Regina Mwalekwa wa Clouds FM alamba shavu BBC!

Regina Mwalekwa wa Clouds FM alamba shavu BBC!

Nchi hii kifaa ni Gaston Msingwa.BBC wabebe jembe hilo.Nasikia hata watangazaji wenzake pale TBC huwa wanamuonea wivu ndiyo maana hawaki awe makao makuu, eti atawafunika.

Mimi taarifa ya habari ya TBC huwa naangali kwa ajili yake tu.
Nashangaa kwa watangazaji wengine hawaigi.

Hili jamaa huwaga limejichimbia songea kama sikosei
 
Ni mtangazaji mzuri huyu mama,anastahili hasa!
Hongera Regina M.
 
Ni kweli mkuu, nadhani wanaodhani REDIO ONE ndiyo ilinayopaswa kushukuriwa watakuwa wanakosea sana. Nakumbuka sana enzi zile yuko na Wakina Rozi Mdami, Tom Chilala na yule Padri Mfaransa (Mzee wa kipindi cha Kahawa au Chai) ambaye aliondoka nchini....si mchezo aisee.....

Umenikumbusha mbali sana hasa yule mfaransa na kipindi cha kahawa au chai nilikuwa napenda kumsikiliza hasa kile kiswahili chake cha lafudhi ya kifaransa!
 
hahaaa wakaja mtoa wakamweka taarifa ya habari then power break saturday morning...yan angebakigi radio one angepaa sana japo maslah ni zero.

hv huyu mang anaesifika ku utajiri ndo hawalipi wafanyikaz wake kumbe ndo utajir wake ulipotokea,pamoja na yote mshahara halilipi? loh ni njia pia ya kujiongezna 0 za mbele
 
Safi sana hongera Dada Rjina lakini pia bila kuwasahau Blauzi FM kwa kumtoa dada tunasubiri kimlima nae aende BBC
 
Kama Ni Kweli Basi BBC Wamepata Jembe Kwani Dada Huyo Ana Karibia Sifa Zote Kuu Na Muhimu Za Mtangazaji Na Mwandishi Wa Habari. Sina Shaka Nae Na Hata Rekodi Yake Ni Nzuri. Binafsi Namtakia Kila La Kheri Huko Uingereza Aendako. Sifa Ziende Kwa Redio One Waliomwibua Kisha Clouds FM Kwa Kumtengeneza Na Kumsafishia Njia Ya Mafanikio. Hongera Na Heko Zako Dada Regie....................!

Acha kudanganya watu Rejina Mwalekwa hajaibuliwa na Radio One kabla ya kwenda radio one alikuwa PRT ambayo sasa ni TBC fm.Au umesahau?
 
Kumbe wengi wamemfahamia redio wani! Huyu alianzia redio Tumaini, akapitia redio nyinyiem {Uhuru FM} akitangaza zaidi kipindi cha zilipendwa {Enzi Hizo) akifundishwa na mkongwe Masoud Masoud, baadae alikuwa na bibie Rachwl Udoba! Ndipo akahamia redio wani na baadae Clouds.
Hongera dada yetu wa Kinyamwezi Regina Mwalekwa!!
 
Afadhali!
Nilikuwa simwelewi anafanya nini Clouds!
Clouds alikuwa hafit popote!pooooopote!
Hongera mamii!
Hapo ndo mahali unatakiwa kuwepo!
 
Kama sikosei (I stand to be corrected) alipitia Radio Tumaini kabla ya kwenda Radio One...Amekaa sana Radio Tumaini ambako alijijengea sifa ambayo ilipelekea Radio One wakamuona...

Upo Sahihi Mkuu..............Akhsante Kwa Kuniongezea Ufahamu Huo. ILA Dada Anatisha Na Yupo Vizuri Sana Na Mno!!!!!!!!
 
Malizia mmoja usipompa ahsante nimtaje......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom