Mwanamalundi
JF-Expert Member
- Aug 30, 2007
- 3,126
- 1,439
[/SIZE]Acheni kumdhalilisha Mwalimu, udikteta, mnajua maana ya udikteta nyie? Mwalimu alimwua nani? Mwalimu alitoa orders zipi ili watu wateswe?
Angalia marais waliomzunguka Mwalimu, wote walikuwa wanachinja watu labda ukiondoa rafiki yake Kaunda.
Mwalimu alikuwa kama baba ambaye alitaka kuwajengea wanawe kwa faida ya baadaye, lakini bahati mbaya mitoto yenyewe imekuwa mijinga na sasa badala ya kuangalia ujinga wao inaanza kumlaumu mzee wa watu ambaye alifanya kila kitu kuwajengea misingi mizuri ya maisha.
Nyerere alikuwa anapambana na watu kwa hoja na sio kwa mtutu wa bunduki. Sawa kuna watu wachache aliwaweka ndani, au kuna watu wachache ambao alipunguza speed yao wasiwe matajiri zaidi lakini huwezi kumwita Nyerere dikteta kwasababu ya kutetea misingi na mambo ambayo alikuwa akiyaamini?
Nyerere alitutengenezea misingi mizuri ya kusimama sisi wenyewe na kuendelea mbele kama binadamu lakini tulivyowajinga tumerudi kule kule. Tunaua elimu na kupeleka wanetu Ulaya, Kenya, Uganda na kwingineko, tumeua hospitali zetu na huduma za afya mpaka watu wanafumuliwa vichwa badala ya miguu. Tumeanza kuua mshikamano wa Kitanzania na sasa hata maofisini ukabila unaanza kujionyesha waziwazi. Sera kama za mtu ni afya zimekufa, leo mitalo ya vinyesi mpaka milangoni, kipindupindu kimekuwa donda ndugu katika karne hii ya 21.
Kibaya zaidi tumeanza kuwa watumwa kwenye nchi yetu. Tunauza nchi kwa kila anayetaka kununua kipande ili mradi ni mzungu. Tunajifanya tuna middle classs wengi ambao hawana uhuru wowote maofisini, wananyenyekea makaburu utafikiri hawajasoma, wanalipwa mishahara kidogo kuliko makaburu na hawawezi hata kulalamika. In fact wanaona furaha kuhudumia Wazungu kuliko Watanzania wenzao, huo ndio uhuru mnaotaka?
Mwacheni mzee wa watu apumzike salama huko aliko, ndio maana alivyokufa hata wale wapinzani wake wakubwa wa magharibi hawakuthubutu hata kutoa neno. Jamaa alikuwa kichwa na hicho kichwa ndio kilimjengea marafiki na maadui.
Lazima ujue Mwalimu alikuwa kiongozi wa miaka ya 60 na 70, miaka ambayo viongozi wengi walitakiwa wawe na misimamo, walikuwa na nguvu kubwa waliyopewa kikatiba na information ilikuwa haba, hivyo mambo mengine ambayo watu walikuwa wanatendewa huku chini ilikuwa sio rahisi kwa mtu wa juu kuyajua. Ni tofauti na sasa ambapo inatosha kuja JF kujua nani katembea na mke wa nani.
Sawa kuna makosa ambayo Nyerere alifanya kama binadamu yeyote anavyofanya lakini athari zake ni kidogo sana. Nyerere aliachia madarama miaka 22 iliyopita, je nini kimekuwa tofauti pamoja na hii demokrasia yetu? Watu wameuawa Zanzibar, tumepata Watanzania wakimbizi wa kwanza, nchi imeuzwa, vyuo vyetu havina watu wenye hoja tena badala yake wanavaa magwanda ya kijani utafikiri punguani. Nyerere hakuingilia uhuru wa wasomi na ndio maana hata watu waliotoka pale walikuwa wanajua kujenga hoja, nenda leo, kazi yao kubeba wanasiasa. Sio kazi ya mwanafunzi wa chuo kikuu kubeba wanasiasa utafikiri Machingas Kariakoo.
Mwafrika wa Kike huna hoja hapa kabisa, kama umekosa cha kuandika kaa kimya na mwache mwalimu wetu apumzike salama.
Nenda Tanzania leo, nenda Sheraton pale kama hujatolewa mkuku, eti changudoa, Mzungu sio changudoa lakini dada zetu ndio Changudoa. Uhuru ambao Nyerere aliamua kuacha kazi yake ya maana ya ualimu na mshahara mnono na marupurupu kibao ili atutetee Watanzania, leo tunaupoteza kijinga kijinga. Hiyo inatofauti gani na Apartheid ambako kama mweusi ilitakiwa ujue kikomo chako cha maeneo ya kwenda? Leo nenda kwenye Beaches zetu, kama Mwafrika kuna sehemu huwezi kufika.
Acheni kumkashifu Mwalimu bila hoja. Kama unataka andika hoja za maana ili tupambane kwa hoja. Huwezi kuandika mistari miwili eti unataka kujua athari za udikteta wa mwalimu. Nenda google na search jina la Mwalimu pamoja na dictator angalia utapata articles ngapi, why? Kwasababu watu walio wengi sasa wanakubaliana kwamba Mwalimu hakuwa dictator.
...Mtanzania, naunga mkono hoja zako nyingi katika hii post.