Raia wa Zanzibar wapigwe marufuku kupiga kura ya kumchagua Rais wa Tanganyika

Acha kuchekesha mkuu!

Zanzibar siyo nchi wakati ina raia wake, Bunge lake na mawaziri wake?

Zanzibar siyo nchi wakati ina wimbo wake wa Taifa?

Zanzibar siyo nchi wakati ina bendera yake?

Zanzibar siyo nchi wakati hata plate namba za magari ya huko ni tofauti na ya magari ya Tanganyika?

Zanzibar siyo nchi Mtanganyika hawezi kuvusha mzigo bila kutozwa Kodi "mpakani"?

Zanzibar siyo nchi wakati Mtanganyika hawezi kuendesha gari huko bila kibali maalum?

Zanzibar siyo nchi wakati Sheria zozote zitakazotungwa Tanganyika hazina mamlaka Zanzibar mpaka zitakaporidhiwa na Bunge la Zanzibar?

Zanzibar siyo nchi? How?

Wewe unaijua Zanzibar kuwazidi Wazanzibar ambao kote waendako wamekuwa wakijitambilisha kuwa nchi yao ni Zanzibar?
Mtu ukiwa hujui kitu fulani, ni mjinga!, mtu kuwa mjinga sio kosa, kwasababu kutokujua kitu fulani sio kosa, ukiisha julishwa, ujinga unakutoka unakuwa mwerevu.

Ili nchi kuwa taifa, sio eneo, sio rais, sio bendera, sio wimbo wa taifa, nchi kuwa taifa ni kitu kinachoitwa sovereignty, dola!, Zanzibar haina sovereignty, sio dola!. Tanzania ni nchi moja ya JMT, ndio yenye sovereignty, yenye dola, yenye vyombo vya dola, yenye sarafu, Zanzibar ni jina tuu, la nchi lakini sio nchi, na rais wa Zanzibar ni rais jina tuu wa sehemu inayoitwa Zanzibar lakini kimataifa sio rais, rais ni mmoja tuu, rais wa JMT na nchi ni moja tuu, JMT, Zanzibar sio nchi ni sehemu ya JMT!.
P
 
Umeongea vizuri sn, ni mjinga pekee anaweza kusema Zanzibar siyo nchi na wakati ina kila kitu chake, kwanza muungano uvunjwe haraka
Kuwa na kila kitu chake hakuifanyi kuwa nchi, kitu pekee kinachoifanya nchi kuwa nchi ni kitu kinachoitwa sovereignty!, Zanzibar haina sovereignty, hivyo sio nchi!.
Hata uwe na kila kitu, kama hauna sovereignty, you are nothing!.
P
 
CCM tunaomba mtuambie Zanzibar inachangia kiasi Gani katika maendeleo ya Tanganyika au ndo ivyo tunawalea wazanzibar.
HAKUNA..
Tanganyika pekee ndo inasaidia maendeleo ya Zanzibar kwa hali na mali.

Hata mikopo kwa ajili ya Zanzibar Tanganyika ndo mkopaji, na Tanganyika pekee ndo mlipaji wa hiyo mikopo
 
Kama ni kweli zimeungana Tanganyika na Zanzibar na ni kweli Tanganyika imekufa Zanzibar inakuwaje hai? Nyerere ni Genius lengo lilikuwa kuelekea nchi moja muda haukutosha sasa ndo mana zimeungana Tanga nyika na Zanzibar na Bado tuna Tanzania na zanzibar
Sasa alishindwa nini wakati Jeshi la Tanganyika lilishiriki kumweka Karume madarakani?

Kama alikuwa na nia hiyo na hakuiteleza ni uzembe. Zanzibar haikuwa kitu cha kumshinda.

Mbona alimwondia Jumbe madarakani, tena kirahisi tu?

Mbona alimficha Jumbe Kigamboni na hakuna Mzanzibar aliyefungua mdomo hata baada ya Nyerere kuondoka madarakani?
 
Kuwa na kila kitu chake hakuifanyi kuwa nchi, kitu pekee kinachoifanya nchi kuwa nchi ni kitu kinachoitwa sovereignty!,
Ndiyo sababu tunataka serikali tatu, ili Tanganyika nayo iwe na kila kitu chake kama Zanzibar, ili kuweza kutetea na kulinda rasilimali zake, siyo zinachumwa tu kama hazina mwenyewe.

Kama hamtaki serikali tatu, ni bora kuvunja huo muungano wa kinyonyaji
 
Mtu ukiwa hujui kitu fulani, ni mjinga!, mtu kuwa mjinga sio kosa, kwasababu kutokujua kitu fulani sio kosa, ukiisha julishwa, ujinga unakutoka unakuwa mwerevu.

Ili nchi kuwa taifa, sio eneo, sio rais, sio bendera, sio wimbo wa taifa, nchi kuwa taifa ni kitu kinachoitwa sovereignty, dola!, Zanzibar haina sovereignty, sio dola!. Tanzania ni nchi moja ya JMT, ndio yenye sovereignty, yenye dola, yenye vyombo vya dola, yenye sarafu, Zanzibar ni jina tuu, la nchi lakini sio nchi, na rais wa Zanzibar ni rais jina tuu wa sehemu inayoitwa Zanzibar lakini kimataifa sio rais, rais ni mmoja tuu, rais wa JMT na nchi ni moja tuu, JMT, Zanzibar sio nchi ni sehemu ya JMT!.
P
Kwahiyo Uncle unataka kusema Zanzibar kimataifa inatambulika kama ilivyo mkoa tu wa Morogoro?

Sent from my SM-A107M using JamiiForums mobile app
 
Nawapongeza Zanzibar kwa kuwa na msimamo, huwezi kupiga kura ya kumchagua rais wa Zanzibar ikiwa wewe si mzanzibari.

Cha ajabu serikali ya Tanganyika inaingiliwa na Zanzibar, yaani raia wa nchi jirani (Zanzibar) wanapiga kura kuchagua Rais wa Tanganyika.

Jambo hilo lingekuwa na mantiki endapo nasisi Watanganyika tungeruhusiwa kushiriki kuwachagulia Rais watu wa Zanzibar. Kwakuwa hatuwaingilii kwenye uchaguzi wao, na wao wazuiliwe maramoja kutuchagulia Rais.
Una hoja aisee .......sema huu muungano ni wa ajabu sana.
 
Naendelea kusisitiza mtu ukiwa hujui kitu ni mjinga!, kuwa mjinga sio kosa, dawa yake ni kuelimishwa. Vatican ni nchi, a City State yenye sovereignty. Zanzibar haina sovereignty hivyo sio nchi!.
P
Lete definition(english na swahili) ya hapa acha kujificha hapa(Sovereignty refers to the supreme authority and power that a state or a political entity possesses to govern itself and make decisions within its own territory without interference from external sources.) Mkuu hapo Zanzibar inakosa kitu gani? acha kudanganya watu
 
Nawapongeza Zanzibar kwa kuwa na msimamo, huwezi kupiga kura ya kumchagua rais wa Zanzibar ikiwa wewe si mzanzibari.

Cha ajabu serikali ya Tanganyika inaingiliwa na Zanzibar, yaani raia wa nchi jirani (Zanzibar) wanapiga kura kuchagua Rais wa Tanganyika.

Jambo hilo lingekuwa na mantiki endapo nasisi Watanganyika tungeruhusiwa kushiriki kuwachagulia Rais watu wa Zanzibar. Kwakuwa hatuwaingilii kwenye uchaguzi wao, na wao wazuiliwe maramoja kutuchagulia Rais.
concept of huu muungano is not clear, wananchi hawajui tumeunganaje unganaje? wa upande huu wanapewa full access kwenye shughuli zote yaani kumiliki ardhi, kugombea uongozi,ajira etc LAKINI kulee, ng'ambo kule mtanganyika harusiwi miliki ardhi, kuchagua au kuchaguliwa nafasi za uongozi na utawala, mambo mengi mno? sijui nini hiki, ulipaswa tuwe na serikali 3, Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar kisha Tuwe na serikali ya Shirikisho au la TUWE na serikali moja ambayo Serikali ya Jamhuri ya Tanzania(kusiwe na serikali ndani ya serikali)
 
Back
Top Bottom