MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
1. Msemaji wenu Hassan Bumbuli na Afisa Mhamasishaji wenu Mkuu Antonio Nugaz baada ya Mechi ya tarehe 3 July, 2021 ambayo Yanga SC ilishinda walisikika wakisema kuwa Simba SC bila Kuwanunua Wachezaji wa Yanga haiwezi Kushinda. Je, Simba SC iliyomfunga au iliyoshinda leo imewanunua Wachezaji wa Yanga SC?
2. Mzee Mpili kuelekea Mechi ya Fainali ya ASFC ya leo alisema kuwa ana Watu je, hao Watu leo hawakuwepo mpaka Yanga SC Kufungwa?
3. Watu au Mashabiki wa Yanga SC kwa nyakati tofauti walisikika wakisema kuwa kuelekea Mechi ya leo ASFC Final wanaenda Kupiga pale pale penye Mshono kwa Kuwafunga Simba SC je, wamefanikiwa Kutonesha Mshono wa Kidonda leo?
4. Yanga SC wamekuwa wakioneka kukwepa kupita katika Geti Kuu au Mageti Makuu ya Viwanja ambavyo hucheza na Simba SC wakiamini kuwa huwa wanategua Mitego ya Kiuchawi ya Simba SC je, leo imekuwaje pamoja na Kukwepa kupita Geti Kuu lakini bado wamechezea Kichapo kutoka kwa Simba SC tena katika Mechi muhimu sana tu ya Fainali?
5. Kabla ya Mechi ya leo ambayo Yanga SC imefungwa na Simba SC Watu wengi wa Yanga SC walisikika wakijigamba kuwa Mkoa wa Kigoma ni Ngome Kuu ya Yanga SC na kwamba Kufungwa huko ni ngumu je, leo imekuwaje wenye Ngome yao Kufungwa wakati walisema Simba SC haikubaliki Kiushabiki Mkoani Kigoma?
6. Baada ya Yanga SC Kuifunga Simba SC katika Ligi Kuu ya VPL walisikika wakisema kuwa haitotokea Yanga SC akafanywa Daraja la Simba SC Kutangaza Ubingwa mbele yao je, Simba SC leo imeshinda na Kuchukua Ubingwa wa ASFC mbele ya Ihefu FC au Gwambina FC?
7. Injinia Hersi Said wa GSM alisema kuwa Yanga SC watafanya kila namna wabebe Kombe la ASFC ili Kuwatuliza Mashabiki zao na Wao kutoonekana kama vile wamebebwa Klabu Bingwa ya CAF na Simba SC je, leo Yanga SC imeshinda? Je, baada ya Yanga SC kushika nafasi ya Pili katika Ligi Kuu ya VPL na leo kukosa Kombe la ASFC huko Klabu Bingwa ya CAF anaenda kwa Msaada wa Timu gani?
Nasubiria Majibu kutoka kwa Yanga SC.
2. Mzee Mpili kuelekea Mechi ya Fainali ya ASFC ya leo alisema kuwa ana Watu je, hao Watu leo hawakuwepo mpaka Yanga SC Kufungwa?
3. Watu au Mashabiki wa Yanga SC kwa nyakati tofauti walisikika wakisema kuwa kuelekea Mechi ya leo ASFC Final wanaenda Kupiga pale pale penye Mshono kwa Kuwafunga Simba SC je, wamefanikiwa Kutonesha Mshono wa Kidonda leo?
4. Yanga SC wamekuwa wakioneka kukwepa kupita katika Geti Kuu au Mageti Makuu ya Viwanja ambavyo hucheza na Simba SC wakiamini kuwa huwa wanategua Mitego ya Kiuchawi ya Simba SC je, leo imekuwaje pamoja na Kukwepa kupita Geti Kuu lakini bado wamechezea Kichapo kutoka kwa Simba SC tena katika Mechi muhimu sana tu ya Fainali?
5. Kabla ya Mechi ya leo ambayo Yanga SC imefungwa na Simba SC Watu wengi wa Yanga SC walisikika wakijigamba kuwa Mkoa wa Kigoma ni Ngome Kuu ya Yanga SC na kwamba Kufungwa huko ni ngumu je, leo imekuwaje wenye Ngome yao Kufungwa wakati walisema Simba SC haikubaliki Kiushabiki Mkoani Kigoma?
6. Baada ya Yanga SC Kuifunga Simba SC katika Ligi Kuu ya VPL walisikika wakisema kuwa haitotokea Yanga SC akafanywa Daraja la Simba SC Kutangaza Ubingwa mbele yao je, Simba SC leo imeshinda na Kuchukua Ubingwa wa ASFC mbele ya Ihefu FC au Gwambina FC?
7. Injinia Hersi Said wa GSM alisema kuwa Yanga SC watafanya kila namna wabebe Kombe la ASFC ili Kuwatuliza Mashabiki zao na Wao kutoonekana kama vile wamebebwa Klabu Bingwa ya CAF na Simba SC je, leo Yanga SC imeshinda? Je, baada ya Yanga SC kushika nafasi ya Pili katika Ligi Kuu ya VPL na leo kukosa Kombe la ASFC huko Klabu Bingwa ya CAF anaenda kwa Msaada wa Timu gani?
Nasubiria Majibu kutoka kwa Yanga SC.