mgonjwa wa ukimwi,
unajua mimi ninapojibu hoja najaribu kuangalia factors nyingi na ninakuwa abstract na wakati huo huo nina acha space for you to digest more,
mfano umekuja na kusema kuwa ujamaa ni siasa ya darasa la saba blah blah..., wakati mwanzoni mwa message yangu nimegusia kuwa wenzetu nchi za magharibi kwenye vyuo vikuu sasa hivi wanasoma ujamaa, na nilialikwa kuhuzuria semina moja inayohusu ujamaa na jinsi gani europeans wanaweza kufaidika nayo.
kitu cha pili nilipokuambia usijilinganishe na mwalimu, nilikuwa na maanisha kitu muhimu,unajua mwalimu kabla haja implement hizi policy alifanya utafiti wa kina, si kwamba alikurupuka tu, kama utakumbuka baada ya kuwa rais alifanya ziara katika nchi za magharibi na baadae akaenda china, kwahiyo niliposema hiyo message nilikuwa nikimaanisha kuwa tusifanye kama vile mwalimu hakuyafikiria hayo unayo yaona wewe sasa hivi,tofauti ni kuwa mwalimu alichagua njia ambayo aliiona ni bora kwa taifa hili kutoka na mazingira ya wakati huo.
mfano unaongelea capitalism katika nchi za magharibi, kumbuka kitu kimoja,capitalists wa magharibi ni raia wa nchi zile, mfano bill gates ni raia wa marekani na pesa zake ziko kwenye benk za marekani na serikali ya marekani inafaidika na pesa zake,
sasa watu tuliokuwa nao hapa tanzania wakati tunapata uhuru walikuwa wanyonyaji au makaburu,interest yao kubwa ilikuwa ni kupata resources na kupeleka kwenye nchi zao, na hata pesa zao walikuwa hawawekezi hapa.
kwahiyo kama unaongelea capitalists be carefull on interest,
you have capitalists with different interests,
kama tungekuwa na capitalists wa kitanzania wengi ambao ndio wangekuwa wana viwanda,mashamba na wana weka pesa zao hapa tanzania na pia wanatoa ajira na kuheshimu haki za binadamu sidhani kama wangetaifishwa,
kwahiyo chazo cha kutaifisha ilikuwa unyonyaji,unyanyasaji unaofanywa na hawa makabaila.
baada ya haya maelezo naomba sasa nijaribu kukujibu maswali yako
(A) Kanusha. Arusha Decralation (AD) haikujenga mazingira ya rushwa na umasikini kwa ku-dismantle the most vital class in economic growth: capitalist class.
jibu:
azimio la arusha lilitokana na ukweli kuwa tanzania ilikuwa(na bado) ni taifa la watu masikini, unapokuwa na watu milioni 20, halafu watu milioni 15 ni masikini wanaoishi vijijini na katika hao milioni tano wapo milioni moja ambao ni matajiri sana na wengi wao ni wazungu, wahindi, waarabu nk na zaidi wana wa exploit wale milioni 15 kama kundi la wanyama , unategemea nini? huu ndio uhuru unao utaka wewe??kwahiyo azimio la arusha lilikuwa ni kurealiize kuwa hili ni taifa masikini na haliko tayari kuwalinda watu wachache kuishi kwa jasho la watu wengi.kwahiyo sioni mazingira ya rushwa unayoyaongelea yametokea wapi,
infact nchi yetu imeengia kwenye wimbi la rushwa baada ya hao viongozi wenu wa siku hizi kwenda zanzibar na kutuletea azimio la zanzibar,kuanzia miaka ya 90 ndio tumeanza kushuhudia wimbi la viongozi kutajirika kupindukia.
ku prove hili nipe mfano mmoja wa rushwa uliotekea wakati wa mwalimu na kama wahusika wamegundulika hawakuchukuliwa hatua kali,
lakini angalia kipindi cha mwinyi, mkapa na kikwete, kuna maskendo mangapi yametokea na hatua gani zilichukuliwa?
(B) Kanusha. Wajanja wachache wakiwamo wahindi na viongozi wa ngazi ya juu (except Nyerere na Sokoine) walikiuka misingi ya AD na hivyo kujitajirisha na kufanya vita dhidi ya rushwa ishindikane, huku ikisababisha kifo cha Sokoine.
hii sio sababu tosha ya kudiscredit azimio la arusha,hiyo ni sawa na kusema kwasababu kuna amri ya Mungu inasema usiibe na kwasababu kuna watu wanakiuka amri hiyo basi ni unasema ni bora amri hiyo iondelewe.
kusababisha kifo cha sokoine?? hizo ni speculations, ukweli tunaoujua ni kuwa sokoine alikufa kwa ajari ya gari morogoro, kama kuna kitu unauhakika nacho tutafurahi ukituwekea wazi.
(C) Kanusha. Misingi ya AD haitekelezeki kwasababu haina reinforcement yeyote, na kwamba inawapa viongozi utajiri na kinga dhidi ya rushwa. Umiliki wa umma wa mali na utajiri wa taifa hautekelezeki (refer to game theory).
hii nayo sio kweli,
misingi ya azimio la arushwa ilitekelezwa na ilikuwa reinfoced.viongozi walikuwa hawaruhusiwi kujitajirisha kwa njia za rushwa na matokeo yake tulikuwa na serikali makini,
the fact ni kuwa mataifa ya magharibi yalikuwa yanaupinga mfumo ule kwasababu wazungu waliathirika na wakatuwekea masharti mengi ndio maana tulishindwa kutoka, more than that, kumbuka kwenye kundi la watu wengi kuna mengi pia, kwahiyo ni kweli kulikuwa na watu walioendelea kutumia mianya mbalimbali na kujitajirisha.
vilevile kumbuka hato nchi za magharibi viongozi wao pia wana code of conduct ambayo sio azimio la arusha lakini semantics ni sawa,kwa maana ya kwamba rushwa haivumiwili katika jamii.
kwa kumalizia nasema kuwa azimio la arusha bado liko "valid" na nafikiri ni muhimu likatekelezwa wakati huu wa uwekezaji kuliko wakati mungine wowote.
tunatakiwa tufanye mabadiriko kadhaa mfano tunahitaji kuwapa wazawa uwezo zaidi wa kumiliki mali, mfano pale reginald mengi alipotakana kununua kilimanjaro hotel halafu akanyimwa,ule ndio ulofa wenyewe,pale mzawa anapoonyesha nia ya kuwekeza ndio tuwape kipaumbele kwanza,
pili tunataka wawekezaji katika sekta ya kilimo na viwanda sio majambazi hawa wanaofata resourse zetu kama madini,gesi nk hivi vitu vikiisha na wao hao wanaondoka zao wanatuachia mashimo.