SEE ME
SEHEMU YA 40/50
Nikamtizama Tyalat nakumuona akitizama kule ambako mimi nipo ambapo nilikuwa nachungulia kupitia tundu la ufunguo wa mlango, akakaza macho na kuanza kuja kule nilipo mimi lakini ni kama alikuwa anashangaa kwa juu, yaani juu ya mlango, sasa nikakaa vizuri kwa ajali ya kumnasa ndege wangu huku nikiwa makini nisijetambulika nikatoa bastola yangu kiunoni na kuikoki vizuri ilitoa sauti ndogo maana ilikuwa ya kisasa zaidi na toleo jipya kwa ajili ya kazi kama hizo za siri, sasa nikamuona akitabasamu na kisha akageuka na kunipa mgongo, sikutaka kujiuliza mara mbili mbili kwa haraka nikabinya kitasa na kufungua mlango huo na nikamuona akishtuka na kutaka kugeuka ila tayari nilikuwa nishamkwida shingoni akawa anajaribu kujivuta vuta ila na kutaka kujinasaua ila mdomo wa bunduki nikaweka kichwani pake na akatulia tuli mithili ya maji ya mtungini,nikamkokota na kumuingiza ndani ya choo kile cha kisasa kisha na kifunga mlango, akaonekana kushangaa sana baada ya kuingia humo ndani, akaona shimo kubwa likiwa wazi ambalo ndipo nilipopita akataka kuzungumza kitu ila nikamuwahi kwa kumsonteshea kidole kuwa anyamaze na akatii huku akitetemeka, macho yake yalikuwa ya rangi ya Brown alikuwa mwembamba na mwenye nywele ndefu kama wazungu wengine sema yeye tu alikuwa na ngozi nyeusi yenye mvuto wa kuvutia kama wanawake wengine warembo wa afrika.
Nikamsonteshea bastola kuwa ashuke chini huku nikimulika kule chini na tochi, nikamuona akitetemeka huku akijitahidi kuficha maungo yake ya mwili maana alikuwa na chupi na sidiria kifuani, akatingisha kichwa kuwa hawezi kushuka ila nikamkazia macho na kukunja ndita kiasi kilichofanya mpaka aogope na taratibu akasogelea shimo lilo na kutanguliza mguu mpaka kwenye makanyigio ya ngazi, uso wake ulihisi kinyaa kila aliponitizama na yeye mwenyewe kuna muda alitaka kutapika, akaanza kwenda chini taratibu huku nikijitahidi kumulika mwanga wa tochi ili akanyage sehemu sahihi, akashuka mpaka umbali haliopo diana na nikaona diana akimvuta kwenda katika lile bomba la pili,
“ Madam”. Nikasikia sauti zikitoka kule upande wa pili kile chumba alichokuwepo tylat kwa umakini nikasikia sauti wakija kule nilipo kwa haraka nikajificha nyuma ya mlango na kuweka silaha yangu vizuri, nikasikia wakitembea kama kwa kunyata na kitasa cha mlango kikaguswa ili kufunguliwa, na ukafunguliwa mlango taratibu huku nikiona buti ya kike ikitangulia, kwa haraka nikajitokeza na kumbana mikono yake na kufanya bastola aloishika kuanguka chini niliweza kutambua ana bastola baada ya kuiona kupitia kivuli cha ukutani, alikuwa ni mwanamke wa kizungu, akafurukuta na kujitoa kwa nguvu kisha akarusha ngumi kwa haraka ila nikainama chini na ikapita na akaacha sehemu zake za mbavu wazi, sikufanya hajuza nikashusha ngumi kwenye ubavu wake wa kushoto ila ni kama nilipiga kitu kigumu mithili ya mgomba, akatabasamu na kuleta shambulizi lake la pili, nalo nikalikwepa na mara hii ngumi ya ubavu ikatua kisawa sawa na akagugumia kwa sauti ya kike yenye maumivu, kitu nilichogundua alikuwa anaacha sana mbavu zake wazi anaonekana hakuwa professional sana wa kupigana akatizama bastola yake iliyoko chini, lilikuwa kosa kwani tayari nilikwisha muangusha chini na kuanza kumfunga na mkanda wake ambaoa hajuhi ni saa ngapi nimeutoa kiunoni, akaanza kupiga kelele ila nikampiga kichwani na akazima, kisha nikafunga mlango na kumsogeza mlangoni, nikaanza sikia sauti za watu wakija, kwa haraka nikarudi kule kwenye lile shimo na kuanza kushuka haraka haraka kupitia zile ngazi, nikawa nasikia kwa mbali wakizungumza kizungu hiyo ni baada ya kufungua mlango ule uliochukua kama sekunde 30 kufunguka maana nililaza mwili wa yule mwanamke pale,
Nikafika kule chini na kuanza kukimbia kuelekea kule tulipotokea na kwa vile diana alikwisha tangulia na yule mwanamke sikuwa na kitu cha kupoteza zaidi ya kukimbia kutoka eneo lile, nikawakuta njiani wakimalizia kushuka bomba la mwisho ili kutoka na kupanda ngazi kwenda juu ya lile tank
“ Tuna sekunde kama 120 kufika kwenye zile ngazi ni kama dakika mbili au tatu”. Nikazungumza huku nikimtizama mwanamke yule ambaye tayari alikwisha tapika siku nyingi.
“ okay dear twende”. Diana akazungumza na tukaanza kwenda huki nikimkokota yule mwanamke au binti wa kizungu,
“ Ongeza mwendo kuna panya wanatoka huko tulipopotoka kwa fujo inaonekana wapo nyuma”. Nikazungumza na kuwatanguliza mbele diana na tylat na wakatembea haraka mpaka kwenye bomba ambalo lina ngazi ambazo zinatufikisha mpaka kule juu, akaanza kupanda diana kwa harka haraka kisha akafata yule binti wa kizungu mwenye asili ya kiiafrika yani mzungu mweusi, na yeye akapanda,kisha nikafata na mimi ile napanda tu na mwanga mkali wa tochi ukamulika pale nilipokuwa nikawasikia wakiteta kwa kizungu kuwa wapo huku.
Nikaongeza kasi na kupanda mpaka juu ya tank kisha kurudisha mfuniko ule wa chuma na kufunga na nyororo zake, milio ya risasi ikaanza kusikika na risasi zikawa zinapiga ndani ya ule mfuniko, nikashuka mpaka chini na tukaingia mpaka ndani ya gari ambalo yule dereva alikuwa akitusubiri,....
Alikuwa alishaliwasha ile naingia tu naye akaliondoa kwa kasi kutoka eneo lile ambalo tupo..
“ ooh sheet kuna gari linakuja”. Diana akazungumza nikageuka nyuma na kuona gari likija kwa kasi kutufata kule tulipo.
“ Mkague ana cheap”. Nikazungumza na diana akaanza kumkagua binti binti yule bila mafanikio yeyote.
“ Mtoe hereni zake”. Nikazungumza na diana akataka kufanya ivyo ila akashindwa baada ya mlio wa risasi kusikika na kuvunja kioo cha nyuma.
“ oooh shit”. Nikazungumza na kuona gari mara hii zikiwa mbili tena jamaa wale wakionekana hawana mchezo kabisa na sisi.
“ Ongeza mwendo”. Nikazungumza huku tukiwa tumeinama na mpenzi wangu chini na pia tumemuinamisha yule msanii chini ili asidhulike maana waokoaji wake walionekana hawana mchezo kabisa,
Milio ya risasi ikazidi kusikika na kutufanya tuwe makini zaidi maana kama ungeinua kichwa basi mwisho wako ungekuwa hapo, ghafla gari ikaanza kupepesuka hiyo ni baada ya gari moja kutugonga ubavuni mwa gari yetu, na kufanya dereva aanze kukosa mwelekeo vizuri wa barabara hiyo ambayo hipo kabisa nje ya mji na makazi ya watu ni machache, sasa zikawa gari mbili moja imetubana kulia nyengine kushoto, nikajikuta nikimtukama dereva wetu kimoyo moyo kwani aliishiwa ujuzi kabisa wa kufanya, jamaa wakaanza kuligonga kwa kupokezana.
“ kumteka huyu binti ni sawa na kumteka raisi wa umoja wa mataifa”. Nikazungumza baada ya kuona kazi imekuwa ngumu sasa nikagundua ndiyo maana wale jamaa walitutumia sisi, na siyo askari wao ili kulinda siri zao kama wakikamatwa, kwahiyo wakatutumia sisi maana siri zao hatuzijuhi ata tukishikwa.
Tukawa tunajigonga kwenye siti huku yule binti akiwa katikati yetu, nikaanza kuona gari ikizidi kujigonga na sisi wa ubavuni uwenda tungevunjika kabisa.
Dereva wetu akapigwa shaba ya kichwa na kuegemea usukani, kitendo kilichofanya miguu yake kufunga breki ya ghafla, na kichwa chake kutua kwenye usukani na kufanya honi ianze kulia tayari alikuwa amekwishafariki. Gari ikasimama katikati ya barabara, nikatoa bastolo na kutizama risasi zilikuwa kwa hesbu ya harka haraka kama 12 na hivi.
Wale jamaa wakashuka maana niliwasikia wakishuka baada ya milango ya magari yao kufunguliwa, nikamshika yule binti mkono kisha nikamtizama diana ambaye naye yupo kwenye hali mbaya, paji lake la uso lilikuwa likivuja damu.
“ Nakupenda sana randy”. Akazungumza na kunitizama
“ unataka kufanya nini?” Nikazungumza baada ya kumuona akishika kitasa cha mlango na kutaka kukifungua, nikachungulia na kuona wale jamaa wakizunguka lile gari letu tuliokuwemo huku wakinyata
“ Niache kwa sasa”.
“ Hapana”.
“ Fanya hivyo randy”. Akazungumza na kwa harka akafungua kitasa cha mlango na kutoka nje kisha kubamiza mlango kwa nguvu kiasi kwamba mpka ukajilock maana ulikuwa ushaharibika kwahiyo ukajilock, nikamuona akinyanyua mikono juu, kwa harka nikamgusa yule binti shingo kwenye mishipa yake ya fahamu na akazima, wakati wale wakimtizama diana nikatumia fursa hiyo kuwahi kusogea mpaka kule mbele alipo dereva, sikufanikiwa kukaa nilikuwa nimeinama kwa chini.. nikapangua gia kwa haraka na gari ikawaka huku nikimsukuma yule dereva kushoto na kumtoa kichwa chake kwenye usukani wale jamaa wakaanza kushambulia kule nilipo na risasi mbili zikanipata kwnye bega langu la kushoto ila tayari nilikuwa nishakanyaga mafuta, lilikuwa ni tukio la sekunde chache sana na la uhatari zaidi lenye kuondoa hata maisha yangu kupita sitemillor nikamuona diana akiwa kapiga magoti huku mikono yake ikiwa nyuma ya kichwa, wale jamaa wakambeba na wengine kupanda kwenye gari haraka, sikuwahi fika afrika kusini kwhiyo nikawa naendesha tu gari hiyo ambayo muda huo ilikuwa ikitoka moshi na muda wowote ule ingezimika au kulipuka, nikaona wale jamaa wakizidi kuja na gari zao kwa kasi ya ajabu, moyo wangu uliuma sana diana kwa kitendo kile alichokifanya, tukafika kwenye daraja kubwa ambalo chini yake kuna mto mkubwa ambao nina uhakika kuna mamba wa kutosha, lile gari likawa sasa linaenda kuzima, sikujishauri nikahama njia na gari lile kupiga kuta za daraja hilo na gari ikaanza kushuka chini kwa kasi huku nikijipiga piga na kupasuka pasuka kichwani, gari ikatumbukia mtoni.
SEE MEE