Nimeonelea niwarahisishie kazi na kufungua hii thread maalum ili tuzungumzie Ubaya wa Nyerere na Ukatili wake!
Kwa kuwa siku zote nimekuwa namfagilia Nyerere pamoja na mapungufu yake, safari hii nitawasaidia mpate ukumbi maalum kuyatoa mliyonayo moyoni ambayo hamuyapendi kuhusu Nyerere.
Nayajua mafupi ambayo nimewahi kuyaona na kubainisha hadharani katika hoja mbali mbali na nitayaweka hapa kama kianzio na kuwapa ukumbi mje mtupe Dataz zaidi ili Ukweli mwingine tusioujua uje machoni mwetu.
- Nyerere alituletea Umasikini kwa Ujamaa wake
- Nyerere alizembea maisha ya watu waliokufa kwa kuburuzwa kutokana an sera ya vijiji vya ujamaa
- Nyerere aliweka watu kizuizini bila makosa
- Nyerere alikuwa haambiliki
- Nyerere alikuwa anachukia Waislamu na usilamu
- Nyerere kwa aibu alienda na kufia Ulaya na si hospitali za Tanzania
- Nyerere alikuwa mkabila
- Nyerere alikuwa na upendeleo
Nawaombeni ongezeeni mengine basi ili tuendelee kujua mabaya ya Rais wetu wa Kwanza!