Watu8
Platinum Member
- Feb 19, 2010
- 70,953
- 93,931
Wewe kweli unaishi Tanzania?
huyu mbona ni mbongo na anaungua jua kama sisi tu
Wewe kweli unaishi Tanzania?
Hapa tunazungumzia suala la Nyamongo. Suala la morogoro na iringa hata mimi natupia lawama polisi. Kweli ukweli nasema ukweli
umeongea ujinga mwingi saana lakini hakuna point yeyote kubwa ulioanisha kama mtu mwenye akili tofauti na kuwalable watu kwa a ni wajeuri wewe una kipimo cha kupima ujeuri hebu tupatie takwimu ya wanaoongoza mpaka wa mwisho,unataka waseme ni mgodi wako au wa kikwete au wa wazungu ile ni natural resourse iliwekwa pale purposely na mungu sio ccm wala mama zao eti waliwazawadia watu mgodi polisi pale wanaiba dhahabu popote wanapoiona na ikumbukwe ile milima ambayo vijana wanaokota mawe ni residue tu za mawe wala watu hawajawahi vamia mgodi mgodi ni kule room pad na plant umewahi kuona mtu huko heri mkoloni mweupe kuliko wapumbavu kama nyie na serikali yenu wajinga
tunazo mpaka namba za polisi na wengine wanauza dhahabu tunazo picha za polisi wamewakata watu wanachukua pesa pale nyamongo polis pale wanacheza dili ikitibuka wanaanza kupiga watu risasi si muda tutaanika humu ukweli hatuwezi kuvumilia mambo ya kijinga na mwisho tutakaa tujadili namna ya kujilinda wenyewe
Hao wananchi walipigwa tu bila sababu za msingi? Kama walivamia eneo la mgodi, sidhani kama kulikuwa na makosa upande wa askari. Askari walikuwa wakitimiza wajibu wao wa kazi kama kawaida.
Hao wananchi walipigwa tu bila sababu za msingi? Kama walivamia eneo la mgodi, sidhani kama kulikuwa na makosa upande wa askari. Askari walikuwa wakitimiza wajibu wao wa kazi kama kawaida.
Ulishawahi kujiuliza ni kwanini askari polisi wanagombania kupangiwa kazi kituo cha nyamongo? ushawahi kujiuliza ni kwanini askari polisi wanatoa rushwa kwa wakuu wao ili wapangiwe kituo cha nyamongo? ushawahi kujiuliza ni kwanini askari polisi wanaofanya kazi mgodini nyamongo wana utajiri mkubwa usiofanana kabisa na kipato chao cha upolisi?
Haya mambo mnapoyajadili msiwe kama mbuni, jitahidini kuangalia kwa upana wake. Mkikaa kusikiliza propaganda za ccm na serikali yake ndio mnabaki kuandika vitu vya hovyo hovyo against watu wa Tarime. Na kwa taarifa yako hata kama polisi wataendelea kuua watu kila siku, watu wa nyamongo na tarime kwa ujumla hawatachoka kupigania haki yao hadi hapo itakapopatikana hata kama ni kwa gharama ya uhai wa watu wengi kiasi gani.
This is ridiculous!Hivi wajibu wa askari wa Tanzania ni kuua?
This is ridiculous!Hivi wajibu wa askari wa Tanzania ni kuua?
Kupiga watu kunawasaidia nini Polisi?Kuna swali halijajibiwa hapa. Polisi walianzaje kupiga watu? Hata kama ni sababu za kijinga tuzijue.
Siyo askari wa Tanzania tu. Dunia nzima kazi ya askari ni kulinda usalama wa raia na kuhakikisha amani inadumishwa katika jamii. Theoretically, utatarajia kuwa matumizi ya nguvu za aina yoyote ile huwa hayahitajiki kufanywa na polisi muda wowote ule. Hata hivyo pale ambapo usalama wa raia unahatarishwa na raia wengine, polisi huwa 'wanalazimika' kutumia nguvu ili kuokoa hawa waliopo hatarini. Logic hapa ni kwamba ni afadhali kuua watu wachache kwa maslahi ya usalama ya watu wengine.
Siyo askari wa Tanzania tu. Dunia nzima kazi ya askari ni kulinda usalama wa raia na kuhakikisha amani inadumishwa katika jamii. Theoretically, utatarajia kuwa matumizi ya nguvu za aina yoyote ile huwa hayahitajiki kufanywa na polisi muda wowote ule. Hata hivyo pale ambapo usalama wa raia unahatarishwa na raia wengine, polisi huwa 'wanalazimika' kutumia nguvu ili kuokoa hawa waliopo hatarini. Logic hapa ni kwamba ni afadhali kuua watu wachache kwa maslahi ya usalama ya watu wengine.
Mwita Maranya ninachosema ni kwamba hali ya usalama maeneo ya Nyangoto, Kewancha, Nyabigena si nzuri hata kidogo. Najua unafahamu kwamba wakurya wana silaha za moto na huwa wanaenda kwenye migodi wakiwa kamili na polisi huwa wanatymia risasi kupiga juu kuwatawanya. Hiyo hali kwa Nyamongo ni ya kawaida sana na Polisi pia hupigwa hata ukiona magari ya Polisi yaliyopo kule Nyammongo utajua tu kule ni kama kuna vita. Suala hapa si Polisi kuua ama Polisi kuuawa, suala la msingi ni kutafuta suluhu kati ya Wanyamongo na wawekezaji kwa kuwa Wanyamongo siyo kwamba wanawachukia Polisi bali wanyamongo wanapigania haki yao. Hapa kuna uchonganishi kati ya Polisi na Wanyamongo na mwisho wa siku ni sisi Watanzania kuuana wakati wazungu wanakunywa kahawa makwao. Hakuna pumba. Sitegemei nawe kutumia neno hili mfu.Punguza pumba mkuu wewe si wa kiwango hicho. Kujustfy mauaji ya raia wasio na hatia kwa kisingizio cha polisi kuuwawa na kutupwa mto tigite ni akili ya kuku. Lete ushahidi hapa wa askari polisi waliouwawa na kutupwa mto tigite.
Sheria gani ya nchi inayowataka polisi kuua kila mtu anayesemekana kutenda kosa mgodini nyamongo ama maeneo ya kuzunguka mgodi? Watu wanaaoshabikia mauaji haya ya kiholela yanayofanywa na polisi wanahitaji kupimwa akili zao kama ziko vizuri.
Siyo kweli. Wajibu wa polisi ni kulinda raia na mali zao. Polisi anapaswa kutumia njia mbalimbali za kukabiliana na raia. Ndiyo maana kuna mabomu ya machozi, maji ya kuwasha, risasi za mpira. Pia wana vifaa na zana madhubuti kujikinga na mawe n.k. Lakini pia mafunzo ya polisi yanamwezesha kupambana na raia kwa kutumia mikono ana miguu yake wakisaidiwa na mbwa au farasi. Polisi wetu ni wavivu ila mafunzo wanayo hivyo wanapenda short cut
Wananchi huwa wanavamia kwenea kutafuta mabaki ya madini wakiwa katika makundi na silaha za jadi.
Siyo kweli. Wajibu wa polisi ni kulinda raia na mali zao. Polisi anapaswa kutumia njia mbalimbali za kukabiliana na raia. Ndiyo maana kuna mabomu ya machozi, maji ya kuwasha, risasi za mpira. Pia wana vifaa na zana madhubuti kujikinga na mawe n.k. Lakini pia mafunzo ya polisi yanamwezesha kupambana na raia kwa kutumia mikono ana miguu yake wakisaidiwa na mbwa au farasi. Polisi wetu ni wavivu ila mafunzo wanayo hivyo wanapenda short cut
Mkuu Kimbunga akili ya kuambiwa changanya na zako.
Kwa taarifa yako wakurya ni kawaida yao kutembea na silaha za jadi kama vile sime, panga, jambia, rungu ama silaha nyingine yoyote ya jadi wakati wowote hasa huko vijijini. Kwahiyo usijaribu kujustfy uongo wako hapa kwa kitu ambacho hukifahamu vizuri.
Mnapokwenda huko nyamongo ama Tarime ni vizuri muende mkiwa na akili ya kutaka kuujua ukweli kuliko mnavyokwenda na propaganda mlizolishwa na serikali yenu halafu mnakwenda kutafuata justification ya hizo propaganda kwa kubase kwenye hoja na ushahidi dhaifu kama huu wa kwako.
Mkuu Mwita Maranya, hayo yote nakubaliana na wewe. Tunachojadili leo ni issue iliyoletwa na mwenzetu kiribo kuwa polisi wamevamia barabara na kuanza kupiga wananchi. Tunachojiuliza ni nini kimesababisha polisi wakafanya hivyo. Mimi sababu iliyopelekea polisi kutumia nguvu, nimeisema na wewe sema yako. Usiwe na dhana kwamba wewe pekee ndo unajua mengi kuhusu nyamongo. Hayo ni madogo, tunafahamu makubwa zaidi ya hayo ya polisi. Mind your tongue
Kimbunga kama ungekuwa umenisoma kwa umakini ungegundua kwamba nimesema wakurya wanatembea na silaha za jadi wakati wote wanapokuwa huko vijijini na sikuwafananisha na wamasai.Mkuu Mwita Maranya linapofika suala la Nyamongo na Wakurya huwa sipendi saaaana kuingia katika malumbano kwa sababu ambazo nazijua na kuna siku nitakupa hizo sababu. Wakurya ni kweli huwa wanatembea na sime lakini siyo kama wamasai.
Acha kudanganya umma wa watanzania wewe. Yaani polisi wavamiwe na watu wenye silaha kali halafu eti wao wajikinge kwa mikono na miguu na risasi za mpira? Hayo mafunzo gani ya hali ya juu waliyoyapata ambayo yanawawezesha kupambana hadi na mabomu. Wewe inaelekea huelewi hali halisi ya Nyamongo ndiyo maana hujui kwanini vifo vinatokea kule.