Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Nilimsikiliza na kumwona laivu pale C10 Mh Zitto akiliongelea suala hili la posho Bungeni na kwenye ajira za serikali na taasisi zake. Na kama kawaida yake alikuwa na takwimu pia. Kwa kweli inasikitisha kuona jinsi watu wanavyojilipa mara mbili au zaidi kwa kazi wlioajiriwa kuifanya kwa mshahara mzuri tu. Haya masuala ya posho yalishakuwa ni utamaduni, ni sehemu ya maisha ya viongozi wetu. Posho hizi ndizo zinazoendesha nyumba ndogo na anasa nyingine. Kwa aina ya Wabunge tulionao sasa sio rahisi kukubali kuziondoa posho hizi lakini ngoja angalau Mh Zitto aziseme Bungeni wananchi wajue nchi inavyotafunwa na wachache.
 
siasa ni mchezo mchafu kuliko matusi yanguoni
kama wako sirias kweli
1.wasikubali kupokea kwa siku posho zao
2.wakifika mwisho wa vikao wamwambie mh spika hela zetu tupelekee kiasi kadhaa hospitl ya muhimbili,kadhaa mawenzi na kadhaa wanunue magari ya wagonjwa nakwambia hizi jamba cheche na kama wamedhamiri wajaribu..wanachofanya wanajua ccm awatakubali so itaishia walitoa wazo la kukataa posho...weee squad nzima iko bungen unafanya mchezo mwaka hu awakutaka ujinga


Umesema kweli kaka! japo pia naamini dhamira ya CHADEMA ni kuondokana na mchezo mchafu ndani ya siasa. So far, hizo red, zimenikuna sana! Na hiyo ndiyo CHADEMA tunayoitegemea! Ni hiyo tuu ndiyo inaweza kumfanya mtanzania awe tayari kuisupport hata kwa uhai wake!.. Yes, watu wametoa uhai wao kwa ajili ya kuitetea haki na kumlinda mnyonge ambalo ndilo jukumu tuliloipa CHADEMA.
 
Kwa kusema hivyo tu, wanaonyesha kuwa wako tayari na wao kukosa posho hizo kwa maendeleo ya nchi. Katika hilo sioni mantiki ya kuanza kuhoji kwanini wao wanachukua posho. Kiongozi ambaye yuko tayari kupunguza maslahi yake kwa maendeleo ya nchi ndio anatakiwa katika zama hizi. Hata hivyo, cha msingi sio uwingi wa posho. Tunaangalia kiasi cha posho hizo na hali za watanzania. Nani anayesema kuwa Chadema hawataki posho hizo. Kama

Hauwezi ukaupima userious wa mtu kwa analoliongea bali lile analolitenda, inawezekana kabisa anayesema haitaki hiyo posho ndiye anayeipenda zaidi ila ameamua kupiga domo tu kwa sababu anauhakika kauli yake hiyo haitasababisha ulaji huo uondoke, sasa totoke huko na tupige hatua mbele..Mbunge yeyote anayeamini hiyo posho sio ya haki, asimame na kuhesabiwa kwa kuzikataa hizo posho sasa, full-stop.
 
nakubaliana na wewe 100%; wabunge wa chadema lazima wawe makini sana na hii kitu. Kanuni ya msingi inasema "usimwamshe aliyelala, utalala wewe". Kama wabunge wa cdm na chadema inafanya hili suala la kuwaamsha watanzania kinafiki inaweza kula kwako viabaya sana kuliko inavyoweza kula kwa ccm. Ni kweli kabisa kama kweli wanataka sisi wananchi tuwaelewe na suala hili likomeshwe moja kwa moja kuanzia kikao hiki wasichukue hizi unjustified allowances; nina imani hii itajenga msingi mzuri sana wa kukabiliana na tatizo hili ambalo ni kubwa sana serikalini na cdm itajijengea kuaminiwa zaidi na wananchi.

Binafisi naamini wabunge wa CHADEMA hawatapinga kama watashauriwa kusema "mwisho wa vikao wamwambie mh spika hela zetu tupelekee kiasi kadhaa hospitl ya muhimbili,kadhaa mawenzi na kadhaa wanunue magari ya wagonjwa" Kinachotakiwa hapa ni muongozo kutoka ngazi za juu za chama. Na nakwambia ikitokea kweli wamefanya hivyo, CHADEMA haitahitaji kutunisha misuri ya shingo kuwashawishi watanzania kuwa wamedhamiria kuwaletea ukombozi wa kweli! Let's walk the talk!
 
Sijakuelewa mkuu umesema kususia posho au kususia vikao vya bunge? nadhani hapo moja linawezekana lakini sio yote mawili mambo hufanywa kwa awamu awamu we wa wapi wewe?
 
Sijakuelewa mkuu umesema kususia posho au kususia vikao vya bunge? nadhani hapo moja linawezekana lakini sio yote mawili mambo hufanywa kwa awamu awamu we wa wapi wewe?

Soma vizuri posts kaka. Katika wachangiaji wote sijaona aliyependekeza kususiwa vikao vya bunge... lol!
 
Hey,
this is about the public policy issue, not party politics.
Ukiondoa posho Bungeni, maana yake ni kuwa, as matter of overall policy directive, hakutakuwa na posho katika idara, wizara wala wakala wa serikali.
Get issues right men!
 
Hauwezi ukaupima userious wa mtu kwa analoliongea bali lile analolitenda, inawezekana kabisa anayesema haitaki hiyo posho ndiye anayeipenda zaidi ila ameamua kupiga domo tu kwa sababu anauhakika kauli yake hiyo haitasababisha ulaji huo uondoke, sasa totoke huko na tupige hatua mbele..Mbunge yeyote anayeamini hiyo posho sio ya haki, asimame na kuhesabiwa kwa kuzikataa hizo posho sasa, full-stop.
Butola ndugu yangu, kinachopiganiwa sio posho ya wabunge pekee,hapo ni pakuanzia tuu. Posho za vikao zitolewazo kwa watumishi wa serikali na mashirika ya umma kwa mwaka ukipata idadi yake utashtuka. Huijui CCM na watu wake wasivyo na haya? Wabunge wa CHADEMA wakisusa wao bila aibu watakuambia ok na mfumo utabaki hivyohivyo. Hauta gusa sekta nyingine na hizo fedha za posho ya Wachadema haziwezi kuleta mabadiliko yeyote.
Nadhani tuunge mkono hoja hii maana ni ya Chama sio ya Zitto au Slaa au mbunge yeyote wa CDM. Wao kama Binadamu binafsi wanaweza kuzipenda hizo pesa lakini wanaheshimu msimamo wa chama kutaka kubadili mfumo huo ili kumsaidia mwananchi wa kawaida katika huduma za jamii anazozikosa kwa ukosefu wa fedha serikalini. Tusichanganye msimamo wa Chama na wa mbunge. Hawa wakina Chiligati wao wanatoa misimamo yao binafsi, tunataka kusikia msimamo wa chama chao. Ingawa CCM ni ngumu sana kujua chama kinasemaje na kauli ya mtu,kwani unaweza pata kauli mia tofauti toka kwa viongozi wake na hawajali/hawaelewi tofauti
 
Kulipwa posho mbili ni wizi, wabunge wanatuibia na wao wanalijua hilo, itabidi niwashangae kidogo mnaowalaumu wabunge wa Chadema kwamba kwa nini wasisusie hizo posho, kusususia sio suluhisho kwa sasa, wao wametoa pendekezo badala ya kuwapongeza japo kwa pendekezo zuri nyie mnawalaumu au na nyie mnafaidika na hizo posho mbili nini?
 
"Hatuwezi kuwaachia nguruwe wale mihogo shamani peke yao"___Hamad Rashid Mohamed (Mp)
 
[QUOTE=Anfaal;tuliwaambia kama hawamtambui Rais then hawana sababu ya kwenda bungeni kwa sababu Bunge linajadili mambo ya serikali inayoongozwa na wasiomtambua. Hapo zilifuata danadana za maneno.

Ushauri wako ulikuwa mbaya coz hujui kama bunge ni mhimili wa dola tena uko independent ndo mana bunge linaweza kukataa uamuzi wa rais na serikal lkn sio rais wala serikali yake kukataa uamuzi wa bunge.
 
Soma vizuri posts kaka. Katika wachangiaji wote sijaona aliyependekeza kususiwa vikao vya bunge... lol!
Mrbwire mkuu, usijichoshe na huyo wewe endelea na majadiliano yenye tija. Wengine wanajaza post za hovyo hapa kisha jioni anaenda pale Lumumba kuchukua sitting allowance ya kuchafua JF
 
Wakuu natanguliza samahani kwa nitakayemkwaza lakini ukweli katika hili siwaelewi viongozi wa vyama vya upinzani including CHADEMA kama wako serious! Hivi wanashindwa nini kususia posho hizo za wabunge??? Je kisingizio ni kwa sababu wakiacha CCM wanachukua?? If yes, Je inaleta mantiki yoyote?? Kama CCM wanaziiba, (na of course ndivyo ilivyo) je wao wanaona wakiziacha watakuwa wamewasusia CCM na hivyo bora na wao waziibe??? Jamani, hili linanikoseha raha na kunipa wasiwasi kama kweli dhamira yetu ya kuikomboa nchi hii inadhihirshwa hasa na tunachokisema na kukikariri kila siku.

Najua CCM hawataruhusu kuziondoa hizo posho ambazo sisi tunaamini kuwa ni kuwaibia wananchi wanyonge wa nchi hii!! Sasa je, kwa sababu CCM watakataa basi na wabunge wa CHADEMA wazichukue!!! Gosh!! Why? Hoping that two blacks will eventually make white??? TUACHE UZEMBE!!! NA TUMAANISHE KWA DHATI TUNAPOSEMA TUNA DHAMIRA YA KUMKOMBOA MWANANCHI ALIYEKATA TAMAA KUTOKANA NA UONEVU WA SERIKALI YA KIKWETE!!!! Viongozi wetu tunaomba mtutoe mashaka na kulifanunua hili!


Naanguliza shukurani kwa viongozi watakaochukua hatua kulifafanua kwa makini suala hili!


Ndugu yangu kususia posho haisaidii na haitasaidia kamwe, sana sana hizo posho zao zinaweza liwa na wahasibu wa bunge. Cha muhimu ambacho hao jamaa wa Chadema wamesema na wanapendekeza ni kwamba posho za "sitting allowance" ziondolewe maana ni mzigo kwa taifa. Labda nikufahamishe kuwa, wabunge wote wanalipwa per diems zao za kwenda Dodoma kuhudhuria vikao vya bunge hata mbunge anayetoka Dodoma mjini!!! Sasa pamoja na hiyo posho ya kuhudhuria vikao vya bunge pia wanalipwa posho ya kuingia kikaoni na ni utaratibu ambao sasa umeenea serikali nzima!!!

Ndiyo kitu ambacho jamaa wa Chadema wanaona ni MATUMIZI MABOVU YA SERIKALI.. Maana hiyo 80,000/= ndiyo perdiem wanayolipwa wakurugenzi na zinawatosha... Wengine sisi tunalipwa mishahara ya 500,000/= kwa mwezi mzima na inatutosha!!! Hapa kinachotakiwa ni kuondoa na kuubadilisha huu mfumo na sio kususia maana kuna msemo wa kiswahili kwamba UKISUSA WENZIO TWALAAA..

Ahsante
 
We must walk the talk. I have written to the Clerk of Bunge that all sitting allowances I am entittled to should be directed to a charity in my constituency up to when the law is changed and sitting allowances scrapped.
I will advise my fellow CHADEMA MPs to take similar measure.
 
Guys, simple minds discuss about people, ordinary minds discuss events, Great minds discuss ideas!
Katika mjadala huu wengi wetu tunajadili watu, matukio n.k. Wachache sana wamejadili hoja jadidi. Suala hapa si nani kachukua nini au kasema nini, nadhani la msingi ni hoja mezani. Je, posho hizi za vikao zina umuhimu wowote katika utendaji wa kila siku? Zinaongeza uwajibikaji kwa wanaozipokea? Zina tija kwa nchi? Kwanini ulipwe posho na mshahara kwa kutekeleza majukumu yako ya kila siku? Je, lilikuwa kosa kuzitoa na sasa imefika muda wa kurekebisha? Tujadili hayo angalau, na si mbona unachukua, susia kwanza tuone! Tujitambue kwamba tunaweza kufikiri na kuamua mambo yetu wenyewe.
 
Hamna aliye serious hapo, hiyo ni domo tu la kisiasa, tulimsikia Dr.Slaa mwaka jana na akapata sana publicity ya kisiasa lakini leo hii hana tena ujasiri wa kuliongelea hilo kwa kuyaramba matapishi yake na hivyo kuonyesha uhalisia wa mtazamo wake halisi aliokuwa ametuficha juu ya hilo.

Sintamuamini mtu yeyote juu ya hizi porojo za kujitafutia cheap popularity,kama mtu yuko serious aanze sasa kwa kuonyesha mfano wa kuzikataa hizo posho na sio vinginevyo.

Mkuu Butola wewe ni mpiganaji ambaye nilikuwa nakuamini sana imekuwaje tena unakuwa mtu wa kuunga mkono posho mbilimbili za hawa waheshimiwa, hata kama watakataa lakini wananchi wengi wakiwa against nao lazima wajue wanachokifanya sio kizuri, na kama mfumo haubadilishwi siungi mkono chadema kuziacha hizo posho kwa nini waziache wakati mfumo haueleweki bado, Mkulo angekuwa ni mtu ambaye anafikiri zaidi ya chama chake lazima pendekezo hilo lingepita, majirani zetu kenya mbona magari ya kifahari walirudisha na juzi juzi tu wananchi wamepiga kelele na ushuru wa mafuta ukapunguzwa kwa nini isiwe kwetu.

Mimi naamini serikali ikelekeza hela zake zitumike vizuri hata nyie wakuu kina Butola ambao ni nguzo za katikati za familia hamtaumia sana, kwa sababu hutalazimika kumununulia mdogo wako kitabu kwa sababu serikali itanunua, hutamhamisha mdogo wako kwenye shule ya kata maana sasa itakuwa na mwalimu ambaye analipwa vizuri, hutapoteza ndugu zako kwa magonjwa yanayotibika kwa sababu hospitali zitakuwa na dawa, hutalazimika kusafirisha mzee wako akatibiwe kwenye hospitali za private kama Aghakan maana hata vituo vya afya vya tarafa vitakuwa na dawa na daktari anayelipwa vizuri, hutalazimika kumhonga askari akakamate mwizi wako maana naye atakuwa analipwa vizuri, yoote hayo hamyaoni nyie mnataka chadema tu waache posho kwa nini msitake wabunge wote waache hizo posho na ziingie kwenye matumizi mazuri ya maendeleo ya nchi hii.
 
huyu wa cuf ni kibaraka.hawezi kuongea kama anakun.a tunataka posho ipunguzwe
 
We must walk the talk. I have written to the Clerk of Bunge that all sitting allowances I am entittled to should be directed to a charity in my constituency up to when the law is changed and sitting allowances scrapped.
I will advise my fellow CHADEMA MPs to take similar measure.
Asante mheshimiwa Zitto, umefanya vizuri sana kuweka kumbukumbu hizi hapa jamvini, na wananchi tunawasupport kwa pendekezo na mimi naamini hata kama watalipiga teke lazima litapita tu miaka ijayo, nchi yetu inahitaji karibia kila senti ya serikali kwa ajili ya maendeleo pamoja na huduma ya jamii, waonyesheni kwa nini mnataka posho ya vikao iondoke haki siku zote hushinda hata kama ni baada ya muda mrefu na nyie mko upande wa haki na lazima mtashinda.
 
Wakuu natanguliza samahani kwa nitakayemkwaza lakini ukweli katika hili siwaelewi viongozi wa vyama vya upinzani including CHADEMA kama wako serious! Hivi wanashindwa nini kususia posho hizo za wabunge??? Je kisingizio ni kwa sababu wakiacha CCM wanachukua?? If yes, Je inaleta mantiki yoyote?? Kama CCM wanaziiba, (na of course ndivyo ilivyo) je wao wanaona wakiziacha watakuwa wamewasusia CCM na hivyo bora na wao waziibe??? Jamani, hili linanikoseha raha na kunipa wasiwasi kama kweli dhamira yetu ya kuikomboa nchi hii inadhihirshwa hasa na tunachokisema na kukikariri kila siku.

Najua CCM hawataruhusu kuziondoa hizo posho ambazo sisi tunaamini kuwa ni kuwaibia wananchi wanyonge wa nchi hii!! Sasa je, kwa sababu CCM watakataa basi na wabunge wa CHADEMA wazichukue!!! Gosh!! Why? Hoping that two blacks will eventually make white??? TUACHE UZEMBE!!! NA TUMAANISHE KWA DHATI TUNAPOSEMA TUNA DHAMIRA YA KUMKOMBOA MWANANCHI ALIYEKATA TAMAA KUTOKANA NA UONEVU WA SERIKALI YA KIKWETE!!!! Viongozi wetu tunaomba mtutoe mashaka na kulifanunua hili!


Naanguliza shukurani kwa viongozi watakaochukua hatua kulifafanua kwa makini suala hili!

yaani mchaga asusie pesa? we wa wapi? watu wameingiza wake na watoto wao we unataka wazisusie? unaishi wapi wewe
 
Kama wanamagamba including Ndugai wameona hoja ya Mh. Zitto kwamba kupokea posho mbili i.e.subsistance allowance na sitting allowance at the same time ni wizi na ufujaji wa pesa zetu (walipa kodi). Kwanini wasifute hiyo posho moja ya sitting allowance kuliko kuja na hizi lame excuse kwamba wabunge wa CDM waandike barua ya kuzikataa?

Kwani wakizikataa wabunge CDM ndiyo zitalekezwa kwenye miradi ya maendeleao?!. Si zitabaki hapo kwenye ofisi ya bunge because ni budget ya bunge. CDM wanapinga huu MFUMO wa kinyonyaji sio tu kwa wabunge hata viongozi wengine wakuu wa serikali.

Yaani mimi nikisoma hizo hoja za wana-Magamba ninatamani kupasuka kwa hasira. Watanzania wengekuwa kama mimi sidhani kama mbunge hata mmoja wa CCM angerudi bungeni mwaka 2015.

Watu wakijiunga na CCM sijui akili zao zinakuwa je? nachelea kumfananisha Ndugai na MBUNI, na anajua tabia za mbuni maana, Ndugai amesoma wildlife management pale UD miaka hiyo ya matusi ya nguoni ya Mzee Rukhusa
 
Back
Top Bottom