Regina Mwalekwa wa Clouds FM alamba shavu BBC!

Regina Mwalekwa wa Clouds FM alamba shavu BBC!

Nimekuwa nikijiuliza nini kinafanya Mtangazaji Bora kabisa kama huyu asipae kimataifa? Nadhani sasa swali langu limepata jibu. Namkubali zaidi ya sana, hasa katika kukuza lugha ya kiswahili na matumizi fasaha ya lugha hiyo....

Kaitangaze Tanzania Mama, Kaikuze Lugha yetu adhimu ya Kiswahili Kimataifa....Kila la heri


CHUKUA 100000 hili suala hata mimi lilinitatiza .
 
Mkuu GENTAMYCINE 11:21 Today
Sio kweli kua IPP ndio waliomtoa Regina bali ni Radio Tumaini ndio wapewe sifa kwakua alitokea huko na umaharufu wake na umahiri wake ulimpa nafasi hadi IPP. Tena kipindi hicho walikuepo wakina Tom Chilala na Rose Mdami. Kwa ukweli tumtakie kila la kheri maana anafanyakazi kwa bidii sana tena anazingatia sana taaluma yake.
 
Last edited by a moderator:
Kama wamemchukuwa huyu dada anatakiwa amshukuru sana mwavile wa radio one
Yeye ndio alikuza kipaji cha mwalekwa kabla clouds hawajatia fitina na kumchukuwa!
 
Hongera sana, hakikisha unaondoka na mumeo, vibaka wamezidi, utakuta patupu
 
Kwani na huko Bush House kuna mashindano ya bibi bomba ama anayapeleka haya ya kwetu huko
 
Kila siku nimekuwa nikifikiria mbona kama huyu dada wafu fm sio mahali pake kabisa! Lumbe mawazo yangu ni sahihi kanisa aisee.
 
Kila la heri dada.........tunafurahi pamoja na wewe.
 
Nimekuwa nikijiuliza nini kinafanya Mtangazaji Bora kabisa kama huyu asipae kimataifa? Nadhani sasa swali langu limepata jibu. Namkubali zaidi ya sana, hasa katika kukuza lugha ya kiswahili na matumizi fasaha ya lugha hiyo....

Kaitangaze Tanzania Mama, Kaikuze Lugha yetu adhimu ya Kiswahili Kimataifa....Kila la heri
Hilo swali hata mie nilijiuliza sana, hasa baada ya kuondoka radio 1 na kwenda Clouds. Kwa kariba ya huyu dada hakutakiwa kwenda redio ya udaku. Ilitakiwa atoke redio 1 moja kwa moja hadi BBC, kama walivyokuwa wengine akina Flora Nducha, Abdalla Majura, Kikeke n.k.
 
Nimekuwa nikijiuliza nini kinafanya Mtangazaji Bora kabisa kama huyu asipae kimataifa? Nadhani sasa swali langu limepata jibu. Namkubali zaidi ya sana, hasa katika kukuza lugha ya kiswahili na matumizi fasaha ya lugha hiyo....

Kaitangaze Tanzania Mama, Kaikuze Lugha yetu adhimu ya Kiswahili Kimataifa....Kila la heri
huyu mama anakubalika sana pia aishukuru sana radio one ndiyo iliyomtoa huko clouds alikuwa amepotea kabisa shimoni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom