Riwaya: See Me (Nione)

Riwaya: See Me (Nione)

Iyo naimalizia wakuu itaisha muda so mrefu msione nip kimy sana
 
Uzi huu unawez isha leo leo lakini pia kuna uzi mpya



Love is a drug abuse
 
Nilipata msiba wanangu ila trh 26 ndio narudi kwangu nitaanza kupost zote
 
Nimerudiiii mwez mzim tupo wote kesho naachia zoye mbili hasubh saa 4
 
SEE ME



SEHEMU YA 37/50……….




Afrika ya kusini


Tulifika mjini cape town city jiji ambalo linazidi kukua kwa kasi ya ajabu kiuchumi na kufanya population ya watu kuongezeka toka sehemu mbalimbali za dunia katika bara hili la Afrika na kufanya ajira nyingi kutopatikana kwa wepesi zaidi kutokana na wingi wa watu. Gari aina ya Alphard likaja kutuchukua mimi na mpenzi wangu diana (X) ndani ya gari hilo kulikuwa na dereva pamoja na jamaa mmoja mwenye umbo dogo yaani mbilikimo jamaa alikuwa mfupi na alionekana mtu mzima kunizidi. Mimi nilikuwa nimekaa siti ya nyuma huku mpenzi wangu akiwa mbele na dereva wa gari hilo.

"Karibuni South Afrika,"

Akazungumza kwa kiswahili fasaha

"Tunashukuru".

Nikamjibu na kumtolea tabasamu bandia, akatabasamu na yeye kwa tabasamu hilo hilo bandia yaani tabasamu la kulazimisha.

"poleni kwa uchovu kwani kutoka Somalia mpaka huku ni umbali mrefu na kwa sasa hakuna safari ya moja kwa moja ya Somalia na Afrika ya kusini maana lazima upite nchi moja jirani." Akajieleza mambo ambayo sikumuuliza. Gari ikasimama kwenye foleni ambayo ni ya Msongamano wa vyombo vya moto na ukilinganisha ni Alfajiri ya jumatatu watu walikuwa wanakwenda kwenye biashara zao na mizunguko yao ya kila siku, Nikachungulia na kuona picha kubwa ya mwanamke ikiwa kwenye bango kubwa lililowekwa Pembezoni mwa barabara, niliona sura ya yule mwanamke au yule binti wa Rais wa umoja wa mataifa mr maclom alexander na huyo ni binti yake Tyalat muimba mziki mkubwa kwa sasa na alikuwa na ziara ya kuja Afrika ya kusini na ndiye mlengwa wetu, gari yetu ikaondoka baada ya foleni kupungua japo siyo kwa kiasi kikubwa,majira ya saa 3 hivi gari ikakunja kwenye barabara ya vumbi na kuacha ya kisasa yaani ya lami dereva akaongeza mwendo tofauti na mwanzo wakati huu sote tulikuwa kimya.

"wewe ni mtanzania?"

Nikazungumza na kumtizama yule mtu mfupi ambaye kama ningesema nifanye fujo basi hasingethubutu ata kunipiga kofi,shavuni kwani mifupa ya shingo yake ningeivunja na kumuua hapo hapo.

"hapana me mtu wa kongo".

Akazungumza na kufanya niamini watu wa kongo wengi wana maumbo madogo japo kuwa asilimia kubwa ya wachezaji wao wa mpira ni warefu, sijui sasa ni ile kongo nyingine au ile ya Kinshasa.

"ooh sawa hongera kwa kuwa gaidi"

Nikazungumza na kufanya diana kushtuka na kunitizama kwa mshangao, yule mtu mfupi akacheka kwa sauti ya juu na kufanya dereva naye kumsapoti kwa cheko kubwa kama majini ya kwenye movie ya Saladini,Kabla hajanijibu honi ya gari hilo ikapigwa na hazikupita sekunde 10 geti likafunguliwa la jumba ambalo lilikuwa kubwa na muonekano wake wa nje lilionekana jumba kubwa la kifahari,gari ikapita na tukaingia ndani na kwenda sehemu ya parking ambapo kulikuwa na gari mbili aina hiyo hiyo. Mtu mfupi akashuka baada ya gari kusimama kisha akanambia kwa ishara nishuke, nami ni kashuka na diana naye akafata, tukawa tuna shangaa jengo hilo ambalo lilikuwa na muonekano wa kisasa zaidi,.

"Haya ndiyo makazi yenu kuna watu mtakutana nao ndani ya hilo jengo". Akazungumza yule mtu mfupi na akanyoosha kidole kwenye lango la lile jengo hilo,

"safari yetu imeishia hapa."

Akazungumza na akarudi ndani ya gari yeye na dereva wake Kisha wakaondoka na mlinzi aliyefungua geti akafunga Kisha akatutazama na kutuonyesha ishara tuingie ndani ya jengo hilo nikatazamana na mpenzi wangu X Kisha tukaanza kupiga hatua kuingia ndani ya jengo hilo nikabisha hodi kama la tatu ila sikupata jibu toka ndani ndipo nilipoamua kufungua mlangi wa nyumba hiyo,haukuwa umefungwa kwahiyo nikatangulia na mpenzi wangu akanifata kwa nyuma tukatembea huku mbele yetu tukiona furnture mbalimbali za kuvutia ilikuwa sebule ya kupendeza sana, tukataka kuketi kwenye masofa ila tukaikia sauti ikituamrisha kuwa tufate korido iliyopo mbele yetu hatukufanikiwa kumuona mtu huyo zaidi ya kusikia sauti yake mpaka tukakutana mlango mmoja mbele, tukasogea na nikashika kitasa na kufungua mlango huo, nikawa wa kwanza kuona sebule kubwa iliyojaa silaha za moto zikiwa zimetundikwa ukutani pia kukiwa na wanaume wenye miili mikubwa kuniliko walikuwa wanne mmoja alikuwa na ngozi nyeusi wengine wote walikuwa waarabu,tukatizamana mimi na mpenzi wangu na kupiga hatua kuwafata wale jamaa walipo.


TANZANIA

Jeradi akabaki njia panda hakujua MAGE amekwenda wapi?,kwani ni siku 4 sasa amepotea katika mazingira ya kutatanisha moyo wake ulifadhaika vya kutosha kwani alimpenda sana mwanamke huyo, akahisi moyo wake unavunjika vipande vipande, maumivu makali yakamtawala moyoni mwake, akamtazama Juliana mke wa marehemu baba yake mr solo. akakumbuka jinsi alivyokuwa anashiriki tendo la ndoa na mke wa baba yake ambaye ni mama yake mlezi, moyo wake ukaanza kufadhaika akahisi ni kama laana inamtafuna moyoni mwake

.”Kwanini nisisafishe Dhambi zangu najihisi mimi sina utofauti na IBILISI”Akawaza na kumuona juliana akitoa nguo zake ili kushiriki tendo la ndoa kitandani tena kwenye kitanda cha marehemu mr solo.

."Vaa nguo" Jeradi akazungumza na kunyanyuka toka kitandani

"Umenichoka Jeradi?".Juliana akazungumza

"Nahitaji kupumzika maana nimechoka".

"Sikumbuki mara ya mwisho kulala na wewe lini sikuhizi umenibania sana yani siyo kama zamani eeh unataka nani anitomb*eh".Juliana akazungumza

"Hivi unaona upo sawa" Jeradi akazungumza na kuanza kuvaa nguo zake.

“Leo ndiyo unajua hilo kipindi unanitomb** eeh"

“Sihitaji kwa sasa baba yangu atakuwa anaumia huko alipo”.

""okay". Juliana akazungumza na kuanza kuvaa nguo zake akatoka chumbani humo huku moyo wake ukiwa katika wasiwasi wa mali, akawaza yaani Jeradi uenda anataka kumsaliti na kumkimbia na mali zote akakumbuka jinsi alivyotukana watu kijijini na kuwatukana mpaka ndugu zake kuwa kwa sasa yeye haendani nao,hakuwa tayari kurudi kule kwenye maisha ya chini kwani ingekuwa ni aibu kubwa ya mwakai, Juliana hakutaka kukubali kuwa maskini tena hakutaka kuvaa nguo za kimaskini kama zamani, akatazama mikufu iliyojaa shingoni mwake iliyokuwa ya thamani kubwa ya pesa kama angeamua kuiuza maana mikufu ile ilikuwa na madini halisia hazikuchakachuliwa mbinu mbaya juu ya Jeradi ikajengeka kichwani mwake akawaza kuwa sasa anahitaji mali hizo ziwe mikononi mwake na ale na kunywa chochote kile pia haishi kwa amani siyo kwa hofu tena, akapanga mipango jinsi atakavyompoteza Jeradi kwenye uso wa dunia.Juliana akaondoka na kuingia ndani ya gari lake aina ya ferrari lilikuwa jekundu akawasha akapangua gia na kuondoka kwenye jumba hilo la kifahari la mr solo

"lazima nimuondoshe jeradi nahisi anataka kunizunguka". Akawaza

."ooh mungu wangu!" jeradi akazungumza kwa sauti iliyojaa majonzi akakumbuka maisha anayoishi hakuwa na huruma hata kidogo, sasa alihitaji kumuomba muumba na kutubu dhambi zake zote na kuwa mtu mwema moyo wake uliumia kupita kiasi, simu yake ikaita akatazama na kukuta ni don john ndiye anapiga, akajishauri na kuipokea."uko wapi? kijana."

"home"

"Nimefanikiwa kumpata mage!" Don john akazungumza

"what". Kwa mshtuko kama bango movie

"ndiyo"

"nielekeze wapi ulipo mzee nashukuru sana umenipa nguvu sasa." Jeradi akazungumza huku sura yake ikijaa furaha ya ajabu ni dhahiri alimpenda sana mage.

"nakutumia location". Don john akazungumza na kukata simu, jeradi akaanza kuruka ruka huku moyo wake ukijawa na furaha ya ajabu akatazama location ambayo tayari alitumiwa na don john."mmh huku nje ya mji mage alifuata nini akatafakari kisha akatazama saa na kuona ni saa 10 za jioni

"nahisi saa 12 hivi nitafika huko”.Akawaza


Afrika ya Kusin


“Najua maelekezo yote kuhusu tyalat mmeshapatiwa sivyo?"

"Hapana siyo yote.

" Nikazungumza"

“Usiku wa leo atakuwa anapiga show kwenye ukumbi MANDELA ARENA,saa mtapelekwa kwa ajili ya kazi hiyo kisha mtarudishwa mpaka hapa kujificha kwa muda hili ndilo litakuwa jumba lenu kwa muda." Jamaa huyo mwenye asili ya kiarabu akazungumza nikawa nimegundua jambo kuwa wale sio Al-shabab wa Somalia kwani wote walikuwa na rangi nyeupe ata nyuso zao hazikuonekana kama waarabu toka Somalia ambao wao ni weusi. Nikagundua wale ni Al-Qaida wa Kundi la osama bin laden na wote walijua Kiswahili fasaha.

"Tupo dunia nzima kwahiyo usishangae tunajua lugha yako." mmoja wapo akazungumza aliweza kungundua mshangao wangu."fanya kazi kwa usahihi, Tunakutizama wewe na si huyu mwanamke!" .Jamaa huyo akazungumza kisha akafungua begi lililokuwa mezani na akaanza kutoa silaha moja moja ndani ya begi lile na kuzieka mezani, alipomaliza akawapa ishara wenzake kuwa waondoke na wakaondoka, kama dakika mbili nikasikia gari ikiunguruma na ikitoka nje, walikuwa wanne. Akabaki pekee yake na akamrushia Diana bastola ndogo na Diana akaidaka na kuitizama. Laiti diana angekuwa kwenye ushetani wake basi jamaa huyo huenda kichwa chake kingekuwa chini huku shingo yake ikitoa damu kwa wingi.



SEE ME

NIPO MPAKA MWISHO
 
SEHEMU YA 38/50



Yule jamaa akazidi kutupatia maelekezo yake, kuwa inatupaswa tufanye kazi hiyo kwa usahihi usiku wa leo hili tuendelee kuwa hai na wapendwa wetu waliowashikilia kule nchini somalia.

“ Mtafatwa na gari usiku kwenda katika majukumu yenu hakuna muda wa kupumzika maana inawapaswa kumteka binti huyo akiwa hai kisha mambo mengine yataendelea”.

“ Ina maana ili jengo ndiyo ukumbi wenyewe”.

“ Ndiyo na kuna bomba kwa siri sana ndani ya hilo jengo hizo zinapitisha maji taka na kinyesi cha watu, ni bomba kubwa ambazo zinawatosha nyie kupita”.

“ Uuuh bomba za vinyesi kwani hakuna njia nyengine”. X akauliza

“Njia nyengine ni kumteka mbele za watu na pia akiwa na walinzi wake na isitoshe ana mlinzi wake hatari ni jasusi wa CIA”.

“ Ina maana kuna mitaro inayomwaga kinyesi huku mjini?”

“ Kuna shimo kubwa mithili ya tank ambalo ni la kisasa zaidi mtafungua mfuniko wake wa chuma, umefungwa na minyororo mikubwa sijuhi utafanyaje, ukisha fungua kuna ngazi mtashuka nayo mpaka chini ambapo ndipo kuna maji taka na vinyesi vyote vya watu wanaoingia katika ule ukumbi, kuna Bomba limeandikwa B123 Mtaingia na kulifata bomba ilo ambalo linapitisha vinyesi, hilo bomba ndiyo litawapeleka kwenye pipe zote za vyoo ni zaidi ya pipe 20, halafu kuna pipe C345 hiyo ndiyo njia ya kwenda mpaka sehemu atakayojiandalia huyo binti na kubadili nguo zake au kuoga, ni chumba cha VIP ni lazima ataingia ndani ya chumba hicho, mkifata hiyo njia moja kwa moja, itawapeleka mpaka chooni kule tushaharibu kila kitu ni wewe kutoa ile sinki na kuingia ndani kumtorosha huyo msichana,” Akazungumza na kufanya nishushe pumzi ndefu kwani analeta mambo ya sinema maarufu ya Prison break.

“ Tumesuka mpango huu wiki tatu kwahiyo fanya kazi kwa usahihi kwa heri mkitaka chakula kuna kila kitu ndani ya friji”. Akazungumza na kuanza kuondoka.

“Ndugu yangu tampataje na mke wangu?”. Nikazungumza na akasimama

“ Maliza kazi yako”. Akanijibu na kuondoka nikatizama ile ramani ya jengo ilo ikionyesha bomba kubwa za maji taka ambazo zilikuwa na ngazi na zimejengwa kisasa zaidi hii ni kutokana na ukumbi huo kuwa wa kisasa zaidi kwani ulishikiliwa na chumba za kutosha ndiyo maana ilijengwa kisasa zaidi hili uendelee kuwa imara.

***********


“Ooooh yeeh yeeh *** me”. Sauti ikamtoka juliana baada ya mboo kubwa na nene kuzama kwenye kitumbua chake, alijihisi sasa anahitaji kukunwa vizuri na mwanamume huyo aliyekuwa naye kitandani hapo

“ oooh yeaah we mwanamke wa moto ooh”. Sauti ya mwanamume ikasikika tena alionekana kupata raha mpaka kufumba macho yake, ghafla simu ikaita akaitizama pembeni na kuona jina la mpigaji, akamtoa jogoo wake kwenye kitumbua cha juliana na kushika simu hiyo

“ oooh nani beiby ingiza bassss”.

“ shhhhh jeradi”. Mwanamume huyo akazungumza na kupokea simu

“ Halooh jeradi”

“ Nimefika nje ya mji Don john ila sioni kitu zaidi ya hilo jengo ambalo naliona kwenye ramani uliyonitumia”.

“ Usiofu jeradi kuna gari itakuja hapo ikiwa na mke wako”.

“ nashukuru sana mzee taja kiasi chochote cha pesa me nitakupa” jeradi akazungumza huku akiangaza angaza huko na huko, akataka kugeuka nyuma ila kitu kizito kikatua kichwani mwake, akadondoka chini kama mzigo na kupoteza fahamu

“ Nimemkamata boss”. Mtu aliyempiga na kitu hicho kizito ambalo ni gogo akazungumza kupitia simu ya jeradi ambayo bado ilikuwa hewani.

“ Hongera kwa kazi nzuri si unajua anatakiwa kutolewa nini?”

“ Ndiyo bossi viungo vyake”.

“ Mpelekeni kule kwenye biashara zangu kesho kutwa kuna matajiri wanahitaji figo imara hakikisheni mnampima vizuri afya yake”.

“ Sawa mkuu”..

“ KAZI NJEMA”. DON JOHN akazungumza na kukata simu kisha akatabasamu na kumtizma juliana ambaye alikosa raha

“ mmh vipi tena”.

“ uuh nimeumia sana kufanya hivyo maana nimemlea huyo kijana”. Juliana akazungumza kwa unyonge

“ ooh kwahiyo hutaki mali”

“ Nataka ila nilihitaji kumuua ndiyo maana nikakueleza wewe”.

“ uuh sasa sindyo atatolewa kiungo kimoja kimoja kila siku mpaka kifo chake”..

“ Ina maana unafanya biashara haramu don john naogopa sasa mwenzako”.

“ Hahaha juliana Nchi yetu ina madeni mengi hatuwezi kulipa madeni hayo hii biashara ndiyo inatusaidia kuendesha taifa letu ata serikali ipo chini ya hili ndiyo maana kila siku watoto wadogo na watu wazima wanapotea maana hii ndiyo biashara kubwa zaidi duniani kuliko bangi, hii kila siku watu wanahitaji moyo,figo, macho na kila kitu kizuri ambacho wao hawana kama we unacho mtu yupo tayari anunue kwa pesa yeyote ile apatae macho yako au figo yako au ngozi yako, damu yako mpka moyo na vengine vingi mpaka mboo kama hii si yangu nikichukua kwa mtu”. Don john akazungumza na kushika shika mboo yake iliyosimam dede

“ nilikuwa na kibamia juliana”. Akazungumza na kucheka kwa sauti

“ Ina maana inawezekana kubadirika”.

“ sayansi imeenda mbali sana kuna mambo mengine huwezi kuelewa”

“ Mabara yote dunia hufanya biashara hii haramu tena hasa wale wanaokosoa serikali”.

“ mmh nahitaji siku moja unipereke huko”.

“ Usijali kesho kutwa tutaenda”. Don john akazungumza na kuanza kushika shika makalio ya juliana…


SOMALIA


mage hakutaka kuendelea kubaki katika ngome ile ya Al shaabb alihitaji kutoroka na kutetea uhai wake hakujihisi amani moyoni mwake,kitu pekee alichowaza ni kuingia katika ma tank makubwa ya mizigo ambayo kila siku yalikuwa yakitolewa na kupakiwa kwenye meli na kuperekwa sehemu asiyoitambua, alihitaji bora kwenda huko kuliko kubaki hapo, hakutaka kabisa mtoto wake amzalie eneo hilo kwai hakujua nil lini Randy hatarudi na je akifa, alihitaji upenyo mdogo tu kuingia na kujificha katika matank hayo ambayo yalipakiwa katika meli.

“ kila baada ya siku mbili yanarudi na kila baada ya siku mbili yanatoka”. Akajisemea kimoyo moyo huku akichingulia kwenye dirisha la chumba alichopewa, akaona wakiingiza matank hayo kwenye scania kisha scania hiyo itaondoka kwenda mpaka baharini ambapo aliweza kuona mpak ufukwe wa bahari kwangi ngome hiyo vyumba vyake vilikuwa juu na vilitizama mpaka ufukweni.

“ Kesho kutwa naondoka nitatoroka baada ya chakula”. Akazungumza na kushika shika tumbo lake ambalo linazidi kukua.

***************



“ Waoooh mwanamke mwenyewe ndiyo huyu”

“ Ndiyo bossi anaitwa marry”

“ mbona hana mguu mmoja”.

“ huyo alipata ajali ya bomu liliripuka na kumuharibu haribu mpaka uso wake huyo ndiyo yule mke wa randy”.

“Oooh bomu alifata nini hyu vitani au?”

“ Hapana bossi ni story ndefu sana”

“ kwahiyo moyo wale ndiyo unaendana na wa binti yangu”.

“ ndiyo bossi na tutambadirisha na binti yako atapona kabisa”.

“ Vipi kama huo moyo ukimuona huyo randy ana ukajua ni mume wake huoni binti yangu hatasumbuka”.

ITAENDELEAAAA
 
SEHEMU YA 39/50

"Hawezi kumpenda randy na haiwezi tokea bossi sisi tunajua namna gani yakufanya".
" Anaonekana binti mwenye mawazo sana natamani nimuone kwa ukaribu zaidi kuliko hizi video zake mlizoniletea".
" Usijali boss kesho kutwa kuna mnada unapigwa wa kimataifa viongozi na matajiri mbalimbali watakuwepo hili kukamirisha jambo hilo".
" Naelewa nishapewa mualiko na president".
" Ndiyo mkuu serikali ina daiwa na hii ndiyo biashara pekee yenye hela kuliko madini". Jamaa huyo akazungumza na kumtizama boss wake
" Uuh kwa sasa nahitaji kupumzika hakikisheni huyo mwanamke mnampa kila kitu anachotaka".
" Sawa mkuu". Jamaa akaondoka na kumuacha boss wake.

Kwa sasa taifa lilikuwa katika deni kubwa la mikopo waliokopa viongozi waliopita mdarakani na kushindwa kulilipa mpka sasa nchi inadaiwa kiasi kikubwa cha pesa, njia pekee ilikuwa ni kuuza viungo vya binadamu, na bangi ili serikali iweze kupata pesa ya kulipia deni hilo linaloikumba taifa toka miaka mingi iliyopita, madini thamani yake ilikuwa imeshuka kwa sasa kwahiyo biashara haramu ndiyo iliyokuwa ikifanyika kwa wakati huu.


Gari aina ya hammer ikaja kutufata mimi pamoja na mke wangu diana huku ndani ya gari hiyo kukiwa na dereva pamoja na yule jamaa aliyekuwa ametupa maelezo yote kuhusu kumteke yule msichana wa raisi wa umoja wa mataifa Mr Malcom.
" fanyeni kazi kwa umakini mkishikwa hatuwezi wasaidia". Jamaa huyo akazungumza kwa msisitizo na kuzidi kutupa maelekezo yake na akatraki simu zetu alizotupa kutumia katika utekaji huo wa Tylat.
" TUMEFIKA". dereva akazungumza alionekana lafudhi yake ni mtu wa huko huko kwao, jamaa yule afungua mlango na tukashuka huku nikiwa makini zaidi kutizam eneo tulilopo lilikuwa eneo lenye giza totoro na vichaka vichaka pembezoni mwake kulikuwa na tank kubwa ambalo nilifanikiwa kuliona baada ya jamaa huyo kumulika kwa tochi, lilikuwa tank kubwa na lenye ngazi..
" ina maana uwanja upo porini au?". Nikauliza
" hapa ni town ila hili tank ndiyo lipo kidgo nje ya mji ko mtapita kwenye pipe zake kama mwendo wa dakika 30 mpka kufika kwenye chumba cha tylat".
" Duuh".
" Wakandarasi wa hili jengo mwanzo walihitaji kujenga ikulu ya raisi, ndiyo maana unaona njia kama hizi, mambo yalitokea yasiyoeleweka ndipo serikali ikahamua kujenga ukumbi mkubwa wa mikutano na burudani za kusheherekea siku ya uhuru wa afrika ya kusini, na utawala wa Nelson mandela". Jamaa huyo akazungumza na kunikabadhi tochi huku akinionyesha ngazi za kupanda,
" Safari njema mtamkuta huyu mtu hapa hapa kazi ni lisaa limoja ma dakika 30". Akazungumza na kupiga simu huku akisema anahitaji kufatwa.
" Kwanini hii kazi msingefanya ninyi kama mmechora ramani yote hiyo".
" hahha tunahitaji uhakika zaidi maana historia yako tuanaijua". Jamaa akazungumza, nikamtizama diana na nikamuonea huruma kwani kipindi icho alikuwa tayari na ujauzito wangu. Nikasogea kwenye zile ngazi na kuzishika zilikuwa tayari zishaweka kutu kwa kukaa muda mrefu bila ya kupewa matunzo yeyote, nikazitingisha ila bado zilikuwa imara, nikaanza kupanda kuelekea juu ya tank hilo lilojengewa kwa zege ngumu ya sement,nikapanda kama sekunde 30 nikawa juu kabisa ya tank hilo na diana naye akafata nikampokea mkono na kumvuta, tukaona mfuniko mkubwa wa chuma ukiwa hauna kufuli kwenye nyororo zake, nikatoa zile nyororo na tukafungua, nikamulika kwa ndani na kushuhudia tu maji taka yakiwa yanaingia kwenye tank hilo ambalo halionekani kujaa leo wala kesho, maana ni matukio muhimu pekee ndiyo ukutanisha watu siyo mizunguko ya kila siku kusema kwamba litajaa. Nikashika ngazi na tukaanza kushuka chini huku panya na mende wakipita huko na huko, tukafika mpaka chini na kukanyaga maji taka ambayo kwa mbele tulijua lazima tukutane na kinyesi, tukaanza sikia harufu kali ya choo cha binadamu..Mwendo wetu ulikuwa ni wa haraka huku tukifata ile ramani kwenye simu, tuliendelea kutembea chini ya bomba ilo kubwa ambalo upokea maji taka toka kwenye bomba zengine,
" uuh" Nikatoa sauti baada ya kuona panya mkubwa ambaye sikuelewa humo anaishije na wenzake, tukafanikiwa kuona ngazi ambayo ndiyo inabomba linalotupereka mpaka juu ya kabisa na ndani ya choo ambacho ni cha kukaa na ndicho tutakachopitia, inawezekana walihitaji kujenga ikulu kweli, siku rais yakimkuta njia hiyo ndiyo iwe ya kumpitisha na inaonekana bado inatumika ata kwenye sherehe za uhuru kama kuna mambo mabaya yatatokea basi raisi au mtawala apitishwe eneo hilo kwa siri na kutoke kule kwenye vichaka, tukaanza kupanda ngazi huku harufu kali ilikiwa imeshatushika, tulitoa harufu ambayo hatukuhitaji ata kuzungumza,
" Baki hapa ". Nikazungumza na Diana huku nikimsisitiza abaki palepele kwenye nagzi akiwa amening'inia ili mimi nipande niende juu kabisa na kuingia ndani kwani tayari tushafika juu kabisa. nikasikilizia kama kuna mtu chooni ila kukawa kimya sasa nikafungua sehemu iliyokuwa imekatwa na hao wakandarasi kumpitisha mtu ilikuwa ya duara yenye mfuniko wa mviringo na ilikuwa ishaharibiwa nilitambua ni wale walotupa hii kazi ya kumteka huyu msichana, nikavuta pumzi na kuishusha kwani sasa naingia kwenye bomba la kinyesi na mkojo, nikaingia huku nikiwa na tochi, cha ajabu sikufanikiwa kuona hata funza wala chochote kile kikipita kwenda kwenye lile bomba.
" Hiki choo hakitumiki, ni mahususi kwa kumtorosha kiongozi wa serikali au mtu yeyote mkubwa". Nikawaza kwani bomba lake likikuwa jipya halina chochote, nikaanza panda ngazi taratibu kwenda juu ya choo icho, nikafanikiwa kuona tundu kubwa ambalo nikisukuma tu lile sinki la kukalia hili kujisaidia basi nakuwa tayari ndani, nikaweka tochi mdomoni na taratibu nikashika lile sinki kwa chini na kuanza kulisogeza taratibu mpaka uwazi mkubwa ukatokea, nilitambua sinki hilo lilikuwa limehalibiwa kwani ilikuwa ni rahisi sana alikutoa saut wakati ndani humo kuna vigae, nilijua walonipa kazi washafanya yao. Nikajinyanyua na kupanda juu sasa nikawa ndani ya choo icho, kilikuwa na mwanga za balbu ya umeme ko niliona kila kitu, nikasogea mlangoni na kuchungulia kupitia tundu la funguo, nikamuona tylat akiwa uchi anajiandaa nikajua kuwa hicho hakikuwa choo, nikamtizma jinsi anavyovaa nguo zake za show alikuwa uchi wa mnyama, ghafla nikamuona akikodoa macho upande niliopo mimi tena akakaza, huku akitizama kwa udadisi nikashtuka na kubaki nimeganda vile vile........

ITAENDELEAAAAAAAAA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom