Rais Samia, Mwinyi Wapokea kwa Shangwe Ushindi wa Karume Boys, Waipongeza kwa Kutwaa Ubingwa wa CECAFA U-15

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt Hussein Mwinyi wameipongeza timu ya Taifa ya Zanzibar chini ya miaka 15 (Karume Boys) kwa kutwaa ubingwa wa mashindano ya CECAFA-U15 yaliyofanyika nchini Uganda.

Karume Boys waliwafunga wenyeji Uganda ambao pia walikuwa mabingwa watetezi kwa changamoto ya mikwaju ya penalti baada ya mchezo kuisha kwa sare ya goli 1-1

Rais Samia ameandika kupitia mitandao ya kijamii

"Hongereni sana Timu ya Taifa ya Soka ya Zanzibar kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 (Karume Boys), kwa kutwaa ubingwa wa CECAFA U15 2023. Mmetupa heshima kubwa. Nawatakia kila la kheri katika ndoto na safari yenu kwenye mchezo wa soka siku za usoni."
Screenshot 2023-11-17 at 08.13.58.png


Ukurasa rasmi wa Ikulu ya Zanzibar ulimuonesha Rais Mwinyi akishangilia ushindi huo wakati akifuatilia mchezo
huo ofisini kwake Ikulu ya Mnazi Mmoja-Zanzibar
Screenshot 2023-11-17 at 08.19.22.png
 
Mbona sisi bara hatujui uwepo wa hayo mashindano?? Kweli hizi ni too kantriz
Ni michuano ya CECAFA ni michuano ya ukanda huu wa afrika, sisi kutokujua uwepo wake ni ushahidi wa kutofautilia masuala ya mpira.

Umekuja na mada ya two countries ili uhamishe mjadala uupeleke kwenye siasa, haya ni masuala ya soka ni mipango ya kimpira haihusiani kabisa na masuala ya siasa.
 
Ni michuano ya CECAFA ni michuano ya ukanda huu wa afrika, sisi kutokujua uwepo wake ni ushahidi wa kutofautilia masuala ya mpira.

Umekuja na mada ya two countries ili uhamishe mjadala uupeleke kwenye siasa, haya ni masuala ya soka ni mipango ya kimpira haihusiani kabisa na masuala ya siasa.
Watu wako bize kuwafatilia wakin zuchu na wakata mauno wengine

Ova
 
Back
Top Bottom