Ndukidi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2012
- 1,498
- 1,297
Nimetoka Nyamongo Jumamosi asubuhi, sina uhakika kwa shambulizi hili la polisi unalolizungumzia lakini Ijumaa jioni wananchi ambao kule wamezoeleka kama Intruders, walivamia mgodi muda wa kama saa kumi na mbili jioni na kuanza kupiga mawe magari na watu wote waliokuwamo mgodini.
Kuna watu wengi tu wanaofanya kazi mgodini wameuawa kwa kuchinjwa au kupigwa mawe na hao intruders. Hivi sasa magari yote kule mgodini inabidi yawekewe wiremesh madirishani kuepuka kupigwa mawe na hao intruders. Kama mmesikia hivi karibuni ABG wanataka kuuza migidi yao hapa nchini na moja wapo ya sababu ni uvamizi kwenye migodi haswa Nyamongo ambao umewatia haswara kubwa , ikiwa ni pamoja na kuamua kujenga ukuta mkubwa kuzunguka mgodo bila mafanikio kwani jamaa wanapanda na kuvamia frequently.
Pamoja na yote hayo mimi sikubaliani kabisa na kitendo cha polisi kupiga raia wasiokuwa na hatia, au kutumia nguvu kubwa kupita kiasi. Lakini kwa hali iliyopo Nyamongo, jamani naomba muulize walioko kule ni hatari sana. Jamaa wanavamia watu mradi tu wakikuona na gari au kuhisi una chochote wanaweza faidika nacho wao wanaona wewe ni halali yao.
Kuna watu wengi tu wanaofanya kazi mgodini wameuawa kwa kuchinjwa au kupigwa mawe na hao intruders. Hivi sasa magari yote kule mgodini inabidi yawekewe wiremesh madirishani kuepuka kupigwa mawe na hao intruders. Kama mmesikia hivi karibuni ABG wanataka kuuza migidi yao hapa nchini na moja wapo ya sababu ni uvamizi kwenye migodi haswa Nyamongo ambao umewatia haswara kubwa , ikiwa ni pamoja na kuamua kujenga ukuta mkubwa kuzunguka mgodo bila mafanikio kwani jamaa wanapanda na kuvamia frequently.
Pamoja na yote hayo mimi sikubaliani kabisa na kitendo cha polisi kupiga raia wasiokuwa na hatia, au kutumia nguvu kubwa kupita kiasi. Lakini kwa hali iliyopo Nyamongo, jamani naomba muulize walioko kule ni hatari sana. Jamaa wanavamia watu mradi tu wakikuona na gari au kuhisi una chochote wanaweza faidika nacho wao wanaona wewe ni halali yao.