Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Mimi nadhan tungekuwa wa kweli tu, ofisi kubwa ya mwanasiasa makini ni jukwaani, sidhan kama kuna dhambi kuyasemea mambo hayo jukwaani, kama hoja ni kuandika barua tu basi hakuna haja ya kukaa bungeni waandikiane barua tu mambo yote yajadiliwe kwa barua.

Hata kama mnawapenda wabunge hawa wengi wao ni watu ambao hawajali wananchi wao, Mtu kama Rashid Mohamed ambaye mimi namheshim na kumkubali kama mbunge makini ila kwa hili alilosema lazima nimpunguzie credit naona kama amekurupuka pengine ni hasira za kukosa ukuu wa kambi ya upinzani.

Na ukweli wa wanasiasa wanakuwa na hotuba mbili pale jukwaani ya kuwaelezea mafala mfano hii ya kupinga posho na ya kweke mwenyewe kwa kuikumbatia na kuipenda ilhali akijua anaweza kupeleka kusudio kwa spika la kufuta posho lakini asifanye hivyo.

Kwahiyo wanasiasa hawana lolote zaidi ya kuangalia maslahi yao usibabaike sana na maneno yao matamu kikubwa tuangalie yetu yanatendeka? tumewachagua majimbo je wapo pamoja na sisi kwenye kuleta maendeleo ya jimbo? wamesaidia nini uwepo wao bungeni kuleta tija kwenye majimbo yanayotoka?
 
Hapa hakuna udini ukitajwa ukristo wala uislam, ni dalili ya kukimbia hoja waelewe.

Originally Posted by AMARIDONG ANAKULA 40,000/= KWA SIKU DU??HUYU MUISLAM NI SOO,HII SI NI BEI YA MBUZI MKUBWA BEBERU NA KRET MBILI ZA KILIMANJARO,NA MAJI KATON MOJA KWELI JAMAA YUKO JUU

ANAMPA DEREVA WAKE 30,000/= PER DAY MAANA YAKE JAMAA ANATENGENEZA

30,000 X 30=900,000/=
SASA BUNGE HILI N LA MIEZI MITATU
900,000 X 3=2,700,000/=
MSHAHARA WA DEREVA SH 900,000/= KWA MWEZI HAIWEZEKANI

SI KWELI HUYU MPEMBA ANADANGANYA UMMA

mnafki tuu hana lolote
 
Na ukweli wa wanasiasa wanakuwa na hotuba mbili pale jukwaani ya kuwaelezea mafala mfano hii ya kupinga posho na ya kweke mwenyewe kwa kuikumbatia na kuipenda ilhali akijua anaweza kupeleka kusudio kwa spika la kufuta posho lakini asifanye hivyo.

Kwahiyo wanasiasa hawana lolote zaidi ya kuangalia maslahi yao usibabaike sana na maneno yao matamu kikubwa tuangalie yetu yanatendeka? tumewachagua majimbo je wapo pamoja na sisi kwenye kuleta maendeleo ya jimbo? wamesaidia nini uwepo wao bungeni kuleta tija kwenye majimbo yanayotoka?
hapo red: **** mwenyewe
 
Na ukweli wa wanasiasa wanakuwa na hotuba mbili pale jukwaani ya kuwaelezea mafala mfano hii ya kupinga posho na ya kweke mwenyewe kwa kuikumbatia na kuipenda ilhali akijua anaweza kupeleka kusudio kwa spika la kufuta posho lakini asifanye hivyo.

Kwahiyo wanasiasa hawana lolote zaidi ya kuangalia maslahi yao usibabaike sana na maneno yao matamu kikubwa tuangalie yetu yanatendeka? tumewachagua majimbo je wapo pamoja na sisi kwenye kuleta maendeleo ya jimbo? wamesaidia nini uwepo wao bungeni kuleta tija kwenye majimbo yanayotoka?

Mkuu unaweza kuchukua maneno yangu, hii ishu ya posho mbili lazima itafika kikomo sio lazima iwe mwaka huu lakini haitafika 2015.
 
Mkuu kula Tshs. 40,000.00 inawezekana. Swali ni kuwa unakula na nani? Kama ana mke zaidi ya mmoja na ameenda nao wote na bado pale Chako ni Chako !!
Hapo mzee, hata hiyo 150000/= haitoshi! Tatizo hawataki kusema wanasubiriwa, badala yake wanapiga porojo tu!
 
Kama kweli tunataka tuendelee,wakae mabwenini.
Huo ndio uanamapinduzi,other than that....tunapiga maktaim!
 
hapo red: **** mwenyewe

Mrembo Merytina sio lazima usome kila neno dada yangu, maneno mengine watu wanaandika ili aya ionekane ina maneno mengi lakini hayana mantiki yoyote kwenye hoja yenyewe.
 
Mkuu Chakaza, nashukuru kwa maelezo:

Binafsi naamini wabunge kujilipa miposho mikubwa kiasi hicho ni wizi na ubinafsi ulioratibiwa na serikali ya CCM! Haiwezekani ukamlipa mtanzania mmoja posho ya mwezi mmoja sawa na mshahara wa miaka minne ya mwalimu au polisi! Huu ni wizi na ukatili mbaya!!. Ambao ulipaswa kupingwa sio tuu kwa sababu ya kupanda kwa mafuta na kuongezeka kwa hali ngumu ya maisha.... Ki uhalisi huu ni uchu mbaya sana wa mali! Kuwalipa mabilioni watu wachache wkt mama zetu wakijifungulia sakafuni! na wangine wakiwa hawana uhakika hata wa chakula!!! ..."kususa" kwa namna hii ni sawa na kutoshiriki kuwaibia wananchi! Ni kuonesha hatuko tayari kujineemesha on the expense ya watanzania! Hebu tusaidiane... tutazpoteza nini tukigoma kuzichukua? Itakiathiri vipi chama?? Nipe madhara ya kususa , nami nitatoa faida za kutopokea pesa inayochangia kumuumiza mwananchi wa Tanzania! (Tuondoe jazba! naamini tunachokijenga ni kimoja)
 
wakuu natanguliza samahani kwa nitakayemkwaza lakini ukweli katika hili siwaelewi viongozi wa vyama vya upinzani including chadema kama wako serious! Hivi wanashindwa nini kususia posho hizo za wabunge??? Je kisingizio ni kwa sababu wakiacha ccm wanachukua?? If yes, je inaleta mantiki yoyote?? Kama ccm wanaziiba, (na of course ndivyo ilivyo) je wao wanaona wakiziacha watakuwa wamewasusia ccm na hivyo bora na wao waziibe??? Jamani, hili linanikoseha raha na kunipa wasiwasi kama kweli dhamira yetu ya kuikomboa nchi hii inadhihirshwa hasa na tunachokisema na kukikariri kila siku.

Najua ccm hawataruhusu kuziondoa hizo posho ambazo sisi tunaamini kuwa ni kuwaibia wananchi wanyonge wa nchi hii!! Sasa je, kwa sababu ccm watakataa basi na wabunge wa chadema wazichukue!!! Gosh!! Why? Hoping that two blacks will eventually make white??? Tuache uzembe!!! Na tumaanishe kwa dhati tunaposema tuna dhamira ya kumkomboa mwananchi aliyekata tamaa kutokana na uonevu wa serikali ya kikwete!!!! Viongozi wetu tunaomba mtutoe mashaka na kulifanunua hili!


naanguliza shukurani kwa viongozi watakaochukua hatua kulifafanua kwa makini suala hili!

siasa ni mchezo mchafu kuliko matusi yanguoni
kama wako sirias kweli
1.wasikubali kupokea kwa siku posho zao
2.wakifika mwisho wa vikao wamwambie mh spika hela zetu tupelekee kiasi kadhaa hospitl ya muhimbili,kadhaa mawenzi na kadhaa wanunue magari ya wagonjwa nakwambia hizi jamba cheche na kama wamedhamiri wajaribu..wanachofanya wanajua ccm awatakubali so itaishia walitoa wazo la kukataa posho...weee squad nzima iko bungen unafanya mchezo mwaka hu awakutaka ujinga
 
Nafikiri hapa tatizo si nani anachukua na nani anasusia posho. Tatizo ni mfumo wa utoaji wa hizo posho. Kususia hakutakuwa na msaada kwa mlalahoi. Kinachotakiwa ni kupigania kufumuliwa kwa mfumo unajustify hizo posho ambazo kwa kweli zimeonekana zinammyonya mlipa kodi wa nchi hii.
 
Hamna aliye serious hapo, hiyo ni domo tu la kisiasa, tulimsikia Dr.Slaa mwaka jana na akapata sana publicity ya kisiasa lakini leo hii hana tena ujasiri wa kuliongelea hilo kwa kuyaramba matapishi yake na hivyo kuonyesha uhalisia wa mtazamo wake halisi aliokuwa ametuficha juu ya hilo.

Sintamuamini mtu yeyote juu ya hizi porojo za kujitafutia cheap popularity,kama mtu yuko serious aanze sasa kwa kuonyesha mfano wa kuzikataa hizo posho na sio vinginevyo.
 
Usicheze na pesa bwana. Ziache kama zilivyo! CDM hawawezi na hawataweza kususia pesa (bunge). Hilo halitatokea. Unakumbuka wakati wanaapishwa wakagoma kumtambua Rais, tuliwashauri nini hapa jamvini? Labda nikukumbushe, tuliwaambia kama hawamtambui Rais then hawana sababu ya kwenda bungeni kwa sababu Bunge linajadili mambo ya serikali inayoongozwa na wasiomtambua. Hapo zilifuata danadana za maneno. Unakumbuka juzi ule mshahara ulioitwa allowances ili kukwepa kodi? lakini pamoja na hayo kumbe hata allowance inalipiwa kodi.
Kwahiyo kwenye ishu ya pesa ni vigumu saana kutekeleza labda ujaribu kufikiria jingine
 
una analyse kwa kutumia makalio
kinachoongelewa ni mfumo.Mfumo ambao utajaribu kuleta usawa na sio kususiwa kwa posho

Nilitanguliza kuomba samahani kwa sababu nilijua hili lingeweza kutokea na ni kawaida. Tujiulize kitu kidogo Mery, Mfumo huundwa na nini? Bila ya shaka mfumo unaundwa vitu kadhaa zikiwemo taratibu, sera, dhamira n.k Tunaweza kuupinga mfumo kama mfumo, lakini pia tunaweza kupinga baadhi ya ellement za mfumo husika. Tunapoandamana kupinga unyanyaswaji wa wananchi waishio karibu na migodi tunaupinga mfumo, lakini pia ni katika eneo ama aspects kadha wa kadha! Si busara kuona mambo yasiyowatendea haki wananchi tukayafumbia macho kwa kisingizio kuwa tunachopambana nacho ni system... Si sawa! Jiulize hiki: Serikali ya ccm imewahi kutoa bonus ya migodi kwa viongozi wake (Reffering Kiwira) Sasa, ikiamua ikasema kila mbunge baada ya kustaafu upewa squre meter 40X40 katika eneo la mgodi, should we expect our leaders to accept kwa dhana kuwa "Kususa" si ufumbuzi? So wachukue? Nakwambia IKO SIKU WATU WENYE UCHUNGU NA NCHI HII WATAWALAZIMISHA KURUDISHA MALI ZOTE WALIZOZICHOTA KUTOKANA NA KODI NA JASHO LA WATANZANIA... When that happens.... sijui, but I wouldnt wish to see the day ambayo viongozi ninaowaamini pia watapaswa kurudisha!
 
mkuu chakaza, nashukuru kwa maelezo:

Binafsi naamini wabunge kujilipa miposho mikubwa kiasi hicho ni wizi na ubinafsi ulioratibiwa na serikali ya ccm! Haiwezekani ukamlipa mtanzania mmoja posho ya mwezi mmoja sawa na mshahara wa miaka minne ya mwalimu au polisi! Huu ni wizi na ukatili mbaya!!. Ambao ulipaswa kupingwa sio tuu kwa sababu ya kupanda kwa mafuta na kuongezeka kwa hali ngumu ya maisha.... Ki uhalisi huu ni uchu mbaya sana wa mali! Kuwalipa mabilioni watu wachache wkt mama zetu wakijifungulia sakafuni! Na wangine wakiwa hawana uhakika hata wa chakula!!! ..."kususa" kwa namna hii ni sawa na kutoshiriki kuwaibia wananchi! Ni kuonesha hatuko tayari kujineemesha on the expense ya watanzania! Hebu tusaidiane... Tutazpoteza nini tukigoma kuzichukua? Itakiathiri vipi chama?? Nipe madhara ya kususa , nami nitatoa faida za kutopokea pesa inayochangia kumuumiza mwananchi wa tanzania! (tuondoe jazba! Naamini tunachokijenga ni kimoja)

haujajibu kuhusu suala la mfumo?
 
Dunia hii ina watu wa ajabu sana. Chadema wamependekeza kuondoa sitting allowance kwa wabunge ili kubana matumizi yasiyo na tija. Fedha zitakazookolewa kutokana na uamuzi huo zitumike kwa maendeleo ya wananchi walio wengi. Badala ya kujadili umuhimu wa mpango huo watu wanaanza kuhoji mbona wao wanachukua posho hizo?

Kwa kusema hivyo tu, wanaonyesha kuwa wako tayari na wao kukosa posho hizo kwa maendeleo ya nchi. Katika hilo sioni mantiki ya kuanza kuhoji kwanini wao wanachukua posho. Kiongozi ambaye yuko tayari kupunguza maslahi yake kwa maendeleo ya nchi ndio anatakiwa katika zama hizi. Hata hivyo, cha msingi sio uwingi wa posho. Tunaangalia kiasi cha posho hizo na hali za watanzania. Nani anayesema kuwa Chadema hawataki posho hizo. Kama watanzania wangekua na maisha bora kama tuliyoahidiwa unadhani posho za wabunge ingekuwa hoja?

Tusiwe wapumbavu na washenzi, tuangalie hali ya wafanyakazi wa kima cha chini, wamachinga wanaozunguka kila kukicha, wanafunzi wanaofanya mitihani wakiwa chini, wakina mama wanaojifungua sakafuni na makundi mengine yaliyo katika shida kubwa. Baada ya hayo jaribu kulinganisha na posho za hao wateule. Tuache ushabiki usiokuwa na maana, tuangalie hoja iliyo mbele yetu na wala sio chanzo cha hoja hiyo. Kama umejiunga na JF kwa ajili ya kupinga tu hoja za upande fulani jaribu kuangalia siku zijazo kwako wewe na vizazi vyako vijavyo hali itakuaje.
 
Usicheze na pesa bwana. Ziache kama zilivyo! CDM hawawezi na hawataweza kususia pesa (bunge). Hilo halitatokea. Unakumbuka wakati wanaapishwa wakagoma kumtambua Rais, tuliwashauri nini hapa jamvini? Labda nikukumbushe, tuliwaambia kama hawamtambui Rais then hawana sababu ya kwenda bungeni kwa sababu Bunge linajadili mambo ya serikali inayoongozwa na wasiomtambua. Hapo zilifuata danadana za maneno. Unakumbuka juzi ule mshahara ulioitwa allowances ili kukwepa kodi? lakini pamoja na hayo kumbe hata allowance inalipiwa kodi.
Kwahiyo kwenye ishu ya pesa ni vigumu saana kutekeleza labda ujaribu kufikiria jingine

Usemacho ni kweli. Lakini pia ni ukweli usipingika kuwa HAKUNA chama chenye uelekeo wa kumkomboa mtanzania mbali na CHADEMA... "HAKUNA" Sasa nini kifanyike; ni kwetu sisi wananchi wenye mapenzi mema na nchi yetu kukishauri na kukisoa (Kwa nia ya kukijenga). Binafisi naamini; kama wakati wanazichukua hizo pesa dhamiri haziwashitaki, then something is seriously wrong!! Na ningeshauri tusiendelee kufanya vitu ambavyo dhamiri zetu zinatushitaki!

Pse CHADEMA MPs! YOU CAN DO IT!!
 
una analyse kwa kutumia makalio
kinachoongelewa ni mfumo.Mfumo ambao utajaribu kuleta usawa na sio kususiwa kwa posho

HAPO KWENYE RED HAPO PENYEWE SANA HII NDIO TABIA YA MAGAMBA YOTE YANAANALYSE KWA KUTUMIA HICHO KIUNGO hahaha
 
nilitanguliza kuomba samahani kwa sababu nilijua hili lingeweza kutokea na ni kawaida. Tujiulize kitu kidogo mery, mfumo huundwa na nini? Bila ya shaka mfumo unaundwa vitu kadhaa zikiwemo taratibu, sera, dhamira n.k tunaweza kuupinga mfumo kama mfumo, lakini pia tunaweza kupinga baadhi ya ellement za mfumo husika. Tunapoandamana kupinga unyanyaswaji wa wananchi waishio karibu na migodi tunaupinga mfumo, lakini pia ni katika eneo ama aspects kadha wa kadha! Si busara kuona mambo yasiyowatendea haki wananchi tukayafumbia macho kwa kisingizio kuwa tunachopambana nacho ni system... Si sawa! Jiulize hiki: Serikali ya ccm imewahi kutoa bonus ya migodi kwa viongozi wake (reffering kiwira) sasa, ikiamua ikasema kila mbunge baada ya kustaafu upewa squre meter 40x40 katika eneo la mgodi, should we expect our leaders to accept kwa dhana kuwa "kususa" si ufumbuzi? So wachukue? Nakwambia iko siku watu wenye uchungu na nchi hii watawalazimisha kurudisha mali zote walizozichota kutokana na kodi na jasho la watanzania... When that happens.... Sijui, but i wouldnt wish to see the day ambayo viongozi ninaowaamini pia watapaswa kurudisha!

nakubaliana na wewe 100%; wabunge wa chadema lazima wawe makini sana na hii kitu. Kanuni ya msingi inasema "usimwamshe aliyelala, utalala wewe". Kama wabunge wa cdm na chadema inafanya hili suala la kuwaamsha watanzania kinafiki inaweza kula kwako viabaya sana kuliko inavyoweza kula kwa ccm. Ni kweli kabisa kama kweli wanataka sisi wananchi tuwaelewe na suala hili likomeshwe moja kwa moja kuanzia kikao hiki wasichukue hizi unjustified allowances; nina imani hii itajenga msingi mzuri sana wa kukabiliana na tatizo hili ambalo ni kubwa sana serikalini na cdm itajijengea kuaminiwa zaidi na wananchi.
 
Back
Top Bottom