PICHA: Jeraha la dereva aliyeng'atwa na trafiki

PICHA: Jeraha la dereva aliyeng'atwa na trafiki

Habari za Usubuhi wana ndugu ni tumaini langu kuwa ni wazima wa Afya na wale ndugu zetu wagonjwa tunawaombea kwa M/Mungu awapatie Shifaa

Kuna habari imeenea sana sasa hivi kwenye vyombo vya habari kuusu sakata la Matrafiki watatu kupigana na Dereva wa Fuso huko Tunduma mkoani Songwe.

Siku ya Jana watu Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ( LHRC) jijini Dar es salam kilitoa tamko la kulaani tukio la Trafiki watatu kutumia nguvu kubwa kupambana na dereva huyo.

Aidha tukio hilo limedaiwa kuwa ni kinyume cha sheria ya kanuni ya adhabu sura 16 ,Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 20 na Sheria ya Jeshi la Polisi na huduma saidizi sura ya 322 kama ilivyoelezwa ktk tamko hilo lilotolewa na watu wa haki za Binadamu.

Binafsi nilichotaka kujuzwa na watu wa Sheria regardless kwamba Polisi au Dereva ndiye aliyekuwa na Makosa, Je kitendo cha Trafiki Kumng'ata Dereva na kumsabishia maumivu makali na kumuachia Kovu la Kudumu dereva huyo kisheria jambo hili likoje? Je nisahihi ?

Naomba mnijuze wataalamu !!!
FB_IMG_1547528527861.jpg
View attachment 994709

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Traffic Wa bongo wanasomea mafunzo aliyopitia Louis Suarez na Mike Iron Tyson.
Shule imekushinda na ngumi zimekushinda, yaaani ulishindwa kupigana kiume uokote hata jiwe au tofali ukaamua kupigana kimama-mama kwa kuuma.
Aibu kubwa sana kwa Polisi Wa New York
Jamaa naye alikuwa na mkono mzima kawachezesha vitasa vya kutosha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni aibu sana kwa askari kumng'ata raia. Ndio yale tunasifia makomandoo wetu kupiga ngumi matofali... Afu tunatamba wanajeshi wetu wako imara.

Dunia ya sasa unawezaje kujisifia kupiga ngumi tofali? Mbeba box komredi Nyani Ngabu nifanyie mpango wa makaratasi nami nije kubeba box. Ulevi wa mavumbi sio ishu wallah
 
Ni aibu sana kwa askari kumng'ata raia. Ndio yale tunasifia makomandoo wetu kupiga ngumi matofali... Afu tunatamba wanajeshi wetu wako imara.

Dunia ya sasa unawezaje kujisifia kupiga ngumi tofali? Mbeba box komredi Nyani Ngabu nifanyie mpango wa makaratasi nami nije kubeba box. Ulevi wa mavumbi sio ishu wallah

Hahahaa unajua nini Komredi?

Niliposikia huyo trafiki kamng’ata jamaa nilicheka sana.

Nikajisemea tu mwenyewe hapa...hao trafiki walikuwa wapo watatu na wote wanamchangia, Sasa kwa nini huyo mmoja amng’ate huyo dreva?

Yaani jibaba zima unamng’ata mwanaume mwenzio?

Kumbe hata wanaume wa mikoani si chochote!

Kazi kuwananga wanaume wa Dar ilhali wao ndo bure kabisa.
 
Hahahaa unajua nini Komredi?

Niliposikia huyo trafiki kamng’ata jamaa nilicheka sana.

Nikajisemea tu mwenyewe hapa...hao trafiki walikuwa wapo watatu na wote wanamchangia, Sasa kwa nini huyo mmoja amng’ate huyo dreva?

Yaani jibaba zima unamng’ata mwanaume mwenzio?

Kumbe hata wanaume wa mikoani si chochote!

Kazi kuwananga wanaume wa Dar ilhali wao ndo bure kabisa.
Tena wanaume wa mikoani wenye mamlaka na silaha.... wanamng'ata mwanaume mwenzao.... Acha niendelee kula biriani la Magomeni kwa bi Shadya
 
Back
Top Bottom