Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Butola ndugu yangu, kinachopiganiwa sio posho ya wabunge pekee,hapo ni pakuanzia tuu. Posho za vikao zitolewazo kwa watumishi wa serikali na mashirika ya umma kwa mwaka ukipata idadi yake utashtuka. Huijui CCM na watu wake wasivyo na haya? Wabunge wa CHADEMA wakisusa wao bila aibu watakuambia ok na mfumo utabaki hivyohivyo. Hauta gusa sekta nyingine na hizo fedha za posho ya Wachadema haziwezi kuleta mabadiliko yeyote.

Upo sahihi mkuu lakini bado haitoshi kwa CDM kuongea tu ilhali wanajua hoja yao haitapita, wanachopaswa kufanya ni kwenda hatua moja mbele na kuzipinga posho hizo kwa vitendo, kukataliwa kwa hoja na kisha wao kuendelea kupokea hizo posho kutauonyesha umma tofauti gani kati yao na wale wanaofurahia malipo yasiyo sawa?

Suala ni kuwa ili kuonyesha userious wao na kwa ajili ya kuuonyesha umma jinsi CDM ilivyo serious kujinyima kwa ajili ya kulinda maslahi ya umma, wabunge wao watapaswa wao sasa waanze kuonyesha mfano kwa kuzikataa posho hizi, na kitendo hiki kitaonyesha tofauti ya dhahiri kabisa kati ya wanaoumizwa na mgawanyo dhalimu wa keki ya taifa na wale ambao maslahi yao binafsi ni muhimu zaidi, kati ya walio kwa ajili ya wananchi na wale walio kwa ajili ya matumbo yao, hii ya kuongeaongea tu bila vitendo haitoshi, tunataka vitendo sasa.
 
Nafikiri wewe ni mmoja wa watu ambao hudandia mada bila ya kuzisoma kisawasawa. Alichosema Mhe Zitto ktk bajeti ya kambi ya upinzani ni kuwa wabunge hulipwa posho za aina mbili kwa siku, ya kwanza inayitwa Sitting Allowance ya SHS 80,000/= kwa ajili ya kukaa katika vikao vya bunge; na ya pili ni posho ya kujikimu kwa lugha ya kigeni huitwa "Subsistence Allowance" ya Shs 70,000/= kwa ajili ya chakula, malazi n.k kwa kuwa viako vya bunge hufanyika nje ya vituo vyao vya kazi kwa maana ya maimbo yao ya uchaguzi. Ndipo akahoji uhalali wa mbunge kulipwa posho ya kukaa katika vaikao vya bunge ilihali kazi aliyoomba ni kuwawakilisha wananchi katika bunge na tayari analipwa mshahara kwa kazi hiyo hiyo.

Hivyo bajeti ya upinzani inapendekeza posho ya kujikumu iendelee na posho ya kukaa katika vikao vya bunge iondolewe. Vivyo hivyo kwa kwa watumishi wa serikalini hususan wakubwa wakikaa katika vikao mwisho hupitishwa bahasha zenye posho ilihali waliomba wenyewe kazi za kutumia akili katika vikao ndio maana hawafanyi kazi za shuruba kama vile kilimo, vibarua n.k. Kiutendo cha watumishi wa serikali tena wa kada ya juu tu, kulipwa posho ya kutimiza wajibu wao ambao tayari wanalipwa mishahara kuutimiza ni ufujaji mkubwa wa fedha za walipa kodi. Ndio maana vikao serikalini haviishi. Kinachotokea wanapanga vikao kufanyika katika mikoa nje ya vituo vya kazi na kupata posho mbili kama wabunge yaani posho ya vikao na posho ya kujikimu.

Je hiyo ndio siasa kwako?

You have analysed clearly! good idea.
 
We must walk the talk. I have written to the Clerk of Bunge that all sitting allowances I am entittled to should be directed to a charity in my constituency up to when the law is changed and sitting allowances scrapped.
I will advise my fellow CHADEMA MPs to take similar measure.

I salute you..

Huu ni wakati sasa wa kuuonyesha umma wale waliopo bungeni kwa ajili ya maslahi yao binafsi na wale waliopo bungeni kwa ajili ya maslahi ya umma, big up Zitto...
 
mpuuzi mkubwa huyu Ndugai
anatumia makalio kuanalyse

Hapa wapinzani wanataka mfumo urekebishwe ili kujaribu kuleta usawa na si kugomea posho.

Wapinzani wanazungumzia MFUMO kugomea posho/mishahara hakutasaidia chochote.

Hakuna mbunge hata mmoja wa CDM anataka posho ipunguzwe, wote wako pale kwa maslahi yao na si ya wananchi, hizo ni daganya toto tu za kisiasa mkuu
 
Kama wanamagamba including Ndugai wameona hoja ya Mh. Zitto kwamba kupokea posho mbili i.e.subsistance allowance na sitting allowance at the same time ni wizi na ufujaji wa pesa zetu (walipa kodi). Kwanini wasifute hiyo posho moja ya sitting allowance kuliko kuja na hizi lame excuse kwamba wabunge wa CDM waandike barua ya kuzikataa?

Kwani wakizikataa wabunge CDM ndiyo zitalekezwa kwenye miradi ya maendeleao?!. Si zitabaki hapo kwenye ofisi ya bunge because ni budget ya bunge. CDM wanapinga huu MFUMO wa kinyonyaji sio tu kwa wabunge hata viongozi wengine wakuu wa serikali.

Yaani mimi nikisoma hizo hoja za wana-Magamba ninatamani kupasuka kwa hasira. Watanzania wengekuwa kama mimi sidhani kama mbunge hata mmoja wa CCM angerudi bungeni mwaka 2015.

Watu wakijiunga na CCM sijui akili zao zinakuwa je? nachelea kumfananisha Ndugai na MBUNI, na anajua tabia za mbuni maana, Ndugai amesoma wildlife management pale UD miaka hiyo ya matusi ya nguoni ya Mzee Rukhusa

Acha kuwa na wivu wa kike wewe, njoo kwangu na wewe unifanyie kazi ntakupa posho zote mbili tuone kama utakataa
 
kusususia sio suluhisho kwa sasa, wao wametoa pendekezo badala ya kuwapongeza japo kwa pendekezo zuri nyie mnawalaumu

Mkuu Masuke.

Nadhani Zitto amemaliza hapa...., tunahitaji wanasiasa wanaoyatenda yale wanayoyahubiri, muda wa longolongo za kisiasa umekwisha.

We must walk the talk. I have written to the Clerk of Bunge that all sitting allowances I am entittled to should be directed to a charity in my constituency up to when the law is changed and sitting allowances scrapped.
I will advise my fellow CHADEMA MPs to take similar measure.
 
Wabunge wa CHADEMA sio kuwa wao hawazitaki hizo posho, hapo ndio watu mnaposhindwa kuwaelewa. Hakuna asiye taka pesa. Ila wao wanapigania mfumo mpya utakao ondoa hizo sitting allowance ili fedha hizo ziweze kufanya majukumu mengine ya manufaa.
Ukiliangalia hili kwa pupa utaona ni jambo la mzaha,ila kama Bunge litajiondolea posho za aina hiyo ina maana hakuna idara au wizara ambayo fedha za aina hiyo zitapitishwa na Bunge tena. Tutaokoa ngapi kama taifa? NYINGI. Kususia sio ufumbuzi wa tatizo
serikali yetu yaajabu kweli mishahara mikubwa na posho kubwa huku wenyeviti wa vitongoji hawalipwi mshahara hata shilingi wakati kimsingi ndiyo wenye jukumu kubwa na madiwa nao wana lamba mshahara wa 120,000, halafu tuna sema tutatokomeza rushwa kweli...!?
 
We must walk the talk. I have written to the Clerk of Bunge that all sitting allowances I am entittled to should be directed to a charity in my constituency up to when the law is changed and sitting allowances scrapped.
I will advise my fellow CHADEMA MPs to take similar measure.
Ndugu yangu Zitto, kwanza nakupongeza kwa uamuzi wako wa mfano bora kwa kiongozi. Ila usiishie/msiishie hapo tu maana CCM hawana mshipa wa aibu hata kidogo. Mlipigie kelele ili sitting allowance za wabunge zifutwe ili huku kwenye Idara za serikali na mashirika muweze kutoa amri tuu ya kuzifuta. Likitimia hilo mtakuwa mashujaa wa ukweli. Big up comred
 
Mkuu Butola wewe ni mpiganaji ambaye nilikuwa nakuamini sana imekuwaje tena unakuwa mtu wa kuunga mkono posho mbilimbili za hawa waheshimiwa, hata kama watakataa lakini wananchi wengi wakiwa against nao lazima wajue wanachokifanya sio kizuri, na kama mfumo haubadilishwi siungi mkono chadema kuziacha hizo posho kwa nini waziache wakati mfumo haueleweki bado,

yoote hayo hamyaoni nyie mnataka chadema tu waache posho kwa nini msitake wabunge wote waache hizo posho na ziingie kwenye matumizi mazuri ya maendeleo ya nchi hii.

Mkuu Masuke, kimsingi napinga hii dhana ya kulipwa mara mbili kazi moja, tupo pamoja sana kwenye hili.

NINACHOPINGA ni tabia ya wanasiasa wetu kuyahubiri yale wasiyoweza kuyatenda, nawafahamu Wabunge wengi wa CDM wanazipenda hizi posho na hawataki zifutwe ila kwa ajili tu ya kutafuta cheap popularity watatamka vinywani mwao kuwa zifutwe lakini nyuma wanaziunga mkono sana na kujifariji kuwa ata wakiongea hazitafutwa.

Walio wa kweli wajipambanue sasa tuwahesabu, walio na uchungu wa kweli wauonyeshe sasa umma namna wanavyokerwa na hili kwa vitendo, hii itatusaidia kuwatambua wanasiasa wanaoumizwa kweli na uozo huu na wenye dhamira za dhati ya kubadillisha taratibu hizi zmbovu na kuweka mgawanyo sawa wa rasilimali za taifa hili, watajionyesha tu kwa kulipinga hili kwa vitendo.

Wahenga walisema matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno, Mh. Zitto ameonyesha mfano kwa vitendo na kuonyesha namna alivyo serious katika hili, Wabunge wengine nao wasimame wahesabiwe.....
 
HEKO comrade Zitto! Ni uamuzi unaopaswa kuungwa mkono na yeyote mwenye mapenzi mema.
Lakini juu ya ushauri wako kwa wabunge wengine wa CDM ningependa kuongeza haya machache.

  1. Waangalie namna nyingine pia za kugawana hizo posho zao na wananchi na si lazima wote wa-focus kwenye charity works majimboni mwao. Nasema hivi kwa kuzingatia nature ya wabunge wa CDM kwamba kwa sehemu kubwa wamelazimika kuwa wabunge wa taifa badala ya majimbo tu. Simuoni mh Lema,mathalani, kama mbunge wa Arusha tu; au Tundu Lissu kama wa Singinda peke yake au Zitto kama ni wa Kigoma kaskazini tu. Hawa wanashiriki na watashiriki katika harakati nyingi nchi nzima na sina uhakika kama wanalipwa au walau wanalipwa na nani wakifanya harakati hizo. Ni nature tofauti kabisa na wabunge wa CCM. Na hata CDM ni tofauti sana na CCM kwa uwezo wa taasisi zao za kifedha. Sababu zinafahamika.
  2. Ifahamike pia kwamba charity inaweza kutolewa kwa siri, wakafahamu tu wale unaowatolea na si lazima sana vyombo vya habari vikawa mashahidi wa charity works. Ukiwepo ulazima wa kutangaza kile ambacho wabunge hawa watatoa au wanatoa mpaka sasa,kama charity basi wafanye hivyo.
  3. Hili jingine ninajaribu tu kufikiria mwenyewe:
Manji akatoa Tsh 100m. kuwanunulia tiketi mashabiki wa soka;Rostam akajitolea kuwalipa posho wajumbe wa mikutano ya chama; mzee ndesamburo na Mbowe wanatumia mali zao kwa ajili ya CDM; Nimrod Mkono anjenga mashule kibao huko jimboni kwake; Mengi anafanya charity works ked kede; Sabodo naye vivyo hivyo....n.k Hivi hii ni homogenous list kweli au nimekosea nikaorodhesha bata,kuku,njiwa, kipepeo, farasi......pamoja?
Lakini mwisho wa yote NAAMINI kwamba prudence katika hili ni kupigania kubadili muundo wa utoaji wa hizo posho za kiwendawazimu,na si kuamua kuziacha. Nyerere alisoma shule kwa ile privilege yake ya kuwa mtoto wa chifu. Alivyofika kwenye power akafutilia mbali priviledges za kichifu chifu na mpaka akina sie tukaweza kusoma Tabora boys.

Ni mtazamo tuu:confused2:
 
BAADA YA WAZIRI KIVULI WA FEDHA MH. ZITO(CDM) KUTANGAZA VIPAOMBELE VYA BAJETI YA UPINZANI NA KUPENDEKEZA KUPUNGUZWA KWA POSHO ZA SEMINA KWA VIONGOZI WA SERIKALI WAKIWEMO WABUNGE, IMEPOKELEWA TOFAUTI NA WABUNGE WA CCM HUKU WENGI WAO WAKIDAI KUWA POSHO ZAO HAZITOSHI.

JOBU NDUGAI, CHILIGATI NA WENGINE WENGI KUTOKA CCM WAMECHARUKA VIKALI KUPINGA KUPUNGUZWA KWA POSHO ZAO. LEO ASUBUHI KTK KIPINDI CHA JAMBO(TBC) MH. NDUGAI AMBAYE NI NAIBU SPIKA ALIKANA KABISA SWALA HILO NA KUSEMA KUWA CDM WAMEPOTOSHA.

SWALI:

Je, kuna ulazima gani wa mbunge kulipwa mara mbili kwa kazi hiyo hiyo moja? mimi nadhani posho wanazopewa kwa siku sh.(1750000) zinatosha kuendesha hata shughuli nyingine wanazofanya ikiwemo semina na kamati. vp kuhusu waalimu, madaktari, maafisa kilimo na wananchi wengine?
 
Sasa kama wameshapewa per diem zao ni busara kwa wapiga kelele kwenye majukwaa wakaandika barua ya kusudio la kuondolewa hizo posho bila ya hivyo itakuwa ni unafiki tu.

Sijafikia hatua ya kuamini kwamba wewe ni mdini lakini wakati mwingine hoja zako zinanivuta kuelekea huko.

Hawa watu wanaokula na kulala na hoja za ubaguzi wa kidini ama kabila ama rangi ni wa kupuuzwa, sasa mtu makini kama wewe hustahili kujiunga nao.

Sidhani kwamba umeishiwa hoja za kushusha hapa jf hadi kushadidia hoja za kipuuzi zisizokuwa na tija kwa taifa letu.
 
Mbunge ni mwakilishi wa jimbo kwa niaba ya wananchi kwa mujibu wa Katiba ya sasa ya TZ, Mimi napinga uchukuaji wa hiyo posho kwakuwa wan mishahara na allowances walizojipangia kwa kanuni zao bila kufuata mwongozo na kanuni za serikali. Tumeambiwa wamekopeshwa Sh 90m kila Mb toka Serikalini na marejesho yake ni nusu yake tu kwa kipindi cha miaka mitano na hakuna riba, pia wakitaka kukopa kwenye banki yeyote TZ wanaweza kupata mkopo max to 200m kwa udhamini waOfisi ya Bunge, sasa wana JF embu tuijadili hii mada! Mfano Nigeria Spika anayemaliza muda wake yupo ndani kwa kukopa USD 60m kwa udhamini wa Ofisi yao ya Bunge, sijui huku kwetu wamekopa kiasi gani kutoka banks kwa kivuli cha Ofisi ya Bunge! Tuijadili
 
Wabunge wapo pale kutetea masilahi ya wapiga kura wao. Kama wanaona kuwa hawawezi kuhudumia wapiga kura bila posho basi waachie ngazi. Wabunge wanaonyesha their true colours .(wapo mjengoni kwa ajili ya posho na siyo kuwakilisha wananchi).
Ingekuwa vizuri ikapatikana takwimu za wale ambao hawataki kukatwa posho. Nape amesema ili linazungumzika.
 
natamani kuwa dereva wa mbunge, 30,000..... kwa siku?
 
ANAKULA 40,000/= KWA SIKU DU??HUYU MUISLAM NI SOO,HII SI NI BEI YA MBUZI MKUBWA BEBERU NA KRET MBILI ZA KILIMANJARO,NA MAJI KATON MOJA KWELI JAMAA YUKO JUU

ANAMPA DEREVA WAKE 30,000/= PER DAY MAANA YAKE JAMAA ANATENGENEZA

30,000 X 30=900,000/=
SASA BUNGE HILI N LA MIEZI MITATU
900,000 X 3=2,700,000/=
MSHAHARA WA DEREVA SH 900,000/= KWA MWEZI HAIWEZEKANI

SI KWELI HUYU MPEMBA ANADANGANYA UMMA

mnafki tuu hana lolote

huyu jamaa haoni uchungu na pesa ya bara. Hivi dereva anapata pesa nyingi kuliko mwl wa Msingi
 
M nafikiri ni wakati mzuri kwa wabunge wa UPINZANI wa kweli kuuthibitishia uma kwamba wapo pamoja nao kwa kuzikataa hizo posho kwa nguvu nzote. Asilimia 99 ya wananchi wote wanaunga mkono hoja hiyo isije ikawa walikuwa wanatafuta umaarufu bila kujitoa mhanga. Kwa mfano idadi ya wabunge wote wa upinzani au watakaokubaliana na hoja hiyo hela zao zikajumulishwa na kufanya kitu cha maana kama kujenga vyoo au kununua madawati tutaona wamefanya la maaana sana ili hata watakapokuwa wankuja kwetu kututambishia waseme tuliokoa kiasi fulani cha hela zikafanya kazi fulani:smiling: Cha kushangaza unaweza kuona hoja hiyo imeishia mdomoni mwa Zitto.
 
Hilo bunge la Tz
wabunge kimaslahi zaidi,10% ndio kinachowaingiza bungeni ingawaje sio wote lakini asilimia kubwa ya wabunge wapo kipesa zaidi,kama mtu analazimisha kupewa posho eti ili aitumie kuwahonga wananchi kuna nini tena hapo? hakuna kitu maslahi binafsi mbele ya taifa nyuma

hivi sisi tunasonga mbele? ama tunarudi nyuma?
 
Its time for action, Mh Waziri Zitto umetoa hoja, kama wabunge hawataki waacheni, lakini kama hili liko ndani ya uwezo wenu CDM litekelezeni ili ukweli wake uonekane.
 
[IMG said:
https://www.jamiiforums.com/template/JamiV1/default/misc/quote_icon.png[/IMG] Originally Posted by Zitto
We must walk the talk. I have written to the Clerk of Bunge that all sitting allowances I am entittled to should be directed to a charity in my constituency up to when the law is changed and sitting allowances scrapped.
I will advise my fellow CHADEMA MPs to take similar measure.
Cheap and populist poitics.
We need to push for the overall public policy as far as the issue of allowances is concerned. Populism won't do anything neither can it help much, dear Zitto.:majani7:
 
Back
Top Bottom