Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nchi inahitaji mapinduzi...Mapinduzi ya kwanza ambayo yame bear hata jina la chama ni hayo ya Zanzibar!

Na huo ndio unafiki wa Mwalimu uliomsababisha asiuwawe kama kina Nkrumah na Lumumba...Alikubaliana na ukweli kuwa Sultan atarudi hapo Zenji na unajuwa tena mvutano wa kidini kati ya mwarabu na mzungu especially miaka ya 60 ambapo hata hapa USA makanisa ya kiinjili kama assemblies of God yalikuwa yalipamba moto huku watu kama kina Billy Graham wakiandaa mikutano mikubwa Afrika ambayo waliita CRUSADES!

CRUSADES ni neno lililokuwa likitumika kama vile hawa mujahidina wa waislam ambao pia walifanya mauwaji miaka ya nyuma wakati wa vita ya wakristo na waislam.

Lakini dunia imebadilika...NI LAZIMA BINADAMU WOTE WAISHI KWA UMOJA NA KUHESHIMIANA NA DHULMA IWE MWIKO!

Sasa tunataka mapinduzi mapya...Ya kimaendeleo.
Hivyo kwa mtizamo wangu...Marais wote hao waliopita bado walikuwa wakifanya kazi kwenye mazingira magumu na unafiki wao ndio unaendelea kuwaponya kwa kujidai ni washirika wa west na huku chini chini wakiwa na masoshalisti.

Na sasa hata JK si ni yale yale ya mwalimu wanaendeleza karata?

Sasa naona mwisho umefika wa kuendelea kuitumia karata ya zenji kinafki kwa kigezo cha mapinduzi ya kutomtaka mwarabu na wakati mwarabu mwenyewe yuko hadi chumbani.

Hatuwezi kuendelea kuyalinda mapinduzi yaliyopitwa na wakati...Ni muda wa kufanya mapinduzi ya kuzilinda rsilimali zetu amabazo ziko kama hazina mwenyewe mara baada ya kuingia kwenye globalization na viongozi hao wote watalaumiwa kwa kutowatayarisha wananchi na kuwapa elimu.

Kama kweli wangekuwa wazalendo...Wangehakikisha hata wanapanda dala dala ili watoto waende shule...Ndio uzalendo huo...Na si kujenga tabaka la mamluki wa kikoloni kwa kuendelea kusomeshana na kurithishana madaraka na huku wananchi wenye mali wakifa!

Kuendesha mashangingi ya hali ya juu yenye ghrama za utunzanji ambazo labda ni sawa na gharama za kuanzisha shule ama hospitali!

Utaratibu wa kuwahudumia mawaziri na kuwajazia mibia na minyama ya groceries shoppings kwa gharama za wananchi wasiojiweza hata kwa mlo mmoja!

Kama kweli tunataka kulikomboa Taifa...Basi tuwajengee viongozi mazingira ya kuwatumikia wananchi na si wananchi kuwatumikia viongozi...Serikali kuwatumikia wananchi na si the other way round.

Kama viongozi wanapita huku na huko na kusema sisi ni masikini...Basi waonyeshe na mfano kuwa sisi ni kweli masikini!

Wananchi wakiandamana kwenda kwenye hayo mahekalu yenu nyie viogogo na kuomba chumvi,sabuni,mafuta na chakula mtawaambia nini?

Maana mkibisha si na wao watagoma kulipa kodi?

WALIPE KODI KWA KIPI MNACHOWAFANYIA NA WAKATI NCHI MNAUZA?

TIME FOR CHANGE IS NOW!
 
Mkuu hapa naona sasa unataka kutupeleka Mtaroni, Mwinyi alikuwepo na anaonekana sio bora kwasababu alipata madaraka kwa ubabe wake kwa Nyerere ndio maana huwezi kuona mazuri yake hali kadhalika Kikwete sasa hivi anachokifanya ni kurekebisha na kushinda na Majini ambayo yalipandwa kipindi cha Che Nkapa na the all issues of UFISADI.

Sikatai kwamba kila mmoja anamapungufu ila sasa sio kihivyo kama ulivyowaacha hao wengine unless kuna thread unazitetea au unajaribu kutafuta Uzani .
Kuntakinte aka Eddy,
Hii habari usiisome kijuu juu. Point imejificha ndani. Point hapa ni kuwa Mwinyi alimonaliza kipindi cha pili, alitaka kuongeza cha TATU na hapo Nyerere akaja na kumpasha. Alimchambua na kutoka siku hiyo amayo NYERERE alihutubia, uandishi wa habari ulipata UHURU MKUBWA SANA. Kumbuka hata Nyerere kile kitabu chake wakati wa MWinyi alishindwa kukichapisha Tz na kukipeleka Zimbabwe kichapishwe. Hivyo si kweli kama alivyosema mmoja kuwa UHURU wa vyombo wa habari alileta Mwinyi ila ni NYERERE. Kutoka siku hiyo hata yeye akawa analimwa. Ila naona alikuwa anafurahi kuwa kama MWalimu somo lake limeeleweka.
Kikwete yeye hana maneno kabisa. Kipindi chake kimoja huyooo anaenda zake Msoga. HATAKI KUNG'ANG'ANIA MADARAKA kama Mwinyi. Hili ndilo Kikwete kamzidi Mwinyi. Hivyo 2010 tuanze kutafuta Rais Mpya na FRESH.
 
Kuntakinte aka Eddy,
Hii habari usiisome kijuu juu. Point imejificha ndani. Point hapa ni kuwa Mwinyi alimonaliza kipindi cha pili, alitaka kuongeza cha TATU na hapo Nyerere akaja na kumpasha. Alimchambua na kutoka siku hiyo amayo NYERERE alihutubia, uandishi wa habari ulipata UHURU MKUBWA SANA. Kumbuka hata Nyerere kile kitabu chake wakati wa MWinyi alishindwa kukichapisha Tz na kukipeleka Zimbabwe kichapishwe. Hivyo si kweli kama alivyosema mmoja kuwa UHURU wa vyombo wa habari alileta Mwinyi ila ni NYERERE. Kutoka siku hiyo hata yeye akawa analimwa. Ila naona alikuwa anafurahi kuwa kama MWalimu somo lake limeeleweka.
Kikwete yeye hana maneno kabisa. Kipindi chake kimoja huyooo anaenda zake Msoga. HATAKI KUNG'ANG'ANIA MADARAKA kama Mwinyi. Hili ndilo Kikwete kamzidi Mwinyi. Hivyo 2010 tuanze kutafuta Rais Mpya na FRESH.

Kama kweli JK ataondoka hiyo 2010 basi si kwa kupenda bali kwa kujua kwamba hana uwezo wa kuiongoza Tanzania na CCM wamtolee uvivu na kumwambia bila kumuonea aibu kwamba kila la heri bye bye!!!, lakini ukiandika kutaka kuonyesha kwamba JK atakuwa anaondoka kwa mapenzi yake mwenyewe ni kuwapotosha watu. Hawezi kumdanganya yeyote kwamba aliingia Ikulu ili akae kwa awamu moja tu.
 
Sasa tofauti ya MWINYI na KIKWETE ni kuwa Kikwete hana UCHU wa madaraka kwa muda mrefu kuwa Rais wetu. Kaona mambo yanamshinda na yamekuwa magumu. Sasa hivi anavuta zake za mwishomwisho na ikifika mwaka 2010 anajiendea zake Msoga na kula za Uzeeni. Hekalu lake kweli zuri na hadi kwenye GOOGLE EARTH unaliona.

Mwaka 2010 unakaribia. Tuanze kufikiri tutamuenzi vipi Kikwete kwa busara zake za kutoendelea na madaraka na kupisha wengine waje wapambane na UFISADI, Mauwaji ya Albino, tatizo la umeme, maji, maisha bora kwa Watanzania, usafiri hasa kwa wanafunzi mijini, nk. Yeye atakuwa Rais wa Pili baada ya Mandela kwa kufanya term 1 na kupisha wengine. Bravo Kikwete.

Sikonge,

Unaota au huu ni uchokozi tu?
 
JK ndo kwanza katimiza nusu ya kwanza ya utawala wake wa awamu ya kwanza.....na hayo yaliyopita hayana mfano...unataka kumfananisha na Mwinyi?

au ujumbe ulikuwa kwa njia ya siri kuwa kikwete asigombee awamu ya pili?
 
Wajameni,
Si dalili zote zinaonyesha kuwa jamaa HATAGOMBEA TENA? Ni Kiongozi gani atafanya mambo kiasi hicho akijua tena kuna second term na upinzani mkali? Au ndiyo siasa za MAFIA za kusubiri LAST TIME afanye MAPINDUZI makali Tanzania na watu wote tumsujudie na kuja kumkumbuka milele kuwa alipigana na UFISADI? Kwangu mie hadi leo hii anajitahidi sana kujijengea nyumba yake MSOGA na kwa speed kali akijua imebaki miaka miwili akapumzike huko. Hata mie kama nisingelikuwa na uwezo na kubebwa walau kwa term moja na baada ya hapo (huku nikiwa sijafanya zuri wala baya yaani sikufanya kitu) ninajiendea kijijini Sikonge kupumzika, ingelikuwa poa sana. Hata wewe unayebisha ungeliKUBALI. Ila Rais wa hivi sidhani kama ni MZURI. Heri awe MBAYA au MZURI SANA na hapo tutajua moja. Mkapa walau tunajua ni FISADI. Kikwete hana baya wala zuri.
 
Hakuna fisadi kushinda Mwinyi hivi waTanzania mnasahau hata methali zetu za kiswahili ,hamuioni ile methali ya Simbwa mwenda kimya ,huyu kama mnaweza kumfuatilia pengine akamshinda Chenge ,watu wengine wanajua kuficha.
Halafu jamaa roho yake mbaya sana huyu ndie aliesimamia zoezi la kupeleka majeshi Unguja ili CCM ishinde kwa nguvu za dola,huyu ni was a dictator to be na mtazameni hadi hii leo bado yupo nyuma nyuma na kila kwenye matatizo utamuona yupo mbelembele ni mnafiki nambari one.
 
Legacy ya Mwinyi
1: kuongoza nchi kutoka ujamaa(tuliodumu nao takriban kwa miaka 25 ) kuingia ubepari
2:kufungua uhuru wa vyombo vya habari (kumbuka wakati huo magazeti yalianza kujitutumua,Mwinyi mwenyewe alikuwa victim wa uhuru mpya)
2:Kuruhusu soko huria na kuwafanya wanachi wawe na wide choice ya bidhaa mbali mbali(bidhaa kama tv, nguo, redio kali, n.k vikaanza kupatikana kwa urahisi zaidi)
3:kupanuka kwa uhuru wa kisiasa (vyama vingi vilirejeshwa, na watu kama Mtikila wakang'ara sana).


JK bado ana Muda, anaweza kurekebisha makosa yake na akajihakikishia nafasi yake katika historia ya Tanzania


Kumbuka soko lilishaanza kufunguliwa hata kabla ya Mwinyi. Nafikiri CCM walishasalimu amri. Kama unakumbuka SAS wakati ule alikuwa waziri mkuu na umaarufu wake ulitokana na hili la kufungua mipaka. Kama unakumbuka mtumba ndiyo ikamwagwa bongo.

Anyway, bora Mwinyi kuliko Kiwete sorry I meant Kikwete!!!!!
 
Gamba la Nyoka
Unataka apewe muda zaidi mpaka lini, akipewa muda zaidi what different will it make. Sasa hivi ameonesha kuwa hakuna lolote alilofanya hata mafisadi anawaogopa, kwanini apewe muda zaidi? Muda amekuwa nao toka alipoingia madarakani, what more time is it that you are talking about. Muda zaidi maana yake more wastage of time.
 
Kile kifimbo kuna wakati kilinadiwa na kuuzwa kwenye fund raising moja hivi, sikumbuki vizuri nani alikinunua, lakini baadae kada maarufu Mustafa Jaffer Sabodo akaamua kukinunua tena toka kwa huyo mtu na kumrudishia Mwalimu. Nadhani sasa kiko mahali fulani huko kwenye Makumbusho ya mwalimu. Angekuwa kabila letu, sisi mzee kama huyo akifariki ile fimbo yake inakabidhiwa kwa mwanae mkubwa wa kiume, ndio symbol ya authority juu ya nduguze.


Mama Maria alisema kwa sababu watu wamekuwa wakitoa madai kuwa kifimbo hicho kina nguvu, wamekichukua (japo suti na vitu vingine vimebaki huko Makumbusho) na sasa kinatunzwa na mmoja wa wana familia (hakutaka kumtaja).



.
 
Nakubaliana na lazydog. Mama maria nyerere aliwahi kuhojiwa na TBC (TVT wakati huo) miaka ya nyuma kuhusu mambo mengi ya Mumewe na kuhusu kifimbo alisema kinatunzwa na ndugu mmoja wa ukoo bila kumtaja ni nani.

story hizi nami pia nilizisikia sana nilipokuwa mdogo na tulimwona mwalimu kama mtu mwenye nguvu kubwa (divine powers). kama kuna mtu wa kuthibitisha haya atuthibithie ili tujue kama ni ukweli au porojo tu.

mtu mmoja akasema kwamba wakati huo kama wewe ni kiongozi wa serikali na ukaenda kinyume na mwalimu then akikuita ofisini lazima utajiuzuru tu maana macho yake yalikuwa yanazunguka zunguka kama ya kinyonga !

ila ushirikina upo maana ipo hotuba yake moja mwalimu alielezea jinsi wazee walivyokuwa wakimsaidia wakati wa kugombea uhuru.

anyway yaweza kuwa porojo au ukweli.
 
Si kweli. Got it from a reliable person who was close to him most of the time.
 
Nakumbuka mama Maria Nyerere alihojiwa wakati fulani kuhusu kifimbo hicho.Alisema kwamba, ni fimbo ya kawaida, isipokuwa kama ina nguvu zozote za ziada, hana uhakika,na akaongeza kwamba mpaka wakati alipohojiwa, ambapo ilikuwa sometimes last year, kilikuwa hakijagawiwa kwa mtu yeyote katika ukoo,ingawa wana mpango wa kumkabidhi mmoja wa viongozi wa ukoo.
 
Naona unataka kuifufua kama ulivyofufua Mwembechai. Go ahead, wachangiaji tupo.
 
Mswahili anaandika:



Je statistics hizi ni za kweli? yaani by implication ina maana mwaka 1985 80% ya watz walikuwa waislamu?

Please educate me...

Prince,

Kwenye miaka ya 70 kuna harakati ilianza Mlimani ya kuchambua waislamu wanavyokandamizwa hapa Tanzania wakati wao ndio wengi. Hili vuguvugu liliongozwa na Prof. moja wa Hesabu (namsahau jina) kutoka Pakistani na ililenga kuliamsha jamii ya kiislamu dhidi ya ubaguzi dhidi yao katika nyanja mbalimbali. Kuna hata data zilitolewa kuonyesha jinsi pamoja na wingi wao nchini, nafasi kwenye utawala na elimu zilikuwa zinatolewa kwa upendeleo dhidi yao. Hata hivyo hayo mambo yaliweza kutulizwa haraka kwa kuwa tulikuwa na serikali makini na iliyojali.

Hata hivyo mwanzoni mwa utawala wa Mwinyi, hayo mambo yaliweza kuibuka tena kwa kasi na kwa kuwa tulikuwa na serikali lege lege na iliyolala, yaliachwa hivyo hivyo. Kuna kundi likiongozwa na Shekh Yahya Hussein lilikuja na data zilizoonyesha kuwa zaidi ya asilimia 75 ya watanzania ni Waislamu. Nakumbuka toleo moja la gazeti la mfanyakazi iliweza kuripoti habari hii lakini hakuna hatua zozote zilichukuliwa na kuna wakati mapendekezo kadhaa ati ya kuwainua yaliibuka yakiambatana na mihadhara.

Hii inanikumbusha sana mambo ya Uganda. Pamoja na kuwa asilimia 70 ya Waganda ni Wakatoliki, asilimia 20 ni Wakristo wa madhehebu mengine na Waislamu ni chini ya asilimia 5, iliwahi kuelezwa wakati wa utawala wa Idi Amin (Muislamu) kuwa waislamu ni zaidi ya nusu ya Waganda wote. Ilifikia wakati Wapalestina na Walibya walipigana bega kwa bega na jeshi la Amin dhidi ya Tanzania kwa kuitetea nchi ya Waislamu wenzao (Uganda).

Kwa mawazo ya Waislamu waishio Zanzibar na mikoa ya Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Lindi na Mtwara asilimia ya kubwa ya Watanzania wote ni Waislamu, period. Kwenye hili utakuwa na kazi kubwa ya kuwafanya waamini vinginevyo kwani hii ndiyo picha halisi ilio nayo pia nchi nyingi za Kiislamu.
 
Back
Top Bottom