Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

Ili kujiita una nguvu kwa dunia ya sasa lazima..
1-uwe na idara bora kabisa ya usalama na vyombo vya usalama ambavyo havijihusishi na siasa wala kutumika kisiasa..

2-silaha za kisasa, teknolojia za kisasa na wataalamu wa cyber security, electronics warfare, ITs n.k .....

3-Wananchi wazalendo ambao wata support nchi yao kwa nguvu moja kipindi cha vita

sasa tujiulize katika hayo tupo hapo kweli?
Mkuu, yanayoendelea Palestine, Iran, Israel, Ukraine na Russia yanatufumbua macho kutuonesha sisi bado tupo nyuma saana ktk medani za kivita za sasa.

Mimi nasema kila siku humu, tukipata mpinzani kama Rwanda, Uganda, Kenya huko Ethiopia, Angola, Misra n.k tusithubutu hata kidogo, hawahawa jirani zetu, endapo tukawapiga basi watatuachia kovu zito saaaana.
 
kwa Africa mashariki nchi ambayo itaisumbua Rwanda ni Kenya.
Watu wa Tall hawako infiltrated ndani ya kenya kama walivyojiingiza ndani ya Tanzania.
Naomba Mungu Amjalie Kagame ujasili wa kuichakaza Tanzania.
 
Tz tumegawanyika sana kwa sasa, kukitoa watu wa nje wanaoweza kutumia hiyo opportunity vizuri lazima tusumbuliwe sana.
Wewe pata picha watu ndugu zao walipotezwa na hawajawahi patikana, wengine wameonewa, wengine Magu akiwazingua mpaja wakafa, tena kuna kakikundi ka watu wachache pamoja na familia zao ndo wanaonekana wanafaidi mema ya hii nchi - kikundi cha WANA CCM wachache- ndo maana ubaona kila watu wanaunga juhudi...etc..Kuna kundi la watu wengi maskini ambayo hawana starting point...
The nation is divided- adui ni rahisi kuingia.
Watu wanalilia katiba mpya - serikali na CCM wanaweka pamba maskioni, wanasahau kwamba wao wenyewe waliianza anza mchakato wa katiba mpya, kupitia bunge la katiba lilijifia kifo cha mende.
 
Lete ushahidi kama ACT ni tawi la CCM!?
Nimeshampa hoja,kama unataka kujadili hoja njoo kiheshima na kwa kutoa hoja,ukija kijinga utajibiwa kwa namna uliyokuja.
Zitto baada ya kutoka chadema alitaka kujiunga na CCM, kwa maelezo yake mwenyewe Zitto alisema Kikwete na marehemu filikunjombe ndio walimshauri asijiunge na ccm, badala yake ndio akaanzishwa ACT
 
Yuko sahihi. Nchi kama Tanzania tumewekeza kwenye chama na kuona Wana CCM ndio wazalendo. Kwahiyo ikitokea vita na Rwanda hasa wakitumia utaratibu uliotimika na Israel kuipiga Iran ni siku mbili Tanzania inaweza pigwa.

Haya ni maoni yangu tumethamini sana chama kuliko taifa. Ule utaifa uliokuwepo sasa hakuna maana Kuna watu kupitia CCM wanafaidi na familia zao na watu wao wa karibu.
Kwahiyo watauza code?
 
Huyo ashazoeleka kuropoka tangu enzi za JAKAYA.
Ila nadhani anajua mziki wa Tanzania ukoje.
Mziki wa Tanzania kwa kigezo gani sasa
Watu wengi ambao ni mazwazwa wakisikia taarifa fulani kubwa kuhusu Rwanda huwa wanaishusha thamani kwa kigezo cha square meter za eneo la nchi yao
Bila kuangalia wanyarwanda ni nani hasa
tukisema wanyarwanda tunamaana image yao imebebwa na kiongozi wao wa nchi
Miongoni mwa watu wachache sana smart sana aliyepata kuishi ukanda huu
Na jeshi lake ndiyo msingi mkuu wa taifa lake analitegea jeshi kuliko kitu chochote unachoweza kukifikiria

Sasa jiangalie wewe upo kwenye level gani kujifananisha na huyo mtu
 
Hiyo mikwara tu mkuu,kwa anayemjua huyo hapati shida.
Kipindi cha Jakaya alipiga mikwara sana aisee,JAKAYA akampiga mkwara wa askari wa mpakani kwa paredi akaufyata.
Mtu si jiwe unajua huu msemo?

Sasa mwenzenu yuko sambamba na teknolojia yuko mbele hatua kumi kutoka wakati huo nyie mmerudi nyuma hatua kumi
Na hata mawazo yenu yamestaki kulekule kwa enzi za jakaya
 
Una uhakika gani kama raia wa Tanzania hawatosimama kutetea taifa lao?
Juzi tu hapo, tumetoka kwenye mashambulizi makali ya Wakenya dhidi ya Rais na Bunge.

Umeona Mtanzania yoyote anawatetea watawala au kuwapambania??

Au unadhani watu hawaoni??


Na unadhani ukiwapa waTZ hao hizo silaha wakapigane wataenda kupambanana siyo ku-SURRENDER??
 
Tukiamua Leo kupigana na Rwanda tunaua tu Budget ya Tamisemi ambayo ni 11 trillion ndio Budget nzima ya nchi ya Rwanda.
Wizara moja tu inabeba Budget ya Nchi nzima
Rwanda is overated
Kagame huyo hata hakuna Wakumjibu Ni kichaaa wacha aongee tu
Vita haijawahi kuwa rahisi hivyo, unaijua budget ya Russia ukubwa wake kulinganisha na Ukraine?? Je imekua rahisi kwa Russia kushinda?
 
Huyu huwa sijui anataka kupima east Africa aone nani ana ubavu, jamaa anaonesha akiendelea ataanza kumega maeneo ya majirani zake akipata nguvu ya jeshi
 
Lini TPDF imepigana vita ikashindwa ndio ukapata conclusion!!?

Kule kongo walienda kulinda amani sio kupigana na waasi!!

Utapigana bila kupewa command ya kupigana!!?

Wale uliowaona walikua wametumwa kulinda amani na sio kupigana na waasi!!

Amani tulio nayo tunadhani ninudhaifu,laiti tungejua kazi inayofanywa na tpdf hapa nchini Wala tusinge beza amani yetu!!

"KAZI na utu tunasonga mbele"

ini
Huu mfano sio relevant, kwa kuwa tuliwahi kushinda vita huko nyuma tafsiri yake tutashinda vita yoyote iliyo mbele yetu? Unamaanisha hata leo hii Egypt au South Africa au hata Iran wakipigana vita na sisi basi tutashinda tu sababu huko zamani hatukuwahi kushindawa?
 
Kwa taarifa yako ni kwamba hapa afrika mashariki hakuna watu wanaolipenda taifa lao na wana uzalendo wa hali ya juu kama wanyarwanda, mnyarwanda tu akizaliwa na kukulia hapa tanzania anakuwa na mahaba kupitiliza kwa Rwanda, sembuse yule aliyezaliwa na kukulia kigali.

Wanyarwanda wanaweza kuwa wametafunwa na ukabila, ila linapokuja suala la kitaifa wanakuwa wamoja,.

Hali hiyo ni tofauti kabisa na nyie wabongo ambao uzalendo mmeshauua siku nyingi sana na ndio maana mada za kuliombea mabaya taifa kama hii zimeshamiri sana.
Usiseme wanyarwanda sema watutsi we kabila moja linahodhi kila kitu halafu useme eti nchi hiyo ina uzalendo. Uzalendo upo ila wa kikabila
 
Mtu si jiwe unajua huu msemo?

Sasa mwenzenu yuko sambamba na teknolojia yuko mbele hatua kumi kutoka wakati huo nyie mmerudi nyuma hatua kumi
Na hata mawazo yenu yamestaki kulekule kwa enzi za jakaya
Muda ni mwalimu mzuri kaka,muda utasema.
 
Huyu huwa sijui anataka kupima east Africa aone nani ana ubavu, jamaa anaonesha akiendelea ataanza kumega maeneo ya majirani zake akipata nguvu ya jeshi
Ameshaanza Congo,Uganda tayari,Burundi tayari naona bado Tanzania tu.
 
Mziki wa Tanzania kwa kigezo gani sasa
Watu wengi ambao ni mazwazwa wakisikia taarifa fulani kubwa kuhusu Rwanda huwa wanaishusha thamani kwa kigezo cha square meter za eneo la nchi yao
Bila kuangalia wanyarwanda ni nani hasa
tukisema wanyarwanda tunamaana image yao imebebwa na kiongozi wao wa nchi
Miongoni mwa watu wachache sana smart sana aliyepata kuishi ukanda huu
Na jeshi lake ndiyo msingi mkuu wa taifa lake analitegea jeshi kuliko kitu chochote unachoweza kukifikiria

Sasa jiangalie wewe upo kwenye level gani kujifananisha na huyo mtu
Kagame hana smartness yeyote,ni dikteta tu ambaye anajificha kwenye uongozi hadi sasa.
Rwanda tukianzia kwa social development haina maendeleo YEYOTE, madaktari wao wanakuja kujifunza Tanzania hapa MUHIMBILI mloganzila na KCMC huko.
Hata wagonjwa wao wengi wa maradhi ya mifupa na moyo India yao ni Tanzania.
Ukienda katika aspects zingine hakuna maendeleo YEYOTE Rwanda,hiyo smartness iko wapi?
Na mind you Rwanda ni nchi ya kitutsi huku wahutu wakiwa wanapuuzwa.
Kama hawatakaa vizuri vita za wenyewe kwa wenyewe hazitachelea kuanza upya.
Kiongozi smart anagombana na majirani zake!?
Burundi ana ugomvi nao,siku akilianzisha tu nchi ya kwanza kuungana nayo kumdhibiti ni Burundi.
Unajiita kiongozi smart na geopolitically uko vibaya!?
 
Kwan ww sio mtusi na mjinga mwenye asili ya Rwanda??
Mimi na watusi wapi na wapi na ningekuwa mtus niogope nini siningesema tu. We endelea kujidanganya kama JWTZ wanauwezo ule wazamani, ni sawa sawa na wewe ujifananishe nguvu zako zakiume na zangu. Si vizee hatujula chips na kuku wanao totolewa na machine. Sisi vyakula vyetu ni nyama fresh, kuku wa kienyeji na mboga za majani. Sio nyie mnakula vyakula vinaitwa genetically modified food
 
Back
Top Bottom