Quinine Rais amepewa na wanancchi mandate ya miaka mitano kuongoza nchi na kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Ndio kwanza tumemaliza mwaka mmoja, kutoa hukumu kwamba Rais atamaliza muda wake akayaacha kama alivyoyakuta ni upotoshaji or rather wishful thinking.
wakati ni muamuzi sahihi wa kufanikiwa kwa Rais...na wakati huo ni miaka mitano na sio mwaka mmoja. Lakini hata ukiamua kumpima kwa mwaka mmoja, umechagua kuyaacha mambo ya msingi yaliyokwishafanyika yenye manufaa kwa wananchi wengi.
Jambo la kwanza na kubwa lililofanyika ni kutoa ELIMU BURE kuanzia msingi hadi sekondari. usipoangalia jambo hili kwa upana,waweza kudhani ni jambo dogo,lakini ukweli ni kwamba familia zote mijini na vijijini zenye watoto wenye umri wa kwenda shule, sasa wana uhakika wa elimu ya watoto wao katika ngazi hiyo ya msingi.
Eneo jingine ambalo Serikali inachukua hatua ambalo watu wengi hawalizungumzi ni kulipa madeni. Tunaposoma habari kwamba serikali imekopa fedha kujenga barabara, hospitali n.k maana yake ipo siku tutatakiwa kulipa. Serikali ya Awamu ya tano imeingia madarakani katika kipindi ambacho madeni yaliyokopwa miaka ya nyuma yamemature na yanatakiwa kulipwa. Kwa kuweza kulipa madeni hayo ndiko kunakoifanyTanzania iendelee kuaminiwa na mashirika ya fedha ya kimataifa kuendelea kukopeshwa fedha kwa ajiili ya kutekeleza miradi mipya ambayo itawagusa wanachi walio wengi
Kuanza hatua za Kutekeleza miradi yenye tija kwa wananchi wengi. hivi sasa Serikali ipo kwenye hatua ya kupata mkandarasi wa kujenga Reli ya Kati katika Kiwango cha kimataifa. Mradi huu utafungua upya fursa za uchumi kwa wananchi wa dar es salaam, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Kigoma, Mwanza.....Reli itakapojengwa itatoa ajira kwa maelfu ya wanannchi, na itakapokamilika itarahisisha usafirishaji wa mizigo na kupunguza gharama za kufannya biashara kutokana na urahisi iwa usafiri...lakini sio hivyo tu ikikamilika itapungusa kasi ya uharibifu wa barabara zetu ambazo zimejengwa kwa pesa nyingi za walipakodi na mikopo tunayoendelea kuilipia
Kupunguza mianya ya upotevu wa fedha za umma kwa njia ya ukwepaji kodi, malipo hewa (mishahara hewa, wanafunzi hewa, zabuni hewa) pamoja na overpricing/overcharging zilizokuwa zinafanywa kwenye manunuzi ya umma ambayo mwisho wake mzigo ulikuwa unabebwa na walipakodi. Juhudi zilizokwishafanyika zinastahili kuungwa mkono,lakini zaidi ushirikiano wa wananchi wazalendo, wenye nia njema ya kuona maovu yanatoweka unahitajika sana....Rais hawezi kujua kila kitu kinachotokea kila mahala.....anahitaji ushirikiano wa wananchi, anahitaji utendaji bora wa vyombo vyake.....
Mnyonge mnyongeni,haki yake mpeni.....ndani ya muda mfupi tumeona ndege yetu iliyokuwa inachechemea miaka nennda rudi inaruka.....tena ikiwa na ndege mbili mpya tunazomiliki wenyewe. Wapo watu wanabeza mafanikio hayo....pengine ni kwakuwa tumesahau tulikotoka......hivi mnajua ATCL iliwahi kukodikukodisha ndege ya zamani na kulipia mabilioni ya shilingi? leo hii tunamiliki ndege,hatudaiwi na mtu...si jambo la kubeza.
Kwa vyovyote vile, yapo mapungufu na changamoto mbalimbali zilizojitokeza ndani ya mwaka mmoja, lakini hazitoshi kutoa hukumu ya kushindwa kazi wakati kuna mafanikio mengi na muda wa miaka minnne wa kutekeleza zaidi. Tumpe nafasi Rais wetu atekeleze wajibu aliopewa na wananchi ili tutoe verdict yetu vizuri baada ya miaka mitano. pale penye mapungufu tuwe wazalendo kutoa solutions zifanyiwe kazi na sio kupinga tu maana nchi hii ni yetu sote.