Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

mzee hayo yanayosemwa humo.. binafsi mengine sikujua yamewahi kutokea... how did he do it.. against such odds..?
 
Mwanakijiji,

..katika interview yako na Dr.Salim Salim ulipoteza nafasi nzuri ya kumuuliza sababu zilizopelekea Mwalimu kuvuruga uchumi kiasi kile?

..ulipaswa kumuuliza hasara tuliyoipata kwa zoezi la vijiji vya ujamaa, na kuvunja vyama vya ushirika.

..pia ungeuliza hasara ya kutaifisha mashamba ya mkonge.


NB:

..uchumi wetu haukuyumba sana kutokana na oil crisis ya miaka ya 70 kwasababu wakati huo kulikuwa na bei nzuri sana ya kahawa.

..actually hilo lilimdanganya Mwalimu akafikiri kwamba uchumi wake ni imara.
 
Ole Ndaskoi said:
Mwalimu Julius Nyerere, it is said, told his wife to keep herself out, far away from politics.


Ole Ndaskoi said:
In an apparent reference to President Mwinyi himself, Nyerere told the journalists that Tanzanians needed a leader who will defend and promote the national constitution. 'It can't be a person that gets advice from his wife, and tomorrow we see some decision has been made. You can't have such a guy. You won't know what his wife will advise him,' Nyerere said amid applause from more than 100 journalists attending the gathering. His boldness speaks volumes. He made sure that Tanzanians got rid Mwinyi.

..sasa mimi hapo naona contradictions kidogo.

..Mwalimu hakutaka Mama Maria ajihusishe na siasa, lakini anageuka na kumhusisha mke wa a sitting President ktk masuala ya kisiasa.

..Mimi nadhani hicho hakikuwa kitu cha kiungwana hata kidogo.

.. Kilikuwa ni kitendo cha kumuonea Raisi Mwinyi na mkewe Mama Sitti.

..Labda niulize: Mwalimu aliyapata wapi mazungumzo kati ya Mzee Mwinyi na mkewe?

..KITU CHA AJABU KABISA MWANDISHI WA MAKALA ANASEMA MWALIMU "ALISHANGILIWA" KWA KAULI YAKE HIYO!!!

NB:

..Mwandishi amejenga hoja dhidi ya Mkapa, lakini at the end ana-conclude kwamba tumburuze mahakamani Frederick Sumaye!! Kaaz kweli!!
 
I like this thread! Soo deep, ahsanteni wakuu 🙂 !!

SteveD,

Hii ni kwa sababu wale mchafua mada mkuu Mwafrika wa kike na mwenzake KadaMpinzani hawako hapa kuharibu mada. Ustaarabu muda mwingine hupotea wale wakiingia hapa JF
 
SteveD,

Hii ni kwa sababu wale mchafua mada mkuu Mwafrika wa kike na mwenzake KadaMpinzani hawako hapa kuharibu mada. Ustaarabu muda mwingine hupotea wale wakiingia hapa JF

Mambo mengine bwana?

Wewe nimekuambia kila mara hapa kuwa uache kunifuatafuata na wala hutaki kusikia. Kila mara unapenda sana kunifuatilia na kuniita majina mara mtoto mara kuwa naharibu mada.

Mimi nachangia mada chache sana hapa JF, mada nyingi naziacha tu zinapita (kama nilivyokuwa nimeiacha hii). Kwa hakika ninapost wastani wa post 10 tu kwa siku wakati kuna mamia na maelfu ya post zinazowekwa hapa JF kwa siku moja.

Hizo mada zingine zote zinazoharibika ni nani anayeziharibu? Tafadhali sana kwa mara nyingine nakuasa uachane na mimi na ukae mbali kabisa na mimi kwa sababu hauna idea hata kidogo kwa nini niko hapa JF na kwa nini ninaandika the way I do.

Stay away from me na hii ni onyo nimekupa kwa mara ya mwisho.

Asante!
 
Mambo mengine bwana?

Wewe nimekuambia kila mara hapa kuwa uache kunifuatafuata na wala hutaki kusikia. Kila mara unapenda sana kunifuatilia na kuniita majina mara mtoto mara kuwa naharibu mada.

Mimi nachangia mada chache sana hapa JF, mada nyingi naziacha tu zinapita (kama nilivyokuwa nimeiacha hii). Kwa hakika ninapost wastani wa post 10 tu kwa siku wakati kuna mamia na maelfu ya post zinazowekwa hapa JF kwa siku moja.

Hizo mada zingine zote zinazoharibika ni nani anayeziharibu? Tafadhali sana kwa mara nyingine nakuasa uachane na mimi na ukae mbali kabisa na mimi kwa sababu hauna idea hata kidogo kwa nini niko hapa JF na kwa nini ninaandika the way I do.

Stay away from me na hii ni onyo nimekupa kwa mara ya mwisho.

Asante!

Vitisho vya nini tena mama? Utanifanya nini kwani?

Yaani we hutajwi tu hapa JF? Nilidhani uko off weekend? Wewe huoni kuwa bila wewe hapa hii thread ilikuwa inaenda vizuri?

Acha utoto na ukue na huu ni ushauri tu.
 
Vitisho vya nini tena mama? Utanifanya nini kwani?

Yaani we hutajwi tu hapa JF? Nilidhani uko off weekend? Wewe huoni kuwa bila wewe hapa hii thread ilikuwa inaenda vizuri?

Acha utoto na ukue na huu ni ushauri tu.

Mimi nimekuambia tu uachane na mimi. Hayo mengine ya ninajua vipi na kuja hapa si business yako.

Asante!
 
I like this thread! Soo deep, ahsanteni wakuu 🙂 !!

Me too!

Nafikiri hii topic has to be repeated in many different ways...ili kuamshana! Ingawa I am too technical kwenye vitu kama hivi..ngoja nituliee nifuatie kwa utizamaji ..hoping I will get gap to drop a pont!! Oherwise... Its a goo thread!!
 
Nyerere ni "Intellectual giant" (siyo 'alikuwa..', bali anaendelea kuwa) Ni mtu aliyeweza kutofautisha miti na msitu. alikuwa si mbinafsi, alikuwa mkweli. Tatizo moja kubwa la Nyerere ni kwamba alikuwa anaona mbali mno, ambapo wengi wetu tunaona karibu tu, hata hatuwezi kufiria mbali. yaani kama ni asubuhi, sana sana tunaweza kufikiria mpaka saa sita tu, jioni hatuoni, kesho ndio kabisaa usiku wa giza.

Mazingira ya utawala wake, nchi ilivyokuwa alivyoanza nayo, na choice ya mambo aliyoamua kuyafanya, inamweka katika class ya aina yake. kiongozi anakuwa na priorities kwa wakati wake. wakati ule priority kubwa ilikuwa kujenga taifa na utaifa. kuna choice zingine mfano sheria ya ardhi iliyopendekezwa na wakoloni wa kiingereza, na TANU ikaikataa, Kenya wakaipitisha, leo hii ndio moja ya sababu inafanya Kenya wanachinjana.

Mtu asiyekuwa na mtazamo mpana huangalia tu vitu ambavyo hana. mwenye busara huangalia vyote: alivyo navyo na asivyokuwa navyo. wakati mwingine mtu anahitaji kutafakari zaidi, hata akisafiri huko nchi za nje. katika kuzunguka nchi mbalimbali, nimeshuhudia watu fukara wa kutupa, aina ya fukara ambaye Tanzania haiwezekani kuwa naye, by definition. Mfano India, ukikutana na ombaomba wa India, huna uhakika kama ataweza kutembea hatua 40 baada ya kuachana na wewe. ombaomba wa Tanzania ni uamuzi na pengine dili tu. Fukara wa nchi kama Kenya hana kitu kabisa, hawezi kwenda mahala akasema afungue shamba, kama walivyofanya vijana wa Bongo walipoamua wanakwenda kulima mpunga Ruvu. hilo nchi nyingine haliwezekani!

Falsafa ya Nyerere ililenga maendeleo ya watu, na ndio maana hata mifumo yake ya elimu ililenga kunufaisha wengi zaidi. lakini pia alijua umuhimu wa elimu ya juu ndio maana TANU ilihusika sana na uanzishwaji wa chuo kikuu. kwa hawa wachache aliwakumbusha kwamba ni waliokabidhiwa chakula ili wakatafute chakula cha kijiji chote. Leo hapa sie tunaoongea humu JF, tunafanya nini kuhakikisha tunarejesha chakula kwa wakulima masikini ambao kwa kukatwa kodi lukuki katika mazao yao, tumenufaika kuelimika? Na wengi wetu tunapozungumzia maendeleo, tunazungumzia majengo marefu, huduma bora mijini, matajiri wachache, na wengine walie tu.

Kumkosoa Nyerere inabidi ujiandae hasa. kwanza ujilinganishe naye katika uwezo wa kuona, uone vizuri kama yeye. kama huoni vizuri mbele, utamkosoaje Nyerere? Wengi wanakosoa Azimio la Arusha, ambalo kimsingi lilidai njia kuu za uchumi zimilikiwe na watanzania. kuna ubaya gani hapo? leo tunashuhudia mali zetu zikiliwa kifirauni. mashirika aliyoyajenga Nyerere, kama NBC, yalivyochukuliwa kirahisi tu. mengine kama TANESCO yanafilisiwa kwanza ili yaonekane hayafai, ili wayauze kirahisi. hata kama ni watanzania binafsi katika makampuni au umoja wao wanamiliki njia hizi, spirit ya Azimio la Arusha itakuwa imetekelezwa. lengo ni milki iwe kwa watanzania. sasa wanamiliki vipi, hilo ni utekelezaji, ambapo tungeweza kumodify kidogo tu. lakini leo utasikia mtu anakandia Azimio la Arusha, wakati hata hajalisoma na kulichambua.

Mwisho, tukumbuke pia kwamba Nyerere alikuwa na maadui wengi tena wenye nguvu. walikuwa na hamu ya "prove him wrong", kwamba siasa zake hazitekelezeki. amehujumiwa sana. lakini hujuma kubwa zaidi ni kutoka ndani ya nchi. wasaidizi wake hasa wenye uroho, alikuwa na kazi kubwa sana ya kupambana nao. hivi mfano ukiangalia wachina wanaokwenda nchi za nje, jinsi wanavyohaha kutafuta tekinolojia ya nje kupeleka kwao. wenzetu japo wanamkosoa Mao, wameendeleza ile spirit yake. sisi watanzania wapi, ndio kwanza hatuna mpango na kwetu kabisa.

Kiswahili ni lulu, wengine wanajua na wanaitukuza. jiulize kwa nini pale chuo kikuu sasa hivi kuna projecti nyingi sana za kiswahili, wageni wanajifunza sana lugha yetu. sisi ndio kwanza tumezubaa katika malumbano yasiyo kichwa wala miguu, kuhusu umuhimu wa Kiswahili. Nyerere alijua yote haya na aliwekeza kweli kweli. Tatizo letu kubwa sio umaskini. tatizo hasa ni ufinyu wa mawazo.
 
After reading on what other contributors have said in their opinions I feel I have to join a little bit.

All Nyerere defenders are trying to exempt him from the blame in which he has caused in Tanzania that the present social, economical and political problems especially in Zanzibar are the results of Nyerere's ideas of socilism but with heavily relience in foreign aid.

This relience of foreign aid has led to the stagnant development in our country and it doesn't look is going to make any better in near future.

If there is anyone who knows Mr Robert Mc Namara, he was IMF' president in 70s and during that time funds from this institution were heavily directed to Tanzania because of friendship between Nyerere and Mc Namara, even when it was known that Nyerere was a friend also to Eastern Block during the Cold War.

So first of all here it shows Nyerere' ambiguity in his foreign policy during 1970's.Also during this time Nyerere was not able to listern to people like Edwin Mtei.

When aid policy was changed during 80's Nyerere and his CCM had no alternalive than to follow Western countries's demands, since their entire political outlook had always been one of accepting Africa's subordination to Western political policies and economic domination.

So here again Nyerere and CCM fails to think how to make Tanzania dependent economically.

Nyerere's limited welfare schemes were always fundamentally a system of patronage, which ensured political and economic benefits for a small elite. Deprived of these benefits, Tanzanian politicians are attempting to preserve their privileged position by carving out for themselves enclaves in which they will control the resources that Western investors want.

Apart from these setbacks, Nyerere has left a huge problem in Zanzibar. After what happened during the elections in Zanzibar in 1995, CCM led by Nyerere has put more cracks which will continue to be there for years to come and until CUF are given there share of leadership, Nyerere' legacy will continue to flourish.

So the only solution is to look very carefully on how to change things including the overhaul of all virsual circle which is dominating our country since independence and replce with one wich will insure all the resources are shared equally by all and for all Tanzanians.
 
Nyerere ni "Intellectual giant" (siyo 'alikuwa..', bali anaendelea kuwa) Ni mtu aliyeweza kutofautisha miti na msitu. alikuwa si mbinafsi, alikuwa mkweli. Tatizo moja kubwa la Nyerere ni kwamba alikuwa anaona mbali mno, ambapo wengi wetu tunaona karibu tu, hata hatuwezi kufiria mbali. yaani kama ni asubuhi, sana sana tunaweza kufikiria mpaka saa sita tu, jioni hatuoni, kesho ndio kabisaa usiku wa giza.

Ukweli huu mzito!!

Mazingira ya utawala wake, nchi ilivyokuwa alivyoanza nayo, na choice ya mambo aliyoamua kuyafanya, inamweka katika class ya aina yake. kiongozi anakuwa na priorities kwa wakati wake. wakati ule priority kubwa ilikuwa kujenga taifa na utaifa.

Watu wangeelewa hili hata baadhi ya ubishi usingekuwepo; mmetoka kwenye Ukoloni, Taifa la makabila 120, katika ulimwengu wa siasa wa miaka 60 na sabini.. ulitakiwa ufanye nini? Kipaumbele!

kuna choice zingine mfano sheria ya ardhi iliyopendekezwa na wakoloni wa kiingereza, na TANU ikaikataa, Kenya wakaipitisha, leo hii ndio moja ya sababu inafanya Kenya wanachinjana.

Wenyewe walitutaka tuwe kama Kenya! Leo tukiwaonesha Kenya wanainamisha vichwa.. Taifa hujengwa halishushwi kama mji wa Yerusalemu uliovishwa kama bibi harusi aliyepambwa kwa vito vya thamani!

Mtu asiyekuwa na mtazamo mpana huangalia tu vitu ambavyo hana.

What a quote! hatukuwa na luninga, hatukuwa na magari mengi, hatukuwa na shule nyingi, hatukuwa na hiki na kile..

mwenye busara huangalia vyote: alivyo navyo na asivyokuwa navyo. wakati mwingine mtu anahitaji kutafakari zaidi, hata akisafiri huko nchi za nje. katika kuzunguka nchi mbalimbali, nimeshuhudia watu fukara wa kutupa, aina ya fukara ambaye Tanzania haiwezekani kuwa naye, by definition. Mfano India, ukikutana na ombaomba wa India, huna uhakika kama ataweza kutembea hatua 40 baada ya kuachana na wewe. ombaomba wa Tanzania ni uamuzi na pengine dili tu. Fukara wa nchi kama Kenya hana kitu kabisa, hawezi kwenda mahala akasema afungue shamba, kama walivyofanya vijana wa Bongo walipoamua wanakwenda kulima mpunga Ruvu. hilo nchi nyingine haliwezekani!

couldn't have said it better!

Falsafa ya Nyerere ililenga maendeleo ya watu, na ndio maana hata mifumo yake ya elimu ililenga kunufaisha wengi zaidi. lakini pia alijua umuhimu wa elimu ya juu ndio maana TANU ilihusika sana na uanzishwaji wa chuo kikuu. kwa hawa wachache aliwakumbusha kwamba ni waliokabidhiwa chakula ili wakatafute chakula cha kijiji chote. Leo hapa sie tunaoongea humu JF, tunafanya nini kuhakikisha tunarejesha chakula kwa wakulima masikini ambao kwa kukatwa kodi lukuki katika mazao yao, tumenufaika kuelimika? Na wengi wetu tunapozungumzia maendeleo, tunazungumzia majengo marefu, huduma bora mijini, matajiri wachache, na wengine walie tu.

Hili la maendeleo ya watu is one of his greatest philosophical contributions in the whole theory of development. Hata haya ya anti-globalization movement kimsingi iko kwenye suala la kutaka maendeleo kwa watu na si vitu! Sisi hatutaki hili tunataka majengo marefu yenye kupendeza.. hata North Korea wanayo! Lakini Cuba hawana mengi lakini nenda kaangalie index ya Human Development wao wako wapi na sisi tuko wapi!

Kumkosoa Nyerere inabidi ujiandae hasa. kwanza ujilinganishe naye katika uwezo wa kuona, uone vizuri kama yeye. kama huoni vizuri mbele, utamkosoaje Nyerere?

Oh snap! (I'm giving a standing ovation here for what an articulation of a reality! simple but very original!)

Wengi wanakosoa Azimio la Arusha, ambalo kimsingi lilidai njia kuu za uchumi zimilikiwe na watanzania. kuna ubaya gani hapo? leo tunashuhudia mali zetu zikiliwa kifirauni. mashirika aliyoyajenga Nyerere, kama NBC, yalivyochukuliwa kirahisi tu. mengine kama TANESCO yanafilisiwa kwanza ili yaonekane hayafai, ili wayauze kirahisi. hata kama ni watanzania binafsi katika makampuni au umoja wao wanamiliki njia hizi, spirit ya Azimio la Arusha itakuwa imetekelezwa. lengo ni milki iwe kwa watanzania. sasa wanamiliki vipi, hilo ni utekelezaji, ambapo tungeweza kumodify kidogo tu. lakini leo utasikia mtu anakandia Azimio la Arusha, wakati hata hajalisoma na kulichambua.

Waulize kwanini tunalia na Buzwagi, Richmond, Tanesco, Posta, n.k ?


Mwisho, tukumbuke pia kwamba Nyerere alikuwa na maadui wengi tena wenye nguvu. walikuwa na hamu ya "prove him wrong", kwamba siasa zake hazitekelezeki. amehujumiwa sana. lakini hujuma kubwa zaidi ni kutoka ndani ya nchi. wasaidizi wake hasa wenye uroho, alikuwa na kazi kubwa sana ya kupambana nao. hivi mfano ukiangalia wachina wanaokwenda nchi za nje, jinsi wanavyohaha kutafuta tekinolojia ya nje kupeleka kwao. wenzetu japo wanamkosoa Mao, wameendeleza ile spirit yake. sisi watanzania wapi, ndio kwanza hatuna mpango na kwetu kabisa.

Naamini moja wapo ya limitations ambazo Nyerere alikumbana nazo ni watu wa kumsaidia. Ukweli ni kuwa hakuwa na wasaidizi wa kuweza kuendesha nchi; hivi alipokuwa mkuu wa nchi ni wakuu wangapi wa mikoa walikuwa wasomi na wakuu wa wilaya? Ni wa ngapi walikuwa na uwezo wa kuendesha makampuni ya kitaifa? Leo tukirudi tunaweza kuona kabisa ni ma AC na RC gani ambao walikuwa wamepewa nafasi kutokana na nafasi zao za TANU lakini si kutokana na rekodi yeyote ya uongozi; angefanya nini?

Njia pekee ambayo angeweza kuifanya ni kuchelewa kupata uhuru zaidi ili tuwe na wasomi wa kutosha. Labda tungepata uhuru mwaka 1980 kama Zimbabwe labda tungekuwa tayari kujitawala. Nadhani Mwalimu aliamini tuko tayari kujitawala. Labda angechelewesha kidogo.. but Zimbabwe ilichelewa and what happened?


Kiswahili ni lulu, wengine wanajua na wanaitukuza. jiulize kwa nini pale chuo kikuu sasa hivi kuna projecti nyingi sana za kiswahili, wageni wanajifunza sana lugha yetu. sisi ndio kwanza tumezubaa katika malumbano yasiyo kichwa wala miguu, kuhusu umuhimu wa Kiswahili. Nyerere alijua yote haya na aliwekeza kweli kweli. Tatizo letu kubwa sio umaskini. tatizo hasa ni ufinyu wa mawazo.


Hapa ndipo umegongomelea msumari; watu hawataki kufikiri! wanataka kuchukua vitu at face value kama YNIM ambaye uchungu wake wote na Nyerere umetokana na Babu yake kunyang'anywa nyumba ya bati or something...
 
Mindi,
hamna la maana lolote ktk post yako ndeeeeefu kama treni!!! mtoto wa darasa la tano wakati ule wa Nyerere, alikuwa anaweza kuandika uloandika hapo juu.........

why don't you dare to write the opposite bila kutumia maneno ya kebehi, matusi, dharau, jenga hoja na point baada ya point ili tuone kama akili zetu zitashawishika.

Kwa sababu hadi hivi sasa nimeamini kuwa huwezi kujenga hoja una react kwa emotions tu not reason. Hakuna mahali hata pamoja kwenye mjadala huu ulipojenga hoja yoyote ya maana, kwa maneno mengine kama mtoto wa darasa la tano anaweza kuandika alichoandika Mindi na wewe huwezi kuandika kama alivyoandika mindi ina maana kuwa mtoto wa darasa la tano....
 
Tunamzungumzia Nyerere wa 1961-1985 na legacy yake!Hivi tujiulize yale mapungufu ya Nyerere yaliyekuwepo kipindi cha utawala wake kama ndiye yapo hivi sasa wananchi wa wakati huu wangeichukuliaje zama hizi?Je angeweza kutawala Tanzania ya leo?
Hizi zama uhuru wa vyombo vya habari,zama za kukosoa serikali katika kutoa huduma za jamii,zama kukosoa viongozi kwa wazi uwazi kabisa!zama za biashara huria dawa za meno na sabuni mpaka vijijini zama za nyerere ilikuwa almasi!Wananchi wa zama hizi wangeweza kuvumulia kama wale waliyo kuwa wakitawalia na Nyerere?Tukianza kuelelezea yalikuwepo zama za Nyerere na wakati huu wengine wanaweza dhania ni ndoto!Zama Nyerere kila kitu anasa!Mwanakijiji sidhani kama angeweza fika Marekani zama za Nyerere labda angedandia meli au uwe mtoto wa balozi wa waziri!Mwananchi wa kawaida ilikuwa kusafiri nje kama unaenda mbinguni!Passport ilikuwa kama kuchimba Tanznanite

Je tangia Nyerere aachie madaraka Tanzania tulikuwa na idadi ya watu wa wangapi?Nyerere ameachia madaraka 1985 ni miaka 23 leo watanzania wangapi wa umri wa miaka 23!watoto wa 1985 walikuwa wangapi na sasa wana umri wa miaka mingapi?

Tukianza kufundisha mazuri ya Nyerere wa wananchi zama hizi ni historia wanaweza kuwa brainwashed kwa kuwa hawajakuwepo katika utawala wake kwamba Nyerere alikuwa superman!

Nyerere amefanya mazuri lakini kwa mwananchi wa kawaida mwenye njaa hana sabuni,hana nguo hana maji wa zama za Nyerere unambia nyerere saint atakushangaa.Salima Ahmed Salim 1984 alipokuwa waziri mkuu alitembelea Lindi na Mtwara akawaona watu wa huko wamevaa majunia ya mbolea hakuna Nguo wana pesa lakini nguo hakuna mpaka zije kwenye maduka ya ushirika ni machache!Leo hii mwananchi gani atakubali kuvaa magunia ya mbolea!
Mie nimesoma zama za Nyerere kulikuwa hakuna madaftari shuleni tuna madaftari 5 tuna ambiwa daftari moja masomo mawili!Leo hii nani anakubali hayo?
Kuna watu walitiwa ndani kipindi za uhujumu uchumi kisa ana dawa za sita za meno na sabuni 6!Nyerere baada ya kuona wananchi wamechoshwa na uadimu wa bidhaa akaanzisha zoezi la uhujumu
uchumi eti bidhaa zipo kwa walanguzi kisa isionekane ni utawala umesabisha hayo.Muulizeni Balozi Mahiga wa UN yeye alikuwa mkurugenzi wa usalama wa taifa wakati ule mpaka Nyerere anataka kupinduliwa yeye alikuwa mkuregenzi wa usalama!
Kuwa na gari dogo anasa lazima upate kibali kutoa state motor coperation ili uweze kumiliki gari dogo.Nyerer mwacheni apuzmike kwa amani kama Kikiwete aliposema mwacheni Mkapa apuzmike!
 
Haya mama tuendelee na mada usijekunimeza bure?!

Mimi sina mpango wa kukumeza ila nakukumbusha tu uniache peke yangu (leave me alone) kwenye mijadala yako. Zaidi ya hapo sina tatizo mkuu tuendelee na debate hapa maana taifa limeshauzwa kwa kiwango kikubwa sana na ccm!
 
Mimi sina mpango wa kukumeza ila nakukumbusha tu uniache peke yangu (leave me alone) kwenye mijadala yako. Zaidi ya hapo sina tatizo mkuu tuendelee na debate hapa maana taifa limeshauzwa kwa kiwango kikubwa sana na ccm!

Sikujua kama unamezaga watu....kwikwikwiiiii
 
Kwi kwi kwi kwi, yaani we acha tu! Huyu baba amekuwa ananisakama sana hapa JF na sijui nimemkosea nini. Kama ni hivi nadhani kuna sababu ya kummeza......lol

Dizaini aliwahi kukutokea ukampiga kibuyu na bado haja get over it.....kwikwikwiiiii
 
Dizaini aliwahi kukutokea ukampiga kibuyu na bado haja get over it.....kwikwikwiiiii

Dont get me started! Bado natafuta kujua sababu hasa ni ipi maana inaonekana jamaa yuko hapa kiwanja...... ila siwezi kushangaa kama hiyo ni sababu.. kwi kwi kwi kwi
 
Back
Top Bottom