Mazindu Msambule
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 7,508
- 6,891
Hahahaa unajua nini Komredi?
Niliposikia huyo trafiki kamng’ata jamaa nilicheka sana.
Nikajisemea tu mwenyewe hapa...hao trafiki walikuwa wapo watatu na wote wanamchangia, Sasa kwa nini huyo mmoja amng’ate huyo dreva?
Yaani jibaba zima unamng’ata mwanaume mwenzio?
Kumbe hata wanaume wa mikoani si chochote!
Kazi kuwananga wanaume wa Dar ilhali wao ndo bure kabisa.
Huwezi jua, labda huyo Shuarezi (mng'ataji ) kahamishiwa mkoani kutoka Dar, halafu we mzee wa Laptop mbona humsifii huyo dereva wa FUSO alivyo wapeleka mchakamchaka hao wauza bucha hadi wakakimbia wote; wanaume wa mikoani hatutakagi UJINGA, sisi asubuhi breakfast yetu ni UGALI dona, mchana hivyo hivyo halafu jioni ndio huo wali wenu wa kwa mama shadya wako.Tena wanaume wa mikoani wenye mamlaka na silaha.... wanamng'ata mwanaume mwenzao.... Acha niendelee kula biriani la Magomeni kwa bi Shadya
Lakini police wajue pia Mungu yupo, nimesikiliza HOJA zao za kumkamata huyo dereva ukweli wanatia HASIRA sana, video tumeiona wote halafu eti wao lawama zote kwa dereva, kweli Mungu yupo mbali sana aise. Matendo ya police dhidi ya raia yanazidi kuwatengenezea chuki tu; tukumbuke lile sakata la trafiki kukamata madereva waliokua wanaendelea na safari kwenye zebra bila kuwasha taa za hazards (wakati kimsingi sio sharia, walijitungia tu na sasa hivi wameacha ) dereva mmoja wa semi aliziba njia Dodoma so kukawa hakuna magari yanayo kwenda wala kurudi, baadae walimuachia aendelee na safari. Nadhani serikali ingeachana na utaratibu wa kutegemea makosa ya barabarani kama revenue