SEE ME
AGE..........................................18+
SEHEMU YA 33/50
(THE LAST CHAPTER).
*********************
"TUMEKWISHA". Nikazungumza baada ya mimi kufungua dirisha jengine na kujionea buti zaidi ya nne zikiwa na watu wawili wawili wenye silaha za kivita, na bendera yao ya wanamgambo wa AL SHAABAB.
" Kwanini ulimuamini Don john". Nikazungumza huku hofu ikiniandama, nikamtizama X nakumuona akiwa dhaifu hakuwa X yule ambaye alikuwa akipotea na kutokuonekana kabisa machoni mwa watu, alikuwa X mpya kabisa tena mjamzito.
Akatoka kitandani na kuinama chini ya uvungu akatoa sanduku refu na kulifungua akatoa jambia lake na kufanya nitamani kumtukana.
" Mikono juu". Nikazungumza baada ya kuona miale mekundu ya taa ikitumulika mwilini mwetu, akaacha ile silaha chini na aknyoosha mikono juu, tukatoka wenyewe mpaka juu ya boat na jamaa wale wakaanza kushangilia walipotuona, baadhi yao wakapanda ndani ya boat yetu na kutufata tulipo huku wakiwa na mitutu ya bunduki kubwa za kivita hazikuwa na usajili wowote ile kuwa inatoka taifa gani, ila nilizitambua bunduki zile siyo za jeshi la somalia, nikawatizama wana mgambo wale wa AL SHAABAB ambao lengo lao kuu ni kutaka kupindua serikali ya somalia na kuunda serikali mpya na nguvu zao mpaka silaha walikuwa wanatoa toka kwa kundi kubwa la kihalifu AL QAIDA, walitaka kupindua serikali yao inayohaminika kuungwa mkono na mataifa ya magharibi pamoja na umoja wa mataifa, walikuwa ni vijana wenye itikadi kali katika jeshi lao la kihalifu nchini humo.
Wakanisogelea na kunitizama kitako cha bunduki kikatua kichogoni mwangu na kufanya macho yangu kuona giza zito, nisipate fahamu nini kinaendelea....
*************
Sauti za milio ya risasi ikafanya nifumbue macho, nikaona kundi kubwa la watoto wadogo wakipiga risasi ovyo ukutani huku wakishangilia kwa kuongea kiarabu ambacho sikukielewa, nikatizama na kugundua nipo katikati ya uwanja mkubwa wa mazoezi na nipo ndani ya ngome yenye kuta ndefu iliyojaa silaha za kivita pamoja na maneno mengi yalichorwa ukutani, yalikuwa maneno ya kiarabu ambayo sikuelewa yana maana gani, ulinzi mkali wa ngome hiyo ukafanya nimeze mate kwani ukuta wake huwezi upanda bila ngazi na pia kwa juu uliwekwa nyavu za chuma ( seng'enge).
Pia ndani ya ngome hiyo kulijaa nyumba ndogo ndogo zilizojengwa kwa tofali imara, nyumba hizo huenda zilikuwa za askari kupumzika au familia zao.
" nikaona jengo kubwa ambalo lilionekana hapo ndipo kiongozi wao na serikali yao yote iko hapo.
Ghafla kitambaa kikubwa kikatelemshwa ukutani yani kikakunjuliwa kule kwenye lile jengo kubwa kitambaa kile kilikuwa na picha kubwa ya mwanamume mweupe mwenye ndevu za kutosha kwenye kidevu chake huku juu ya kichwa chake akiwa amejifunga kilemba cheusi, nikameza mate baada ya kumtambua kuwa ni mtu niliyemuua miaka 6 iliyopita.
Sauti ikatoka kwenye kipaza sauti na kufanya kutoelewa chochote kwani walizungumza kiarabu,ghafla kundi la watu wanne likaja na farasi toka lango kuu la jengo lile kubwa, walikuwa na silaha za jadi, kila mmoja alikuwa na panga mkononi mwake, wakawa wanakuja kule nilipo taratibu na farasi zao, kile kitambaa kikapandishwa juu na kikashushwa kengine,ambacho kilikuwa na picha ya mtoto wa rais wa umoja wa mataifa, alikuwa ni mwanamziki mkubwa duniani na alipendwa na watu wengi kutokana na nyimbo zake, pia alikuwa ni binti mrembo wa kuvutia kila mwanamume na mpenzi wake inavyosadikika alikuwa ni rais wa marekani, jambo ambalo binti huyo amekuwa akilikana.
" Unashangaa".? Wale jamaa wenye farasi mmoja wapo akazungumza kwa kiswahili tena fasaha, kidogo nikapata haueni
" Mnataka nini?". Nikapata ujasiri wa kuuliza
" tulia bro umesahau una mke wako humu ndani". Akazungumza na kufanya nimkumbuke X mwenye mimba yangu pia moyo wangu ulikwishaanza kumpenda mwanamke huyo.
" sio mke wangu". Nikazungumza
" ile mimba tuitoe". Akazungumza na kufanya nitingishe kichwa kwa kukataa kuwa asiitoe kwani sikuhitaji mtoto wangu mwengine kupotea.
nikaona wanatizama nyuma yangu na wakashuka wote kwenye farasi zao, nikageuka nyuma kuona wanatizama nini? Nikaona wanaume wawili wakiwa wamemuweka mtu kati huku wakiwa wamemfunga kamba mikononi mwake, na uso wake wameufunika na gunia zito jeusi, huku mwili wake ukiwa na boksa pekee, na alionekana amechoka kwa mateso kwani mwili wake ulionekana dhaifu. Wakatufikia tulipo na kumsukuma mtu yule chini, ambaye akadondokea miguuni mwangu.
"Maji". Akazungumza kwa tabu huku akijaribu kujitoa gunia usoni mwake.
" Una mfahamu ndugu yako?". Jamaa yule akazungumza na kufanya nimtizame kwa mshangao.
" Hahaha una shangaa Ina maana mama yako akukuambia mlizaliwa mapacha". Jamaa huyo akazungumza na kufanya nishtuke na kuona ni mchezo huenda ananichezea.
" Don john ina maana hakukuambia ukwel?".
" sijuhi unazungumza kuhusu nini?" Nikazungumza na kumtizma mtu huyo aliyechini, ni kama gunia lake lilionyesha ila sisi ndiyo hatukuweza kumuona uso wake yani ni kama vile vioo ambavyo wa ndani anakuona wa nje ila wa nje hakuoni wewe wa ndani, jamaa yule akashika mguu yangu kwa nguvu na kuanza kulia kwa uchungu, inaonekana alinijua
" unataka kunichezea game"?
" Hahah ina maana Don john ajakuleza kila kitu mr zengo alimpatia mama yako grace watoto mapacha".
" Mmh". Nikaguna huku nikitamani ardhi ipasuke inimeze.
" huyo anakujua vizuri tu anajua wewe ni kaka yake mtu gani yupo radhi, apigwe risasi ili wewe upone". Akazungumza na kufanya nishtuke na kukumbuka tukio la miezi mingi iliyopita la mtu aliyenisaidia afu sikumfahamu
" Alikufa na haiwezi kuwa ivyo sura yake haifanani na mimi kabisa hii ni drama". Nikawaza
" Randy!". Mtu yule akazungumza na akaanza kulia kwa uchungu huku akishika miguu yangu kwa shida kutokana kamba aliyofungwa mikononi.
Jamaa mmoja wapo akamvuta lile gunia na nikapigwa na bumbuwazi baada ya kuona sura ya marehemu wa siku nyingi.
" AMI...DU"....
SEE ME
ITAENDELEAA.......