Love is a drug abuse

Love is a drug abuse

hancy Abdon

Member
Joined
May 24, 2026
Posts
78
Reaction score
58
Picsart_26-08-05_14-12-53-567 (1).jpg








SEHEMU YA KWANZA

AGE.............................18+

THE STORY MASTER

AUTHOR...................... Hancy A abdons



"Kuna mwanafunzi mgeni!".

Nikazungumza na kumtizama mtu aliyeniletea hiyo taarifa alikuwa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza.

"Ndiyo mkuu".

akazungumza kwa uwoga baada ya mimi kusimama

juu ya meza niliyokalia huku mkononi nikiwa na kitabu cha mabara mbalimbali ambacho kilihusu mabara ya duniani siyo mabara the farmer akaanza kurudi nyuma huku midomo ikimtetemeka.

"Nishakukataza kuniita mkuu!".

Nikazungumza na kumshika shati yake shingoni nikamkamata vizuri shingo yake.

"Mwalimu anakuja."

sauti ikasikika nyuma yangu nikageuka na kumtazama Ray

"Kwahiyo"?.

Nikamjibu kisha nikamwachia yule kijana mdogo wa mwaka wa kwanza chuoni hapo akapepesuka kutaka kuanguka, mwili wake ulikuwa mdogo kama mnyoo.

"Mlete kule chini."

Nikazungumza na kuondoka ndani ya darasa hilo ambalo tulikuwa humo watu wanne pekee, Wenzangu watatu wakanifuata nyuma, na yule kijana akabaki amesimama huku ametupa mgongo; alikuwa bado anaogopa."Tabia yako bado hujaacha!" Sauti ya mwalimu ikanifanya nimtazame kwa dharau kwani nilikutana naye kwenye mlango. Alikuwa ni madam mwenye umbo kubwa; hips zake zilikuwa nene zilizoshiba mithili ya shape ya Kajala, yaani makalio ya Kajala halafu hips ya Mobetto, sura Mungu hakumjalia kivile. Nikanyanyua lips zangu huku nikimtazama kwa matamanio."Dominick unanitazamaje? Hili jambo naliripoti kwa mkuu wa chuo!" Madam akazungumza na kisha akasogea dirishani na kumwita yule kijana wa mwaka wa kwanza."Una roho mbaya, unatesa wenzako kisa kwenu mna hela, kisa baba yako ni Rais!" Akazungumza kwa uchungu ila sikujali nikapiga hatua kwenda napo kwenda.

"Na nyie mnaomfuata mwandike barua ya utovu wa nidhamu!".

Akazungumza na akaondoka na yule kijana mdogo kuelekea ofisini huku maumbo yake ya nyuma yakitingishika kama mfuko wa rambo wenye maji.

"Huyu madam mshenzi sana,"

Ray akazungumza. Nikatingisha kichwa na kuelekea darasani kwenye kipindi ambacho kilikuwa kinaanza muda mchache ujao, lilikuwa somo linalohusu mambo ya biashara na uchumi."Sitaki kelele!" Nikazungumza baada ya kuingia darasani na kukuta watu wakipiga kelele. Waliposikia sauti yangu wote wakatulia tuli, hata walioniona kabla sijazungumza walirudi kwenye siti zao. Nikaenda kwenye kiti changu kwa ajili ya kuketi, nikakunja ndita..

Baada ya kuona kalamu yangu ikiwa chini,

"Wewe ndiye uliyeangusha hii kalamu?". Nikamuuliza swali jirani yangu ambaye akanitazama kwa woga.

"Ni upepo," akanijibu.

"Na ukaiacha? Baadaye uje kule chini,". Nikazungumza na kuiokota."

"Husikii kupulizia marashi yako hayo?." Nikamuuliza swali msichana aliyekuwa pembeni yangu upande wa kulia. Marashi yake sikuyapenda toka siku ya kwanza nilipoyasikia.

"Mama hajanunua mengine," .Akanijibu na kuendelea kuandika kwenye kitabu chake kidogo mithili ya diary.Nikatazama katikati ya darasa na kumwona kijana niliyempiga juzi kipigo cha mbwa koko akiwa amelalia dawati. Nikatabasamu kwa furaha kwani napenda toka moyoni mwangu kuona mtu akiteseka, napenda kuona mtu akiwa na damu puani, mdomoni au popote pale.

Napenda kuona mtu akilia kwa maumivu makali huku akiniomba msamaha. Sipendi kuona mtu akifurahi au kutabasamu.Mwalimu wa somo la biashara akaingia darasani. Tukampatia heshima ambayo kila mwanafunzi anatoa kwa walimu au wakufunzi wake toka vidudu mpaka chuo kikuu. Alikuwa ni madam mwembamba mwenye umbo la Kisomali; alivutia kama twiga mbugani. Nikaacha kumkagua mwili wake baada ya kuanza kuzungumza."Jana sikumaliza kipindi, kwa hiyo nitafanya double!" Akazungumza na kufanya nitabasamu kwani huwa napenda kumwona kila muda.Ghafla darasa zima likalipuka kwa shangwe na furaha zilizoambatana na miluzi ya vijana wa kiume. Nikamtazama Ray na wenzake wawili ambao nao wakawa wananitazama, mimi.

Hatukujua kwa nini watu wale wanapiga kelele za kufurahi bila uwoga. Nikatazama mlangoni ambako watu wanatazama, nikamwona kijana wa kiume anaingia, mrefu mwenye umbo la misuli (mazoezi). Nikatabasamu baada ya macho yetu kugongana na yeye akatabasamu.

"Alex, Alex, Alex!" Watu wakaanza kutaja jina lake kama shujaa waliyemmiss kwa muda mrefu. Nikamtazama mkono wake nilioutegua (vunja) miezi mitatu iliyopita ulikuwa mzima, ulikuwa hujafungwa na P.O.P pia hata shingo yake ilikuwa nzima.

"Nitakuua, Dominick,"

Akazungumza kwa sauti nzito iliyofanya wanafunzi wote kutulia.

"Alex, maneno gani hayo?"

Madam akazungumza,Na kumtizama alex aliyenikazia macho, Nikasimama na kuelekea kule mbale ya darasa,alipo Alex, nikamtazama juu mpaka chini, mguu wake wa kulia niliouvunja miezi 2 iliyopita ulikuwa mzima.

Akatabasamu baada ya kuona namkagua.

"Baba yako amekupeleka India?" Nikazungumza na akatabasamu kwa kejeli.

"Nitahakikisha nakulaza miezi 6 kitandani!" .Akazungumza na kufanya watu wote kushangilia kwani hakunaaliyenipenda hata mmoja kutokana na tabia zangu mbaya za uonevu nilizokuwa nazo chuoni hapo. Kila mtu alionekana kumpenda Alex ambaye alikuwa ni head boy chuoni hapo na alikuwa mkarimu machoni mwa watu, alikuwa na roho safi na ndiyo mpinzani wangu mkubwa chuoni hapo yeye alikuwa mtoto wa Rais mstaafu, hakupenda tabia zangu ijapo kuwa mimi niliona niko sahihi.

"Demu wako nitambusu tena ili uje upambane na mimi!" Nikazungumza na kugeuka kumtazama Clara ambaye ni demu wa Alex, Clara akamtazama...

Alex huku machozi yakimlengalenga kwani nilimdhalilisha mbele za watu, nikaona hasira za Alex kifuani mwake zikipanda na kushuka kama mtu mwenye presha."Ukimshika tena Clara..." Alex akashindwa kumaliza kuongea, sauti ya mkuu wa chuo ikasikika."Njooni ofisini wazazi wenu wamekuja." Tukatazama dirishani na kumwona mkuu wa chuo akitutazama kwa macho makali, Alex akageuka na kuondoka nami nikafuata kwa nyuma na kundi la watu wachache wakaanza kunizomea, nikarudi kwa haraka darasani na wakatulia tuli.

"Ray, wakabili wote watakaonizomea.

""Sawa Domy," Ray akanijibu na nikaondoka bila ya kusikia sauti yoyote ile, nikaona msafara mkubwa wa magari ukiwa pembezoni mwa geti kuu, ofisi ilitazamana na geti kuu la chuo, ofisi ya mkuu wa chuo.

"Huyu mzee vipi?" Nikawaza na kuingia kwenye ofisi ya mkuu wa shule. Nikamwona baba akiwa amekaa upande wa kushoto huku Rais aliyepita madarakani mwaka uliopita naye akiwa ameketi upande huo huo wa kushoto na wanaume wawili waliovaa suti wakiwa nyuma ya mgongo wa baba. Nikamwona Alex akiwa katikati ya duara kubwa lililochorwa kwenye sakafu ambalo chuoni hapo tunaliita kikaango cha watukutu. Nikapiga hatua nami nikaingia kwenye lile duara, mkuu wa shule tukawa tunatazamana naye pamoja na wazazi wetu.

"Mnataka kuwa mabondia tumlete Tyson nchini?". Baba akazungumza huku akinitazama kwa macho makali ambayo kama angemtazama mtoto mdogo angelia na kulala usingizi fofofo. Nikatingisha kichwa kukataa alichozungumza.

"Mnataka kila siku mtuone hapa chuoni, hivi mnaleta picha gani nchini? Nashindwa kutatua changamoto za wananchi, tunashindwa kupanga mipango jinsi ya kuinua taifa letu toka uchumi wa kati mpaka wa juu, tena tuwaze na watu kama nyie wenye mapumbu!" Baba akazungumza kwa ukali zaidi huku akinikazia macho. Nikatizama pembeni.

"Alex, nitakuhamisha chuo." Rais aliyepita madarakani akazungumza.

"Baba haiwezekani, sitakubali!" Alex akazungumza kwa upole.

"Kwahiyo unataka ugomvi uendelee? Unataka mpaka wakuue au uue na wewe? Umelala hospitali miezi 3 hujitambui, mifupa imeteguliwa bado unataka nini?!" Baba Alex akafoka.

"Tupeni nafasi ya mwisho," nikazungumza na kuwatazama wote wawili.

Wakanitizama."Sababu ya kuonewa wenzako nini?" Baba akaniuliza, nikabaki nimetumbua macho.

"Mkuu hebu wachape viboko, inaonekana hamuwafundishi adabu."

Baba akazungumza na mkuu wa shule akasimama na kutoa heshima.

"Samahani mheshimiwa Rais na mstaafu, hawa tunawaonya sana na kuwaadhibu kwa kuwapa adhabu. Chuo chetu akiruhusu kuwatia fimbo wanafunzi wetu." Akazungumza.

"Nitamteua mtu mwengine." Baba akazungumza na kufanya mkuu wa shule ashtuke, akapiga simu hapo hapo.

"Nenda Form Six niletee fimbo za kutosha!"

"Zilete ofisini kwangu sasa hivi." Akazungumza na akakata simu.

"Hatuwezi lea ujinga kisa wazazi wenu wakubwa, mnafanya upuuzi chuoni!" Baba Alex akazungumza.

"Hawa wanatugombanisha, mitoto mjinga sana hii, mzee mwenzangu." Baba akakazia.Madam akaingia ofisini akiwa na mwanafunzi wa Form Six ambaye alikuwa kabeba fimbo za kutosha, mwanafunzi yule alipowaona wazazi wetu akashtuka sana, hakutegemea kama angeweza kuona watu kama hao.

"Shikamooni wakubwa," akazungumza kwa uchangamfu kuficha mshangao wake na uwoga, wakamuitikia wote kwa pamoja.

"Form Six?" Baba akamuuliza.

"Ndiyo kiongozi!" Akajibu.

"Sawa, sawa, kazana!" Baba akazungumza.

"Asante sana." Akaondoka huku uso wake na macho yake yalionyesha mshangao wa wazi kabisa.



ITAENDELEA.....
 
SEHEMU YA PILI

Yule madam akatoa heshima na yeye kisha mkuu wa chuo akachukua fimbo.
"Chukua hiyo kubwa!" Baba akazungumza na kusontesha kidole kwenye fimbo nyingine ambayo kweli ilikuwa kubwa. Nikameza mate huku kijasho chembamba kikaanza kunitoka.
"Malaya mkubwa wewe! Leo nakuua, unatembea na kaka yangu!" Sauti hiyo ikapita kwenye masikio yangu, lilikuwa ni tukio la zamani lililopita likanijia kichwani mwangu.
"Domy siyo mwanangu, yaani umezaa na kaka yangu!"
Sauti ya baba ikafanya nizidi kupata, maumivu kwenye kumbukumbu yangu. Nilimwona mama akipigwa na baba kipigo cha mbwa mwizi wakati huo nikiwa na miaka 7.
Fimbo ya makalio ikafanya nishtuke toka kwenye dimbwi la mawazo ya miaka mingi iliyopita. Nilikuwa naogopa fimbo kwani nimeshuhudia fimbo ikimchapa mama yangu mzazi, tena toka kwa baba yangu aliyeketi hapo ofisini.
"Shuka chini!" Mkuu wa chuo akazungumza kwa sauti kali ambayo sikumbuki mara ya mwisho kuisikia ilikuwa lini.
"Mkuu!" Nikazungumza ila nikajikuta tayari nipo chini. Fimbo ikashuka juu ya makalio yangu na ikapenya vizuri kwenye ngozi yangu. Nikapigwa fimbo za haraka haraka na za nguvu toka kwa mkuu wa chuo; zilikuwa fimbo 7 za moto. Nilisikia maumivu yake mpaka kwenye ubongo. Akafuatwa na Alex ambaye yeye alikuwa tayari amekwisha shuka chini; mwenzangu alikaza akupepesuka kama mimi.
"Head boy unakuwa mjinga kiasi hiki!" Baba yake akazungumza.
"Nikisikia tena nakuhamisha chuo." Baba akazungumza na kunyanyuka.
."Niwaongeze mheshimiwa?"
Mkuu wa chuo akazungumza na nikamkazia macho hasa jicho la kushoto, mpaka akajishtukia Baba akatoka kwenye siti yake na kupiga hatua kuja nilipo.
"Dada yako kamaliza kusoma Marekani hii wiki anakuja, jiandae kwenda kumpokea." Akazungumza na kunishika bega.
"Sawa Baba."
"Masomo mema!" Akazungumza na kumshika Alex mkono kisha akatoka na mlinzi mmoja akatoka naye huku aliyebaki akasimama mlangoni."Sitasikia fujo tena, Domy." Baba Alex akazungumza na akaondoka na yeye, tukabaki na mkuu wa chuo
."Ona Mambo yenu sasa," na yeye akatoka na kuwafata wale wageni wake, tukabaki ndani watatu, mimi, Alex na yule madam ambaye alikuwa amesimama mbali kidogo.
"Yote yameisha," akazungumza na kutusogelea."Sawa madam!" Alex akazungumza.
"Kumbatiani!". Akazungumza na sote tukamtazama kwa mshangao kwani hakuna aliyekuwa tayari.
"Haiwezekani," nikazungumza.
"Hivi kwnini una mdomo sana domy " Akazungumza na kuinua fimbo.
"Mkumbatie mwenzako," akazungumza na kunisontesha fimbo, ncha ya ile fimbo ikawa inatazamana na jicho langu la kulia.
"Huyu mtoto siyo wangu najua!"
“"Lakini kumbuka wewe mwenyewe ulisema nitafute mwanamume wa kuzaa naye ufiche aibu yako mume wangu". Sauti ya mama ikasikika vyema masikioni mwangu kipindi hicho nikiwa mtoto mdogo miaka 6.
“ Ndiyo, uzae na kaka yangu!" Baba akazungumza na akavua mkanda wa ngozi wa suruali yake, akaukunja na kushika kule kwenye kitasa. Akawa anatutazama mimi na mama tukiwa chini, huku mama akiwa amenikumbatia kwa nguvu. Baba akaanza kushusha mikanda ya nguvu ambayo mingine ilinipata na kufanya nianze kulia kwa sauti, na mama akanikinga na kunikumbatia kwa nguvu na mikanda yote ikatua kwenye mwili wake.
"Hata kama sina nguvu za kiume, ndiyo uzae na pacha wangu? Kwa hiyo ulitaka damu isitoke mbali?!"
Akafoka na kuzidi kushusha mikanda ya nguvu
“ Nisamehe mume wangu, nimezaa na kaka yako ili damu isitoke nje ya kabila letu,maana mila zetu hazirujusu kuzaa nje , pia huenda mwanaume wa nje angekusumbua sana!" Mama akazungumza kwa uchungu.
"Wewe mpuuzi!"
Sauti kali ikasikika na kunitoa kwenye dimbwi zito la mawazo na mchanganyiko wa maluelue niliyokuwa nayo, nikamwona mwalimu mkuu akikusanya faili zake huku Alex akiwa anaelekea mlangoni na yule madam akiwa na fimbo zake."Toka humu, husikii tu!" Akafoka.
"Samahani!". Nikazungumza na kushika kichwa changu kisha nikaondoka kuelekea darasani na kujifanya kuwa hakuna kilichotokea ofisini. Nikamwona Alex akiwa na mpenzi wake Clara wakionekana kufurahi, nikakunja ngumi baada ya kuona tabasamu lao tena toka ndani, kitu ambacho sipendi nikuona mtu au watu wakiwa katika furaha uwa nahisi wananicheka.
ITAENDELEA….
 
LOVE IS A DRUG ABUSE
SEHEMU YA TATU



Nikashika rungu na kuanza kulirusha rusha huku nikimsogelea kijana aliyekuwa mbele yangu, huku akiwa amepiga magoti chini na damu kutoka kwenye tundu moja la pua yake, nikamshika kidevu na kukibinua juu.

"Kwanini kalamu yangu hukuichukua?". Nikazungumza na kutizama rungu langu ambalo ndilo lililomraza alex miezi mitatu hospitali, ndiyo silaha yangu kubwa chuoni hapo.

"Sitarudia domy!!" Akazungumza na kulia kwa uchungu, moyo wangu ukafarijika baada ya kuona machozi yake

."Nenda ole wako useme chochote." Nikazungumza na nikamfuta damu yake ya pua kwa kutumia kitambaa chake na nikamkabidhi na kwa haraka akakimbia na tukaanza kumcheka mimi na jopo langu.

“ Kuna msichana mzuri kaletwa ni kisu hatari!!"

"Siyo vitu vyangu hivyo" Nikazungumza.

"Ah domy yaani unasema hivyo ujamuona huyo binti yani mweusi fulani hivi kama mwarabu wa kisomali nywele zake ndefu tena asilia siyo ma wigi kama ya jamila halafu sasa anakaa mbele yako"

."Mbele yangu?"

"Ndiyo leo si ukuingia darasani kaletwa huyo binti yaani Mwarabu yule mtoto amekamilika".

"Poa siyo kitu cha ajabu hicho." Nikazungumza na kumkazia macho.

"Sawa basi samahani." Akazungumza kwa upole.

“Ray yuko wapi leo?"

"Alitoka kidogo kuna mambo anafuatilia".

"Sawa" ghafla kishindo kama cha kuanguka kitu kilisikika "puuh" kwa haraka tukatoka nje na kutizama huku na kule, tukafanikiwa kuona mwili wa mtu ukiwa chini unavuja damu...

Tukamsogelea na kwa taharuki nikashtuka baada ya kumuona yule msichana ambaye kila siku nagombana naye kuhusu manukato yake mabaya yenye harufu kali. Tukatizama juu na kuona mgongo wa mtu ukiishia juu ya ghorofa lile la darasa letu.

"Ameanguka toka juu" .Raja akazungumza na tukatizama ghorofa lile ambalo ni darasa letu ulikuwa umbali mrefu zaidi ya ghorofa kama 3 hivi na ameanguka kwenye sakafu ya vigae vya mawe ambavyo vimejaa chuo kizima kwa ajili ya kuzuia vumbi na pia uchafu na kuvutia chuo chetu tofauti na vyengine.

"Anapumua". Nikazungumza na kwenda kumshika msichana yule, alikuwa ameshika tumbo lake damu zilikuwa zikimtoka puani na mdomoni kwa wingi pia kichwa chake kilikuwa kinavuja damu ya kutosha, na nyengine zikichuruzika toka sehemu za siri maana alivaa sketi fupi ambazo ndiyo sare zao.

"Nenda katoe taarifa" .Nikazungumza

."Tukimbie Domy hii kesi!" Rajah akazungumza.

" Kwani jengo si lina kamera inapiga upande wetu". Nikazungumza na kutizama kamera kisha nikashuka chini na kuanza kubeba mwili wake.

"Hazifanyi kazi domy". Rajah akazungumza na kunisisitiza kuwa hiyo ni kesi.

" Hapa chuo hakuna anayekuhamini kuwa wewe ujafanya chochote kama ukikutwa eneo hili".

" huyu kapatwa na tatizo". Nikazungumza na kubeba mwili wake vizuri na kuanza kumkimbiza hospitali ya chuo ambayo ni mita chache tu toka nilipo, watu wakabaki wamenikodolea macho kwani kila mtu alishangaa nini kinaendelea,jopo kubwa la madaktari likaja na kitanda cha kusukuma kwa haraka wakamlaza yule binti na kuanza kukisukuma kwa haraka kwenda ndani ya vyumba vya matibabu.

" Kawaje huyu". Dokta akaniuliza huku uso wake ukionyesha kunikazia kama nahusika katika hilo kwani hata siku moja sijawahi msaidia mtu.

" Amesukumwa". Rojah akazungumza na kufanya daktari kumtizama.

" Na nani?".

" Tuliona tu mgongo wa mtu".Nikazungumza na daktari akatingisha kichwa chake na kuelekea kwenye majukumu yake.

"Nimefanya nini sas?". Nikazungumza huku nafsi ikinisunta kwa kumsaidia au kumpeleka binti yule hospitali, hali yake ilikuwa mbaya mno na anaonekana alikuwa mjamzito.

"Umetaka tuwe mashahidi we ungesema tumemkuta chini". Nikazungumza na kumtizama rajah

" Nimesema hivyo kukulinda mkuu ili uchunguzi ufanyike ibainike ni nani aliyefanya hilo tukio". Rajah akazungumza na kufanya hasira kidogo zipungue.

" Umesema kamera za pale hazifanyai kazi?"

" ndiyo sasa zingekuwa zinafanya kazi uhalifu wetu wa kule chini tungeonekana kila siku". Akazungumza na kutingisha kichwa chake huku akitabasamu juu ya matukio yetu maovu ya kupiga watu bila huruma.

" Ni Mjamzito". Nikazungumza na rajah akanishangaa.

" Umemtambuaje". Akaniuliza ila sikumjibu tuka toka hospitai na kukutana na jopo la uchunguzi likiwa nalo linafika.

Lilikuwa jopo la uchunguzi hapo hapo chuo, uchunguzi wake ni siku moja pekee halafu taarifa ndiyo inafika polisi, walifanya hivi ili matatizo ya chuo yasitoke nje pia jopo hilo lilipewa kibari na polisi kwa siku moja pekee na pia kulikuwa na polisi wawili katika jopo hilo hili kuhakikisha hakuna kitu kinachoharibika yani kilikuwa chuo ambacho kila idara ilikuwepo.

" Domy na wenzako tunawahitaji". Kiongozi wa hilo jopo akazungumza na kunitizama kwa hasira za wazi wazi, kwani kesi zake nyingi akinishtaki nilikuwa namshinda, akanisogelea,

" Hii kesi najua uchomoki hata kama baba yako ni rais ni ngumu sana kujinasua". Akazungumza na kutabasamu, nami nikatabasamu na kumnong'oneza sikioni kwa sauti ya chini sana.

" Najua wewe ndiye uliyefanya ilo tukio". Nikazungumza na kumuona jinsi alivyoshtuka na kutizama kulia na kushoto kama kuna mtu amesikia kauli yangu, nikamuona jinsi uso wake ulivyobadirika ukawa wa mshangao zaidi.

" Najua ni vita ya mapenzi". Nikazungumza na kumuona mkuu huyo wa jopo hilo la uchunguzi akizidi kuchanganyikiwa zaidi.

" Unasema kuhusu nini?". Akazungumza baada ya kumuona mkuu wa chuo anakuja kule tulipo.


ITAENDELEA
 
LOVE IS A DRUG ABUSE
SEHEMU YA TATU



Nikashika rungu na kuanza kulirusha rusha huku nikimsogelea kijana aliyekuwa mbele yangu, huku akiwa amepiga magoti chini na damu kutoka kwenye tundu moja la pua yake, nikamshika kidevu na kukibinua juu.

"Kwanini kalamu yangu hukuichukua?". Nikazungumza na kutizama rungu langu ambalo ndilo lililomraza alex miezi mitatu hospitali, ndiyo silaha yangu kubwa chuoni hapo.

"Sitarudia domy!!" Akazungumza na kulia kwa uchungu, moyo wangu ukafarijika baada ya kuona machozi yake

."Nenda ole wako useme chochote." Nikazungumza na nikamfuta damu yake ya pua kwa kutumia kitambaa chake na nikamkabidhi na kwa haraka akakimbia na tukaanza kumcheka mimi na jopo langu.

“ Kuna msichana mzuri kaletwa ni kisu hatari!!"

"Siyo vitu vyangu hivyo" Nikazungumza.

"Ah domy yaani unasema hivyo ujamuona huyo binti yani mweusi fulani hivi kama mwarabu wa kisomali nywele zake ndefu tena asilia siyo ma wigi kama ya jamila halafu sasa anakaa mbele yako"

."Mbele yangu?"

"Ndiyo leo si ukuingia darasani kaletwa huyo binti yaani Mwarabu yule mtoto amekamilika".

"Poa siyo kitu cha ajabu hicho." Nikazungumza na kumkazia macho.

"Sawa basi samahani." Akazungumza kwa upole.

“Ray yuko wapi leo?"

"Alitoka kidogo kuna mambo anafuatilia".

"Sawa" ghafla kishindo kama cha kuanguka kitu kilisikika "puuh" kwa haraka tukatoka nje na kutizama huku na kule, tukafanikiwa kuona mwili wa mtu ukiwa chini unavuja damu...

Tukamsogelea na kwa taharuki nikashtuka baada ya kumuona yule msichana ambaye kila siku nagombana naye kuhusu manukato yake mabaya yenye harufu kali. Tukatizama juu na kuona mgongo wa mtu ukiishia juu ya ghorofa lile la darasa letu.

"Ameanguka toka juu" .Raja akazungumza na tukatizama ghorofa lile ambalo ni darasa letu ulikuwa umbali mrefu zaidi ya ghorofa kama 3 hivi na ameanguka kwenye sakafu ya vigae vya mawe ambavyo vimejaa chuo kizima kwa ajili ya kuzuia vumbi na pia uchafu na kuvutia chuo chetu tofauti na vyengine.

"Anapumua". Nikazungumza na kwenda kumshika msichana yule, alikuwa ameshika tumbo lake damu zilikuwa zikimtoka puani na mdomoni kwa wingi pia kichwa chake kilikuwa kinavuja damu ya kutosha, na nyengine zikichuruzika toka sehemu za siri maana alivaa sketi fupi ambazo ndiyo sare zao.

"Nenda katoe taarifa" .Nikazungumza

."Tukimbie Domy hii kesi!" Rajah akazungumza.

" Kwani jengo si lina kamera inapiga upande wetu". Nikazungumza na kutizama kamera kisha nikashuka chini na kuanza kubeba mwili wake.

"Hazifanyi kazi domy". Rajah akazungumza na kunisisitiza kuwa hiyo ni kesi.

" Hapa chuo hakuna anayekuhamini kuwa wewe ujafanya chochote kama ukikutwa eneo hili".

" huyu kapatwa na tatizo". Nikazungumza na kubeba mwili wake vizuri na kuanza kumkimbiza hospitali ya chuo ambayo ni mita chache tu toka nilipo, watu wakabaki wamenikodolea macho kwani kila mtu alishangaa nini kinaendelea,jopo kubwa la madaktari likaja na kitanda cha kusukuma kwa haraka wakamlaza yule binti na kuanza kukisukuma kwa haraka kwenda ndani ya vyumba vya matibabu.

" Kawaje huyu". Dokta akaniuliza huku uso wake ukionyesha kunikazia kama nahusika katika hilo kwani hata siku moja sijawahi msaidia mtu.

" Amesukumwa". Rojah akazungumza na kufanya daktari kumtizama.

" Na nani?".

" Tuliona tu mgongo wa mtu".Nikazungumza na daktari akatingisha kichwa chake na kuelekea kwenye majukumu yake.

"Nimefanya nini sas?". Nikazungumza huku nafsi ikinisunta kwa kumsaidia au kumpeleka binti yule hospitali, hali yake ilikuwa mbaya mno na anaonekana alikuwa mjamzito.

"Umetaka tuwe mashahidi we ungesema tumemkuta chini". Nikazungumza na kumtizama rajah

" Nimesema hivyo kukulinda mkuu ili uchunguzi ufanyike ibainike ni nani aliyefanya hilo tukio". Rajah akazungumza na kufanya hasira kidogo zipungue.

" Umesema kamera za pale hazifanyai kazi?"

" ndiyo sasa zingekuwa zinafanya kazi uhalifu wetu wa kule chini tungeonekana kila siku". Akazungumza na kutingisha kichwa chake huku akitabasamu juu ya matukio yetu maovu ya kupiga watu bila huruma.

" Ni Mjamzito". Nikazungumza na rajah akanishangaa.

" Umemtambuaje". Akaniuliza ila sikumjibu tuka toka hospitai na kukutana na jopo la uchunguzi likiwa nalo linafika.

Lilikuwa jopo la uchunguzi hapo hapo chuo, uchunguzi wake ni siku moja pekee halafu taarifa ndiyo inafika polisi, walifanya hivi ili matatizo ya chuo yasitoke nje pia jopo hilo lilipewa kibari na polisi kwa siku moja pekee na pia kulikuwa na polisi wawili katika jopo hilo hili kuhakikisha hakuna kitu kinachoharibika yani kilikuwa chuo ambacho kila idara ilikuwepo.

" Domy na wenzako tunawahitaji". Kiongozi wa hilo jopo akazungumza na kunitizama kwa hasira za wazi wazi, kwani kesi zake nyingi akinishtaki nilikuwa namshinda, akanisogelea,

" Hii kesi najua uchomoki hata kama baba yako ni rais ni ngumu sana kujinasua". Akazungumza na kutabasamu, nami nikatabasamu na kumnong'oneza sikioni kwa sauti ya chini sana.

" Najua wewe ndiye uliyefanya ilo tukio". Nikazungumza na kumuona jinsi alivyoshtuka na kutizama kulia na kushoto kama kuna mtu amesikia kauli yangu, nikamuona jinsi uso wake ulivyobadirika ukawa wa mshangao zaidi.

" Najua ni vita ya mapenzi". Nikazungumza na kumuona mkuu huyo wa jopo hilo la uchunguzi akizidi kuchanganyikiwa zaidi.

" Unasema kuhusu nini?". Akazungumza baada ya kumuona mkuu wa chuo anakuja kule tulipo.


ITAENDELEA
We jamaa huaminiki jinsi ulituacha solemba kule kwenye Ile sea m nilijiapiza sitasoma tena hzi ngonjela.. yaan duh
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom