Hii ya leo kali sana sana

Hii ya leo kali sana sana

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
372,654
Reaction score
863,518
Trafiki kajichanganya kachukua ufunguo wa gari la raia kachafukwa kamuweka chini maeneo ya lugalo
IMG-20260908-WA0030.jpg
IMG-20260908-WA0031.jpg

Ndugu zangu;
Kila mtu anafahamu wazi,

Kwamba, Askari waliopewa mamlaka za kusimamia sheria za usalama barabarani ni Trafiki police!

Lakini zipo changamoto nyingi sana katika baadhi ya maaskari wa usalama barabarani!

Mfano: Askari Andrew aliyehusika na tukio la kupigana na dereva (Conrad A. Kayoza mkazi lugalo-JWTZ)
Pamoja na mamlaka aliyonayo kisheria kama trafiki lakini huyu bwana ANDREW Huwa hana weledi katika majukumu yake!

Huyu andrew anatabia hata kutoa lugha za matusi kwa dereva ( Mfano; wee msenge nimekwambia nipe leseni yako) .

Shida nyingine ambayo Andrew aliyonayo huwa akishika leseni anaweza kukuandikia makosa kwa lazima au kukupotezea muda makusudi,
Kibaya zaidi Trafiki huyu anatabia za kuchomoa funguo kwa nguvu huku akitoa lugha chafu!

Ni kweli tunatambua Trafiki anayo mamlaka ya kisheria lakini hana mamlaka ya kutumia lugha chafu na kutweza utu wa watu kwa maneno tena wakati mwingine unatukanwa mbele ya mzazi au mke. Inaumiza sana na kutia hasira kwa wasioweza kujizuia

Tunaomba sana watu wote tuzingatie sheria lakini Askari wa usalama barabarani waelekezwe weledi katika kutekeleza majukumu yao pasipo kutweza utu wa mtu!

BAADHI YA TRAFIKI HAWANA WELEDI WANAZALILISHA SANA MADEREVA BILA WELEDI NA KUZINGATIA KANUNI
 
Atapata shida nyingi sana huyo Jamaa, Huo sio utaratibu, naona mnamsifia, huko aliko atakuwa anajua!

Wanasema alishambuliwa na wananchi, watakuwa wamemuivisha vizuri sana anachecheme huko Maabusu!

Update:

#HABARI Jeshi la Polisi Dar es Salaam linamshikilia Conrad Agonza Kayoza, mwenye umri wa miaka 35, kwa tuhuma za kumshambulia kwa ngumi na mateke askari wa Usalama Barabarani aliyekuwa akitekeleza majukumu yake eneo la Lugalo, Kinondoni.

Tukio hilo limetokea leo Septemba 8, 2026, majira ya saa 1:30 asubuhi katika Barabara ya Bagamoyo, ambapo Askari Polisi namba F.8886 SGT Andrew aliwaelekeza madereva kutotumia Service Road nje ya utaratibu, ikiwemo gari aina ya Toyota Runx lenye namba T 455 EER.

Polisi imesema baada ya kusimamishwa, Conrad alishuka kwenye gari na kuanza kumshambulia askari huyo. Baadaye mtuhumiwa naye alishambuliwa na wananchi waliokuwa eneo hilo, kabla ya kupelekwa hospitalini kwa matibabu.

Jeshi la Polisi limesema mtuhumiwa atahojiwa kwa kina baada ya kupata nafuu ili hatua za kisheria zichukuliwe, huku likitoa onyo kali kuwa halitasita kuchukua hatua dhidi ya mtu au kundi lolote litakalowashambulia askari wakati wakitekeleza majukumu yao.
#EastAfricaTv #TogetherTunawakilisha
 
Back
Top Bottom