu zangu ambao ilifikia hatua wakaniona kama niliyewadhalilisha sana. Sasa kila mtu akawa ananihurumia, wengine wakidiriki hata kunipatia pole kwa yaliyonikuta, wakanishuri nimwachie Mungu kwani yeye ndiye hakimu wa kila mtu. Nilizipokea pole hizo, nami nikatoa za kwangu maana sikuwa gizani kama wao, niliijua siri ya maiti maana mimi ndiye nilikuwa muoshaji halisi. Licha ya yote hayo, bado baba yangu alikuwa mgumu sana, hakunikunjulia nafsi kama ilivyokuwa mwanzo. Ilinilazimu kukaa kijijini kwa miaka miwili, nikaijenga upya imani ya wazazi wangu kwa kuishi maisha ya kuwapendeza, maisha safi ambayo nadiliki kusema kwamba ndiyo yalikuwa maisha yangu bora sana. Zile tambo za baba yangu zikalejea tena, akaanza kujisifu kwamba mwanaye nilikuwa na tabia njema kuliko vijana wote pale kijijini. Hapo ndipo nilimshirikisha wazo langu la kurudi shule naye akaniunga mkono kwa zaidi ya asilimia miamoja. Kwa kutumia watu aliojuana nao alifanikiwa kunitafutia shule, mipango ya maandalizi ikakamilika. Sasa nipo najiandaa kwa safari, narudi shuleni kwa awamu nyingine nikiwa na kumbukumbu mbaya ya matokeo ya kidato cha nne. Naenda kuwa mwanafunzi wa chuo cha ufundi (VETA).
ITAENDELEA.
(Kila kitu kimeshakamilika, Simulizi ipo tayali. Ili kujua nini kiliendelea, tembelea uzi huu jioni ya kila siku kuanzia leo.)