Rais kaishiwa pumzi, karudi square one

Rais kaishiwa pumzi, karudi square one

Hayo ni yako. Haya hujayaona?

Ununuzi wa ndege
Ujenzi wa reli
Elimu bure
Nidhamu makazini
Kuwajali masikini
Nafuu ya maisha
Kujitegemea
Kuwathibiti mafisadi
Kurejesha mashamba


Acha porojo wewe. Waswahili husema ukiona manyoya ujue keshaliwa. Ukiona mtu anaandika hayo uliyoandika ujue amekamatika katika mojawapo.
 
Kweli ni vigumu ku judge performance ya mtu kwa kipindi kifupi, lakini umeshajiuliza na wewe kwanini umpongeze kwa kipindi kifupi kwanini usimpe muda wa miaka mitano ndipo umpongeze.
wapi nimepongeza?
 
Nashangaa umeangalia upande mmoja tu ilhali Rais kafanya mambo mengi makubwa yanayofuta hayo uliyoandika
Lizaboni, kuuwa mzizi wa ditina ungeyataja mambo hayo.... otherwise nimeona tu umeyakubli maelezo ya jamaa...
 
Umeongea vinzuri , tatizo yote aliyofanya hayana msingi shirikishi, yaani hakuna utendaji Wa kitaasisi rushwa IPO wapi nguvu ya takukuru, uwajibikaji Wa w/umma sipo wapi taasis za maadili au n hawa wakuu Wa mikoa, reli , ndege liko wapi bunge, kwenda Dodoma IPO Wa nguvu ya kibudget. Alafu eti waungwe mkono upi they know everything, future hakuna. Ila hata hivyo tumezoea kupata kidogo, tutasifia. Nchi zingine zikifanya kweli tunawaza std gauge angalia Ethiopia wanaongelea nini?, wakati maamuzi ya madiwani si kitu, nguvu ya miji,majiji Na halmashaur hoi siasa mbele, maneno matupu, macho kwenye kura hakuna lolote, ok, ok, ok.

Five Years my friend, kuwa na subira.. Mabadiliko ni kazi isiyo ya lele mama. Kwote tunakosifia leo wamepiga hatua China, Vietnam, Singapore,Indonesia, na nchi zinazochipukia hivi sasa Ethiopia, Rwanda nk zimepitia changamoto kubwa zaidi ili kufika walipofika....
 
Kila kitu alichodhani atakirekebisha kimeanza kurudia hali yake ya zamani.

Moto wa kupambana na mafisadi ni kama umezimika baada ya kuambiwa mahakama ya mafisadi imekosa kesi, tumerudi palepale.

Wakati anaingia alikuta TRA inakusanya bn 900 hadi tn1, yakaongezeka hadi tn1.5 leo yamerudi kule kule bn 900 sijui ya Nov inawezekana yameshuka zaidi.

Spidi ya kubomoa nyumba zilizojengwa mabondeni na kinyume cha sheria ulianza kwa mkwara ukapiga breki kwa mama Lwakatare, leo tumerudi kule kule.

Machinga ni vurugu mechi, ondoa rudisha ondoa, tatizo halijatatuliwa limebaki palepale.

Tumbua tengua teua mwisho tumeishia kuteua walewale tuliowatumbua hatuja solve kitu tumerudi kule kule.

Mikopo ya wanafunzi sio tu tumerudi tulipokuwa yaani square one bali hata uwezo wa serikali kulipa umepungua kulinganisha na serikali iliyopita.

Serikali imeshindwa hata kuajiri na kupandisha madaraja watumishi wake, ni kama tumerudi square one.

Alipoingia alizuia safari za nje akazuia sikukuu za kitaifa, leo watumishi wanasafiri kama kawaida na juzi tumesherehekea sikukuu ya Uhuru aliyoikataa mwaka jana, mambo yamekuwa business as usual.

Mapigano kati ya wakulima na wafugaji ni kama ndiyo yamezidi, pamoja na ahadi ya serikali yake kutatua kadhia hiyo ni kama tumerudi kule kule.

Kuna mengi ambayo alidhani rahisi kuyafanya yameanza kumshinda mfano, sukari ya Bharesa, pembe za ndovu, madawa ya kulevya, majangili. Nina uhakika anaweza kumaliza muda wake akayacha kama alivyoyakuta.

Naomba kutoa hoja.

Quinine.
Ukweli mchungu
The ugly truth
 
Five Years my friend, kuwa na subira.. Mabadiliko ni kazi isiyo ya lele mama. Kwote tunakosifia leo wamepiga hatua China, Vietnam, Singapore,Indonesia, na nchi zinazochipukia hivi sasa Ethiopia, Rwanda nk zimepitia changamoto kubwa zaidi ili kufika walipofika....
Mwanzo mlisema tumpe muda,hata mwaka bado?leo kuwa na subira 5yrs,then itakua mitano michache tumwongeze tena mitano amalizie[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
MvDSM inasubiri mda gani?
 
du ni hataree! kwani wale wa Escrow wote wameisha! au kiwango cha pesa walichgawana ni pesa ya madafu?
 
Ni kwa waliopungukiwa maarifa tu ndo wanaoweza kuunga mkono hoja hii ya hovyo. Ka una maarifa timamu huwezi kuleta hoja hii ukafikiri ndo jambo jema kwa nchi na kwamba tulishabikie hapa JF. Sisi kama watu waungwana yatupasa kumuunga mkono mheshimiwa raisi kuhakikisha nchi inakaa kwenye mstari na inakuwa na maendeleo chanya na si kumdhihaki na kuonyesha juhudi zake ni bure na kwamba nchi iendelee kuendeshwa hovyohovyo kwa kuendekeza wahujumu uchumi, wauza madawa ya kulevya, mafisadi na majanga mengineyo ktk nchi.
1.Kwani nchi ilikuwa nje ya mstari. 2.Unaweza mtaja aliyeendesha nchi hovyo hovyo.
3.unawezaeleza maana ya neno maarifa
4.unaweza eleza uhusiano baina ya uzi huu hapo juu na kukosa maarifa.
 
  1. Kanunua ndege sita
  2. Ujenzi wa Reli ya Kati kwq Standard Gauge
  3. Ujenzi wa Bomba la Mafuta toka Uganda hadi Tanga
  4. Kudhibiti ufisadi na matumizi mabaya ya fedha za umma
  5. Ujenzi wq Hostel pale UDSM
  6. Nyumba za Magomeni Kota
  7. Kupandisha bei ya korosho kutoka shilingi 1000 hado 4000
  8. Ujenzi wq Barabara ya Mwenge hadi Morocco
  9. Ununuzi wa Meli mpya Ziwa Tanganyika na Victoria
  10. Umeme wa uhakika. Hakuna mgawo kwa sasa
  11. Nk nk
Uko juu
 
Kutawala si sawa na kuongoza, kutawala ni rahisi kwa sababu kunahitajika kitu kimoja tu...nguvu
kulazimisha matakwa.

Kuongoza ni kugumu zaidi kwani kunahitajika vitu vitatu...ushawishi, busara na hekima, vitu adimu sana kwa baadhi ya watu.

Watawala hushindwa, viongozi hufaulu. Tulicheza pata potea kumchagua mtawala na sasa tunaonja ladha ya kosa letu.
Hilo linajulikana dhahiri, na nilishawaambia wadau kipindi kile. Wakasema kwa taifa lilipofikia anahitajika mtawala si kiongozi,. Ila hata hivyo kama uko na free mind, mwaka jana hapakuwepo na kiongozi kati ya wale ambao chapuo lingeweza kuwafikisha magogoni.
 
Ni kwa waliopungukiwa maarifa tu ndo wanaoweza kuunga mkono hoja hii ya hovyo. Ka una maarifa timamu huwezi kuleta hoja hii ukafikiri ndo jambo jema kwa nchi na kwamba tulishabikie hapa JF. Sisi kama watu waungwana yatupasa kumuunga mkono mheshimiwa raisi kuhakikisha nchi inakaa kwenye mstari na inakuwa na maendeleo chanya na si kumdhihaki na kuonyesha juhudi zake ni bure na kwamba nchi iendelee kuendeshwa hovyohovyo kwa kuendekeza wahujumu uchumi, wauza madawa ya kulevya, mafisadi na majanga mengineyo ktk nchi.
Sasa ulitaka aseme uongo?Mahakama ya mafisadi kukosa kesi nikweli inchi hii mafisadi wametubu na hawapo?
 
Huwezi kuua mfumo wa ccm kwa mwaka mmoja, sumu yao itawatafuna marais wengi hata akija malaika ni vigumu sana kuubadili mfumo ccm
Na ukitaka kuthibitisha hilo wala huna haja ya kuwa masters mfumo wa ccm ulizipiga kumbo raslimu za Warioba.wakaja na katiba myeyusho pendekezwa na viongozi na makada wa ccm wote walikuwepo.
 
Hivi hiyo Mahakama ya mafisadi kukosa kesi,kuanzishwa kwake kulilenga kuwashitaki mafisadi WAZAMANI au WAPYA? Jamani nauliza tu hivi Dhambi ya zamani na ya sasa zinatofautiana?
 
Kutegemea mabadiliko ndani ya CCM ni sawa na kupiga ngumi ukuta.
Hivi kwani watanzania wanataka mabadiliko gani? Mi sikipendi ccm kwakuwa kimeleta mabadiliko makubwa sana yaliyonikera, nadhani kingeendelea kulekule kilipokuwepo. Mabadiliko yapi tunayoyazungumzia hapa? Tulivunje azimio la Zanzibar tulirudishe la Arusha au yote hamyataki? Yapi sasa.
 
Nenda kanywe maji mengiiiii roho uliyonayo ya kwanini ikuishie karibu awamu ya tano ujionee maendeleo ya kweli
Mh Magufuli nyoosha nyoosha waandike kila hoja
2017 loading
 
Back
Top Bottom