Mkandara,
naunga mkono maelezo yako. lakini ninayo haya ya kuongezea:
baada ya kuvunjika kwa jumuiya ya afrika mashariki tanzania iliingia ktk zoezi la kuanzisha viwanda vyake yenyewe. kiongozi aliyepewa jukumu hilo nakumbuka alikuwa cleopa msuya.
walioandaa industrial master plan ya tanzania naamini kabisa walikuwa wachapakazi wazuri na walikuwa wanajua wanalolifanya. tatizo hawakupewa nafasi ya kufanya kazi yao kwa uhuru.
tatizo letu tuliingiza siasa ktk kuendesha uchumi. mameneja waliteuliwa kisiasa. chama kilishika hatamu na kuingilia katika maamuzi ya kiufundi na kiutaalamu ktk uendeshaji mashirika yetu.
matawi ya ccm wakati mwingine yaliwalinda wafanyakazi wazembe na wahujumu wa mashirika na viwanda tulivyoanzisha. nidhamu ya kazi na tija viliathirika sana kutokana na majungu ya ccm ndani ya haya mashirika yetu.
mara nyingine siasa iliingilia mpaka ni wapi kiwanda kijengwe. mfano wa siasa kuingilia maamuzi ya wataalamu ni kujengwa kwa kiwanda cha kukata almasi iringa!!
siasa chama zililazimisha mashirika haya kuingia maamuzi yasiyo ya lazima. mfano mzuri ni kudhamini mikutano ya chama, timu za soka,vikundi vya ngoma na bendi za muziki n.k.
matawi ya chama yalikuwa kama menejimenti ya pili katika haya mashirika. huo ulikuwa ni mzigo mkubwa wa gharama. kiongozi wa chama alipojisikia hamu ya kuku, au mbuzi, basi aliamua kutunga ziara kutembelea shirika la mifugo. na alipofika huku basi walimpa mbuzi watano, au hata kuku hamsini!!
ilizuka tabia ya mameneja, ili kulinda ajira zao, wakaanza kutoa zawadi na kuwakarimu viongozi wa chama.
wale waliopewa jukumu la kuendesha uchumi, wakina mtei,msuya,rweyemamu,...walipiga kelele kuhusu chama na siasa kuingilia utendaji wa mashirika ya umma. tatizo lililojitokeza ni Nyerere na kikundi fulani cha wakereketwa wa chama kukataa ushauri wa kitaalamu, na wakati mwingine hata kuanzisha hujuma na majungu ya kisiasa dhidi yao.
mgongano huo nilioueleza hapo juu ndiyo uliosababisha: kwanza ,mashirika yetu kudorora; pili; mapato ya serikali yakashindwa kuhimili matumizi yake. wataalamu wakamshauri tena Nyerere apunguze, kwa muda, matumizi ya serikali yake, na akaribishe mitaji toka nje. Nyerere alikataa vyote hivyo. Matokeo yake wafadhili wakatugomea, nchi za Nordic zilichelea kidogo, lakini nazo zikagoma kutusaidia kwasababu Nyerere aligeuka "haambiliki."
Nyerere alishauriwa ayabinafsishe haya mashirika kwa masharti yake yeye mwenyewe. Kama alikataa mpaka yakafikia kuwa magofu ni nani wa kulaumiwa? Hizi lawama ni zake Nyerere. Alipoondoka nakumbuka hazina ilikuwa imekauka na aliyetuokoa ni Robert Mugabe. Meli za mafuta ziligoma kupakua mzigo kwa sababu nchi ilikuwa mufilisi na haiaminiki tena.
Mwalimu ndiye aliyepaswa kurudisha nidhamu na ufanisi katika kuendesha mashirika yetu. Kwa bahati mbaya aliyafumbia macho au kuyaonea aibu matendo ya hujuma yaliyokuwa yakiendelea.
Mwalimu ndiye aliyepaswa kusitisha tabia ya wakereketwa wa chama kuingilia menejimenti za mashirika ktk kufanya maamuzi ya kibiashara.
Mwalimu vilevile alipaswa kuwa jasiri na kukubali ushauri wa kukaribisha mitaji toka nje, at the time when he could enforce discipline and ethics.
WE HAD A CHANCE TO ATTAIN ECONOMIC DEVELOPMENT AND WE SQUANDERED IT. UNFORTUNATELY, OUR BELOVED MWALIMU WAS AT THE CENTER OF IT.