Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,645
- 164,792
Tuone mara ngapi mkuu?Nyie ngojeni tu mtaona.... Hii awamu inaweza kuwa awamu mbovu kuliko zote zilizotangulia!!
Tuone mara ngapi mkuu?Nyie ngojeni tu mtaona.... Hii awamu inaweza kuwa awamu mbovu kuliko zote zilizotangulia!!
Yapi? Yalete hapa mjengoniNashangaa umeangalia upande mmoja tu ilhali Rais kafanya mambo mengi makubwa yanayofuta hayo uliyoandika
Hovyo! Ishukuru demokrasia.Ndege sita isije kuwa hela za rambirambi zimetumika, bomba la mafuta kwani tunajenga sisi, reli ya standard gauge hivi imefika wapi vile, meli mpya isije kuwa kama ahadi ya Kigoma kuwa Dubai.
Safari zikizuiwa kelele,watu wameanza kusafiri tena kelele,hivi sisi tunataka nini hasa?Kila kitu alichodhani atakirekebisha kimeanza kurudia hali yake ya zamani.
Moto wa kupambana na mafisadi ni kama umezimika baada ya kuambiwa mahakama ya mafisadi imekosa kesi, tumerudi palepale.
Wakati anaingia alikuta TRA inakusanya bn 900 hadi tn1, yakaongezeka hadi tn1.5 leo yamerudi kule kule bn 900 sijui ya Nov inawezekana yameshuka zaidi.
Spidi ya kubomoa nyumba zilizojengwa mabondeni na kinyume cha sheria ulianza kwa mkwara ukapiga breki kwa mama Lwakatare, leo tumerudi kule kule.
Machinga ni vurugu mechi, ondoa rudisha ondoa, tatizo halijatatuliwa limebaki palepale.
Tumbua tengua teua mwisho tumeishia kuteua walewale tuliowatumbua hatuja solve kitu tumerudi kule kule.
Mikopo ya wanafunzi sio tu tumerudi tulipokuwa yaani square one bali hata uwezo wa serikali kulipa umepungua kulinganisha na serikali iliyopita.
Serikali imeshindwa hata kuajiri na kupandisha madaraja watumishi wake, ni kama tumerudi square one.
Alipoingia alizuia safari za nje akazuia sikukuu za kitaifa, leo watumishi wanasafiri kama kawaida na juzi tumesherehekea sikukuu ya Uhuru aliyoikataa mwaka jana, mambo yamekuwa business as usual.
Mapigano kati ya wakulima na wafugaji ni kama ndiyo yamezidi, pamoja na ahadi ya serikali yake kutatua kadhia hiyo ni kama tumerudi kule kule.
Kuna mengi ambayo alidhani rahisi kuyafanya yameanza kumshinda mfano, sukari ya Bharesa, pembe za ndovu, madawa ya kulevya, majangili. Nina uhakika anaweza kumaliza muda wake akayacha kama alivyoyakuta.
Naomba kutoa hoja.
Quinine.
Bora wa mabunz japo unaumiza machoMoto wa kifuu cha nazi
Phd HewaNaunga mkono hoja
tumuunge mkono kwa lipi sasa ??? Looh hakuna kiongozi mpumbavu kama huyoNi kwa waliopungukiwa maarifa tu ndo wanaoweza kuunga mkono hoja hii ya hovyo. Ka una maarifa timamu huwezi kuleta hoja hii ukafikiri ndo jambo jema kwa nchi na kwamba tulishabikie hapa JF. Sisi kama watu waungwana yatupasa kumuunga mkono mheshimiwa raisi kuhakikisha nchi inakaa kwenye mstari na inakuwa na maendeleo chanya na si kumdhihaki na kuonyesha juhudi zake ni bure na kwamba nchi iendelee kuendeshwa hovyohovyo kwa kuendekeza wahujumu uchumi, wauza madawa ya kulevya, mafisadi na majanga mengineyo ktk nchi.
Ebu nitajie moja lililofanikiwa labda kujenga Airport Chato.
Kwani Ilipinda?na kama ilipinda nani aliipindisha?kama aliipindisha au waliipindisha wamechukuliwa hatua gani?na tunahakikishiwa vipi kama haitapinda tena?Ni kwa waliopungukiwa maarifa tu ndo wanaoweza kuunga mkono hoja hii ya hovyo. Ka una maarifa timamu huwezi kuleta hoja hii ukafikiri ndo jambo jema kwa nchi na kwamba tulishabikie hapa JF. Sisi kama watu waungwana yatupasa kumuunga mkono mheshimiwa raisi kuhakikisha nchi inakaa kwenye mstari na inakuwa na maendeleo chanya na si kumdhihaki na kuonyesha juhudi zake ni bure na kwamba nchi iendelee kuendeshwa hovyohovyo kwa kuendekeza wahujumu uchumi, wauza madawa ya kulevya, mafisadi na majanga mengineyo ktk nchi.
Akina Faru Khadija eeenhMahakama ya mafisadi itafanyaje kazi wakati vibaka wote mmenyooka? Thats the whole point....unapaswa kulalamika ikiwa ufisadi unaendelea huku watuhumiwa hawafikishwi mahakamani
Yako wapi mazuri?? Makusanyo sasa hivi TRA hawakurupuki kutangaza kamweNashangaa umeangalia upande mmoja tu ilhali Rais kafanya mambo mengi makubwa yanayofuta hayo uliyoandika
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] ndio vipaumbele??? Hivi mbona mnadandia mambo Bomba ni la Sizonje?? Reli gani imejengwa?? Ndege sita ziko wapi mi najua mbili tuu
- Kanunua ndege sita
- Ujenzi wa Reli ya Kati kwq Standard Gauge
- Ujenzi wa Bomba la Mafuta toka Uganda hadi Tanga
- Kudhibiti ufisadi na matumizi mabaya ya fedha za umma
- Ujenzi wq Hostel pale UDSM
- Nyumba za Magomeni Kota
- Kupandisha bei ya korosho kutoka shilingi 1000 hado 4000
- Ujenzi wq Barabara ya Mwenge hadi Morocco
- Ununuzi wa Meli mpya Ziwa Tanganyika na Victoria
- Umeme wa uhakika. Hakuna mgawo kwa sasa
- Nk nk
Ina taabu ukilewa unakuja kutapika jf [emoji4] [emoji4] [emoji4] [emoji4]CHADEMA wamechanganyikiwa sana. 2020 hawana Mgombea
Mkuu hata wazee wanasema kuwa ukiona utawala mwaka wa kwanza tuu hakuna mvua hizo ni salaam toka juu kuwa kuna laana ya aina fulani imewashukia.Huu ni utawala uliofitinika na kulaanika