Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Hamad hana jipya ndio maana CUF wamemsogeza pembeni apeleke siasa zake za udini hukooooo pemba
 
Ila katika hali ya kawaida, inawezekana kweli kwa mbunge au mfanyakazi yeyote wa serikali au wa makampuni binafsi kutoka nje ya kituo chake cha kazi for official duties bila ya kulipwa posho??? Kuwa muwazi weka siasa kando

Nafikiri wewe ni mmoja wa watu ambao hudandia mada bila ya kuzisoma kisawasawa. Alichosema Mhe Zitto ktk bajeti ya kambi ya upinzani ni kuwa wabunge hulipwa posho za aina mbili kwa siku, ya kwanza inayitwa Sitting Allowance ya SHS 80,000/= kwa ajili ya kukaa katika vikao vya bunge; na ya pili ni posho ya kujikimu kwa lugha ya kigeni huitwa "Subsistence Allowance" ya Shs 70,000/= kwa ajili ya chakula, malazi n.k kwa kuwa viako vya bunge hufanyika nje ya vituo vyao vya kazi kwa maana ya maimbo yao ya uchaguzi. Ndipo akahoji uhalali wa mbunge kulipwa posho ya kukaa katika vaikao vya bunge ilihali kazi aliyoomba ni kuwawakilisha wananchi katika bunge na tayari analipwa mshahara kwa kazi hiyo hiyo.

Hivyo bajeti ya upinzani inapendekeza posho ya kujikumu iendelee na posho ya kukaa katika vikao vya bunge iondolewe. Vivyo hivyo kwa kwa watumishi wa serikalini hususan wakubwa wakikaa katika vikao mwisho hupitishwa bahasha zenye posho ilihali waliomba wenyewe kazi za kutumia akili katika vikao ndio maana hawafanyi kazi za shuruba kama vile kilimo, vibarua n.k. Kiutendo cha watumishi wa serikali tena wa kada ya juu tu, kulipwa posho ya kutimiza wajibu wao ambao tayari wanalipwa mishahara kuutimiza ni ufujaji mkubwa wa fedha za walipa kodi. Ndio maana vikao serikalini haviishi. Kinachotokea wanapanga vikao kufanyika katika mikoa nje ya vituo vya kazi na kupata posho mbili kama wabunge yaani posho ya vikao na posho ya kujikimu.

Je hiyo ndio siasa kwako?
 
Naibu Spika Job Ndugai, amewaambiwa wabunge wa kambi ya upinzani wanaosema posho za wabunge ziondelewe waonyeshe mfano kwa kuiandikia ofisi ya bunge (Spika) kuomba kuondolewa posho zao na wao wataziondoa haraka>

Amesema kitendo cha wabunge hao kuongea kwenye majukwaa ya kisiasa kuhusu kuondolewa kwa posho hizo hakina tija na wanapaswa kuongoza kwa mfano kwa kuandika barua kwa spika ili posho zao zianze kuondolewa kwanza.

Source: TBC 1 asubuhi hii, kipindi cha Jambo Tanzania.

Hakika kazi ipo kupata viongozi wenye uchungu na wananchi.Wachumia tumbo wengi wao wanajua tabu za Watanzania ila hayawaumi.
 
ANAKULA 40,000/= KWA SIKU DU??HUYU MUISLAM NI SOO,HII SI NI BEI YA MBUZI MKUBWA BEBERU NA KRET MBILI ZA KILIMANJARO,NA MAJI KATON MOJA KWELI JAMAA YUKO JUU

ANAMPA DEREVA WAKE 30,000/= PER DAY MAANA YAKE JAMAA ANATENGENEZA

30,000 X 30=900,000/=
SASA BUNGE HILI N LA MIEZI MITATU
900,000 X 3=2,700,000/=
MSHAHARA WA DEREVA SH 900,000/= KWA MWEZI HAIWEZEKANI

SI KWELI HUYU MPEMBA ANADANGANYA UMMA

mnafki tuu hana lolote

Mkuu kula Tshs. 40,000.00 inawezekana. Swali ni kuwa unakula na nani? Kama ana mke zaidi ya mmoja na ameenda nao wote na bado pale Chako ni Chako !!
 
Swali lipo pale pale. Kama wao TShs 80,000 hazitoshi, zianatoshaje kwa wafanyakazi wa nchi hii ambao wanapewa kiwango hicho?
 
kazi ipo mwaka huu yani kwa siku 150000 kwahiyo mbunge mmoja hadi kikao kikiisha atakuwa kashalamba mshahara wa mwalimu wa ngazi ya cheti au constable wa polisi wa miaka takribani mitatu hivi,jamani hii hali ni mbaya kwani hizo millioni 7 hazitoshi kuishi,mbona wafanyakazi wengine wanalipwa 150000 kwa mwezi na ndio mpango mzima.:glasses-nerdy::glasses-nerdy::glasses-nerdy:
 
Okey, Na hiyo posho hapo juu ni sawa??, kwa siku au figa yangu mbovu??

Sekulu:- Huyo dereva wa Mbunge analipwa 30,000/= kwa siku wakati vikao vinapoendelea au muda wote mpaka mheshimiwa atakapotimuliwa au kuangushwa katika uchaguzi???????????????????????
 
Ila katika hali ya kawaida, inawezekana kweli kwa mbunge au mfanyakazi yeyote wa serikali au wa makampuni binafsi kutoka nje ya kituo chake cha kazi for official duties bila ya kulipwa posho??? Kuwa muwazi weka siasa kando

Kwa wafanyakazi wengine ukiachana na wabunge na wakubwa wa serikali, wanaposafiri nje ya vituo vyao vya kazi wanalipwa posho moja tu per diem!

Lakini kwa hawa wabunge pamoja na wakubwa wa serikali wao wanalipwa posho mbili, kwa mfano wabunge wanavuta sitting allowance na subsistance allowance. Kwanini walipwe sitting allowance wakati wanatekeleza majukumu yao yanayowafanya walipwe mishahara??

Ukiweka kando siasa ndipo utaweza kuona hoja ya upinzani, lakini kama unazungumza kwa kutumia akili ya ndugai, basi utabaki unazunguka humo humo.
 
Kimsingi hizi posho zinatakiwa kuangaliwa ktk nyanja zote, kwanzia watumishi wa kawaida wa serikali hadi wabunge, Haina maana mtu kukaa kwenye kikao hapo hapo ofisini(Bila kutoka nje ya Kituo cha kazi) na Ktk muda wa kazi alafu unamlipa pesa!, jamani mambo mengine tuangalie, hizo ni pesa za wananchi!, Wengine utakuta wanaenda pale kibaha, na wanapigwa mahela kisa kibaha ni mkoa mwingine na kila jumapili wanaenda ibadani na kutoa sadaka!. Sidhani kama kuna watu wazalendo,

Kama ikifanyika kama kambi ya upinzani wanavopendekeza na ikaingia mpaka kwenye taasisis zingine, na kukawa kuna sheria kali ambazo zinahusika na watu wanaofuja hela. nina uhakika ndani ya miaka 15 tutakuwa mbali sana!, Tanzania ina pesa nyingi ila watu ni wezi sana jamani, na wizi mwingine umehalalishwa na sheria.

Mwisho ile hela wanazopata wabunge baada ya kumaliza muda wa kuhudumu ziangaliwe upya, naona kuna watu wnakofia mbili za ubunge na uwaziri, nadhani sheria zaingaliwe upya kudhibiti wizi huu!, unaweza kukuta Mtoto Wa mkulima analipwa Pesa ile Mara Mbili ya ubunge na Uwaziri!
 
CCM ni malimbukeni,wanalididimiza taifa kwa ujumla ni wakati mwa kuichukia ccn
 
TBC muda huu Kuna mahojiano,

Mh Ndugai Kaulizwa swali kuhusu kupunguziwa posho zao kashindwa kutoa jibu na msimamo wake

Na Mh. Hamad Rashid wa CUF yeye kasema posho analipwa 150,000 analala hotel shiling 80,000 Anamlipa dereva wake sh 30,000/= na kula elf 40,000/= na kumaliza kwa kusema kuwa haoni kama kuna hela inabaki hapo,

Swali langu ni, Hivi dereva wa mmbunge analipwa na Mbunge??,
Hivi wabunge wanalipwa shilingi ngapi kama posho??, coz hiyo figa nanikumbuka na ni ya kitambo, nikosoeni kama nimekosea, nielimisheni inapowezekana!

Kweli kabisa,anakula elf40 anaona ni poa kabisa,wanafunzi wanasema elf5 haitoshi wabunge
wana washangaa,....wapuuzi kabisa!

Devera analipwa elf30 kwa siku kweli?
so dereva anakula nini?
ana lala wapi kwa hiyo hiyo elf30 kwa siku?

Kweli,PATA HELA TUJUE TABIA YAKO!!!!!
 
Na Mh. Hamad Rashid wa CUF yeye kasema posho analipwa 150,000 analala hotel shiling 80,000 Anamlipa dereva wake sh 30,000/= na kula elf 40,000/= na kumaliza kwa kusema kuwa haoni kama kuna hela inabaki hapo,

Jameni, mbona Mh. Hamad hakutoa mchanganuo wa dereva wake? Posho anayomlipa ni ndogo kulinganisha na pesa anayotumia kwa chakula tu. Yeye anatumia ngapi kwenye kulala, kula na kuitumia familia yake huko kwao? Nadhani viongoz wetu wanadhan wao ndo wana haki ya kupata hivyo wanavyopata.

Hata hivyo, upinzani umetoa mawazo yao tu. Kama wangekuwa wao wanaandaa bajeti kwa ajili ya watanzania wangewafanyia nini. Sasa kuanza kuona mjadala ya kupinga mawazo yao na mapendekezo mimi nashangaa kabisa. Kwa kweli mimi sioni hata maana ya wabunge kulipwa mishahara, kwangu mimi ubunge sio fani ya mtu kujivunia hadi kustahili kupata mshahara. Ndo mana rushwa kwenye uchaguzi zinazidi kuongezeka kwani watu hufuata maslahi badala ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Its good because we now begin to know true colours of our leaders. Hawako tayari kupunguziwa maslahi yao kwa ajili ya kuwaletea wananchi ustawi ambao walijinadi kuwa wataupigania. Kiama chao kinakuja kwani 2015 sio mbali kama wanavyodhani.
 
siku tukipata wabunge wa CCM ambao wapo kwa ajili ya wananchi hoja kama hizi hawatozipuuza, lakini wale wapo kwa ajili ya mitumbo yao ndio maana utayaona hayo. Katika Hili mimi ningeomba media zote zitangaze hoja moja tu ya Posho kuondolewa na hoja ya chiligati abakie nayo mwenyewe na ndugai wake, naamini ikitangazwa kama vile alivotangazwa Babu wa loliondo mpaka wagonjwa wakakimbia mahospitali na kwenda kufia kule loliondo basi tutafanikiwa. Kwa vile jamaa wamejifanya vichwa ngumu ktk hili basi wabunge wa upinzani wote msirudi nyuma litekelezeni hili kwa vitendo halafu media zote ziitangaze sana tena sana kwa wananchi juu ya kinachofanywa na wabunge wa ccm ambao watang'ang'ania kuchukua posho hiyo na wawe wanatajwa majina uone kama hawaachii wenyewe, nakwambia wataanza kusutana kwahili na watakuwa wamejitengenezea picha mbovu sana kwa wapiga kura wao.
 
Swali lipo pale pale. Kama wao TShs 80,000 hazitoshi, zianatoshaje kwa wafanyakazi wa nchi hii ambao wanapewa kiwango hicho?

alafu hiyo 80,000 ndo ambayo watu wa upinzanii wanaipinga coz hiyo ndo sitting allowance sasa!, hawa jamaa ni wabinafsi sana na wakisema wapunguziwe hiyo wanaweza kutuuza!

kazi ipo mwaka huu yani kwa siku 150000 kwahiyo mbunge mmoja hadi kikao kikiisha atakuwa kashalamba mshahara wa mwalimu wa ngazi ya cheti au constable wa polisi wa miaka takribani mitatu hivi,jamani hii hali ni mbaya kwani hizo millioni 7 hazitoshi kuishi,mbona wafanyakazi wengine wanalipwa 150000 kwa mwezi na ndio mpango mzima.:glasses-nerdy::glasses-nerdy::glasses-nerdy:

Kiukweli kuna haja ya kufikiria upya, ukiwaambia tupunguzeni hayo matumizi hawataki, pandisheni kima cha chini cha mshahara hawataki na ndo maana watu wanazidi kujifunza na kuijua Serikali yao zaidi. Haya mambo wao wanaona kama wananchi hawajui wanasiasa wakiongea utasikia mnachochea vurugu!

Sekulu:- Huyo dereva wa Mbunge analipwa 30,000/= kwa siku wakati vikao vinapoendelea au muda wote mpaka mheshimiwa atakapotimuliwa au kuangushwa katika uchaguzi???????????????????????

Gwallo hapo sijaua vizuri kama ni muda wa vikao au lah, ila nadhani ni muda wa vikao na safari za Mh. kutokana na Nature ambayo hizo hela zinapatikana. Sijajua vizuri wakati ambao sio wa vikao inakuaje
 
Nilishasema kuwa Wabunge wa CCM wamejisahau kabisa. Wamejiwekea viwango vyao vya maisha mbai sana na wananchi. Wamesahau kuwa hizo pesa ni za wananchi hazitoki kwenye biashara inayomilikiwa na bunge.

Wakikosa hoja ya kujitetea wanabisha kijinga. Wananchi tunawasikia na tutawawajibisha kwa aibu. Hawajifunzi kwa wabunge wengine waliochezea wapigakura wao wakawajibishwa.
 
Back
Top Bottom