LIKUD
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 19,899
- 37,699
Habari za Usubuhi wana ndugu ni tumaini langu kuwa ni wazima wa Afya na wale ndugu zetu wagonjwa tunawaombea kwa M/Mungu awapatie Shifaa
Kuna habari imeenea sana sasa hivi kwenye vyombo vya habari kuusu sakata la Matrafiki watatu kupigana na Dereva wa Fuso huko Tunduma mkoani Songwe.
Siku ya Jana watu Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ( LHRC) jijini Dar es salam kilitoa tamko la kulaani tukio la Trafiki watatu kutumia nguvu kubwa kupambana na dereva huyo.
Aidha tukio hilo limedaiwa kuwa ni kinyume cha sheria ya kanuni ya adhabu sura 16 ,Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20 na Sheria ya Jeshi la Polisi na huduma saidizi sura ya 322 kama ilivyoelezwa ktk tamko hilo lilotolewa na watu wa haki za Binadamu.
Binafsi nilichotaka kujuzwa na watu wa Sheria regardless kwamba Polisi au Dereva ndiye aliyekuwa na Makosa, Je kitendo cha Trafiki Kumng'ata Dereva na kumsabishia maumivu makali na kumuachia Kovu la Kudumu dereva huyo kisheria jambo hili likoje? Je nisahihi ?
Naomba mnijuze wataalamu !!!View attachment 994710View attachment 994709
Sent using Jamii Forums mobile app
Watz na elimu ya ukimwi tupo nyuma sana .Yani unamngata kabisa mtu. Kama ana ngoma?