Waziri Tabia Mwita Amshukuru Dkt. Mwinyi kwa Kombe la CECAFA U15 Kutua Zanzibar

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,903
945

WAZIRI TABIA MWITA AMSHUKURU DKT. MWINYI KWA KOMBE LA CECAFA U15 KUTUA ZANZIBAR

Mabingwa wa CECAFA U15, Karume Boys wametua nyumbani Zanzibar wakitokea nchini Uganda na ubingwa wao walioupata kwenye michuano ya CECAFA U15 Boys Championship.

Karume Boys wamepokelewa na Makamu wa Pili wa Rais, Mhe. Hemed Suleiman, Waziri wa Michezo, Mhe. Tabia Mwita, Mkuu wa Mkoa, Mhe Idrisa, viongozi mbalimbali, Wazazi na wadau wa soka visiwani Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais, Mhe Hemed Suleiman, Waziri wa Michezo, Mhe Tabia Mwita, Mkuu wa Mkoa, Mhe. Idrisa wamepata bahati ya kuwa viongozi wa kwanza kubeba kikombe cha ubingwa wa CECAFA U15 kilicholetwa na vijana wa Karume Boys.

Karume Boys wameletwa na Ndege maalum iliyotolewa na Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi ambayo imewafikisha vijana wa Karume Boys nchini wakitokea Entebbe, Uganda.
 

Attachments

  • F_JZBGPWIAAr7tw.jpg
    F_JZBGPWIAAr7tw.jpg
    126.2 KB · Views: 5
  • F_JaNeVWQAAvksn.jpg
    F_JaNeVWQAAvksn.jpg
    183.2 KB · Views: 5
  • F_JaOSwWsAAgiOn.jpg
    F_JaOSwWsAAgiOn.jpg
    157.2 KB · Views: 4
  • F_JaN37XAAAok60.jpg
    F_JaN37XAAAok60.jpg
    144.8 KB · Views: 4
  • F_JaOuHWcAALm2g.jpg
    F_JaOuHWcAALm2g.jpg
    172.4 KB · Views: 4
  • F_JcpXRXEAA11WQ.jpg
    F_JcpXRXEAA11WQ.jpg
    147.1 KB · Views: 5
Back
Top Bottom